Ole Sendeka aongezewa mashitaka
Monday, 20 April 2009 16:49
Na Glory Mhiliwa, Arusha
KESI inayomkabili Mbunge wa Simanjiro (CCM), Bw. Christopher Ole Sendeka ambaye anashitakiwa kwa kumpiga Mwenyekiti wa vijana wa CCM Mkoa wa Arusha, Bw. James Milya imeendelea kunguruma jana Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ambapo mwendesha mashtaka wa Serikali ameongeza mashitaka ya kutishia kwa bastola.
Akisoma mashitaka hayo, Mwendesha Mashtaka, Bw. Agustine Komba aliiambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Bw. James Karayemaha kuwa yameongezwa mashitaka mengine ambayo awali hayakuwepo.
Alidai kuwa Ole Sendeka anatuhumiwa Januari 9 mwaka huu wilayani Monduli katika semina ya wazee wa kimasai ambayo iliandaliwa na Mbunge wa Mbulu, Bw. Edward Lowassa alimtishia kwa bastola na kumdhuru mwili Bw. Milya.
Hata hivyo Mwendesha mashtaka huyo aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza kesi hiyo ambayo imeshatajwa kwa mara mbili baada ya upelelezi kukamilika.
"Mheshimiwa hakimu naomba tarehe kwa ajili ya kuanza kusikilizwa na kutolewa ushahidi ambapo upande wa upelelezi umeshakamilika. Tutaleta mashahidi 13, bastola iliyotumiwa na mshitakiwa kutishia, fomu namba tatu aliyotibiwa nayo mlalamikaji," alisema Mwendesha Mashtaka.
Aliwataja mashahidi watakaotoa ushahidi kuanzia Mei 27 kuwa ni askari polisi wawili ambamo pia atakuwepo Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bw Vicent Kone ambapo siku ya tukio alikuwepo kwenye semina hiyo.
Hakimu Karayemaha aliahirisha kesi hiyo mpaka Mei 27 ambapo itaanza kusikilizwa.
Akizungumza nje ya mahakama hiyo. Mbunge huyo aliwashukuru wananchi wa jimbo lake waliojitokeza kwa wingi kwa ajili ya kujua hatma ya kesi yake ambapo aliwataka kuendelea na kazi za ujenzi wa Taifa kwa vile sheria itachukua mkondo wake.
"Nawashukuru sana naona ni vyema wakulima muendelee na kilimo na wafugaji muendelee na ufugaji. Msihangaike kuja mahakamani tuache sheria ichukue mkondo wake," alisema Sendeka.
Powered by Business Times Limited
Monday, 20 April 2009 16:49
Na Glory Mhiliwa, Arusha
KESI inayomkabili Mbunge wa Simanjiro (CCM), Bw. Christopher Ole Sendeka ambaye anashitakiwa kwa kumpiga Mwenyekiti wa vijana wa CCM Mkoa wa Arusha, Bw. James Milya imeendelea kunguruma jana Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ambapo mwendesha mashtaka wa Serikali ameongeza mashitaka ya kutishia kwa bastola.
Akisoma mashitaka hayo, Mwendesha Mashtaka, Bw. Agustine Komba aliiambia mahakama mbele ya Hakimu Mkazi Bw. James Karayemaha kuwa yameongezwa mashitaka mengine ambayo awali hayakuwepo.
Alidai kuwa Ole Sendeka anatuhumiwa Januari 9 mwaka huu wilayani Monduli katika semina ya wazee wa kimasai ambayo iliandaliwa na Mbunge wa Mbulu, Bw. Edward Lowassa alimtishia kwa bastola na kumdhuru mwili Bw. Milya.
Hata hivyo Mwendesha mashtaka huyo aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza kesi hiyo ambayo imeshatajwa kwa mara mbili baada ya upelelezi kukamilika.
"Mheshimiwa hakimu naomba tarehe kwa ajili ya kuanza kusikilizwa na kutolewa ushahidi ambapo upande wa upelelezi umeshakamilika. Tutaleta mashahidi 13, bastola iliyotumiwa na mshitakiwa kutishia, fomu namba tatu aliyotibiwa nayo mlalamikaji," alisema Mwendesha Mashtaka.
Aliwataja mashahidi watakaotoa ushahidi kuanzia Mei 27 kuwa ni askari polisi wawili ambamo pia atakuwepo Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bw Vicent Kone ambapo siku ya tukio alikuwepo kwenye semina hiyo.
Hakimu Karayemaha aliahirisha kesi hiyo mpaka Mei 27 ambapo itaanza kusikilizwa.
Akizungumza nje ya mahakama hiyo. Mbunge huyo aliwashukuru wananchi wa jimbo lake waliojitokeza kwa wingi kwa ajili ya kujua hatma ya kesi yake ambapo aliwataka kuendelea na kazi za ujenzi wa Taifa kwa vile sheria itachukua mkondo wake.
"Nawashukuru sana naona ni vyema wakulima muendelee na kilimo na wafugaji muendelee na ufugaji. Msihangaike kuja mahakamani tuache sheria ichukue mkondo wake," alisema Sendeka.
Powered by Business Times Limited