Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Ninaomba kuwasilisha ombi langu kwa Mzee Mwanakijiji na wengine wenye uwezo kama wake wa kujenga hoja ili wasaidie kutengeneza vipeperushi vitakavyosambazwa nchi nzima hasa maeneo ya vijijini ili viweze kutoa elimu ya urai.
Ningependekeza weledi hawa waandike na kujenga hoja kuelimisha yafuatayo:
Hii ni nchi yetu na tunatakiwa sote tupambane na wote wanaotaka tuendelee kuwa gizani kwa propaganda zisizo na mashiko kama ambazo zinatumiwa sasa na chama twawala.
Naomba kuwasilisha
Ningependekeza weledi hawa waandike na kujenga hoja kuelimisha yafuatayo:
- Dhana kuwa vyama vya upinzani vitaleta vita vikichaguliwa kushika dola
- Umuhimu wa kuwa na katiba mpya - Wengi wa wanavijiji hawajui na hawaoanishi umasikini uliopo na mfumo mbovu wa kiutawala unaosababishwa na katiba ya enzi za ukoloni na vita baridi
- Umuhimu wa watawala wa mikoa na wilaya kuchaguliwa na wananchi ili kuongeza uwajibikaji
- Dhana kuwa huduma za elimu na afya haiwezekani kutolewa bure
Hii ni nchi yetu na tunatakiwa sote tupambane na wote wanaotaka tuendelee kuwa gizani kwa propaganda zisizo na mashiko kama ambazo zinatumiwa sasa na chama twawala.
Naomba kuwasilisha