Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
baada ya kazi nzito iliyofanywa na nguvu ya umma huko arumeru mashariki dalili zinaonyesha wakati umefika kwa gharika hili kuhamia jimbo pacha la arumeru magharibi.
Kijografia majimbo haya mawili yako chini ya wilaya moja inayojulikana kama arumeru.wilaya hii pia imegawanyika katika halmashauri mbili za meru DC na arusha DC.
Kimaendeleo halmashauri ya meru(jimbo la arumeru mashariki) linaonekana kuwa mbele kimaendeleo kulinganisha na halmashauri ya arusha(jimbo la arumeru magharibi)
wakazi wengi wa arumeru magharibi ni wa kabila la waarusha huku wakazi wengi wa arumeru mashariki ni kutoka kabila la wameru.
matatizo ya wananchi wa majimbo haya yanalingana sana.
1.Ukosefu wa maji safi na salama licha ya kuwa na chanzo muhimu cha maji(mlima meru).maji haya yanaanzia arumeru kwenda monduli bila kutumiwa na wakazi wa arumeru.
2.wananchi kudhulumiwa ardhi na mafisadi pamoja na mabeberu ya kizungu.
Kama mnakumbuka halmashauri ya arusha iliuza mashamba ya burka katika hali iliyoacha manunguniko kwa wananchi(wafanyakazi wa kipato cha kati,wakulima na wafugaji wadogo).Ardhi hii ilienda kwa vigogo mfano chaz kimey,rizwani,ole medey(mbunge na naibu waziri wa ardhi)
pia ukienda maeneo ya selian estate utakutana na makaburu walioigeuza Tanzania kama sehemu ya south afrika.
Kwa upande wa arumeru mashariki mengi yalisemwa na mbunge Nassari.
Kuna matatizo mengine mengi yanayofanana na sehemu nyingi za Tanzania kama vile kwenye sekta ya afya,elimu na miundo mbinu.
Baada ya wakazi wa meru kushtuka sasa ni zamu ya wananchi wa jimbo la arumeru magharibi kufanya maamuzi ya kiukombozi.
Ni wakati wa chadema ku-organize nguvu ya umma iliyoko jimbo la ole medey.
Siku za ole medei na ccm kuwakilisha waarusha zinaelekea ukingoni.
Siku za ole medey kuwasalimia wananchi wa jimbo lako kwa kutumia mkia wa ng'ombe zinahesabika.nguvu ya umma inakuja..
Naomba kuwasilisha kwa niaba ya NGUVU YA UMMA(PEOPLES POWER)
UPDATES:uamuzi wa ole millya kujivua gamba na kuamia chadema ni sehemu muhimu ya kumuondoa ole medey arumeru magharibi.kada huyu aliyetoka ccm anaungwa mkono na wakazi wa arumeru magharibi hivyo kazi ya uhamasishaji kwa cdm itakuwa rahisi kuliko maelezo.
Kijografia majimbo haya mawili yako chini ya wilaya moja inayojulikana kama arumeru.wilaya hii pia imegawanyika katika halmashauri mbili za meru DC na arusha DC.
Kimaendeleo halmashauri ya meru(jimbo la arumeru mashariki) linaonekana kuwa mbele kimaendeleo kulinganisha na halmashauri ya arusha(jimbo la arumeru magharibi)
wakazi wengi wa arumeru magharibi ni wa kabila la waarusha huku wakazi wengi wa arumeru mashariki ni kutoka kabila la wameru.
matatizo ya wananchi wa majimbo haya yanalingana sana.
1.Ukosefu wa maji safi na salama licha ya kuwa na chanzo muhimu cha maji(mlima meru).maji haya yanaanzia arumeru kwenda monduli bila kutumiwa na wakazi wa arumeru.
2.wananchi kudhulumiwa ardhi na mafisadi pamoja na mabeberu ya kizungu.
Kama mnakumbuka halmashauri ya arusha iliuza mashamba ya burka katika hali iliyoacha manunguniko kwa wananchi(wafanyakazi wa kipato cha kati,wakulima na wafugaji wadogo).Ardhi hii ilienda kwa vigogo mfano chaz kimey,rizwani,ole medey(mbunge na naibu waziri wa ardhi)
pia ukienda maeneo ya selian estate utakutana na makaburu walioigeuza Tanzania kama sehemu ya south afrika.
Kwa upande wa arumeru mashariki mengi yalisemwa na mbunge Nassari.
Kuna matatizo mengine mengi yanayofanana na sehemu nyingi za Tanzania kama vile kwenye sekta ya afya,elimu na miundo mbinu.
Baada ya wakazi wa meru kushtuka sasa ni zamu ya wananchi wa jimbo la arumeru magharibi kufanya maamuzi ya kiukombozi.
Ni wakati wa chadema ku-organize nguvu ya umma iliyoko jimbo la ole medey.
Siku za ole medei na ccm kuwakilisha waarusha zinaelekea ukingoni.
Siku za ole medey kuwasalimia wananchi wa jimbo lako kwa kutumia mkia wa ng'ombe zinahesabika.nguvu ya umma inakuja..
Naomba kuwasilisha kwa niaba ya NGUVU YA UMMA(PEOPLES POWER)
UPDATES:uamuzi wa ole millya kujivua gamba na kuamia chadema ni sehemu muhimu ya kumuondoa ole medey arumeru magharibi.kada huyu aliyetoka ccm anaungwa mkono na wakazi wa arumeru magharibi hivyo kazi ya uhamasishaji kwa cdm itakuwa rahisi kuliko maelezo.