Ondoa ''misconception'' kuhusu Wanyarwanda

msumeno

JF-Expert Member
Aug 3, 2009
2,827
1,729
Waungwana kaka yenu nakaribia kurudi nyumbani baada ya kuishi hapa DRC kwa Takriban miaka 2.

Katika kipindi chote nilichokaa hapa nimejifunza mengi sana ila leo nitazungumzia kuhusu hawa jirani zetu Wanyarwanda.Maana nimekua nikipita hapa mara kwa mara. Kwa kifupi ondoeni dhana potofu kuhusu hawa jamaa maana mimi dhana hiyo tayari nimesha ifuta. Wengi wenu kama sio wote mnadhani kuwa wanyarwanda ni watu ''wasio poa'' au ni wenye majivuno labda wengine mnadhani eti hawatupendi Watanzania.

Dhani hizi ni potofu kweli kweli, mwanzoni nikipita hapa sikua nikiongea kiswahili ili nisitambulike maana niliogopa kweli hawa jamaa. Baadae nikagundua dhana yangu sio sahihi kabisa na Mungu anisamehe.

Hawa jamaa hawana shida kabisa na wageni hasa Watanzania. Nimekaa Hoteli mbali mbali hapa nikiwa transit kwenda DRC au kurudi Home Tanzania, na kote huko nimechukuliwa vizuri sana tu.

Sio hotel tu , nimepanda boda boda, nimefika masokoni, msikitini , madukani kote huko hawa jamaa ni wakarimu sana na nimetendewa vizuri kwa kweli.

Wacha niweke mifano michache hapa mnielewe, nasisitiza michache mana nimengi nimeyaona positive.

1. Nikitoke DRC kurudi home ( niko njiani) tukiwa pale Kingarama Restaurant nikapata shida kidogo ya chenji ya Dollar kwa FRC ya Rwanda ili nipate Supu, wakati nikitaka kutoka nikatafute nje chenji mzee mmoja akasema kumwambia mhudumu mwache apate hiyo supu nitalipa mimi kama 'felistation' maana walitufunga kombe la CHAN huyu mzee alijua mimi ni Mkongo, nikala na wala hakukaa kuni bore kwa vile ameninunulia supu alitimua.... nikashangaa maana DRC husema hawa jamaa hawawapendi

2. Mh PK alitoa ma Bus kadhaa kuja pale Gisenyi kuchukua mashabiki wa DRC bure ili waje washangilie timu yao .... BUS zilijaa wakongo na walilindwa na wakarudi kwa amani.

3. Nilipofika Kigali na baada ya kuchukua Hotel, nikataka kwenda Masjid kusali , nikauliza Reception , kwa mshangao akadakia jamaa mmoja na kuniambia ''msikiti uko mbali ila subiri nitakupeleka maana naelekea njia hiyo hiyo huyu hakua musilam na hakua akinijua , ni tax man tu alie leta mteja pale. Njiani tulipiga soga sana.

4. Nikiwa hapa kwa siku ya pili na ticketi yangu ikiwa ya jioni nikaona ni negotiate nikae mpaka jioni kwa kulipa kidogo chumba maana check out ni saa tano asubuhi... Manager akasema ''kaa tu usilipe chochote , karibu tena wakati mwingine''.

5. Huko mitaani niliko kwenda kutembea jana usiku, nilikutana na ukarimu sana hasa unapouliza direction na mengine. hawa jamaa wana smile sana na sio ya smile ya kinafiki au ya kutegemea kitu

(a) Kitu nimegundua labda unaweza sema cha kushangaza au sio kizuri ni kwamba watu hapa hawaongelei siasa sana , ni aghalabu kukuta watu wakiongelea siasa hapa tofauti na home TZ kila mtu politician

(b) Printing media sio nyingi ila TV station wanazo nyingi tu

(c) Polisi ni vijana na hawacheki cheki wako serious kweli ila ukiuliza kitu wanakujibu vizuri tu

(e) Rushwa hapa sio sana labda niseme hakuna, polisi akikumata unaandikiwa charge hakuna zile za kuvutana nyuma ya gari na watu wanatii sheria kweli kweli

(f) Ule mfumo wa ukusanyaji kodi kila duka hapa, na kuna ka machine kama ka fingure print sijauliza ni ka nini ila ni ka mamlaka ya Kodi ya Rwanda. ( hapa nikakumbuka zile machine zetu sijui zilishia wapi maana zilileta sintofamu)

(g) Taxi zina Automatic Counter kama za Europe


NIMEONA MENGI WACHA NIACHIE HAPA NA WENGINE WACHANGIE MAANA NATUMAINI KUNA WENGI WAMEPITA HAPA PIA, WITO WANGU KAMA UNA JIRANI YAKO MNYARWANDA USIMTENDEE VIBAYA HAWA WATU WENGI WAO NI WAZURI SANA KWETU
 
Rwanda wanajua madhara ya siasa za uhasama, hawataki kabisa kusikia mawazo ya kipumbavu kuhusu huyu ni mtutsi na huyu ni mhutu. Damu iliyomwagika mwaka 1994 na hata kabla ya hapo ni nyingi na huwa inawakumbusha umuhimu wa amani. Paul Kagame is a genious. Kaitumia CHAN katika kuitangaza Rwanda kimataifa. Kavitumia viwanja vinne kuandaa mashindano makubwa kabisa barani Afrika. Sisi tuna viwanja vinavyoendelea kuzeeka kama viwanda ambavyo vilitaifishwa enzi za Mkapa. Kagame anayo bahati kwamba wanyarwanda sio watu biased kama sisi Watanzania, wanyarwanda wanajenga akili za kimaendeleo, sisi tunajenga akili za kipumbavu za kutazamana kisiasa, yule mwanaCCM huyu mwana CHADEMA.

Rwanda ya miaka 10 ijayo itakuwa mbali zaidi yetu, lakini Rais Magufuli anao uwezo wa kuanza kuifanya Tanzania iwe katika spirit ya kuikimbiza Rwanda. Na alipokaa madarakani kwa siku chache tayari balozi wa Rwanda akaenda Ikulu kuongea biashara za kimataifa. Paul Kagame mtu mwenye progressive mentality, nasikia alimwambia rais wa awamu ya nne nipe bandari ya Dar nikuendeshee nchi yako. Afrika inahitaji viongozi wenye kuweza kuthubutu.
 
Kuna tofauti ya maisha ya kawaida na maisha ya siasa hao wanyarwnda wa asili ya kitusi ni kama panya wanakula na huku wana puliza. Unaweza ishi na mnyarwanda hata miaka 20 na usijuwe alicho nacho moyoni ila siku ikifika ndipo utamjua ni nani! Wewe kaa kimya tu huwezi jua ukarimu na uzuri wa watu kwa safari zako za hapa na pale siku mbili unarudi na kusema ni watu wazuri wewe kuwa makini unapo towa post kama hizi, kuna watu wameisha ishi na hao watu zaidi ya miaka kumi na wana wafahamu vema. Kiufupi sio watu wazuri kwa jamii tofauti naya kitusi.
 
Of all the countries hatuwezi kuwaiga wala kuwaonea wivu Wanyarwanda na ni ujinga kufananisha Rwanda na Tanzania. Pengine ufananishe Rwanda na Mkoa wa Kigoma. Serikali ya Rwanda inanuka damu na dhuluma kwa wahutu iliyowaua na kwa madini wanayoyiba huko DRC. Sisi tuna Serikali ya kedemokrasia na tunaruhusu uhuru wa mawazo wakati huko Rwanda kuna udikteta na utawala wa kiimla tu. Tuna ma-Rais watatu wamebadilishana madaraka katika kipindi ambacho Rwanda ina Rais mmoja anayeendelea kuua wapinzani wake wa kisiasa. Kimsingi hatuna cha kujifunza toka Rwanda
 
Rais huyo moja Paul Kagame ambaye amekaa madarakani kwa muda mrefu ameweza kusimamia economic goals walizojiwekea. Kwenye afya na elimu Rwanda wapo vizuri kuliko sisi. Wanaheshimu professions za wanyarwanda wote walio kila kona ya dunia hii. Wapo watanzania wanaofanyiwa fitina ili wasiweze kufanya mambo makubwa kwa nchi yao!. Rwanda hawanyimani nafasi za kutumia vipaji vyao kwa faida ya nchi yao, mtanzania akiwa na uwezo wa kufanya kitu kwa ufasaha, atatazamwa kwa jicho baya la kumtakia kushindwa ili aonekane hajui lolote.
 
Kuna tofauti ya maisha ya kawaida na maisha ya siasa hao wanyarwnda wa asili ya kitusi ni kama panya wanakula na huku wana puliza. Unaweza ishi na mnyarwanda hata miaka 20 na usijuwe alicho nacho moyoni ila siku ikifika ndipo utamjua ni nani! Wewe kaa kimya tu huwezi jua ukarimu na uzuri wa watu kwa safari zako za hapa na pale siku mbili unarudi na kusema ni watu wazuri wewe kuwa makini unapo towa post kama hizi, kuna watu wameisha ishi na hao watu zaidi ya miaka kumi na wana wafahamu vema. Kiufupi sio watu wazuri kwa jamii tofauti naya kitusi.

Nadhani uko sahihi kwa comment hii...
 
Acha Uongo wewe, nini umekatazwa kafanya Tanzania. Unyama unaofanywa huko Burundi na Rwanda unafananishaje na Tanzania. Hebu kaa kwenye hizo nchi uone kama utaruhusiwa kujadili ubaya wa serikali. Mauaji ya Albino mbona hupigii kelele acha wanayoipata wapinzani wa serikali ya Rwanda na Burundi.
Kujadili ubaya wa serikali au uzuri wake kunakusaidia nini wewe ikiwa mfukoni huna kitu na hujui lini utakuwa na fedha?. Akili za kitanzania zimemezwa kwenye ujinga wa kufuatilia siasa badala ya kuwa wabunifu katika utafutaji wa maendeleo yetu binafsi. Nimekupa mfano wa mauaji wa alibino ambayo ni aibu yetu kimataifa. Maadili bora tulikuwa nayo enzi hizo za Mwalimu Nyerere, sasa hivi hakuna kitu, kila mtu amejawa na kiburi na dharau. Kila mtu anajifanya anajua kila kitu.
 
Mapinduzi ya kimaendeleo kwa nchi ndogo kama Rwanda, hata ukipewa wewe Urais unaweza tena kwa kipindi kifupi sana. Na hasa ukiwezeshwa kwenda kuiba raslimali za nchi zilizo jirani na wewe
ni bora yule anayeenda kuiba kwa ajiri ya watu wake kuliko hawa ambao wanacho lakin wanagawa bwelele kwa wazungu
 
Ukarimu wetu uliondoka na Mwalimu Nyerere, upendo wetu uliondoka na awamu ya kwanza enzi zile za wapigania uhuru wa afrika ya kusini walioishi Mazimbu Morogoro. Tanzania iliyofuata imejaa ubinafsi na kila aina ya unyama, yakiwemo mauaji ya albino. Tanzania ya sasa imejaa ushenzi mwingi tu ambao wala haustahili kuandikwa kwenye mitandao.
Wale watutsi na wahutu wanaoishi kwenye makambi ya wakimbizi ndio mabalozi wetu wazuri wanaoweza kukuambia maana ya ukarimu tulionao.
 
Wale watutsi na wahutu wanaoishi kwenye makambi ya wakimbizi ndio mabalozi wetu wazuri wanaoweza kukuambia maana ya ukarimu tulionao.
Nilibahatika kuwaona wakimbizi wa afrika ya kusini enzi zile za Mwalimu Nyerere wakiishi kwa amani hapa Dar. Kila Ijumaa walikuwa wana matamasha yao pale IFM, ninafahamu sana ukarimu wetu. Ninachokipinga ni ile dhana potofu wa kumshambulia Kagame kana kwamba sisi ni wasafi sana. Tanzania ya sasa licha ya kuwakarimu wageni, imejaa mambo mengi ya kishenzi tu, likiwemo suala la ukatili kwa walemavu wa ngozi.
 
Kujadili ubaya wa serikali au uzuri wake kunakusaidia nini wewe ikiwa mfukoni huna kitu na hujui lini utakuwa na fedha?. Akili za kitanzania zimemezwa kwenye ujinga wa kufuatilia siasa badala ya kuwa wabunifu katika utafutaji wa maendeleo yetu binafsi. Nimekupa mfano wa mauaji wa alibino ambayo ni aibu yetu kimataifa. Maadili bora tulikuwa nayo enzi hizo za Mwalimu Nyerere, sasa hivi hakuna kitu, kila mtu amejawa na kiburi na dharau. Kila mtu anajifanya anajua kila kitu.
Wewe huo ubunifu wa kimaendeleo umeufanya hapa Tanzania ukakataliwa?. Hiyo Dhambi ya kuua Albino mbona Kenya na Burundi ipo. Hicho kiburi na dharau ni hulka ya mtu ambayo dunia nzima wapo wenye tabia hizo. Usishindwe kufanikiwa ki Uchumi ukadharau mahali ulipo. Hata Kagame hawawekei watu wake pesa mfukoni,na ukishindwa kuishi Tanzania na watu wake basi hata kwa mungu utapaona pabaya
 
Wewe huo ubunifu wa kimaendeleo umeufanya hapa Tanzania ukakataliwa?. Hiyo Dhambi ya kuua Albino mbona Kenya na Burundi ipo. Hicho kiburi na dharau ni hulka ya mtu ambayo dunia nzima wapo wenye tabia hizo. Usishindwe kufanikiwa ki Uchumi ukadharau mahali ulipo. Hata Kagame hawawekei watu wake pesa mfukoni,na ukishindwa kuishi Tanzania na watu wake basi hata kwa mungu utapaona pabaya
Tanzania ni nchi ninayoipenda, ujumbe wangu ni mpana zaidi kwani tulipaswa kuwa na maendeleo kuliko hali ilivyo sasa. Baadhi ya yale yanayotukwamisha ni tabia zetu wenyewe. Roho mbaya zetu wenyewe. Tabia za kusubiri fulani akwame ili mtu afurahiye. Tusijenge dhana potofu kwamba hapa ni mbinguni we have a lot of our own problems.
 
Nilibahatika kuwaona wakimbizi wa afrika ya kusini enzi zile za Mwalimu Nyerere wakiishi kwa amani hapa Dar. Kila Ijumaa walikuwa wana matamasha yao pale IFM, ninafahamu sana ukarimu wetu. Ninachokipinga ni ile dhana potofu wa kumshambulia Kagame kana kwamba sisi ni wasafi sana. Tanzania ya sasa licha ya kuwakarimu wageni, imejaa mambo mengi ya kishenzi tu, likiwemo suala la ukatili kwa walemavu wa ngozi.
Una hakika hayo mambo unayoita ni ya kishenzi hayakuwepo wakati wa Nyerere? Watu kama wewe ndio wale wakiona vijana wamevaa modo wanasema vijana wa siku hizi wamekuwa wahuni tofauti na wale wa enzi za mwalimu huku wakiwa hawatambui kwamba, hata wakati wa mwalimu modo zilikuwepo.

Kuhusu kagame ningependa kujua kama ni vibaya kumsema na kwanini asemwe yeye?
 
Tanzania ni nchi ninayoipenda, ujumbe wangu ni mpana zaidi kwani tulipaswa kuwa na maendeleo kuliko hali ilivyo sasa. Baadhi ya yale yanayotukwamisha ni tabia zetu wenyewe. Roho mbaya zetu wenyewe. Tabia za kusubiri fulani akwame ili mtu afurahiye. Tusijenge dhana potofu kwamba hapa ni mbinguni we have a lot of our own problems.
Tunapotofautina mimi na wewe, ni kitendo cha wewe kuona kama watanzania wote tuna shida katika hizo kasoro ambazo kwako wewe unaona ni kikwazo cha maendeleo. Pole,:Inawezekana ulikuwa muhanga wa jambo lillilopelekea wewe kukwama katika juhudi zako, hivyo ukalibeba kuwa ndiyo janga la kitaifa. Nimefanya kazi na watu wa mataifa mbalimbali, kama hujui binadamu wote tunafanana kwa tabia, chuki dharau, husda na hata wazungu wapo baadhi yao wasofurahia maendeleo ya mwenzake. Seuse sisi watanzania?
 
Tunapotofautina mimi na wewe, ni kitendo cha wewe kuona kama watanzania wote tuna shida katika hizo kasoro ambazo kwako wewe unaona ni kikwazo cha maendeleo. Pole,:Inawezekana ulikuwa muhanga wa jambo lillilopelekea wewe kukwama katika juhudi zako, hivyo ukalibeba kuwa ndiyo janga la kitaifa. Nimefanya kazi na watu wa mataifa mbalimbali, kama hujui binadamu wote tunafanana kwa tabia, chuki dharau, husda na hata wazungu wapo baadhi yao wasofurahia maendeleo ya mwenzake. Seuse sisi watanzania?
Kaka mimi sio mtoto mdogo ni mtu mzima, jaribu kuelewa concept ya mtu anapoandika kitu. Mimi ni mwenyeji wa mkoa ambao hao wakimbizi wanapotoka huko Rwanda na Burundi wanaufikia kwanza kabla hawajasafiri na kwenda katika mikoa ya mbali. I know what I'm talking about. Sijamaanisha kila mtanzania sio mtu mwema. Jaribu kuyasoma maandishi yangu halafu uyaelewe vizuri.
 
Una hakika hayo mambo unayoita ni ya kishenzi hayakuwepo wakati wa Nyerere? Watu kama wewe ndio wale wakiona vijana wamevaa modo wanasema vijana wa siku hizi wamekuwa wahuni tofauti na wale wa enzi za mwalimu huku wakiwa hawatambui kwamba, hata wakati wa mwalimu modo zilikuwepo.

Kuhusu kagame ningependa kujua kama ni vibaya kumsema na kwanini asemwe yeye?
Ndugu yangu mimi sina tabia ya kuyachukulia mambo generally, kabla sijatoa maoni ninaangalia pande zote mbili za jambo fulani. Kama modo zilikuwepo enzi za Nyerere halafu zikawa ni kielelezo kibaya mbele ya jamii hata leo hii zikivaliwa zitakuwa na impact ile ile ya zamani. Kagame anayo haki ya kusemwa akifanya mambo ya kishenzi, pia anayo haki ya kusemwa anapofanya mambo ambayo yanamjengea heshima nje na ndani ya Afrika.
 
Waungwana kaka yenu nakaribia kurudi nyumbani baada ya kuishi hapa DRC kwa Takriban miaka 2. Katika kipindi chote nilichokaa hapa nimejifunza mengi sana ila leo nitazungumzia kuhusu hawa jirani zetu Wanyarwanda.Maana nimekua nikipita hapa mara kwa mara. Kwa kifupi ondoeni dhana potofu kuhusu hawa jamaa maana mimi dhana hiyo tayari nimesha ifuta. Wengi wenu kama sio wote mnadhani kuwa wanyarwanda ni watu ''wasio poa'' au ni wenye majivuno labda wengine mnadhani eti hawatupendi Watanzania. Dhani hizi ni potofu kweli kweli, mwanzoni nikipita hapa sikua nikiongea kiswahili ili nisitambulike maana niliogopa kweli hawa jamaa. Baadae nikagundua dhana yangu sio sahihi kabisa na Mungu anisamehe. Hawa jamaa hawana shida kabisa na wageni hasa Watanzania. Nimekaa Hoteli mbali mbali hapa nikiwa transit kwenda DRC au kurudi Home Tanzania, na kote huko nimechukuliwa vizuri sana tu. Sio hotel tu , nimepanda boda boda, nimefika masokoni, msikitini , madukani kote huko hawa jamaa ni wakarimu sana na nimetendewa vizuri kwa kweli.

Wacha niweke mifano michache hapa mnielewe, nasisitiza michache mana nimengi nimeyaona positive.

1. Nikitoke DRC kurudi home ( niko njiani) tukiwa pale Kingarama Restaurant nikapata shida kidogo ya chenji ya Dollar kwa FRC ya Rwanda ili nipate Supu, wakati nikitaka kutoka nikatafute nje chenji mzee mmoja akasema kumwambia mhudumu mwache apate hiyo supu nitalipa mimi kama 'felistation' maana walitufunga kombe la CHAN huyu mzee alijua mimi ni Mkongo, nikala na wala hakukaa kuni bore kwa vile ameninunulia supu alitimua.... nikashangaa maana DRC husema hawa jamaa hawawapendi

2. Mh PK alitoa ma Bus kadhaa kuja pale Gisenyi kuchukua mashabiki wa DRC bure ili waje washangilie timu yao .... BUS zilijaa wakongo na walilindwa na wakarudi kwa amani.

3. Nilipofika Kigali na baada ya kuchukua Hotel, nikataka kwenda Masjid kusali , nikauliza Reception , kwa mshangao akadakia jamaa mmoja na kuniambia ''msikiti uko mbali ila subiri nitakupeleka maana naelekea njia hiyo hiyo huyu hakua musilam na hakua akinijua , ni tax man tu alie leta mteja pale. Njiani tulipiga soga sana.

4. Nikiwa hapa kwa siku ya pili na ticketi yangu ikiwa ya jioni nikaona ni negotiate nikae mpaka jioni kwa kulipa kidogo chumba maana check out ni saa tano asubuhi... Manager akasema ''kaa tu usilipe chochote , karibu tena wakati mwingine''.

5. Huko mitaani niliko kwenda kutembea jana usiku, nilikutana na ukarimu sana hasa unapouliza direction na mengine. hawa jamaa wana smile sana na sio ya smile ya kinafiki au ya kutegemea kitu

(a) Kitu nimegundua labda unaweza sema cha kushangaza au sio kizuri ni kwamba watu hapa hawaongelei siasa sana , ni aghalabu kukuta watu wakiongelea siasa hapa tofauti na home TZ kila mtu politician

(b) Printing media sio nyingi ila TV station wanazo nyingi tu

(c) Polisi ni vijana na hawacheki cheki wako serious kweli ila ukiuliza kitu wanakujibu vizuri tu

(e) Rushwa hapa sio sana labda niseme hakuna, polisi akikumata unaandikiwa charge hakuna zile za kuvutana nyuma ya gari na watu wanatii sheria kweli kweli

(f) Ule mfumo wa ukusanyaji kodi kila duka hapa, na kuna ka machine kama ka fingure print sijauliza ni ka nini ila ni ka mamlaka ya Kodi ya Rwanda. ( hapa nikakumbuka zile machine zetu sijui zilishia wapi maana zilileta sintofamu)

(g) Taxi zina Automatic Counter kama za Europe


NIMEONA MENGI WACHA NIACHIE HAPA NA WENGINE WACHANGIE MAANA NATUMAINI KUNA WENGI WAMEPITA HAPA PIA, WITO WANGU KAMA UNA JIRANI YAKO MNYARWANDA USIMTENDEE VIBAYA HAWA WATU WENGI WAO NI WAZURI SANA KWETU
Mkuu hongera kwa kutuhabarisha. Ukarimu huo kuupata Tanzania labda kwa wasukuma vijijini huko. Watanzania tumebakiwa na sifa ya Magufuri tu na kila Mtanzania kwa sasa kajivika uanaharakati yaani ni upuuzi mtupu. Vipi mkuu hujaopoa mtoto huko? Samahani lakini
 
Back
Top Bottom