On STAR TV: Ipi misingi ya Amani? Sehemu ya Pili

Je ni namna gani jeshi la polisi na lenyewe linatii sheria bila shurti katika kudumisha amani? Nani anatakiwa kulisimamia litii sheria?

sheria za nchi yetu ndizo mbovu siku zote. Ukisoma katiba sheria mama, haki ya mtu haiombi wala haitolewi na mtu bali na katiba yenyewe. Sheria iliyoanzisha vyama vya siasa, inatambua haki ya mtu si ya kuomba, ipo na haitolewi na mtu yeyote.

Lakini Penal code, Inakataza baadhi ya mambo yaliyotambuliwa kama haki ya watu mfano kukusanyika, inatmbua kama unlawful assembley, hii ndiyo inayotumiwa na POLICE wenye kuamini watafanikiwa kimadaraka kwa kuzifinya haki hizo kwa maslahi ya CCM.

Swali kwa Tundu, sheria hizi zimekaaje na ni nini mwafaka wake?
 
Habari za asubuhi,

Ndugu ni uwazi kabisa misingi ya Tanzania itakuwepo kama kuna haki, usawa, uwajibikaji kwa viongozi, uhuru wa kutii sheria ambazo siyo sheria kandamizi kwa public na kupunguza nguvu nyingi kwa jeshi la police ambazo hazina tija kwa vyama vingine vya siasa ambazo hizo nguvu wangezipeleka kwenye vibaka na majambazi tungelala hata kufunga milango nyumba zetu.
 
Swali kwa Nape:

Kama waziri mkuu ameweza kutoa amri kwamba ma- rc na ma- dc lazima wafanye kazi za CCM maeneo wanayoyaongoza. Je, ni sababu zipi zinakufanya utuaminishe kwamba hatoi maagizo ya polisi kuhujumu shughuli za vyama vya upinzani ikiwepo mikutano ya siasa?
 
Hatuwezi kupata haki kwa vile waziri mwenye zamana yakulinda watu hawezi hata kidogo ni kada mtiifu wa CCM.

Pia huwezi kugawa keki katika vipande vinne usijue sehemu yako nape anashidwa kusema kuwa wanabebwa mbona sektariti ya wakina Nape iliteuliwa saa kumi jioni alafu kesho mchana wakafanya mkutano je kibali walipata wapi
 
Ushauri wa bure kwa NApe, tendeni haki na muwe wakweli. Hakika mtawekwa huru. Kura za chuki ndo mnasubiri
 
Jeshi la polisi linaendeshwa na watawala kwani kuna wakati vijana wa CCM waliandamana bila kibali Arusha na hawakuzuiwa bali walilindwa kwanini iwe nongwa wengine hata wakifuata taratibu!?
 
Raia ama mwananchi yeyote katika nchi huru yenye kufuata utawala wa sheria anao wajibu wa kutimiza katika kulilinda na kuliendeleza Taifa hili.,haitoshi kwa mtu kunadi kuwa sikumuua kwa kuwa sikushika bunduki kumuua lakini ni lazima kupima na kufikiri zaidi juu ya kauli tunazotoa zinazopelekea watu wetu kufa.

Kimsingi ni kuwa Chadema wanatamani madaraka na wanatumia njia zozote wanazofikiria zitawawezesha kufika ikulu, hata ikiwa njia hizo ni za kuharibu na kutoa uhai wa watu wetu. Amani ya nchi hii ni kitu kikubwa kuliko U-CCM na U-CHADEMA
 
Nape anasemaje kuhusu kauli ya mnadhimu mkuu wa jeshi 2010 ndugu bilionea Shimbo? 2010 jimbo la Msalala mbunge Ezekiel Maige akishirikiana na polisi waliiba maboksi ya kura jimbo la Msalala huko Kahama, Nape anasemaje?
 
Amani ni muhimili mkuu katika maendeleo ya nchi yoyote ile.

Kwa Tanzania ili Amani ilete maana inayokusudiwa, si kuwaachia wana-Siasa ndo waitolee maamuzi kama vilanja wakuu, cha msingi ni kuvihusisha vyombo vingine kama vile Taasisi za Dini, Wanaharakati na Wanataaluma wa kada mbalimbali kufanya kazi sambamba na kwa ukaribu sana na Taasisi za Serikali huku Sera ya Uwazi na Ukweli ikipewa nafasi ya juu.

Kinyume na hapo Amani Tanzania tutabaki kuisoma kwenye vitabu na kuisikiliza kama historia tu.
 
Nape amefafanua sawa juu ya mgawanyo baina ya serikali na Chama, utendaji na mgawanyo wa majukumu, hakuna katika utaratibu ambao wengine wanaufikiria kuwepo kuwa unatoa fursa na upenyo kwa chama tawala kuwabana wapinzani kwa kutoa direct order kwa wakuu wa polisi, utaratibu huu unafuatwa...!
 
Moja kati ya vitu vilivyosababisha uvunjifu wa amani kule nyololo ni ufahamu wa sheria na taratibu zinazoendesha nchi yetu.

Nilisikiliza kwa makini sana mahojiano kati ya waandishi wa habari na maaskari (RPC KAMUHANDA na vijana wake) na tafsiri ya kikao cha ndani ikakosekana kabisa toka upande wa polisi.

Huko vyuoni wangechukua muda mwingi kusoma taratibu zaidi za kiutendaji zaidi ya kuchukua mazoezi mengi ya kutumia nguvu zaidi. Nadhani kila mmojawapo akijua wajibu wake ni nini katika kutekeleza wajibu wake kwa kufuata sheria na taratibu kila upande utaridhika na amani itakuwepo
 
Raia ama mwananchi yeyote katika nchi huru yenye kufuata utawala wa sheria anao wajibu wa kutimiza katika kulilinda na kuliendeleza Taifa hili.,haitoshi kwa mtu kunadi kuwa sikumuua kwa kuwa sikushika bunduki kumuua lakini ni lazima kupima na kufikiri zaidi juu ya kauli tunazotoa zinazopelekea watu wetu kufa.

Kimsingi ni kuwa Chadema wanatamani madaraka na wanatumia njia zozote wanazofikiria zitawawezesha kufika ikulu, hata ikiwa njia hizo ni za kuharibu na kutoa uhai wa watu wetu. Amani ya nchi hii ni kitu kikubwa kuliko U-CCM na U-CHADEMA
Kwani CHADEMA walitoa kauri gani iliyopelekea polisi kumuua kikatili Daud Mwangosi pale Nyororo?
 
Swali kwa Nape

Kwanini iwe dhambi kwa CDM Nyololo na iwe Haki kwa CCM BUBUBU?
 
Nape amefafanua sawa juu ya mgawanyo baina ya serikali na Chama, utendaji na mgawanyo wa majukumu, hakuna katika utaratibu ambao wengine wanaufikiria kuwepo kuwa unatoa fursa na upenyo kwa chama tawala kuwabana wapinzani kwa kutoa direct order kwa wakuu wa polisi, utaratibu huu unafuatwa...!
Huu ni utetezi dhaifu sana kutoka kwa mtu dhaifu, angalia influence ya viongozi wa CCM kwa jeshi la polisi.
 
Ukweli unabaki kuwa nape na ccm yake ndio wanahatarisha amani pale wanapokumbatia mafisadi,kupandikiza hila za udini na ukabila.wawape uhuru na wenzao wafanye mikutano maana hata hao pia wanaweza kuwa watawala hapo baadae
 
Conclusion: tufike mahali tuwe na mjadala wa kitaifa utakaotoa mwongozo namna ya kuenenda jeshi la polisi. Raia wajue haki zao na polisi wajue wajibu wao.
 
CHADEMA wanakosoa kiwango cha elimu cha askari na wanaponda uelewa wao juu ya sheria na mitazamo ya kiutawala,katika hili wanajijengea uadui katika kufanya hili na wajue kuwa hata wakiingia madarakani watalindwa na jeshi gani ikiwa wao hawana mnasaba mzuri na jeshi.
 
Back
Top Bottom