Ona jeuri ya muwekezaji

......aisee.........attachment zako tunaziogopa........come clean first, please.......kwi kwi kwi kwi
 
Shy,
Mkuu hapa hakuna haja ya kuwalaumu Barricks isipokuwa ujinga wa mtu maskini... Kisheria hata nchi za juu ikiwa wanachama wa Union (workforce Bargaining Agent) inayowakilisha maslahi ya wafanyakazi ni chini ya asilimia 50 mkuu shirika linaweza kutokitambua chombo hicho kama ni sole representantive wa wafanyakazi..

Bila shaka mashirika mengi hutumia vitisho na mbwembwe kuhujumu Union kwa kupitisha maazimio mabaya ikiwa ni pamoja na kutowapandisha vyeo wananchama wa union hizi lakini kinachotakiwa ni wafanyakazi kuelewa kwamba wanapokuwa nje ya Union wanapoteza kinga za kibepari dhidi yao..Kuna faida ndogo sana za kebehi kuwa nje ya Union kuliko kuwa ndani ya Union ambayo ni shield yenu against exploitation...
Sasa ikiwa utakutana na Kabuntas na hasa maskini ambao future ya maisha yao inategemea kinachoingia mfukoni leo basi ni rahisi sana kughiribiwa na mashirika makubwa kama haya. hadi leo ni wachache sana wanaelewa umuhimu wa Union ktk sehemu ambazo zinaongozwa na mashirika makubwa ya kibepari kama Barricks...

Kwa hiyo lawama mkuu ni zetu wenyewe kwa umaskini wetu na pia kuwa na viongozi wa hizi Union ambao wanashindwa kuwafahamisha vizuri wafanyakazi kuhusiana na athari za Ubepari kwa sababu wao wenyewe hawajawahi ku experience tactics za makampuni makubwa... matokeo yake ndio hayo Union inakuwa na members chini ya asilimia 50..na hivyo kupoteza nguvu ya hoja zake kusimamia maslahi ya wafanyakazi wote.
 
Back
Top Bottom