Omega Ngole,Never Say Never

Andrew Nyerere

JF-Expert Member
Nov 10, 2008
3,007
2,429
Inashangaza kuona kwamba Nd. Omega Ngolle anasema kwamba ofisi ya DPP haioni sababu ya kuwataja wahusika katika Kampuni ya Kagoda Agr. Ltd.
Hili ni jambo ambalo linawakatisha tamaa wananchi kwamba haki itatendeka. Bado wanachi wanaombwa kuwa na subira,ili majalada yatazamwe. Hayo majalada yanasomwa mpaka lini. Wananchi wameonyesha subira kubwa sana. Tokea Waziri Mkuu,Mizengo Kayanza Peter Pinda alipoanza kazi,aliwaambia wawe na subira. Mpaka leo unawaambia wawe na subira. Kwa kufanya hivi,wanataka watu wafikirie kwamba wamiliki wa Kampuni ya Kagoda ni wa maana sana kiasi kwamba hawawezi hata kutajwa. Kama amri imetoka kuwakamata hao watu,DPP lazima awakamate na kuwapeleka Mahakamaini ,aendelee kwa kasi kubwa kufanya kazi yake,mpaka hiyo amri itakapobadilishwa. Asitafakari amri. Kama amri haijabadilika,aendelee na utekelezaji.
 
Yangekuwa ni mafaili ya Viongozi wa wanafunzi wa vyuo vilivyogoma au kina Mkoba yangeshafika mara moja kwa DPP pia wangeshatajwa publicly siku nyingi sana!
 
jAMANI JAMANI HAO WAMILIKI SI WANAJULIKANA TU?RA NA LOWASA.......PIA CHANGANYIKENI EL NAE YUMO
 
Kweli madaraka mazuri..Omega Ngole alikuwa mpiganaji, mfuasi mwema na muadilifu wa Chachage na Shivji alipokuwa Ud hasa kunapotokea suala la haki. Leo amegeuka porojoziiiiiiiiiiiiii nyingi well well ushauri kwa Omega, tumia hekima kijana, umri na uwezo wako unakuruhusu ku influence hao wahusika wa Kagoda watajwe...wape haki yao Watanzania waliovuta subira bila kheri
 
Inashangaza kuona kwamba Nd. Omega Ngolle anasema kwamba ofisi ya DPP haioni sababu ya kuwataja wahusika katika Kampuni ya Kagoda Agr. Ltd.
Hili ni jambo ambalo linawakatisha tamaa wananchi kwamba haki itatendeka. Bado wanachi wanaombwa kuwa na subira,ili majalada yatazamwe. Hayo majalada yanasomwa mpaka lini. Wananchi wameonyesha subira kubwa sana. Tokea Waziri Mkuu,Mizengo Kayanza Peter Pinda alipoanza kazi,aliwaambia wawe na subira. Mpaka leo unawaambia wawe na subira. Kwa kufanya hivi,wanataka watu wafikirie kwamba wamiliki wa Kampuni ya Kagoda ni wa maana sana kiasi kwamba hawawezi hata kutajwa. Kama amri imetoka kuwakamata hao watu,DPP lazima awakamate na kuwapeleka Mahakamaini ,aendelee kwa kasi kubwa kufanya kazi yake,mpaka hiyo amri itakapobadilishwa. Asitafakari amri. Kama amri haijabadilika,aendelee na utekelezaji.
Mkuu Andrew, kumbe huyajui mamlaka ya DPP!, hafanyi kazi kwa shinikizo la yoyote, akisema fulani hana kesi, hana kesi na sio hana kosa!. Kagoda imekwapua bilioni 40 kwa ajili ya kugharimia uchaguzi wa Chama chako CCM!, DPP ameangalia watu wa kuwakamata angeanzia kwa aliyekuwepo, aliyepo, MOF, Director wa TISS na hao players wa RA, akaona sii busara kuwakamata, akaamua wasikamatwe na Kagoda haina kosa. Maamuzi ya DPP ni final na hayahojiwi na mamlaka yoyote!.

Kwa kukusaidia tuu, pia DPP anayo mamlaka yanaitwa Nolle ambayo ana uwezo wa kuingilia kesi yoyote ya jinai ikiwa katika hatua yoyote kabla ya hukumu na kuiondoa mahakamani pasi kutoa sababu wala kuhojiwa na yoyote!.

Kwa maoni yangu, uamuzi wa DPP kutoishitaki Kagoda, ni uamuzi wa busara sana unaozingatia maslahi ya taifa kama alivyofanya kwa kutoichunguza Meremeta na Deep Green etc, kwa maslahi ya Taifa!.

Wewe hili ulilijua?. Na baada ya kukutajia wahusika wakuu wa Kagoda, bado ungependwa wachunguzwe?.

Pasco.
 
Mkuu Andrew, kumbe huyajui mamlaka ya DPP!, hafanyi kazi kwa shinikizo la yoyote, akisema fulani hana kesi, hana kesi na sio hana kosa!. Kagoda imekwapua bilioni 40 kwa ajili ya kugharimia uchaguzi wa Chama chako CCM!, DPP ameangalia watu wa kuwakamata angeanzia kwa aliyekuwepo, aliyepo, MOF, Director wa TISS na hao players wa RA, akaona sii busara kuwakamata, akaamua wasikamatwe na Kagoda haina kosa. Maamuzi ya DPP ni final na hayahojiwi na mamlaka yoyote!.

Kwa kukusaidia tuu, pia DPP anayo mamlaka yanaitwa Nolle ambayo ana uwezo wa kuingilia kesi yoyote ya jinai ikiwa katika hatua yoyote kabla ya hukumu na kuiondoa mahakamani pasi kutoa sababu wala kuhojiwa na yoyote!.

Kwa maoni yangu, uamuzi wa DPP kutoishitaki Kagoda, ni uamuzi wa busara sana unaozingatia maslahi ya taifa kama alivyofanya kwa kutoichunguza Meremeta na Deep Green etc, kwa maslahi ya Taifa!.

Wewe hili ulilijua?. Na baada ya kukutajia wahusika wakuu wa Kagoda, bado ungependwa wachunguzwe?.

Pasco.
Wanabodi, hoja hii ya Andrew Nyerere kuhoji mamlaka ya DPP, iliibuliwa mwaka 2008, na haya yalikuwa majibu yangu mwaka huo, juzi DPP ameyatumia mamlaka haya kuiondoa kesi ya Rwakatare, nimesoma mahali humu jf kuwa wanasheria wa Chadema wanafungua kesi mahakama kuu kuhoji mamlaka hii ya DPP, kwa maoni yangu, this is wastage of time!, kwa vile mamlaka hayo, yako kikatiba, the right forum ni au kufungua kesi ya kikatiba, mahakama kuu itamke mamlaka hayo ni kinyume cha katiba kwa sababu yanakinzana na kifungu fulani cha katiba, hivyo kuiamuru serikali kupeleka bungeni marekebisho ya katiba, au kushinikiza katiba mpya kuyapunguza mamlaka hayo ya DPP.
 
Back
Top Bottom