Ofisi ya waziri mkuu yageuka kuwa mahakama kuu katika sakata la madaktari

vimon

Senior Member
Apr 3, 2008
183
195
[h=6]TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, leo (*Alhamisi Machi 8, 2012) *imetoa
... uamuzi wa kusitishwa mara moja kwa mgomo wa Madaktari ulioitishwa nchi
nzima tangu jana (*Jumatano Machi 7, 2012).

Katika amri yake ya pili, Mahakama Kuu pia imekitaka Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari kuwatangazia wanachama wao mara moja kupitia
Vyombo vya Habari kusitishwa kwa mgomo huo nchi nzima kama
walivyowatangazia wakati wanauitisha mgomo wenyewe.

Mahakama Kuu pia imeamuru pande zote mbili, yaani Serikali kwa upande mmoja
na Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari, kwa upande mwingine,
kutumia fursa zilizopo katika kutatua mgogoro wa kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.


Uamuzi huo wa Mahakama Kuu imetolewa na Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya
kusikiliza ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha
Madaktari na Jumuiya ya Madaktari kuitaka itoe zuio kwa mgomo huo.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Rweyemamu alisema anazingatia madhara ambayo mgomo
huo ungeleta kwa jamii kwa vile huduma za tiba ambazo madaktari walitaka
kugoma kuzitoa ni miongoni mwa huduma muhimu zilizotajwa kwenye Sheria ya
Ajira na Mahusiano Kazini, Namba 6 ya Mwaka 2004.

Uamuzi huo, ni kama ifuatavyo:

Leo, tarehe 8, Machi 2012, Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, mbele ya Jaji
R.M. Rweyemamu
, baada ya kusikiliza Ombi No. 24 la 2012 lililowasilishwa na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Mwombaji) dhidi ya Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari (Walalamikiwa), imetoa uamuzi ufuatao:

i) Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari
pamoja na Wanachama wao, kusitisha Mgomo waliouanzisha rasmi tarehe 7 Machi
2012 nchi nzima na kurejea kazini mara moja kwa kuendelea na kazi zao kama
kawaida, mara tu Amri hii itakapowafikia. Aidha, waombaji watatakiwa kutoa
Kiapo cha kuthibitisha kwamba wamewasilisha Amri hiyo kwa Walalamikiwa na
kuwasilisha Kiapo hicho Mahakama Kuu – Divisheni ya Kazi kesho tarehe 9,
Mach 2012.

ii) Mara baada ya Amri hii kuwasilishwa kwa Walalamikiwa
(Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari) watatakiwa
kuwatangazia Wanachama wao kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa Mgomo
huo Nchi nzima kama walivyowatangazia wakati wa kuitisha Mgomo huo;

iii) Mahakama inaamuru pande zote mbili (Serikali na Chama
cha Madaktari Tanzania pamoja na Jumuiya ya Madaktari) kutumia fursa za
Kisheria zilizopo katika kutatua Mgogoro wa Kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.
(mwisho)
Imetolewa na:

Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM.
Alhamisi Machi 8, 2012
[/h]Siku hizi kazi za ofisi ya PM zimekuwa za kimahakama au ndio kuzuia PM asiachie madaraka,pinda jiuzulu umeiabisha.
 
Hizi siasa hizi yaani mahakama inatoa taarifa halafu chini inaandikiwa kuwa imetolewa na ofisi ya Waziri Mkuu
 
Hii haikubaliki;Mahakama ni muhimili unaojitegemea kabisa;ningekuwa mm Dr ningeendelea kugoma kudai mafao yangu maana kinachofanyika sasa ni uhuni!

Mkiwalazimisha ma dr ukienda unaumwa kichwa wanaweza kukuandikia sindano za kuponya kaswende,mahakama haiwezi mlazimisha dr kufanya kazi kama wanavyotaka kufanya serikali bali ni kwa majadiliano tu!
 
njia mojawapo ya kutatua migogoro ni haki ya mfanya kazi kugoma. halafu hao madaktari wataongea na nani? wakati mtu mwenyewe wa kuongea naye wapo kwenye mgogoro nae? na Pm aliwaahidi kutekeleza mambo yao ni 3/3/12 kupeana taarifa ya kilichofikiwa na kile bado lini, ikiwemo mamlaka husika kushughulikia suala la waziri na naibu waziri. yaani gharama zote hizi kwa serikali ni kwa ajili ya wanasiasa, kama ilivyo kuwa ndege ya raisi kwamba anayo haki, ya hayo matumizi hata kama sisi tutakula nyasi.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, leo (*Alhamisi Machi 8, 2012) *imetoa
... uamuzi wa kusitishwa mara moja kwa mgomo wa Madaktari ulioitishwa nchi
nzima tangu jana (*Jumatano Machi 7, 2012).

Katika amri yake ya pili, Mahakama Kuu pia imekitaka Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari kuwatangazia wanachama wao mara moja kupitia
Vyombo vya Habari kusitishwa kwa mgomo huo nchi nzima kama
walivyowatangazia wakati wanauitisha mgomo wenyewe.

Mahakama Kuu pia imeamuru pande zote mbili, yaani Serikali kwa upande mmoja
na Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari, kwa upande mwingine,
kutumia fursa zilizopo katika kutatua mgogoro wa kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.


Uamuzi huo wa Mahakama Kuu imetolewa na Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya
kusikiliza ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha
Madaktari na Jumuiya ya Madaktari kuitaka itoe zuio kwa mgomo huo.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Rweyemamu alisema anazingatia madhara ambayo mgomo
huo ungeleta kwa jamii kwa vile huduma za tiba ambazo madaktari walitaka
kugoma kuzitoa ni miongoni mwa huduma muhimu zilizotajwa kwenye Sheria ya
Ajira na Mahusiano Kazini, Namba 6 ya Mwaka 2004.

Uamuzi huo, ni kama ifuatavyo:

Leo, tarehe 8, Machi 2012, Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, mbele ya Jaji
R.M. Rweyemamu
, baada ya kusikiliza Ombi No. 24 la 2012 lililowasilishwa na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Mwombaji) dhidi ya Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari (Walalamikiwa), imetoa uamuzi ufuatao:

i) Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari
pamoja na Wanachama wao, kusitisha Mgomo waliouanzisha rasmi tarehe 7 Machi
2012 nchi nzima na kurejea kazini mara moja kwa kuendelea na kazi zao kama
kawaida, mara tu Amri hii itakapowafikia. Aidha, waombaji watatakiwa kutoa
Kiapo cha kuthibitisha kwamba wamewasilisha Amri hiyo kwa Walalamikiwa na
kuwasilisha Kiapo hicho Mahakama Kuu – Divisheni ya Kazi kesho tarehe 9,
Mach 2012.

ii) Mara baada ya Amri hii kuwasilishwa kwa Walalamikiwa
(Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari) watatakiwa
kuwatangazia Wanachama wao kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa Mgomo
huo Nchi nzima kama walivyowatangazia wakati wa kuitisha Mgomo huo;

iii) Mahakama inaamuru pande zote mbili (Serikali na Chama
cha Madaktari Tanzania pamoja na Jumuiya ya Madaktari) kutumia fursa za
Kisheria zilizopo katika kutatua Mgogoro wa Kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.
(mwisho)
Imetolewa na:

Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM.
Alhamisi Machi 8, 2012


Siku hizi kazi za ofisi ya PM zimekuwa za kimahakama au ndio kuzuia PM asiachie madaraka,pinda jiuzulu umeiabisha.[/QUOT

VIMON mbona unatufanya kama hatuna shule kama wewe. Una-edit anwani ya aliyetoa tamko hilo alafu unatuletea humu. Tupe source ya hilo tamko. Kweli mfa maji haachi kutapatapa. Acha hao wauaji(Madaktari )wabanwe mbavu mpaka kitaeleweka na wakichezea mahakama Itawakenyarize
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, leo (*Alhamisi Machi 8, 2012) *imetoa
... uamuzi wa kusitishwa mara moja kwa mgomo wa Madaktari ulioitishwa nchi
nzima tangu jana (*Jumatano Machi 7, 2012).

Katika amri yake ya pili, Mahakama Kuu pia imekitaka Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari kuwatangazia wanachama wao mara moja kupitia
Vyombo vya Habari kusitishwa kwa mgomo huo nchi nzima kama
walivyowatangazia wakati wanauitisha mgomo wenyewe.

Mahakama Kuu pia imeamuru pande zote mbili, yaani Serikali kwa upande mmoja
na Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari, kwa upande mwingine,
kutumia fursa zilizopo katika kutatua mgogoro wa kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.


Uamuzi huo wa Mahakama Kuu imetolewa na Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya
kusikiliza ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha
Madaktari na Jumuiya ya Madaktari kuitaka itoe zuio kwa mgomo huo.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Rweyemamu alisema anazingatia madhara ambayo mgomo
huo ungeleta kwa jamii kwa vile huduma za tiba ambazo madaktari walitaka
kugoma kuzitoa ni miongoni mwa huduma muhimu zilizotajwa kwenye Sheria ya
Ajira na Mahusiano Kazini, Namba 6 ya Mwaka 2004.

Uamuzi huo, ni kama ifuatavyo:

Leo, tarehe 8, Machi 2012, Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, mbele ya Jaji
R.M. Rweyemamu
, baada ya kusikiliza Ombi No. 24 la 2012 lililowasilishwa na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Mwombaji) dhidi ya Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari (Walalamikiwa), imetoa uamuzi ufuatao:

i) Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari
pamoja na Wanachama wao, kusitisha Mgomo waliouanzisha rasmi tarehe 7 Machi
2012 nchi nzima na kurejea kazini mara moja kwa kuendelea na kazi zao kama
kawaida, mara tu Amri hii itakapowafikia. Aidha, waombaji watatakiwa kutoa
Kiapo cha kuthibitisha kwamba wamewasilisha Amri hiyo kwa Walalamikiwa na
kuwasilisha Kiapo hicho Mahakama Kuu – Divisheni ya Kazi kesho tarehe 9,
Mach 2012.

ii) Mara baada ya Amri hii kuwasilishwa kwa Walalamikiwa
(Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari) watatakiwa
kuwatangazia Wanachama wao kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa Mgomo
huo Nchi nzima kama walivyowatangazia wakati wa kuitisha Mgomo huo;

iii) Mahakama inaamuru pande zote mbili (Serikali na Chama
cha Madaktari Tanzania pamoja na Jumuiya ya Madaktari) kutumia fursa za
Kisheria zilizopo katika kutatua Mgogoro wa Kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.
(mwisho)
Imetolewa na:

Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM.
Alhamisi Machi 8, 2012


Siku hizi kazi za ofisi ya PM zimekuwa za kimahakama au ndio kuzuia PM asiachie madaraka,pinda jiuzulu umeiabisha.

hahahaaaaa siku-notice hii kitu watakuwa wameipika hii msg. Hawako makini kwakweli
 
Ikiwa tangazo hili halijaeditiwa basi madaktari wanayo haki ya kuishitaki mahakama pamoja na waziri mkuu kwa kuwahadaaa wananchi pamoja na madaktari. What a shame................. Kwanza haina hana nembo.
 
Back
Top Bottom