Henge
JF-Expert Member
- May 14, 2009
- 6,933
- 1,510
nafikiri alikuwa na nia kuwa malipo wanayopata wabunge yabakie kama mshahara na si vinginevyo
achana na huyu anayesubiri mwongozo wa spaka aliyewekwa na mafisadi!
nafikiri alikuwa na nia kuwa malipo wanayopata wabunge yabakie kama mshahara na si vinginevyo
Naomba msiwe distracted na watu. Msimamo upo wazi kabisa. Hakuna posho za vikao (sio tu nyongeza bali mfumo mzima wa posho za vikao twataka ukome. Watu wameamua kutwist nilichosema bungeni jana. Narudia, lazima tupinge posho hizi. Kwa nini wabunge walipwe kwa kukaa kitako? Huyu anayesema mie mnafiki yeye aseme anaunga mkono posho za kukaa au la. Wapiganaji msiwe distracted.
Naomba msiwe distracted na watu. Msimamo upo wazi kabisa. Hakuna posho za vikao (sio tu nyongeza bali mfumo mzima wa posho za vikao twataka ukome. Watu wameamua kutwist nilichosema bungeni jana. Narudia, lazima tupinge posho hizi. Kwa nini wabunge walipwe kwa kukaa kitako? Huyu anayesema mie mnafiki yeye aseme anaunga mkono posho za kukaa au la. Wapiganaji msiwe distracted.
Mama Padri ni nani mkuu?cjakuelewa!!!!!kwa mbali kama vile humpendi Zitto!!!hii nchi bwana afadhali nisingezaliwa,maana ni vituko tupu!!!!!!sasa nikueleje mama Padri!!msaada pls!
kinyesi.Jana nimeisikitikia sana nchi yangu Tanzania, na haswa kwa kuwa na kizazi cha viongozi vijana ambao nilikuwa naona kama wangeliweza kuja kulisaidia hili taifa hapo siku zijazo , lakini nimegundua kuwa kumbe ni wanafiki. Naomba kurudia ni wanafiki.
Hawa ni kijana Zitto Kabwe ambaye kwa kweli ananiheshimu na mimi namheshimu sana kutokana na hoja zake pamoja na kuwa tuko itikadi mbili tofauti.
Jana tukiwa kwenye kikao cha kamati ya wabunge wote kwa ajili ya kupewa briefing na wenzetu walioko serikalini kama ulivyoutamaduni wetu kabla ya kikao cha bunge kuanza ,mjadala mkubwa sana ulikuwa kwenye suala la posho za wabunge.
Zitto , ni mtu ambaye alijipambanua kuwa yeye anapinga ongezeko la posho hizo kwa nguvu zote , baadhi yetu tulimwamini pamoja na ukweli kuwa wengine hatuwezi kusema kutokana na sababu mbalimbali ila leo kaonyesha unafiki wake mbele yetu na hata wabunge wa chama chake walimpinga waziwazi bila hata kujali kuwa ni kiongozi wao na alikuwa ndiye mkuu wa kambi ya Upinzani kwani Mbowe hakuwepo.
Naomba ninukuu kauli yake na kama anamheshimu Mungu na kumwogopa atakubaliana nami na kuwaomba radhi watanzania , alisema Kimsingi mimi sipingi suala la kuwaongezea wabunge Maslahi yao hata kama nyongeza hiyo ikikubaliwa kufikia kiasi cha shilingi milioni 12 kwa mwezi, ila ninachopinga ni nyongeza hiyo kuitwa posho .
Hayo ndio maneno ya kiongozi huyu na alipomaliza kusema akabanwa na wabunge wengine ambao walimtaka awaombe radhi kwa kuwadhalilisha mbele ya umma , kumbe anakubaliana na kuongezwa kwa masilahi ya wabunge , kibaya zaidi alipobanwa akaomba radhi kwa kusema Kama kuna mtu ambaye nimemkwaza kwa maneno yangu juu ya suala hili basi ninaomba aniwie radhi sana
Kauli hii ikanifanya nimuone Zitto kuwa mnafiki kwani alipaswa kusimamia maneno yake na huo ndio uongozi , kuanzia leo nitaanza kumtazama kwa macho mawilimawili.
Kilichoniudhi ni hii tabia ya undumilakuwili, yaani akiwa kwa wananchi anapinga kuongezwa kwa masilahi ya wabunge na yeye anasema kuwa hilo sio sawa kwani maisha yamepanda pia kwa wananchi na watumishi wengine , sasa kusema kuwa hapingi nyongeza ila anapinga jina la hiyo nyongeza ni jambo la ajabu kabisa, kwani inaonyesha hana Principal ya msingi anayoisimamia.
Kwa kifupi na kwa kuwa leo nimeandika kwa mara ya kwanza naomba kuishia hapo, Ahsanteni sana.
wewee ni mbunge? huoni kama hata wewe una jukumu la kupinga kwa nafasi yako kwani zitto alizaliwa kukuonesha kila mwelekeo na kama uligundua hoja ya zitto awali ilikuwa sahihi mbona hukutoka hadharani kumuunga ili asikate tamaaa weka pia sababu kwa nini huwezi wewe kupinga hadharani? lakini pia kumbuka zitto si msaafu wa vijana nchi hii wala siye QURAN AU BIBLIA kuna vijana wengi bado tunawangazia macho
Huyu mbunge feki hata sijui wajimbo gani, wewe unategemea zitto atetee nchi na wewe umshangilie tu pembeni hv wewe ni wale wakupewa nini?
Zitto ni mnafiki hakuna anachotetea , ila anatafuta hoja za kuugilibu umma wa watanzania ,huku akiwa kwenye vikao ni unafiki mtupu anaendekeza , nimeamua kuweka wazi hapa na kama anabisha aeleze kwenye press yake anayotegemea kuifanya leo nini alisema kwenye kikao.
Huyo aliyeleta huu upuuzi ni kibaraka wa mafisadi.Tuko na CDM hata mfanye nini.Kumbuka Zitto anaongea kwa niaba ya wanachama wote.Tafuteni uongo mwingine wa kufitinisha CDM na wananchi
mkuu ata kama unamahaba na cdm kiasi icho uko umeenda mbali sana..yani kila kauli ya Zitto ndio msimamo wa wanachama wote??sikuwai kutambua ili.