Elections 2010 Ombi kwa professors na wasomi wa Tanzania

Wasomi hawaihitaji kujiunga na chama na siasa kwani itikadi za kisomi ni kuwa unasimamia principles za fairness and truth. Kujiunga na chama fulani cha siasa ni kuhama kutoka kuwa msomi na kuwa mwanasiasa. Kuna msemo mmoja maarufu unasema " A Politician is a failed academician" . Hivyo sidhani Tanzania inahitaji wasomi kujiunga na chama fulani cha siasa bali ni suala la Watanzania kujitoa katika limbi la ujinga na kuelewa nini kinaendelea. Kwani tukiwa na taifa lenye kujua nini kinaendelea nadhani changes will come otherwise hata wasomi wote wakijiunga na chadema hakuna changes zozote zitatokea Tanzania. Kumbuka wanaopiga kura tanzania si wasomi pekee bali watanzania wenye kujua na wasiojua kusoma.

Si kweli. Wasomi wenye mapenzi ya kweli ya nchi yao na wenye upeo wanatakiwa kuingia katika siasa ili kuweza kuleta mabadiliko ya kweli. Katika nchi zetu maskini siasa ni kila kitu na hivyo kuacha nchi iendeshwe kishikajishikaji ni uhaini. Kama Mwalimu alivyosema ili tuendelee twahitaji, watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Kwa bahati mbaya Tanzania haina siasa safi na kibaya zaidi uongozi bora. Hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ule tunahitaji kuwa na wasomi wazalendo na sio wale wanaokwenda kuganga njaa au kulamba nyayo za watawala-uchwara ili kuweza kuipatia nchi yetu siasa safi na uongozi unaostahili. Nimesoma na baadhi ya wale ambao sasa ni mawaziri katika serikali ya CCM, mtu unajiuliza hivi kweli huyu kwa uelewa na upeo wake mdogo pamoja na kukosa kwake uzalendo ilikuwaje akawa waziri? Hao watu wameingia katika uongozi kutafuta mali na kuifuja nchi yetu kushinda ambavyo hata wakoloni.

Rai yangu ni kuwa Tanzania inahitaji uongozi mzuri na sera nzuri kutoka kwa viongozi wasomi wenye nia njema nayo hali kadhalika ni lazima viongozi hao wawe tayari kujisadikisha kwa manufaa ya watu wao.
 
Si kweli. Wasomi wenye mapenzi ya kweli ya nchi yao na wenye upeo wanatakiwa kuingia katika siasa ili kuweza kuleta mabadiliko ya kweli. Katika nchi zetu maskini siasa ni kila kitu na hivyo kuacha nchi iendeshwe kishikajishikaji ni uhaini. Kama Mwalimu alivyosema ili tuendelee twahitaji, watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Kwa bahati mbaya Tanzania haina siasa safi na kibaya zaidi uongozi bora. Hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ule tunahitaji kuwa na wasomi wazalendo na sio wale wanaokwenda kuganga njaa au kulamba nyayo za watawala-uchwara ili kuweza kuipatia nchi yetu siasa safi na uongozi unaostahili. Nimesoma na baadhi ya wale ambao sasa ni mawaziri katika serikali ya CCM, mtu unajiuliza hivi kweli huyu kwa uelewa na upeo wake mdogo pamoja na kukosa kwake uzalendo ilikuwaje akawa waziri? Hao watu wameingia katika uongozi kutafuta mali na kuifuja nchi yetu kushinda ambavyo hata wakoloni.

Rai yangu ni kuwa Tanzania inahitaji uongozi mzuri na sera nzuri kutoka kwa viongozi wasomi wenye nia njema nayo hali kadhalika ni lazima viongozi hao wawe tayari kujisadikisha kwa manufaa ya watu wao.

Kaka sijui dada ndio maana nasema kuwa "A politician is a failed academician" (which by the way sio msemo wangu tu nimeupata kwa Albert Einstein. kwasababu kwanza kaa ukijua uzalendo unakuja katika kusimamia haki pili ni kwamba uzalendo unakuja kwa kutenda kwa uadilifu pasina kuangalia mtu dini yake, itikadi wala umri. Sasa wasomi wetu walioingia katika siasa kama hana ufisadi wa mali ana ufisadi wa kikabila au dini matokeo yake yanakuwa kizunguzungu kitupu. La msingi wasomi wawe ni chachu na mwamko wa mabadiliko na sio kuzungumza vizuri na kutengeneza CV nzuri ambazo hazisaidii jamii.
 
Silas karibu Nzega 2015 kama uko tayari kushindana na mimi!na mimi natangazA nia ya kugombea ubunge nzega 2015! Kwa miradi ya maendeleo niliyokusudia, kwa uwezo wangu wa kufuatilia utekelezaji wa sera za chama changu sidhani kama utafua dafu labda utafute jimbo lingine legelege! Nzega itakuwa ngumu sana kwako ndg yangu!

Nakushauri u-track my record ili ujue Kigwangala ni mtu wa aina gani ndipo uanze mkakati wako usije ukapoteza muda wako bure tu!

Hamisi!!!!!!! kumbe ni wewe uliyeukwaa ubunge huko nzega, hongera sana, mi nakuaminia, ninavyokujua wewe ni mpiganaji, Kapambane na akina Zitto, ZAO la KG SEC au siyo.Kila la kheri.
 
Hata mimi huyo Jasson Rweikiza hapo Bukoba vijijini ajiandae kwa kimbunga hapo 2015 kwani nafahamu naye ni kama Karamagi; hatafanya lolote la maendeleo kwa wana Bukoba vijijini.
 
Anyisile iyo signature yako naomba umalizie SHAKE WELL B4 USE imetuliaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Silas karibu Nzega 2015 kama uko tayari kushindana na mimi!na mimi natangazA nia ya kugombea ubunge nzega 2015! Kwa miradi ya maendeleo niliyokusudia, kwa uwezo wangu wa kufuatilia utekelezaji wa sera za chama changu sidhani kama utafua dafu labda utafute jimbo lingine legelege! Nzega itakuwa ngumu sana kwako ndg yangu!

Nakushauri u-track my record ili ujue Kigwangala ni mtu wa aina gani ndipo uanze mkakati wako usije ukapoteza muda wako bure tu!

Kigwangala;

Kwanza naomba nikupe pongezi za dhati kwa kuchaguliwa kuwa mwakilishi wa wananchi na kuwatumikia. Kwa kuwa wewe ni kijana msomi bila ya shaka hutatuangusha kama baadhi walivyofanya na kufanya vijana au wasomi waonekana hawana uzalendo na nchi.

Baada ya hapo nina machache naomba utupatie ufafanuzi.

1. Je ni kweli unafanya kazi WAMA kama moja wa wasaidizi wa Mama Salma Kikwete?
2. Je ni kweli kuteuliwa kwako kugombea kulikuwa na influence na shinikizo la uswahiba wako na familia ya JK?
3. Je, Hussein Bashe ambaye ndiye aliyeshinda kura za maoni, alifanyiwa mizengwe ya wazi na kuondolewa ili wewe upite?

Tafadhali maswali haya usiyajibu kisiasa, tupatie facts tu.
 
"Kitu kikubwa ambacho wanaweza kusaidia kwa mtazamo wangu ni kuzungumzia mapungufu ya katiba tunayo tumia kwa sasa na kuunga mkono
watu wote wanaopigania usawa katika medani za siasa. Naamini wanaweza kuanzisha motion ya mabadiliko ya katiba kwa manufaa ya taifa na siyo chama fulani, kwani TZ ni yetu wote. Kama inakufever sasa hivi ujue kuna wanaoumia na ipo siku itakugeuka kama sio wewe basi kizazi chako."
Mbona wewe umetumia jukwaa la CCM kufikia lengolako lakuwa fisadi? Acha porojo na kutuongopea.
 
"Kitu kikubwa ambacho wanaweza kusaidia kwa mtazamo wangu ni kuzungumzia mapungufu ya katiba tunayo tumia kwa sasa na kuunga mkono
watu wote wanaopigania usawa katika medani za siasa. Naamini wanaweza kuanzisha motion ya mabadiliko ya katiba kwa manufaa ya taifa na siyo chama fulani, kwani TZ ni yetu wote. Kama inakufever sasa hivi ujue kuna wanaoumia na ipo siku itakugeuka kama sio wewe basi kizazi chako."
Mbona wewe umetumia jukwaa la CCM kufikia lengo lako la kuwa fisadi? Acha porojo na kutuongopea.
 
Kigwangala;

Kwanza naomba nikupe pongezi za dhati kwa kuchaguliwa kuwa mwakilishi wa wananchi na kuwatumikia. Kwa kuwa wewe ni kijana msomi bila ya shaka hutatuangusha kama baadhi walivyofanya na kufanya vijana au wasomi waonekana hawana uzalendo na nchi.

Baada ya hapo nina machache naomba utupatie ufafanuzi.

1. Je ni kweli unafanya kazi WAMA kama moja wa wasaidizi wa Mama Salma Kikwete?
2. Je ni kweli kuteuliwa kwako kugombea kulikuwa na influence na shinikizo la uswahiba wako na familia ya JK?
3. Je, Hussein Bashe ambaye ndiye aliyeshinda kura za maoni, alifanyiwa mizengwe ya wazi na kuondolewa ili wewe upite?

Tafadhali maswali haya usiyajibu kisiasa, tupatie facts tu.

Ahsante Superman kwa kutaka kuujua ukweli, nao ni huu hapa sasa:

1. Mimi Dr. Hamisi A. Kigwangalla, sijawahi kufanya kazi WAMA kama mmoja wa wasaidizi au wafanyakazi waajiriwa wa Taasisi ya WAMA. Katika maisha yangu kama Consultant nimewahi kufanya three contracts na taasisi hiyo, lkn mama Salma Kikwete sikuwa na mahusiano yoyote yale ya kikazi na Mama Kikwete na wala sikuwahi kuripoti kwake wala kuonana naye hata siku moja! Mimi nilipewa kazi na wataalamu wa taasisi hiyo na ndo niliokuwa nikiwasiliana nao siku zote!

2. Mimi sina uswahiba wowote ule na familia ya JK japokuwa ingekuwa hivyo ningefurahi sana! Chama kama chama wanazo sababu kwa nini waliniteua, sizijui na mimi si msemaji mkuu wa CCM, ila mi naona niliteuliwa kwa sababu nina sifa za kutosha kuwa Mbunge na nawashukuru wanaNzega kwa kunichagua kuwawakilisha!

3. Bila shaka kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo ya kisiasa utakuwa unazifahamu sababu za kwanini Hussein Bashe hakuteuliwa, na kwa nini Selelii pia hakuteuliwa, maana walizitaja viongozi wa kitaifa wa CCM! Mimi sina capacity ya kuzisema. Japokuwa mimi kuteuliwa si jambo la ajabu na wala mimi si wa kwanza, angeweza kuteuliwa hata mtu aliyeshika nafasi ya 9 kwenye kura za maoni! Huu ni utaratibu wa kawaida tu ndani ya chama chetu!
 
Silas karibu Nzega 2015 kama uko tayari kushindana na mimi!na mimi natangazA nia ya kugombea ubunge nzega 2015! Kwa miradi ya maendeleo niliyokusudia, kwa uwezo wangu wa kufuatilia utekelezaji wa sera za chama changu sidhani kama utafua dafu labda utafute jimbo lingine legelege! Nzega itakuwa ngumu sana kwako ndg yangu!

Nakushauri u-track my record ili ujue Kigwangala ni mtu wa aina gani ndipo uanze mkakati wako usije ukapoteza muda wako bure tu!
Kwa sasa unasema haya kwa furaha lakini kauli hii itakuwa ngumu sana kuitamka itakapofika 2015. Najua kupitia chama ulichotumia kuingia bungeni hautaweza kubadili kitu chochote Nzega kwani utaishia kutumikia mafisadi tu. Kama utaweza kuibadili Nzega basi mimi sitakuwa na haja ya kuja kugombea huko maana ninachotaka ni mabadiliko ya kweli bila kujali nani kayaleta. Kaza buti uhakikishe unatimiza azima yako vinginevyo usije ukanilaumu maana hutaweza kushindana na mimi.
Bahati nzuri kabisa nakujua A-Z na mapungufu yako ndiyo mtaji aliotumia hata Bashe kukutepetesha. Nahisi 2015 ushindani utakuwa kati yangu na Bashe lakini siyo wewe labda ubadilike na kurudisha imani kwa wananchi wa Nzega. Nakuombea tu ujitahidi ili ulete maendeleo kwani ndiyo ninayoyataka mimi.
 
Kwa sasa unasema haya kwa furaha lakini kauli hii itakuwa ngumu sana kuitamka itakapofika 2015. Najua kupitia chama ulichotumia kuingia bungeni hautaweza kubadili kitu chochote Nzega kwani utaishia kutumikia mafisadi tu. Kama utaweza kuibadili Nzega basi mimi sitakuwa na haja ya kuja kugombea huko maana ninachotaka ni mabadiliko ya kweli bila kujali nani kayaleta. Kaza buti uhakikishe unatimiza azima yako vinginevyo usije ukanilaumu maana hutaweza kushindana na mimi.
Bahati nzuri kabisa nakujua A-Z na mapungufu yako ndiyo mtaji aliotumia hata Bashe kukutepetesha. Nahisi 2015 ushindani utakuwa kati yangu na Bashe lakini siyo wewe labda ubadilike na kurudisha imani kwa wananchi wa Nzega. Nakuombea tu ujitahidi ili ulete maendeleo kwani ndiyo ninayoyataka mimi.

@kaka Silas, niambie mimi nina mapungufu gani aliyoyatumia Bashe kunishinda? Ili nijirekebishe!
 
JAMANI kama nimefanya dhambi mnisamehe ila mimi ni mwalimu wa ziada ktk shule flani, nimeamua kuwafundisha wanafunzi wangu siasa halisi na jinsi ya kuchagua kiongozi kwa maslahi yao na baada ya somo kueleweka kuanzia form 1-6 nimeamua sasa kuondoka na kurudi kwene field yangu, naamini kua nimebadilisha vichwa zaidi ya 590 na kwamba nimewasihi nao wapeleke ujumbe kwa wengine na through clubs zao wawe wanazungumzia mambo ya siasa!! Tunawapa ukweli kwa ajili ya future yao!!!!
 
Mbona JF imekuwa kama kijiwe cha CCM na CHADEMA, kama vile Yanga na Simba! SIONI fikra katika mada hii hata kidogo. Sidhani hoja ni CCM au Chadema kuwa madarakani! Great thinkers hawana haja ya kuwa wanazi wa chama bali wanapaswa wasimamie yale yenye kuleta tija kwa taifa. Kama CCM watajirekibisha na kuleta maendeleo yale tunatoyatamani kwa taifa, kwa nini wasiendelee. Hatuhitaji mabadiliko kwa ajili tu ya mabadiliko.

Suala la kuwataka wahadhiri kujiunga na siasa sio la msingi. Tumewaona wale waliokwenda huko na kilichotokea! Kapuya, Jumanne, nk hawajaonyesha jinsi gani utaala wao unavyoweza kubadili au kusisimua maendeleo.

Nimependa jinsi huyu Mbunge mteule wa Nzega alivyojibu kwa unyenyekevu hoja ya Superman! Huku ni kupevuka.

Mimi ni non-aligned na chama chochote cha siasa! Naangalia maendeleo, na kwa wakati huu nilisapoti sana CHADEMA maaana walikuwa na agenda nzito za maendeleo na mwelekeo wa dhati kabisa wa kuyasimamia hayo waliyoyaasisi. Lakini kama Chadema ya 2015 itakuwa tofauti basi nitawatafuta hao watakaochukua nafasi yao, siwezi kuwa mnazi wa Chama!
 
Back
Top Bottom