Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Zanzibar kujiunga na OIC kivyake
2009-01-27 10:14:33
Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imetangaza kwamba itaiomba Serikali ya Muungano kuiruhusu Zanzibar kujiunga na Umoja wa Nchi za Kiisalm(OIC) endapo mpango huo utashindwa kufikiwa na Serikali ya Muungano.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alipokuwa akijibu maswali ya wajumbe wa baraza la wawakilishi waliotaka kujua Serikali ina mikakati gani kuhakikisha Zanzibar inakuwa mwanachama wa jumuiya hiyo.
Alisema kimsingi sula hilo bado linashughulikiwa na Serikali ya Muungano hasa kwa kuzingatia linahusu utaifa ``kwani Zanzibar ni nchi wakati taifa ni moja la Tanzania hivyo tutajiunga kama Nchi ,ndo maana yake.
Alisema Zanzibar haijuingi katika jumuiya hiyo kwa matakwa ya kidini bali inatetea kuchukua hatua hiyo kutokana na sababu za kiuchumi.
``Ikiwa itashindikana kwa Serikali ya Muungano kujiunga, Serikali ya Zanzibar tutaomba tujiunge kwa kujitegemea badala ya kuwa wanachama kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano,`` alisema Waziri Hamza.
Alisema kitendo cha kuchelewa kujiunga katika jumuiya hiyo kunachangia kutochangamsha maendeleo ya Zanzibar kutokana na misaada ya kijamii na kiuchumi inayotolewa na OIC.
Alitoa mfano kwamba endapo Zanzibar ingekuwa mwanachama ingesaidiwa matrekta 50 kupitia jumuiya hiyo na kusaidia katika sekta ya kilimo Zanzibar ambayo ingewanufaisha wananchi wote bila ya kujali imani zao za dini.
2009-01-27 10:14:33
Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imetangaza kwamba itaiomba Serikali ya Muungano kuiruhusu Zanzibar kujiunga na Umoja wa Nchi za Kiisalm(OIC) endapo mpango huo utashindwa kufikiwa na Serikali ya Muungano.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alipokuwa akijibu maswali ya wajumbe wa baraza la wawakilishi waliotaka kujua Serikali ina mikakati gani kuhakikisha Zanzibar inakuwa mwanachama wa jumuiya hiyo.
Alisema kimsingi sula hilo bado linashughulikiwa na Serikali ya Muungano hasa kwa kuzingatia linahusu utaifa ``kwani Zanzibar ni nchi wakati taifa ni moja la Tanzania hivyo tutajiunga kama Nchi ,ndo maana yake.
Alisema Zanzibar haijuingi katika jumuiya hiyo kwa matakwa ya kidini bali inatetea kuchukua hatua hiyo kutokana na sababu za kiuchumi.
``Ikiwa itashindikana kwa Serikali ya Muungano kujiunga, Serikali ya Zanzibar tutaomba tujiunge kwa kujitegemea badala ya kuwa wanachama kama sehemu ya Jamhuri ya Muungano,`` alisema Waziri Hamza.
Alisema kitendo cha kuchelewa kujiunga katika jumuiya hiyo kunachangia kutochangamsha maendeleo ya Zanzibar kutokana na misaada ya kijamii na kiuchumi inayotolewa na OIC.
Alitoa mfano kwamba endapo Zanzibar ingekuwa mwanachama ingesaidiwa matrekta 50 kupitia jumuiya hiyo na kusaidia katika sekta ya kilimo Zanzibar ambayo ingewanufaisha wananchi wote bila ya kujali imani zao za dini.
Last edited: