Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Oksana akiwa hospitali baada ya kukatwa miguu yake na mkono wake wa kulia baada ya kuchomwa moto baada a kubakwa | Thursday, March 22, 2012 4:01 AM Mwanamke mwenye umri wa miaka 18 wa nchini Ukraine yuko mahututi hospitali baada ya kubakwa mtungo na wanaume watatu na kisha kuchomwa moto uliopelekea akatwe miguu yake yote miwili na mkono wake mmoja. |
Oksana Makar, 18, alikuwa ni mrembo mwenye umbile na sura ya kuvutia lakini ghafla maisha yake yamegeuka juu chini baada ya kubakwa na wanaume watatu ambapo wanaume wawili kati yao ni watoto wa vigogo wa serikali nchini Ukraine. Mbali ya kubakwa, Oksana alivalishwa matambara na kutelekezwa porini na kuchomwa moto ili afariki. Lakini nusura yake ilitokea kwa mmoja wa wapita njia aliyesikia kelele zake za kuomba msaada na kwenda kumuokoa. Kutokana na moto kumuunguza vibaya Oksana, madaktari wamelazimika kuikata miguu yake yote miwili na mkono wake wa kulia. Katika VIDEO iliyorekodiwa na mama yake na baadae kurushwa kwenye mitandao, Oksana anasema kuwa wanaume waliomfanyia kitendo hicho wakikamatwa basi wakatwe makende yao na makende hayo wapewe mbwa wale. Oksana alibakwa baada ya wiki iliyopita kualikwa kwenye mojawapo ya nyumba waliyokuwa wakiishi wabakaji hao. Watuhumiwa wa ubakaji ni pamoja na Maxim Prisyjnikov, 23, mtoto wa mkuu wa mkoa na Artyon Pogosyan, 21, mtoto wa mwanasheria wa mkoa. Wabakaji hao walikamatwa na kuachiwa huru siku hiyo polisi wakisema kuwa hakuna ushahidi wa kutosha. Kuwekwa kwa VIDEO online kumepelekea wananchi wengi waandamane wakitaka haki itendeke. Hatimaye rais wa Ukraine aliamuru uchunguzi wa kina ufanyike na ndipo wabakaji hao watatu walipotiwa mbaroni na kufunguliwa mashtaka ya kujaribu kuua. Angalia VIDEO ya Oksana akitaabika kwenye kitanda cha hospitali ambako anatibiwa majeraha yake ya kuungua moto VIDEO - Mwanamke Abakwa na Wanaume Watatu na Kisha Kuchomwa Moto |
<tbody>
</tbody>
Last edited by a moderator: