Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Uchumi wa Tanzania uko mitatani. Hili ni kweli. Kuporomoka kwa thamani ya shilingi kumefanya bei ya vitu mbalimbali kuwa ya juu kulinganisha na kipato cha watu. Ili watu wamudu mambo waliyokuwa wanayamudu mwaka mmoja tu uliopita wanahitaji ongezeko la maana ya kipato. Bahati mbaya hawawezi kujiongezea kiwango na hivyo watu wanalazimika kubadilisha yao na kubana matumizi. Mamilioni ya Watanzania wanajikuta wanalazimika kuishi hivyo. Wale wenye nafasi ya kufanya ufisadi wanaweza kutumia nafasi hiyo kufanya ufisadi zaidi ili kujiongezea kipato kumudu maisha. Lakini hawana uwezo wa kuamua kujiongezea posho au mishahara ili wamudu maisha.
Hili si kweli kwa wabunge wetu. Habari kwamba wabunge wamejiongezea posho kadhaa kwa karibu asilimia zaidi ya 150 ni habari za kuudhi, kukera na kama ni za kweli kabisa ni za kumfanya kila Mtanzania kupinga kwa nguvu zote dhulma hii ya wazi kwa wananchi wetu maskini wanaohenyeka kila siku kujitafutia ridhi zao. Ndugu zangu, wabunge ndio watu pekee ambao wanaweza kujipangia mishahara na posho zao bila kusimamiwa na chombo kingine chochote. Hata Rais hajipangii mshahara au posho!
Ukweli ni kuwa hakuna sababu yoyote ya kiakili ya kuhalalisha posho zilizoongozwa kwa wabunge. Katika nchi ambayo watu wanadaiwa kuna hali mbaya ya kiuchumi na hasa kwenye mporomoko wa shilingi Wabunge kuongezewa posho ni unyonyaji wa hali ya juu na dhulma kwani fedha zote hizo zinatoka kwa wafanyakazi wanaohenyeka kila siku kujipatia maisha bora. Ni wizi na dhulma kwa utu wa Watanzania maskini ambao fedha kidogo waliyonayo wanaipanga wakijua kuwa uchumi uko katika hali mbaya. Kuhalalisha wizi huu wa mchana kweupe ni kuwa washirika wa dhulma hiyo.
Tunapozungumzia "matumizi mabaya ya madaraka" mara nyingi watu wanafikiria mtu mmoja akitumia madaraka yake vibaya. Ukweli ni kuwa kuna wakati taasisi au vyombo vinaweza kutumia madaraka vibaya. Polisi wanapoua pasipo uhalali ni matumizi mabaya ya madaraka na wabunge wanapotumia haki zao za Bunge kujinufaisha wao wenyewe ni matumizi mabaya ya madaraka.
Kisingizo pekee ambacho kinatolewa kuhalalisha wizi huu wa mchana ni kuwa wabunge wanahitaji fedha ili kusaidia wapiga kura wao. Wengine wanajenga hoja kuwa wabunge hutumia posho hizo kutoa misaada mbalimbali. Ndugu zangu, mtindo huu ni mitndo ambao umewafanya wabunge wasiwajibike Bungeni kwa sababu wanajua wanaweza kutumia fedha zao hapa na pale kutuliza wapiga kura wao. Lakini kama tukipiga marufuku wabunge kutoa fedha yao Bungeni kwa namna yoyote ile wabunge wagenfanya nini? Ni wazi wangejitahidi kuihimiza serikali kufanya mambo mbalimbali, kusimamia mapato, kufuatilia nidhamu n.k
Bahati mbaya mfumo ulioruhusiwa chini ya CCM unaruhusu wabunge kutoa misaada na fedha zao wenyewe. Huu ni mfumo mbaya kwani kwa kisingio cha kutoa misaada wao huchota kwenye hazina ya taifa. Wanatumia hiki kama kisingizo cha kwanini wanastahili zaidi. Lakini wanashindwa kujiuliza ni mfanyakazi gani wa Tanzania ambaye haitaji kutoa misaada ya hapa na pale kwa watu wa familia yake? Karibu kila mfanyakazi wa Tanzania ana majukumu ya kusaidia hapa na pale kwenye familia yake ndugu zangu na hata jamaa zake kijijinbi. Sasa je huyu anaweza vipi wakati fedha anazopata ni za mshahara?
Hivi ni Mtanzania gani ambaye akiulizwa kama anahitaji nyongeza ya posho au mshahara ili imsaidie kwenye matatizo yake anaweza kusema haitaji. Sasa kwanini Wabunge wanaamini kuwa wao ndio wanahitaji sana kuwasaidia watu wa majimbo na vijijini kwao na hivyo kujihalalishia posho. Kwanini wanafikiria wao ambao wanapewa posho za kufuru wanastahili zaidi katika kipindi hiki cha hali mbaya ya uchumi ambapo vijana wamekosa ajira, gharama ya kufanya biashara iko juu na bei ya bidhaa na huduma mbalimbali inazidi kupanda juu kila siku?
Tuwe wa kweli. Bunge kama limehalalisha ongezeko hili la posho limekuwa mshiriki wa wizi wa mali za watu. NI sawasawa na kumkuta mkulima aliyelima na kutoka jasho ambaye baada ya kuvunja anaambbiwa hawezi kula alichovuna na badala yake arudi kulima tena. NI sawasawa na kuchomeka mrija wa unyonyaji kwenye mgongo wa mkulima na mfanyakazi wa Tanzania, mgongo ambao tayrai umekuwa na mirija mingine (bei ya umeme, mafuta, mafuta ya taa, nauli, nyumba, elimu n.k!).
Tunachoweza kuomba tuambiwe ni kuwa hali ya uchumi imekuwa nzuri kuwweza kufanya jambo hili. Na tuna sababu kuwa hali ya uchumi imebadilika na kuwa nzuri. Vinginevyo, tutaelezea vipi ongezeko la posho za wabunge wakati wa hali mbaya ya uchumi. RAis Kikwete na chama chake wanaweza vipi kuhalalisha hili? Binafsi ningependa kusikia viongozi wa CCM wanaweza kuhalalisha vipi ongezeko hili. Hivi kweli kuna mtu anaamini kuongeza posho ndio kutawafanya wabunge kuwa wawajibikaji? Tunajuaje kama kiwango kilichoongezwa kinatosha kuwashawishi kuwajibika? Itakuwaje mwezi mmoja baadaye wakitaka kuongezewa zaidi ili wawajibike zaidi? Je hatuoni kuwa ni kama tumewadekeza - kwamba wasipoongezewa posho basi hawawajibiki. Je, yawezekana wabunge wa CCM wamelichukua taifa nyara na sasa taifa zima liko mbele ya huruma yao - posho au hatuwajibiki!
Kwa kweli hii ni dhulma dhidi ya wafanyakazi wa Tanzania ambao kwa kweli hawana mtetezi kwani vyama vya wafanyakazi navyo vimelala kwenye kitanda cha ufisadi pamoja na watawala wetu walioshindwa. Binafsi sitaki kusikia mbunge ati analalamikia posho; hivi wabunge wakilalamikia posho wakati wao ndio wanatunga sheria na watu walioko nje wafanye nini? Kama kuna mbunge anaona posho hazistahiki walete miswada Bungeni kutengeneza sheria ya kusimamia posho na kura za roll call zipigwe ili tujue ni mbunge gani anapinga sheria hiyo iili wananchi wajue nani ni adui yao. Haitoshi kwa wabunge na wenyewe kulalamikia posho kwa sababu ndio watu pekee wanaoweza kubadilisha sheria ; haiitaji serikali kufanya hivyo. Sasa kwanini hakuna mswada wa mabadiliko ya sheria ya fedha au hata sheria ya kusimamia posho?
MMM
Hili si kweli kwa wabunge wetu. Habari kwamba wabunge wamejiongezea posho kadhaa kwa karibu asilimia zaidi ya 150 ni habari za kuudhi, kukera na kama ni za kweli kabisa ni za kumfanya kila Mtanzania kupinga kwa nguvu zote dhulma hii ya wazi kwa wananchi wetu maskini wanaohenyeka kila siku kujitafutia ridhi zao. Ndugu zangu, wabunge ndio watu pekee ambao wanaweza kujipangia mishahara na posho zao bila kusimamiwa na chombo kingine chochote. Hata Rais hajipangii mshahara au posho!
Ukweli ni kuwa hakuna sababu yoyote ya kiakili ya kuhalalisha posho zilizoongozwa kwa wabunge. Katika nchi ambayo watu wanadaiwa kuna hali mbaya ya kiuchumi na hasa kwenye mporomoko wa shilingi Wabunge kuongezewa posho ni unyonyaji wa hali ya juu na dhulma kwani fedha zote hizo zinatoka kwa wafanyakazi wanaohenyeka kila siku kujipatia maisha bora. Ni wizi na dhulma kwa utu wa Watanzania maskini ambao fedha kidogo waliyonayo wanaipanga wakijua kuwa uchumi uko katika hali mbaya. Kuhalalisha wizi huu wa mchana kweupe ni kuwa washirika wa dhulma hiyo.
Tunapozungumzia "matumizi mabaya ya madaraka" mara nyingi watu wanafikiria mtu mmoja akitumia madaraka yake vibaya. Ukweli ni kuwa kuna wakati taasisi au vyombo vinaweza kutumia madaraka vibaya. Polisi wanapoua pasipo uhalali ni matumizi mabaya ya madaraka na wabunge wanapotumia haki zao za Bunge kujinufaisha wao wenyewe ni matumizi mabaya ya madaraka.
Kisingizo pekee ambacho kinatolewa kuhalalisha wizi huu wa mchana ni kuwa wabunge wanahitaji fedha ili kusaidia wapiga kura wao. Wengine wanajenga hoja kuwa wabunge hutumia posho hizo kutoa misaada mbalimbali. Ndugu zangu, mtindo huu ni mitndo ambao umewafanya wabunge wasiwajibike Bungeni kwa sababu wanajua wanaweza kutumia fedha zao hapa na pale kutuliza wapiga kura wao. Lakini kama tukipiga marufuku wabunge kutoa fedha yao Bungeni kwa namna yoyote ile wabunge wagenfanya nini? Ni wazi wangejitahidi kuihimiza serikali kufanya mambo mbalimbali, kusimamia mapato, kufuatilia nidhamu n.k
Bahati mbaya mfumo ulioruhusiwa chini ya CCM unaruhusu wabunge kutoa misaada na fedha zao wenyewe. Huu ni mfumo mbaya kwani kwa kisingio cha kutoa misaada wao huchota kwenye hazina ya taifa. Wanatumia hiki kama kisingizo cha kwanini wanastahili zaidi. Lakini wanashindwa kujiuliza ni mfanyakazi gani wa Tanzania ambaye haitaji kutoa misaada ya hapa na pale kwa watu wa familia yake? Karibu kila mfanyakazi wa Tanzania ana majukumu ya kusaidia hapa na pale kwenye familia yake ndugu zangu na hata jamaa zake kijijinbi. Sasa je huyu anaweza vipi wakati fedha anazopata ni za mshahara?
Hivi ni Mtanzania gani ambaye akiulizwa kama anahitaji nyongeza ya posho au mshahara ili imsaidie kwenye matatizo yake anaweza kusema haitaji. Sasa kwanini Wabunge wanaamini kuwa wao ndio wanahitaji sana kuwasaidia watu wa majimbo na vijijini kwao na hivyo kujihalalishia posho. Kwanini wanafikiria wao ambao wanapewa posho za kufuru wanastahili zaidi katika kipindi hiki cha hali mbaya ya uchumi ambapo vijana wamekosa ajira, gharama ya kufanya biashara iko juu na bei ya bidhaa na huduma mbalimbali inazidi kupanda juu kila siku?
Tuwe wa kweli. Bunge kama limehalalisha ongezeko hili la posho limekuwa mshiriki wa wizi wa mali za watu. NI sawasawa na kumkuta mkulima aliyelima na kutoka jasho ambaye baada ya kuvunja anaambbiwa hawezi kula alichovuna na badala yake arudi kulima tena. NI sawasawa na kuchomeka mrija wa unyonyaji kwenye mgongo wa mkulima na mfanyakazi wa Tanzania, mgongo ambao tayrai umekuwa na mirija mingine (bei ya umeme, mafuta, mafuta ya taa, nauli, nyumba, elimu n.k!).
Tunachoweza kuomba tuambiwe ni kuwa hali ya uchumi imekuwa nzuri kuwweza kufanya jambo hili. Na tuna sababu kuwa hali ya uchumi imebadilika na kuwa nzuri. Vinginevyo, tutaelezea vipi ongezeko la posho za wabunge wakati wa hali mbaya ya uchumi. RAis Kikwete na chama chake wanaweza vipi kuhalalisha hili? Binafsi ningependa kusikia viongozi wa CCM wanaweza kuhalalisha vipi ongezeko hili. Hivi kweli kuna mtu anaamini kuongeza posho ndio kutawafanya wabunge kuwa wawajibikaji? Tunajuaje kama kiwango kilichoongezwa kinatosha kuwashawishi kuwajibika? Itakuwaje mwezi mmoja baadaye wakitaka kuongezewa zaidi ili wawajibike zaidi? Je hatuoni kuwa ni kama tumewadekeza - kwamba wasipoongezewa posho basi hawawajibiki. Je, yawezekana wabunge wa CCM wamelichukua taifa nyara na sasa taifa zima liko mbele ya huruma yao - posho au hatuwajibiki!
Kwa kweli hii ni dhulma dhidi ya wafanyakazi wa Tanzania ambao kwa kweli hawana mtetezi kwani vyama vya wafanyakazi navyo vimelala kwenye kitanda cha ufisadi pamoja na watawala wetu walioshindwa. Binafsi sitaki kusikia mbunge ati analalamikia posho; hivi wabunge wakilalamikia posho wakati wao ndio wanatunga sheria na watu walioko nje wafanye nini? Kama kuna mbunge anaona posho hazistahiki walete miswada Bungeni kutengeneza sheria ya kusimamia posho na kura za roll call zipigwe ili tujue ni mbunge gani anapinga sheria hiyo iili wananchi wajue nani ni adui yao. Haitoshi kwa wabunge na wenyewe kulalamikia posho kwa sababu ndio watu pekee wanaoweza kubadilisha sheria ; haiitaji serikali kufanya hivyo. Sasa kwanini hakuna mswada wa mabadiliko ya sheria ya fedha au hata sheria ya kusimamia posho?
MMM