Ole Sendeka amtwanga konde M/kiti UVCCM!

Kaizer

Platinum Member
Sep 16, 2008
25,320
17,822
Wakuu hii imekaaje kama wameanza kupigana wenyewe kwa wenyewe? Kuna watu wana hatimiliki ya majimbo?

Mbunge CCM amtwanga konde M'kiti UV-CCM

Na Mussa Juma, Monduli

MBUNGE wa jimbo la Simanjiro (CCM), Christopher Ole Sendeka, jana alisababisha kizaazaa wakati alipompiga ngumi mwenyekiti mpya wa jumuiya ya vijana ya chama hicho, UV-CCM, mkoani Arusha wakati wa mapumziko ya semina iliyoandaliwa kuzungumzia matatizo ya ardhi.

Kilomita chache kutoka eneo hilo, mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete alikuwa akizindua nyumba za wanajeshi wa kambi ya Monduli, akiwa ameongozana na viongozi wengi wa chama hicho na leo anatarajiwa kuja mjini hapa kuendelea na ziara yake.

Sakata hilo lilitokea wakati wajumbe wa semina hiyo wakitoka nje ya ukumbi kwa ajili ya kupata chakula cha mchana na ndipo Ole Sendeka, mmoja wa watu machachari bungeni, kumwendea mwenyekiti huyo wa UV-CCM, James Ole Milia na kumpiga konde lililompeleka hadi chini.

"Alitumia mada yake kunishambulia," alisema Ole Sendeka akizungumzia mada iliyowasilishwa na Ole Milya kwenye semina hiyo kuhusu matumizi ya ardhi na jinsi wanasiasa wanavyotumia Sheria ya Ardhi kudhulumu wafugaji iliyofanyika kwenye Chuo cha Elimu Monduli.

"Alisema waziwazi kuwa baadhi ya wanasiasa wanatumia Sheria ya Ardhi kudhulumu wafugaji... kibaya zaidi ilifikia wakati akawa anatoa mifano ya Simanjiro wakati akijua mimi ndiye mbunge wa jimbo hilo.

"Huyu anatumiwa na mafisadi kunimaliza... najua ameshaeleza kuwa anataka kugombea ubunge wa Simanjiro ndio maana ameona aanze leo kunishambulia.

"Ninajua kuwa ameandaliwa mapokezi Simanjiro siku ya Jumapili kwa kisingizio cha kumpongeza kwa kuchaguliwa kuongoza vijana Arusha, lakini anataka kuwania ubunge."

Ole Milia, ambaye ni mwanasheria, alikanusha tuhuma hizo za kutumia mada yake kumshambulia Ole Sendeka, akisema alilenga kuzungumzia matatizo ya ardhi na Sheria ya Ardhi.

"Nitamchukulia hatua za kisheria," alisema Ole Milia wakati akipata matibabu kwenye Hospitali ya Wilaya ya Monduli. "Amenijeruhi na amenidhalilisha mbele ya watu, hivyo ni lazima nimchukulie hatua za kisheria.

Tayari mwenyekiti huyo wa UV-CCM amesharipoti tukio hilo polisi na sasa anasubiri kesi.

Source: Mwananchi Read News[/COLOR][/SIZE][/B]
 
"Huyu anatumiwa na mafisadi kunimaliza... najua ameshaeleza kuwa anataka kugombea ubunge wa Simanjiro ndio maana ameona aanze leo kunishambulia.

Kunani Bungeni, yani wakishapata Ubunge wanataka kuwa kama Kamuzu Banda. Mara usikie anatembelea jimboni kwangu anataka kugombea, ila kugombea ni haki ya mtu, Sendeka endelea kupigania Haki ya Wananchi, ila usizuie watu kugomea jimboni mwako, manake kila aliyetimiza masharti ana haki naye kugombea.
 
It's too sad and disappointing to hear Ole Sendeka is involved in these kinds of politics! Ni kweli Ole Sendeka ameshindwa kupambana kwa hoja?
 
Ndugu wanajamii nimepokea kwa masikitiko makubwa suala hili la kitendo cha kuchukua sheria mkononi kiasi hichi, kwa viongozi wa juu wa chama cha siasa wanaoshikilia nafasi za juu za dola na chama chao.

Wananchi wanaotuongoza tujifunze nini kutoka kwao, nadhani siasa hataki jazba ni ushindani wa hoja na si suala la nguvu, kuna haja kubwa kwa mh. ubunge Ole-Sendeka kuwaomba radhi wananchi wake wa simanjiro na cham chake cha CCM kwa ujumla kwa hili alilotenda.

Vilevile kwa upande wa mwenyekiti wa UVCCM wa Mkoa wa Arusha It is very unproffessional to address the subject matter to the audiunce by pointing finger straight to someoneelse and with vivid examples to him/her.

I advise them to shake hands and forgive each other for the benefits of simanjiro society and the ruling party CCM and the whole country of Tanzania.

Lets them understand that this country which governing by the rule of laws,practicing democracy,good governace,fighting corruption which it is also clearly elaborated in CCM Manifesto of 2005-2010 of which Hon.Ole and Mlia must implement it with all their efforts as CCM advocate.

Natumaini nimeeleweka na halitokea tena kwa wanajamii hasa viongozi wa vyama vya siasa na serikali kwa ujumla.

Kwa katiba na siasa za Tanzania hakuna mtu mwenye jimbo lake kila mtu anayo haki ya kuchaguliwa na kuchagua katika uongozi.

wanajamii sehemu yeyote ya nchi hii unaweza kwenda kuomba kuchaguliwa kuongoza katika katika ngazi yeyote ya unogozi katika vyma vya vya siasa na dola kwa ujumla.

Wananchi wa sehemu husika ndiyo wenye haki ya kuamua nani wa kuwaongoza bila kurubuniwa kwa namna yeyote hili.

Andrew Mwanga.

+255 787 403865
 
It's too sad and disappointing to hear Ole Sendeka is involved in these kinds of politics! Ni kweli Ole Sendeka ameshindwa kupambana kwa hoja?

Hata mimi nimekuwa astonished kwa kwlei,,, Ole Sendekaanajulikana kama ni mpambanaji, ila inabidi aheshimu Demokrasia.....la sivyo hizi ndo siasa za maji taka alizosemaga Spika!
 
Kunani Bungeni, yani wakishapata Ubunge wanataka kuwa kama Kamuzu Banda. Mara usikie anatembelea jimboni kwangu anataka kugombea, ila kugombea ni haki ya mtu, Sendeka endelea kupigania Haki ya Wananchi, ila usizuie watu kugomea jimboni mwako, manake kila aliyetimiza masharti ana haki naye kugombea.


Hii kwa lugha ya kingumi tunasema amepiga chini ya mkanda!
 
Ukisoma kwa makini hotuba ya mama Kahama baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa, basi hili tukio haliwezi kushangaza sana.
 
Hata Ole Sendeka? Sasa watabaki na nini?

Hii dhana ya watu kumiliki majimbo ni moja ya kansa mbaya sana. Kama taifa tungali tunajifunza siasa za ushindani.Ni utaraibu ambao tunachukua mda mrefu sana kuuzoea.

Kama huwa ana hasira hizo nashangaa mpaka leo hajatwanga mtu bungeni, akiweza kuvumilia upuuzi wa maelezo na majibu ya mawaziri ni kipi kingemshinda?

Ni mmoja wa wabunge waliofanya vyema sana mwaka jana, kwa haiba yake alipaswa kuwa juu ya haya aliofanya. Inasikitisha sana.
 
Hata Ole Sendeka? Sasa watabaki na nini?

Hii dhana ya watu kumiliki majimbo ni moja ya kansa mbaya sana. Kama taifa tungali tunajifunza siasa za ushindani.Ni utaraibu ambao tunachukua mda mrefu sana kuuzoea.

Kama huwa ana hasira hizo nashangaa mpaka leo hajatwanga mtu bungeni, akiweza kuvumilia upuuzi wa maelezo na majibu ya mawaziri ni kipi kingemshinda?

Ni mmoja wa wabunge waliofanya vyema sana mwaka jana, kwa haiba yake alipaswa kuwa juu ya haya aliofanya. Inasikitisha sana.


Ni tatizo la kujifanya kwamba jimbo ni la kwake na hakuna mtu yoyote mwenye haki ya kugomebea tena katika jimbo hilo mpaka yeye atakapokufa au kupenda mwenyewe.

Ni dhana ya jimbo langu ambayo mbunge anaona kwamba yeye pekee ndio mwenye haki na mamlaka ya kuligombea eneo hilo na wananchi haki yao ni kumptisha tuu hata kama hawampendi au hajawaletea maendeleo yoyote.
 
Wakuu tumeusikiliza upande wa pili lakini???

Upande upi mkuu? Labda kama Ole Sendeka atakanusha kumpiga makonde mwenzie (tuliyaona haya kwenye uchaguzi wa UWT)! Kama ni kweli amempiga ngumi, then sidhani kama kuna justification ya kutumia ngumi kwenye siasa.
 
Wabunge ni kazi njema tu, .itakayowafanya wapiga kura wajimbo lako wakurudishe kazini Mabavu na Rushwa Wananchi wanaanza kuvishitukia, na jimbo si haki au mali ya mbunge fulani ni uwanja huru unaoipa nafasi Demokrasia itambe. unapojaza fomu yakumbuke hayo usiweke mawazo katika Shangingi tu.
 
CCM limekuwa jalala bovu na linanuka kweli kweli. Inakuwaje tunachagua wabunge kama hawa ambao hata hawajui maadili ya uongozi?

Badala ya kupambana kwa hoja yeye anapambana kwa mangumi?

Inabidi JK afike mahali aanze kuwawajibisha hawa watu, vinginevyo kuna siku watakuja kuuana huko CCM.
 
Upande upi mkuu? Labda kama Ole Sendeka atakanusha kumpiga makonde mwenzie (tuliyaona haya kwenye uchaguzi wa UWT)! Kama ni kweli amempiga ngumi, then sidhani kama kuna justification ya kutumia ngumi kwenye siasa.
Lazima akanushe, manake hilo ni kosa kumpiga mtu, kama kweli alitoa kisago.
 
Lazima akanushe, manake hilo ni kosa kumpiga mtu, kama kweli alitoa kisago.

Mi nadhani hapo ni mkono wa sheria tu, madamu tunahubiri utawala wa sheria! na bahati mbaya kampiga mwanasheria, sasa apo ndo mchezo utanoga!
 
Ataombwa Radhi na Vijisent kadhaa litakwisha....!!! Kama akimchukulia hatua itakuwa safi ili kukomesha tabia ya watu kujifanya wababe!!! Suppose huyu M/Kiti wa vijana nae angekuwa ngangari kinoma ingekuwaje?.....
 
...tulikuwa tukishangaa sana tukisikia wabunge wa nchi jirani wakitwangana ngumi bungeni. sasa imehamia kwetu. wameanzia barabarani kisha wataingia mpaka bungeni!
 
Kumbe Sendeka alikuwa anarudisha mapigo hakuanza yeye uTyson, kajieleza mwenyewe. Soma habari ifuatayo.

Mkutano wa Lowassa wazua balaa Monduli
2009-01-10 12:13:37
Na Mwandishi Wetu

Mkutano wa viongozi wa jadi wa kabila la Kimasai ulioitishwa na kiongozi wake aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, umezua balaa, baada ya mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Mkoa wa Arusha, James Milya, kurushiana makonde mazito hadharani.

Tukio hilo lilitokea jana baada ya mkutano huo wa viongozi wa jadi wa Kimasai kuahirishwa kwa muda kwa ajili ya chakula cha mchana.

Mkutano huo uliokuwa wa siku mbili ulimalizika jana, lakini kwa mujibu wa Ole Sendeka, Lowassa hakuwepo wakati tukio la purukushani hiyo lilipotokea.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Ole Sendeka alisema aliamua kujitetea baada ya Milya kumrushia konde ambalo alilikwepa.

Alisema kutokana na hali hiyo, aliamua kujitetea kwa kumrushia konde moja ambalo lilimpata hadi kuanguka chini.

Akizungumzia zaidi juu ya mkutano huo, Ole Sendeka alisema kwa ujumla haukuwa wa kisiasa na haukupangwa kwa lengo la kumhujumu.

Alisema wakati akichangia mada, katika mkutano huo uliokuwa na ajenda mbili, ya kuzungumzia elimu ya mtoto wa kike kwa jamii ya wafugaji na nyingine ya matatizo ya ardhi, baadaye Milya alichangia hoja hiyo akiwashutumu wanasiasa na hasa katika jimbo la Simanjiro kwamba ni mafisadi na wanafiki.

``Huyu bwana mdogo alinishambulia akidai kuwa sisi wanasiasa na hasa wa Simanjiro ni wanafiki na kwa nini hatuchukuliwi hatua.

Alitamka wazi ingawa hakutaja jina langu, lakini alisema `kama mchangiaji huyo aliyemaliza kuzungumza sasa hivi` akimaanisha jina lake (Sendeka),`` alisema.

Alisema baada ya kuahirishwa kwa muda kwa ajili ya kupata chakula, alimuuliza Milya kwa nini alimshambulia kiasi hicho naye akamjibu kwamba sasa ameanza vita.

Alisema bila kutegemea alirushiwa ngumi, ambayo hata hivyo, alifanikiwa kuikwepa.

``Katika kujitetea niliamua kumrushia ngumi moja ambayo ilimpata na akaanguka chini, nilichofanya ni kujitetea tu katika mazingira kama yale...`` alisema.

Lakini kwa upande wake Milya alisema hakumrushia ngumi, isipokuwa Ole Sendeka ndiye aliyempiga hadi akaanguka chini.

Alisema baada ya kuanguka Ole Sendeka alitaka kuendelea kumpiga, lakini wajumbe wa mkutano huo walimnusuru.

Hata hivyo alisema aliripoti tukio hilo katika kituo cha polisi cha Monduli na kufungua jalada namba Monduli/RB/35/09.
Source: Nipashe
 
Wakuu tumeusikiliza upande wa pili lakini???

Yees nilikuwa nagojea hili dokezo kama la Nyambala.
Ole Sendeka anapigwa vita na si ajabu the whole thing ni stage managed.
HINT 1:Ole hawaivi na Edo
HINT 2:Edo na "aliyepigwa ngumi" ni maswahiba
Conclusion..mwana JF jazaj mwenyewe!
 
Back
Top Bottom