engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Mwakilishi wa Matemwe, Abdi Mosi Kombo (CCM), amedai kuwa madawa ya kulevya yanaingizwa nchini na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao hufanikisha zoezi hilo kupitia Viwanja vya ndege na kupokewa na Polisi baada ya kupigiwa saluti.
Kabla ya kauli hiyo, Mwakilishi wa Mwajuni, Mbarouk Wadi Mussa (CCM) alisema, Hili suala naona hatujalifanyia kazi kikamilifu, kwa sababu wanaofanya biashara hiyo wapo na wanajulikana na wengine wamo humu humu wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Kwa kauli hizo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Othman Masoud Othman, aliwataka wajumbe hao kuthibitisha kauli zao kwa kuwa baadhi zinatoa shutuma nzito kwa Serikali na taasisi nyingine za kisheria, Hizi ni kauli nzito sana na zinatakiwa kuthibitishwa na mjumbe ... kauli hizi zinadhalilisha wawakilishi na baadhi ya taasisi kama Jeshi la Polisi na wananchi kwa kusikia watadhani kwamba kumbe dawa za kulevya zinaletwa na viongozi, alisema Othman.
Mwanasheria Mkuu alimtaka Kombo kuthibitisha madai yake au kuomba radhi, ambapo Mwakilishi huyo aliomba radhi na kusema ni makosa ya kibinadamu tu. Othman aliwakumbusha wajumbe kuheshimu kanuni zinazoendesha Baraza la Wawakilishi, ikiwamo kutoa kauli kwa kuthibitisha na si kwa dhana tu.
- HabariLeo
Kabla ya kauli hiyo, Mwakilishi wa Mwajuni, Mbarouk Wadi Mussa (CCM) alisema, Hili suala naona hatujalifanyia kazi kikamilifu, kwa sababu wanaofanya biashara hiyo wapo na wanajulikana na wengine wamo humu humu wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.
Kwa kauli hizo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Othman Masoud Othman, aliwataka wajumbe hao kuthibitisha kauli zao kwa kuwa baadhi zinatoa shutuma nzito kwa Serikali na taasisi nyingine za kisheria, Hizi ni kauli nzito sana na zinatakiwa kuthibitishwa na mjumbe ... kauli hizi zinadhalilisha wawakilishi na baadhi ya taasisi kama Jeshi la Polisi na wananchi kwa kusikia watadhani kwamba kumbe dawa za kulevya zinaletwa na viongozi, alisema Othman.
Mwanasheria Mkuu alimtaka Kombo kuthibitisha madai yake au kuomba radhi, ambapo Mwakilishi huyo aliomba radhi na kusema ni makosa ya kibinadamu tu. Othman aliwakumbusha wajumbe kuheshimu kanuni zinazoendesha Baraza la Wawakilishi, ikiwamo kutoa kauli kwa kuthibitisha na si kwa dhana tu.
- HabariLeo