Gembe
JF-Expert Member
- Sep 25, 2007
- 2,483
- 159
lidaiwa wanafunzi hao walibeba mabango yaliyokuwa na ujumbe mbalimbali ambao ulikuwa umejielekeza kuleta hasira na kujenga chuki kwa watu wengine.
Baadhi ya ujumbe uliokuwemo katika mabango hayo ni, "Nyerere angefufuka leo angelia machozi ya damu", "Kweli Kikwete umesahahu umaskini wa Watanzania wako", "Hivi Pinda wewe ni mtoto wa mkulima", "Wazazi wetu tuoneeni huruma tunateseka jamani" na "Vyuo vya uma vimeuzwa kwa matajiri".
Mheshimiwa Rais ,
Naomba nikupe pole na jinsi khali ya uchumi inavyoendelea hapa nchini,Naona jitihada zako mpya za kuweza kufufua uchumi wa nchi hii zikianza kwa nguvu mpya na kasi mpya tena.Mikutano yako na viongozi wa BOT,Wizara ya Fedha itasaidia sana japo kuwapa watanzania maisha bora waliyoyasubiri toka 2005.
Mhe. Rais,
Najua tumekuwa tukikushauri kwa muda mrefu sana kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu na tumekusaidia sana katika kuongoza nchini yetu ya Tanzania,tumeweza kuvumbua uozo wa ACTL,Ufisadi katika sehemu mbali mbali,tumekusaidia mambo magumu ambayo kwa khali ya kibinadamu na kirafiki haikuwa rais kufanyika(rejea kashfa ya RDC).
Mhe Rais najua kuna mambo mengine tumekukera sana kwa kuwa haukutaka tuyazungumze hapa .Yawezekana ulifikia hatua ya kuchukia wachangiaji hapa kama alivyofanya mwandishi aliyemmjibu Mzee Mwanakijiji katika akala ya ndege inayopaa ya mwaka 2007.Rais wetu mpendwa tulifanya hivyo ajili ya maslahi ya nchi yetu na kama kuna sehemu tulikosea tunaomba utusamehe
Mhe Rais,Leo nina ombi moja tu naombakwako,Ombi lililo maalum.Naomba uagize Jeshi la Polisi liwaachie hawa vijana wawili,Rais wa DARUSO Mhe. MAchibya na steven Owawa ambaye ni katibu wa TGNP,inawezekana wana kosa ila hawana Hatia,Nakuomba sana utoe maelekezo sasa.Nimesoma habari ya kukamtwa kwao kwa masikitiko makubwa sana sababu hii inajenga picha kwamba watanzania walio wadogo hawawezi kuzungumza lile wanaloliamini ni sahihi.
Mhe Rais,
umekekuwa ukizungumzia demokrasia kwa muda mrefu sasa,Tena inayotoa uhuru kwa watu kuchagu aviongozi waaadilifu .Hawa vijana ni waadilifu sababu wanatetea jamii nzima ya wanafunzi wa vyuo vikuu.
Mhe Mwenyekiti wangu,
Nakuomba sana huku nikikusihi sana uwaachie sababu hawa vijana wanapigania yale yaliyo kweli kwa sasa na wanafanya hivyo kwa ajili ya watanzania masikini(walio wengi).ambao wanategemea msaada wa serikali yao katika maendeleo.
Kwa wanafunzi wa vyuo,Naomba muwe watulivu wakati serikali ikiangalia njia ya kuweza kutatua jambo hili,na nina uhakika Mhe. Rais ataingilia kati jambo hili kwa kuwa linagusa maisha ya watanzania walio wengi.
Mhe. Naomba unisaide japoo hili tu.
Mungu akubariki sana na wasaidie Vijana hawa