Ok.. somebody explain this (Picha)

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Watumishi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakiwa wanaendelea kupiga kambi nje ya Ikulu ya Mtukufu Rais Mpendwa wa Watu aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya wapiga kura ambaye chama chake kinapendwa na kukubalika na wananchi wengi na ambaye ni Amir Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Chaguo la Mungu na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Siku chache zijazo, mmoja wao atafia kwenye lango la Ikulu.

1216826425_wasitaafu_ikulu.jpg

Hii ni leo

1216042751_3web.jpg

Wiki iliyopita

Ina maana kuwa katika Taifa letu, katika safu nzima ya uongozi, kuanzia wale waliotangulia na wale ambao wanashikilia nafasi zao hadi hivi sasa, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kutumia kiungo kiitwacho Ubongo kutatua mara moja na daima tatizo la wastaafu hawa wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Ushauri:
Kwa vile Ikulu, ofisi ya Waziri Mkuu na idara nyingine zote hazina watu wenye uwezo wa kufikiria utatuzi wa tatizo kama hili na ambao wameamua kutolijali wala kukosa usingizi kwalo basi hatuna budi wazalendo kutaka serikali ifanye kitu ambacho angalau tunajua inaweza.

Serikali iagize wataalamu toka Ubelgiji au Sweden wawape ushauri wa jinsi gani ya kuweza kufikiria njia ya kumaliza tatizo la wazee wetu hawa ambao waliitumikia nchi yao kwa uaminifu na sasa wanasota juani kudai (siyo kuomba) haki inayotokana na jasho lao.

Ikiwezekana serikali itoe mwaliko kwa nchi kama Uingereza au Marekani wawatangazie kama kuna mtu anayeweza kuja kufikiria kwa niaba yao jinsi ya kulimaliza jambo hili kabla wazee wetu hawa wote hawajatuacha kabla ya kupokea fidia ya jasho la utumishi kwa nchi yao.
 
Mwanakijiji, haya matatizo ya bongo (na Afrika kwa ujumla) yatakukondesha bure.
 
Unajua hapa washauri wa Rais wa mambo ya utawala wanamdanganya. Nafikiri wanamuambia kuwa akitatua matatizo yao kwa Style hii basi ndio itakuwa mchezo. Kila wakati watu watakimbilia ikulu na ndio maana wameamua kuwaacha. lakini ukiangalia kiundani ni kuwa mpaka watu wanafikia kuja kukaa nje ya ikulu kuna nini?. Ni kwamba urasimu umezidi, Rais anatakiwa kufanya mabadiliko makubwa ya watendaji wake ambao wamekuwa na woga wa kuanzia kuwashughulikia mafisadi(e.g polisi, takukuru,n.k) mpaka kwa wanaotakiwa kuwalipa hawa jamaa.

Hapo mi nawaambia kuwa jamaa watakaa mpaka watachoka na kuondoka wenyewe kwani style ya sasa ya JK ambayo ameipata kwa BM ni kwamba kaa kimya wenyewe watachoka. Kwa kifupi nchi inapitia katika wakati mgumu wa kukosa uongozi Tangu tupate UHURU.
 
Nyani ,

Mambo mengi yanayofanyika Afrika ayaingii akilini kabisa na mtu ukiyafuatilia sana unaweza kuwa Schizophrenia....Cha kushangaza zaidi mwaka 2010 hao wazee wote wanaodai mafao yao watampigia kura Kikwete...
 
Wamesahahu ya wanafunzi wa Ukraine na pale alipomtetea Chitalilo kwa kusema kelele za wabongo hazimnyimi usingizi..Sasa hao wasataafu kama hata hawapigi kelele bali wanalala hapo njee then wajuwe ndivyo hivyo tena.
Ni kama TUPAC ambaye licha ya weusi wote kumfagilia Clinton yeye aligoma kabisa...Kwani aliotowa mfano wa wale omba omba ambao wako accross the street from white house na wakati huo huo kwenda Afrika na kuwasadia omba omba wao marais.
 
Ninavyoona mimi hili hata si tatizo la Ikulu.. hili ni tatizo la Bunge, ningekuwa mimi ni hawa wazee ingekuwa ni kupiga kampeni Bungeni na kuwatishia wabunge kuwa wasiposupport haki yao basi wazee hawa watatumia nafasi yao kuwapiga vita. Tatizo ni kuwa wazee wenyewe sitoshangaa kuwa wengi ni wanachama wa CCM hivyo hawaoni kuwa matatizo yao yameunganamana na chama tawala na wabunge wao.
 
Nyani ,

Mambo mengi yanayofanyika Afrika ayaingii akilini kabisa na mtu ukiyafuatilia sana unaweza kuwa Schizophrenia....Cha kushangaza zaidi mwaka 2010 hao wazee wote wanaodai mafao yao watampigia kura Kikwete...
Hao wametumwa kwenda kumwongezea umaarufu.
Tuone kama hajawapa pesa..Janja yao hiyo na ndio maana hata hao CUF wanaanza kudai kuwa BOT inaweza kuwa ni illegal!
Subiri utaona gemu.
 
Nyani ,

Mambo mengi yanayofanyika Afrika ayaingii akilini kabisa na mtu ukiyafuatilia sana unaweza kuwa Schizophrenia....Cha kushangaza zaidi mwaka 2010 hao wazee wote wanaodai mafao yao watampigia kura Kikwete...

Na kwa vile hayaingii akilini, mimi nikisema ninachosemaga naambiwa eti nina complex.....Lol
 
Ninavyoona mimi hili hata si tatizo la Ikulu.. hili ni tatizo la Bunge, ningekuwa mimi ni hawa wazee ingekuwa ni kupiga kampeni Bungeni na kuwatishia wabunge kuwa wasiposupport haki yao basi wazee hawa watatumia nafasi yao kuwapiga vita. Tatizo ni kuwa wazee wenyewe sitoshangaa kuwa wengi ni wanachama wa CCM hivyo hawaoni kuwa matatizo yao yameunganamana na chama tawala na wabunge wao.

Sasa kama ni hivyo wao wanadhani yanatokana au kuungamana na nini? Is this rocket science?
 
Tatizo ni kuwa wazee wenyewe sitoshangaa kuwa wengi ni wanachama wa CCM hivyo hawaoni kuwa matatizo yao yameunganamana na chama tawala na wabunge wao.

Mkjj ninakuhakikishia kuwa 90% ya wana CCM wanajiunga na chama wakitarajia kupata upendeleo fulani na hasa msaada lakini si waabudu wa kweli wa DINI ya CCM. Kwani wanajua kabisa kuwa CCM ndio iliyowafanya wafikie hatua hii ya umasikini kwa wachache kujilimbikizia mali, ila ukijitenga nao utakosa hata nafasi ya kumuomba muheshimiwa shs 1000 ya mafuta ya taa, sasa kipi bora ni kujifanya unamsapoti ili akuruzuku kwa hela zako mwenyewe alizokuibia.
 
Mimi naamini hawa wazee wakiamua kutangaza kuwa wameamua kuzirudisha kadi za CCM na kuziacha hapo Ikulu itakuwa ni big news kuliko wao kudai fedha zao, na ninawahakikishia kina Makamba na Chiligati watakimbia kuzungumza nao. Kumbukeni Ibara ya 15:1
 
Watumishi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakiwa wanaendelea kupiga kambi nje ya Ikulu ya Mtukufu Rais Mpendwa wa Watu aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya wapiga kura ambaye chama chake kinapendwa na kukubalika na wananchi wengi na ambaye ni Amir Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Chaguo la Mungu na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Siku chache zijazo, mmoja wao atafia kwenye lango la Ikulu.

1216826425_wasitaafu_ikulu.jpg

Hii ni leo

1216042751_3web.jpg

Wiki iliyopita

Ina maana kuwa katika Taifa letu, katika safu nzima ya uongozi, kuanzia wale waliotangulia na wale ambao wanashikilia nafasi zao hadi hivi sasa, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kutumia kiungo kiitwacho Ubongo kutatua mara moja na daima tatizo la wastaafu hawa wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Ushauri:
Kwa vile Ikulu, ofisi ya Waziri Mkuu na idara nyingine zote hazina watu wenye uwezo wa kufikiria utatuzi wa tatizo kama hili na ambao wameamua kutolijali wala kukosa usingizi kwalo basi hatuna budi wazalendo kutaka serikali ifanye kitu ambacho angalau tunajua inaweza.

Serikali iagize wataalamu toka Ubelgiji au Sweden wawape ushauri wa jinsi gani ya kuweza kufikiria njia ya kumaliza tatizo la wazee wetu hawa ambao waliitumikia nchi yao kwa uaminifu na sasa wanasota juani kudai (siyo kuomba) haki inayotokana na jasho lao.

Ikiwezekana serikali itoe mwaliko kwa nchi kama Uingereza au Marekani wawatangazie kama kuna mtu anayeweza kuja kufikiria kwa niaba yao jinsi ya kulimaliza jambo hili kabla wazee wetu hawa wote hawajatuacha kabla ya kupokea fidia ya jasho la utumishi kwa nchi yao.
Wiki


Wakitatuliwa matatizo hawa zile safari zitapungua. Canada watalalamika!
 
Halafu utakuta pesa zenyewe wanazodai sana sana ni milioni tano tano mpaka kumi, if that much.

Wakati huo huo watu wanafisadi mamia ya mamilioni- siyo ya shilingi- ya dola za kimarekani!

Hawa watu wanafikia "the sunset of their lives" halafu mnawatesa hivi?

No empathy, no commitment, full of excuses and bs!
 
Mkuu MMJJ unayosema ni kweli kwamba sio ajabu tukaona mmoja wa hawa wazee anafia hapa ikulu akisubiri mafao yake wakati Kikwete amekaa Tanga zaidi ya siku 5 akishangiliwa na wacheza bao kuhusu kudanganywa kwamba anavalia njuga mimba za mashuleni. Mimi naona alikuwa anawaambia mwaka huu nitawatia mimba watoto wenu mpaka mshangae...! na wazee wakashangilia. Hata hivyo kama nilivyosema nilimwona akipandisha suruali na mkanda ulikuwa upande, hali yake kiafya sio nzuri ingawa namwona Mrs ananona sasa, huenda kila mtu kachukua time yake hapa.

Kuhusu kuagiza mtaalam wa kufikiria lingeweza kuwa usanii mzuri wa kuvuta muda lakini ni ngumu maana si pesa walipewa na hao hao halafu ccm wakazila? Ingekuwa sivyo usishangae sana JK kuagiza wataalam kutoka nje kuwapeleka semina ya wiki 2 pale Ngurdoto kuhusu namna ya kukabiliana na matatizo na administration kwa ujumla, ingeitwa "special administration seminar" kutoka kwa JK through wafadhili.

Mimi nadhani tumefika wakati wa kuongea wazi au tufanye jambo wazi ili serikali ijue kuna mambo ya kunyamazia na ya kufanyia kazi, this is too much. Yaani inakuwa kama vile wale wazee huwa wanaenda kupiga soga pale viwanja vya ikulu na hakuna mwenye time nao. Au ndio maana jamaa alitokomea Tanga kuhubiri kuhusu mimba? huenda aliwatoroka, sasa muda unavyokwenda itakuwaje? Je mmoja wao akifia hapo itakuwaje? Mbona wale wasabato waliokuwa wanataka kwenda nje bila vibali Kandoro aliwafuata pale uwanja wa ndege ingawa aliwakosa? ina maana hakuna wa kuwafuata hawa wazee akawaambia lolote? INA MAANA WAMESHASEMA UONGO WOTE, SASA WANAJIULIZA NANI AKAWADANGANYE NINI TENA SASA? Serikali yetu imezidi ufedhuli.

Tunaomba hapa tujiunge tufikiri la kufanya kabla hawa wazee hawajaacha laana ambayo haitwakwepeka kwa taifa hili, hapa JF si pabaya sana kujadili kwa haraka mambo ya kufanya. Tusijadili kuhusu mapanga sana hapa maana mission itashtukiwa haraka halafu itashindikana.
 
Mkjj ninakuhakikishia kuwa 90% ya wana CCM wanajiunga na chama wakitarajia kupata upendeleo fulani na hasa msaada lakini si waabudu wa kweli wa DINI ya CCM. Kwani wanajua kabisa kuwa CCM ndio iliyowafanya wafikie hatua hii ya umasikini kwa wachache kujilimbikizia mali, ila ukijitenga nao utakosa hata nafasi ya kumuomba muheshimiwa shs 1000 ya mafuta ya taa, sasa kipi bora ni kujifanya unamsapoti ili akuruzuku kwa hela zako mwenyewe alizokuibia.
Hofstede nakubaliana na wewe,

Najiuliza kwamba Lowasa alikuwa mwenye mabavu sana kwenye kuchangisha pesa za ccm kutoka kwa wafanyabiashra, ila nyakati za mwisho kabla hajavuliwa majoho yake ilishaanza kuwa ngumu kwa wafanyabiashra wengi kupeleka pesa ccm maana usanii ulishazidi kiwango. Walikuwa hawaogopi tena ccm kama walivyoogopa zamani kwamba usipotoa ati mambo yako yanaharibika, wafanyabishara wengi walifikia kuzima simu na kutokomea mitini Lowasa alipoitisha vikao vya kunyonya watu pesa kwa nguvu.

Swali langu ni kwamba baada ya Lowasa kuvuliwa majoho, ni nani kachukua joho lake kuchangisha wafanyabishara pesa kwa nguvu? Kama hakuna ina maana wafanyabishara wamepata nguvu na hawako tayari kuwapa mafisadi pesa tena. Je ni nini kinaendelea na wafanyabiashara kuhusu hicho chama cha majambazi?
 
Mimi naamini hawa wazee wakiamua kutangaza kuwa wameamua kuzirudisha kadi za CCM na kuziacha hapo Ikulu itakuwa ni big news kuliko wao kudai fedha zao, na ninawahakikishia kina Makamba na Chiligati watakimbia kuzungumza nao. Kumbukeni Ibara ya 15:1
Mkuu nadhani katika ushauri laini lakini ambao ni powerful niliowahi kuuona hapa tangu niingie (ingawa ni mgeni), huu ni ushauri mzito sana, nadhani lingekuwa jambo ambalo kwanza ni la amani, pili halihitaji nguvu, lakini impact yake ingekuwa mbaya sana upon ccm. Hatuna mtoto au mjukuu wa mmoja wa hawa wazee tuwashauri hilo mkuu???
 
Mkjj, Kama JK ni chaguo la Mungu, basi ni Mungu wa mafisadi maana hata wao wana mungu wao anaweza kuwa hata sanamu. Tatizo ni la Rais wala si la Bunge, hili Bunge uchwara la CCM linaweza kufanya lolote kwa maslahi ya Watanzania? tangu lini? Maana tuliambiwa Bunge hili la kikao cha bajeti lingewaka moto kuhusiana na ufisadi wa EPA, Richmond, Kiwira n.k. lakini hata cheche hatukuziona wachilia mbali kuuona moto na ndiyo linaelekea ukingoni huku mafisadi wakiendelea kupeta. Wanalipwa mishahara, marupurupu ya petroli na mengine ambayo ni mabilioni ya pesa, lakini hawana umuhimu wowote kwa nchi yetu. Hata likivunjwa leo hii Watanzania hatutaona tofauti yoyote ile maana sasa hivi ni kama hatuna Bunge.

Pesa za wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimeshatafunwa na mafisadi. Wenzao wa Kenya na Uganda walilipwa mafao yao miaka chungu nzima iliyopita, lakini hawa wadanganyika bado wanahangaishwa kila kukicha kwa sababu hawana mtetezi wa kusaidia kudai haki zao.
 
hivi upinzani unatarajiwa usaidie mangapi tanzania? kweli mbunge mmoja wa ccm anashindwa kulivalia njuga suala hili akawapatia haki wazee hao!!
hivi kweli wabunge wa ccm hawana utu kiasi hichi?
rais ndio kabisa tusimuongelee, anaenda kukisaka kibibi kizee anapiga picha nacho wakati hao hapo nje ya anapolala anawadharau.
shame on him
 
[B said:
Mzee Mwanakijiji;253065[/B]]Watumishi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakiwa wanaendelea kupiga kambi nje ya Ikulu ya Mtukufu Rais Mpendwa wa Watu aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya wapiga kura ambaye chama chake kinapendwa na kukubalika na wananchi wengi na ambaye ni Amir Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Chaguo la Mungu na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Siku chache zijazo, mmoja wao atafia kwenye lango la Ikulu.

1216826425_wasitaafu_ikulu.jpg

Hii ni leo

1216042751_3web.jpg

Wiki iliyopita

Ina maana kuwa katika Taifa letu, katika safu nzima ya uongozi, kuanzia wale waliotangulia na wale ambao wanashikilia nafasi zao hadi hivi sasa, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kutumia kiungo kiitwacho Ubongo kutatua mara moja na daima tatizo la wastaafu hawa wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
[B said:
La kuhuzunisha ni kuwa serikali ilikabidhiwa hizi fedha iwafikishie hao wastaafu zaidi ya miaka 30 iliyopita. Pamoja na kwamba zilikuwa ni fedha zao zilizotokana na makato kwenye mishahara yao wakati wakitumikia hiyo jumuiya, serikali kwa makusudi yasiyoeleweka iliamua kuzitumia kinyume na ilivyotarajiwa. Ukweli ni kuwa serikali iliamua kuwaibia hawa wananchi wake mchana kweupeee.

Ule uwezo wa kuibana serikali ndio hawa wazee hawana na si kweli kwamba wana ubia wowote na serikali ya CCM. Wabunge wengi wa CCM wa sasa inawezekana walishiriki kikamilifu katika kutafuna fedha hizo kutokana na nyadhifa walizokuwa nazo wakati huo. Hata hivyo ombi liende kwa wachache wao ambao wameonyesha kuwatetea wananchi walivalie njuga kuwasaidia hawa wazee.
 
Watumishi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki wakiwa wanaendelea kupiga kambi nje ya Ikulu ya Mtukufu Rais Mpendwa wa Watu aliyechaguliwa kwa asilimia 80 ya wapiga kura ambaye chama chake kinapendwa na kukubalika na wananchi wengi na ambaye ni Amir Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Chaguo la Mungu na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Siku chache zijazo, mmoja wao atafia kwenye lango la Ikulu.

1216826425_wasitaafu_ikulu.jpg

Hii ni leo

1216042751_3web.jpg

Wiki iliyopita

.
MzMwkjj. naomba kusemea juu ya picha Hizi kwa kutoa mfano ufuatao:Wasanii huchora picha fulani hivi,halafu huwaachia watizamaji/Mlengwa kufanya tafsiri juu ya yatakayo onekana katika picha hizo.
Iwe ni mchanganyo wa rangi mbaliX2 alizotumia msanii,jinsia zilizotumika,au hata mavazi...basi alimradi tu Mtazamaji akaridhika kwa tafsiri yake binafsi bilashaka picha hiyo hupewa umuhimu fulani,hatimaye thamani.
**Kama JK atatafsiri niliyo tafsiri miye ktk picha hizo, basi hana budi 'kuwasaidia' wazee hao kupata mafao/malipo yao....Imeshindikana kiserikali,kichama.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom