Oh Your Excellence! (Picha)

pamoja na hilo mkuu pia kuna aina ya matukio hayaitaji presence ya Raisi hata kidogo otherwise tunakuwa too cheap.... mimi ningeunga mkono ningemwona mkulu anapokea msaada wa kuanzisha kiwanda cha hayo ma Yebo yebo (if not hizo tukutuku) bongo .... not kupokea maYeboYEBO bana
ha ha ha ha!
UKIKUBALI KUOLEWA SHARTI USILALE NA CHUPI.......!
habari ndiyo hiyo
 
huu sio utaratibu na ninaamini lipo la chini ya kapeti katika misaada hii,ni bora wangepeleka misaada hii hata kwa mkuu wa mkoa.....hivi wasaidizi wa raisi wanafanya kazi gani? kumkabidhi raisi yeboyebo na baiskeli ikulu.....KWELI JK UNA KAZI...
 
Mwalimu aliwaomba Wachina hawa watujengee kwa mikopo nafuu kiwanda cha URAFIKI, UFI, reli ya TAZARA (tukaviua wenyewe!), misaada mikubwa ya kijeshi,.....JK yeye analetewa yeboyebo, pikipiki, wakati vitu hivi tayari vimejaa Kariakoo, mitaani!?
 
Kweli mfungwa hachagui gereza...! maskini ukipewa msaada wowote kama (yeboyebo) unajipokelea tu, tena ikulu, aah inauma sana... tutakuwa hivi hadi lini? Eeeh Mungu tusaidie na utupe moyo wa utoaji kwa watanzania wenzetu na wengine wengi.
 
Mwalimu aliwaomba Wachina hawa watujengee kwa mikopo nafuu kiwanda cha URAFIKI, UFI, reli ya TAZARA (tukaviua wenyewe!), misaada mikubwa ya kijeshi,.....JK yeye analetewa yeboyebo, pikipiki, wakati vitu hivi tayari vimejaa Kariakoo, mitaani!?

Dah naskia uchungu mwingi sana, kama kiongozi wetu wa juu anapokea yeboyebo na baiskeli hali ya kuwa vimejaa kariakoo, je wasaidizi wake yaani wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, wenyeviti wa vijiji na vitongoji watapokea nini??? ua ameamua kuwapa kaheshima cha kuwaita ikulu kwa sababu anafahamiana nao... huwezi jua
 
Smelly AIDS!

Halafu zote ni feki! How come ulete MSAADA wa yeboyebo za shi'ng 1500, na kumkabidhi raHISI WETU??
 
Rais hana kazi ya kuhamasisha maendeleo:: Zaidi ya kupokea na kuomba misaada na ndicho anachokifanya akiwa nje ya nchi ama nchini si mmeona!! Tutafika? kaza kweli kweli
 
Kwani hawa ndugu zangu kilosa wanahitaji mipira au hiii mipira ni kwa Maximo?walichangia vyote kwa mpigo?
 
hasa pale watoa msaada wanapoonekana kufurahia kuwa ni kitu kikubwa sana wamefanya, vitu vyebyewe quality yake inatisha na hilolinajulikana so tufanyeje kwa hili bora ashauriwe
 
yaani wa TZ tumekwishilia mbali. jamaa anatoa promo heavy kwa Mil 51? just imagine hao wachina wakitumia hiyo picha kufanya promo.
 
yaani wa TZ tumekwishilia mbali. jamaa anatoa promo heavy kwa Mil 51? just imagine hao wachina wakitumia hiyo picha kufanya promo.

hapo zidisha hiyo mil 51 uifanye ni usd mil 51 X1000! ndo gain watayopata wachina hapa kwa kutudanganya, watapewa miradi mikubwa, watawinda, madini watachukua, imagine tumekuwa tukuwacheka mababu zetu eti wazungu waliwapatia gololi na nakoti ya suti wao wakawapa DHAHABU! je kuna tofauti gani na leo hii? tena sisi ni wajinga zaidi kwani tupo well informed but ignorance imegandisha na kufreez brain zetu!
 




jkviatu.jpg

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia Yeboyebo zilizotolewa msaada na balozi wa China nchini Tanzania Bwana Liu Xinsheng katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini dar es Salaam jana asubuhi.Rais Kikwete alitangaza kuwa misaada hiyo itapelekwa kwa waathirika wa mafuriko wilayani kilosa,Mkoani Morogoro.​


Kikwete kakabidhiwa yeboyebo na Wachina?
Kwi kwi kwi.
Mzee Mwanakijiji acha utani bwanaaaa!
 
this is too much,kwanza sielewi wachina wanatafuta nini africa hivi sasa,maana wako busy na hii misaada yao uchwara uchwara,wengine wapo hapo rwanda sasahivi na wanafanya same shit.
 
Hiyo picha ya Rais akiwa amepanda pikipiki ilipigwa na Kamera aina ya Canon EOS-1D Mark III, mnamo tarehe 29 Machi 2010, saa nne na dakika 32 asubuhi. Mpiga picha kwa makusudi alitumia flashi kwenye picha. Kutokana na bei ya kamera, inaonesha kwamba mpigapicha ama ni Al-watan, au alitumia kamera ya ofisi. Baada ya kupiga picha hizi, aliziimport kwenye kompyuta kwa kutumia softiwea ya Picasa toleo la 3.0. Kwa kuwa Picasa ni softiwea ya bure, na ina toleo jipya la Picasa, mpigapicha wetu si mtumiaji sana wa kompyuta, zaidi ya kutumia kwa shughuli zake za kazi kama wajibu. Sherehe hii muhimu ilitumia zaidi ya masaa mawili toka ianze saa mbili za asubuhi.
 
Kama anaweza kupokea jezi ya Ronaldo na kutangazwa na vyombo vyote vya habari ambayo thamani yake ni chini ya hiyo milioni 51 haishangazi na inabidi tuzoee tu.
 
"Baiskeli za Cheng shang kwa madaha ndio zenyewe zina nguvu imara kama simba. zinabeba mzigo zaidi ya punda."

Nimelikumbuka tangazo la baiskeli. Hivi kiwanda chetu cha baisikeli kipo? kinafanya kazi?
Kiwanda cha swala waliuziwa wahindi ambao wakakibadili kiwe cha kutengeneza tembe (dawa) kinaitwa shellys kipo pale mwenge. Hiyo ndo faida ya mwekezaji bana teh teh! utumbo mtupu nchi hii dah!
Brother MM, na kakako mwenyewe sometimes amezidi mno. Nafikiri wewe ni rafiki yake wa karibu, jaribu basi kumshauri ajaribu kudeligate baadhi ya mambo. Waziri anayeshughulikia maafa si yupo, kwanini asipokee yeye?
Akimpa waziri nafasi hiyo atakuwa anajipunguzia repyutesheni mbele ya jamii. Kwa taarifa yako ninategemea kufungua chekechea yangu kule kijijini na nitamualika mkulu aje na kumuhakikishia 100% coverage naamini atakuja tu!
Huyu bwana hata hajui anafanya nini Ikulu, wakina Rostam walimburuza kumpeleka ikulu wakijua ufahamu wake ni mdogo sana ili wamtumie kwa manufaa yao, ona sasa anavyojizalilisha na kuidhalilisha nchi kwa ujumla. Hiyo hafla inaweza kuwa imeigharimu nchi zaidi ya thamani ya hiyo misaada ya kichina
Mliambiwa mkanywe nae chai lakini ninyi mkafanya vinginevyo. Mtajiju sasa
mambo mengine ni aibu sana kwetu...tumekuwa kama vipofu tusio na mwongozaji
...Muda si mrefu tutatumbukia shimoni pasi shaka. Wana TARIME wameanza tifu kama mbuzi wasio na mchungaji na subirini itaenea nchi nzima ndipo aliye shambani asikimbilie jikoni.
 
Ah! hii kali. Yaani Presda mzima anapokea msaada wa milioni 51. Aibu. Hana mambo muhimu ya kufanya.
 
Back
Top Bottom