CHIEF MVUNGI
Member
- Apr 6, 2012
- 99
- 14
eeeh Nape bado haamini tu kama polisi ndo wameua! kisha kwahili naye ajiulize kwann kila polisi wanapokuwepo watu ndo wanakufa?
Ili kutoa maoni kwa njia ya simu punde line itakapofunguliwa, zifuatazo ni namba za mawasiliano hayo:
+255 732 782788
+255 658 782788
hakika, kwani wakati mwangosi anauwawa, mwanza kulikuwa na mkutano wa hadhara ukiendeshwa na wenje. Walipeleka barua ya kutoa taarifa juu ya mkutano wao, walikataliwa na ocd nyamagana, walikaidi katazo hilo, wakafanya mkutano bila baraka za polisi, polisi iliamua kuwapotezea, mkutano ulimalizka salama, kila mtu alirudi nyumbani kwa furaha na amani.eeeh nape bado haamini tu kama polisi ndo wameua! Kisha kwahili naye ajiulize kwann kila polisi wanapokuwepo watu ndo wanakufa?
MLIWAHI KUWA NA NAMBA YA VODA, ILIENDA WAPI YAHAYA? 0754732732 au ya RFA?
Swali. Je Tanzania tunayoitaka ndio hii?
Hi, Mada nzuri Yahya, kwa kuwa hakuna kinachoweza kufanyika kama hakuna amani
Nadhani msingi mkuwa wa amani ni usawa na haki. Usawa katika ugawaji wa rasilimali, usawa katika demokrasia, usawa katika elimu na katika kila nyanja ya maisha na maendeleo.
Kunapokuwa na double standards amani haiwezi kuwepo, kunapokuwa na kuonewa amani ni ndoto. Kunapokuwa na wengine kuneemeka, wengine wakipunjwa amani mtaisikia kwa wenzenu.Wengine wanajichotea mapesa ya nchi na kuyaficha uswisi wengine hata mlo wa siku hakuna, amani haiwezi kuwepo. Wengine wanachukua ardhi ya nchi tena kwa kupora wengine, tusitegemee amani hapo.Chadema wananyimwa kufungua matawi, CCM wanazindua kampeni amani itapatikana wapi.Usawa na Haki ndio vitaleta amani.
Swali kwa Nape, anazungumziaje kutotii sheria kulikofanywa na CCM kule Bububu kwa kufanya mkutano licha ya katazo la Polisi? Na mbona hawakuchukuliwa hatua yoyote?
nape, kusema zanzibar sensa ilikamilika ni kutudanganya watanzania, lile katazo lilikuwa la nchi nzima, halikuhusu bara pekee, kwa nini usikubali kwamba mlivunja sheria? Na hizi ndio double-standards ninazozizungumzia.
Yahaya Hiyo Background ya studio dar badilisheni imekaa ki ccm zaidi.