Ofisi ya Mwanasheria Mkuu yapangua hoja ya Dr. Slaa

Wandugu tatizo la maelezo ya Mwanasheria Mkuu liko wapi?................naomba mnielimishe............
Nilivyomuelewa AG.......amesema kulingana na utaratibu wa Bunge AG akisha draft......inarudishwa Bungeni kuridhiwa..........au?

TAARIFA KWA UMMA


Kwa kuzingatia taaluma ya uandishi wa sheria ilibidi kuongeza masharti yenye amri ya kisheria (Legislative rules) katika kifungu hicho ili tafsiri ya "Timu ya Kampeni" ijitosheleze. Masharti hayo ni yale yanayohitaji uthibitisho wa watu waliomo katika "Timu ya Kampeni". Kwa maelezo haya ni dhahiri kuwa, kifungu cha 7 kilirekebishwa na kupitishwa na Bunge.

Huu ni utaratibu uliozoeleka wa kutekeleza maelekezo ya Bunge katika Mazingira ambayo Bunge linakaa kama Kamati ya Bunge Zima. Katika hatua hii, Wabunge wanaweza, kupitia Kanuni ya 86(II) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007, kupendekeza mabadiliko katika Muswada. Endapo Waziri ataafiki mapendekezo ya Mbunge yeyote,atamjulisha Mwenyekiti na Mwenyekiti akiridhia atamuelekeza Mbunge aliyetoa mapendekezo asome maelezo anayotaka yaingizwe kwenye Muswada. Ikiwa Mbunge aliyependekeza marekebisho hayo hana maelezo mahsusi, Mwenyekiti atamuagiza Katibu wa Bunge ashirikiane na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuweka maneno au Kifungu kinachoweka masharti yenye maudhui aliyopendekeza Mbunge. Mwenyekiti atawahoji Wabunge kama mapendekezo yakubaliwe au la, wakikubali basi waandishi watakwenda kuandika kifungu kwa namna ambayo inatafsiri nia na uamuzi wa Bunge.

Imetolewa na
OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI

29 Machi, 2010

Pia ukipitia hansard hili jambo linaeleweka.......au?

BTW: Hivi wewe Chenge pamoja na ndondo zako zote hizo.........ilikuwaje ukatuingiza mikengeni (mikataba mibovu na manunuzi ya hovyo) namna ile............yaani naendelea kuridhika kuwa wewe ni FISADI kweli kweli.............damn
 
Wote hapa mnaongea kishabiki sana Hoja ya Dr'.Slaa ina hoja muhimu sana cha msingi hapa kama waliongeza kipengele chochote kile
 
Buchanan,Approval itoke wapi sasa? Ujue Tume yetu ya Taifa ya Uchaguzi haina maofisa wake katika ngazi yoyote ile ya chini kama mkoa, wilaya, jimbo au kata. Tumwamini AG wetu. Ni mtu makini sana ingawa sio malaika.

Suala la approval halijaongelewa Bungeni ndugu na ndio hoja ya msingi ya Dkt Slaa! Huoni hapa AG amepiga chenga ya mwili, hakuongelea hata kidogo Schedule of Amendments ambazo hazina mambo ya Approval, amezungumzia tu hoja za Shellukindo ambazo hazijibu hata kidogo hoja za Dkt Slaa! Nafikiri umeelewa sasa!
 
Maelezo ya AG yamejitosheleza mengine yatabaki kuwa kazi za wanasiasa.
Bravo AG!
Si lazima uwe mwanasheria ili uweze kutunga sheria, lakini ni lazima uwe mwanasheria ili uweze kuandika sheria.

Hebu onesha ni wapi kwenye Hansard mambo ya Approval yaliongelewa Bungeni wakati wanajadili kifungu cha 7 cha Sheria za Gharama za Uchaguzi, 2010, Na. 6 ya 2010, kisha umpe Bravo AG kama atakuwa anastahili!
 
Mimi sioni ni kwa namna gani hoja za Mh Shellukindo na Mh Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge zima kama nilivyoziquote hapo juu zizae maelezo ya watu wanaotakiwa ku - approve campaign team kama nilivyoonesha (in green) hapa chini:
7. (3) For the purposes of subsection (2), "campaign team"
means a group of' persons formed by a candidate in the
nomination process or a contested election for purpose' of
presenting or assisting that candidate in the election campaigns,
who have been approved-
(a) in the case of a Presidential candidate, by the
Registrar;
(b) in the case of a Member of Parliament, by the
District Administrative Secretary; and
(c) in the case of a Councilor, by the Ward Executive
Officer.
Nimekukubali mkuu. Hakuna popote walipokubaliana kuwa pawe na mtu wa ku-approve campain team! Na hii ndiyo hoja ya Dr. Slaa. Wao walichosema ni kudefine campain team kwenye interpretation. Suala la kuapprove, lingepaswa kujadiliwa upya kwani ni ku-establish approving authority ambayo nayo ingewekwa kwenye interpretation na kutaja hao waliowekwa na mwanasheria; inawezekana wabunge wangewakubali au wangewakataa, Kuwaweka hao makatibu tarafa nk hakukujadiliwa na bunge wala kukubaliwa na bunge hata by implication; NI NYONGEZA YA MWANANSHERIA TU.
 
WildCard,
Ni kweli unasema tuache ianze kazi kwanza. Sababu yako ni kuwa kuna sheria nyingi mbovu. Nadhani, huja hapa siyo tu kuwa Sheria hii ni mbovu. Tofauti na Mwanasheria Mkuu wa Serikali alivyojipiga piga hapa, Tatizo ni kuwa dhana ya "Approving Authority", ni dhana mpya kabisa. Vinginevyo, kama Legislative rules zinataka hivyo hakuna sababu ya kuwa na Bunge kwa sababu Serikali ingeliweza kusikiliza tu Bunge, na kwenda kuyaweka maneno wanayotaka kuweka wao. Bunge ndio linalotunga Sheria Siyo Serikali. Hivyo, hakuna ruksa kwa wakati wowote ule dhana mpya kuingizwa kwenye Sheria, vinginevyo Serikali kama inaiingiza dhana mpya ilitakiwa kuleta tena sheria hiyo Bungeni.
Pili, WildCard, kwa mtu anayetaka kujua, madhara yako dhahiri. Kampeni Team ni chombo cha mgombea. Siri zote za ushindi zinatokana na mipango safi na sahihi inayowekwa na Kampeni Team. Hivyo, huwezi kuweka mamlaka ya kuthibitisha Kampeni Team kwa mtu nje ya Mgombea na Chama chake. Vinginevyo, ni dhahiri hapa siyo tu wamefanya bahati mbaya bali wamefanya kwa makusudi kabisa kwa lengo la kudhibiti siyo tu Kampeni Team bali pia kupitia Kampeni Team hizo mikakati yote ya Kampeni ya Wagombea. Hii ni kinyume na dhana ya Demokrasia na ni Tanzania tu ndiyo itakuwa na Sheria ya namna hiyo duniani. Anayefahamu mfano mwingine atumwagie hapa.
Mwanasheria Mkuu ameendelea kupotosha jamii, kwa kutumia utaalamu wake. Nimekaa Bungeni, ni mara ya kwanza jambo kubwa kuingizwa kwenye sheria, na rudia "Kinyemela". Mapambano kuhusu jambo hili ndio kwanza yameaanza, mpaka tutakapopata haki zetu. Ukondoo huu, na kutokufanya utafiti wa kina na au kukubali kila kitu ndio umetufikisha hapa tulipofika. Safari hii tumezinduka na Mwanasheria Mkuu ajue hivyo.

Sheria hii imewahangaisha wabunge wetu wengi akiwemo Dr Slaa. Kifungu kinacholalamikiwa hapa kuingizwa "kinyemela" kina madhara gani? Nilidhani Dr Slaa kwa msimamo wake usioyumba angeisimamia vilivyo sheria hii lakini inaonekana inaelekea kumkwaza tangu mwanzo. Sheria hii na nyingine zote sio msahafu. Tuiache ianze kufanya kazi na kama kutahitajika marekebisho itarudi tena Bungeni. Tuna sheria nyingi mbovu ambazo akina Jaji Nyalali walipendekeza zifutwe lakini bado zipo na sisikiii zikilalamikiwa!
 
Jasusi,
Salaam kutoka Johannesburg. Kwa bahati mbaya wakati Mwanasheria Mkuu alipotoa Tafsiri yake, nilikuwa vijijni, na sasa niko nje ya nchi, lakini nimeona nitembelee Jamvi letu ndio nimekutana na hoja hii. Kutokana na umuhimu wake kwa demokrasia, nimeona nisilaze damu. Hivyo nachangia kama ifuatavyo:-

Hoja yako ni sahihi.i) Hapo ndio kuna utata. Nashukuru kuwa Mwanasheria Mkuu anakiri kuwa "kifungu cha 7(3) kiliongezwa".. Kwa wale wenye kumbukumbu ya Hansard, Kauli ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge Zima (Full House Committee- yaani Bunge inapokaa kama Kamati wakati wa kupitisha kifungu kwa kifungu), ni kuwa Tafsiri hiyo iwekwe kwenye "Definition". Kifungu cha (3) siyo Definition. Hivyo ni dhahiri kuwa Serikali kwa kuweka kifungu cha 7(3) imekwenda kinyume kabisa na maelekezo ya wazi na dhahiri ya Kamati ya Bunge zima. ii) Kama nilivyoeleza awali, kilichokuwa kikijadiliwa ni katikakipengele cha 7 ni "Vikundi vya Sanaa. Kampeni Team imetokea wapi katika kifungu hiki iii) Hata kama ilikuwa lazima kukiingiza, je ilikuwa lazima waondoe mamlaka ya kuamua nani awe kwenye Kampeni Team kutoka kwa mgombea na chama chake na kuyahamisha mamlaka hayo kwa Serikali ( je kutakuwa na fair play ground- wakati wanaopewa mamlaka hayo wanajulikana kuwa makada wa Chama Tawala?).
kifungu kidogo cha (3) kiliongezwa kwenye kifungu cha 7 cha Muswada wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ambapo tafsiri ya msamiati “Timu ya Kampeni” iliwekwa katika kifungu ambacho msamiati huo umetumika. Hii ndiyo sababu kifungu kidogo cha (3) kiliongezwa.

Hapo ndipo penye utata. Kifungu hicho kiliongezwa na nani? Na nani aliyeamua kuwa atakayesimamia "Timu ya Kampeni" ni nani?

 
Buchanan,
Sahihi kabisa. Namshukuru sana aliyeweka Nukuu ya Hansard kwenye Jamvi. Hoja yangu ya msingi ni kuwa " wapi katika mjadala wote uliokuwepo kwenye Kamati ya Bunge zima suala la "Approving Authority" acha kujadiliwa, hata kutajwa na yeyote kati ya wabunge waliokuwa wakichangia hoja hiyo? Hii ndio hoja, na kwa msngi huo ndio maana nimesema kuwa Mwanasheria Mkuu amepotosha ukweli, kwa sababu yeyote anayoijua yeye. Nadhani wana JF wote watapata nafasi ya kuipitia kumbukumbu hiyo ya Hansard, na watajadili kwa kina hali hii inayotia mashaka,

Mimi sioni ni kwa namna gani hoja za Mh Shellukindo na Mh Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge zima kama nilivyoziquote hapo juu zizae maelezo ya watu wanaotakiwa ku - approve campaign team kama nilivyoonesha (in green) hapa chini:
7. (3) For the purposes of subsection (2), "campaign team"
means a group of' persons formed by a candidate in the
nomination process or a contested election for purpose' of
presenting or assisting that candidate in the election campaigns,
who have been approved-
(a) in the case of a Presidential candidate, by the
Registrar;
(b) in the case of a Member of Parliament, by the
District Administrative Secretary; and
(c) in the case of a Councilor, by the Ward Executive
Officer.
 
WildCard,
Kama hoja ni kumwamini "AG" kwa kuwa ni mtu "Makini" basi hatuna sababu ya kuwa na Bunge. Kwanini tupoteze fedha na muda mwingi kuwa na Bunge wakati tuna mtu makini tunayemwamini? Nadhani ni hoja dhaifu sana. Sina hakika kama umefuatilia mjadala wote, na kama umeielewa vizuri sheria hii, dhan ya Tume ya Taifa ya uchaguzi umeitoa wapi?

Buchanan,Approval itoke wapi sasa? Ujue Tume yetu ya Taifa ya Uchaguzi haina maofisa wake katika ngazi yoyote ile ya chini kama mkoa, wilaya, jimbo au kata. Tumwamini AG wetu. Ni mtu makini sana ingawa sio malaika.
 
WildCard,
Ni kweli unasema tuache ianze kazi kwanza. Sababu yako ni kuwa kuna sheria nyingi mbovu. Nadhani, huja hapa siyo tu kuwa Sheria hii ni mbovu. Tofauti na Mwanasheria Mkuu wa Serikali alivyojipiga piga hapa, Tatizo ni kuwa dhana ya "Approving Authority", ni dhana mpya kabisa. Vinginevyo, kama Legislative rules zinataka hivyo hakuna sababu ya kuwa na Bunge kwa sababu Serikali ingeliweza kusikiliza tu Bunge, na kwenda kuyaweka maneno wanayotaka kuweka wao. Bunge ndio linalotunga Sheria Siyo Serikali. Hivyo, hakuna ruksa kwa wakati wowote ule dhana mpya kuingizwa kwenye Sheria, vinginevyo Serikali kama inaiingiza dhana mpya ilitakiwa kuleta tena sheria hiyo Bungeni.
Pili, WildCard, kwa mtu anayetaka kujua, madhara yako dhahiri. Kampeni Team ni chombo cha mgombea. Siri zote za ushindi zinatokana na mipango safi na sahihi inayowekwa na Kampeni Team. Hivyo, huwezi kuweka mamlaka ya kuthibitisha Kampeni Team kwa mtu nje ya Mgombea na Chama chake. Vinginevyo, ni dhahiri hapa siyo tu wamefanya bahati mbaya bali wamefanya kwa makusudi kabisa kwa lengo la kudhibiti siyo tu Kampeni Team bali pia kupitia Kampeni Team hizo mikakati yote ya Kampeni ya Wagombea. Hii ni kinyume na dhana ya Demokrasia na ni Tanzania tu ndiyo itakuwa na Sheria ya namna hiyo duniani. Anayefahamu mfano mwingine atumwagie hapa.
Mwanasheria Mkuu ameendelea kupotosha jamii, kwa kutumia utaalamu wake. Nimekaa Bungeni, ni mara ya kwanza jambo kubwa kuingizwa kwenye sheria, na rudia "Kinyemela". Mapambano kuhusu jambo hili ndio kwanza yameaanza, mpaka tutakapopata haki zetu. Ukondoo huu, na kutokufanya utafiti wa kina na au kukubali kila kitu ndio umetufikisha hapa tulipofika. Safari hii tumezinduka na Mwanasheria Mkuu ajue hivyo.

Dr. Slaa.. labda niongeze kuelewesha tatizo la serikali kwenye hili. Kwenye kesi ya wagombea binafsi mojawapo ya sababu za rufaa ni madai ya serikali kuwa Mahakama imejipa madaraka ya Bunge ya kutunga sheria kwa kitendo chake cha kufuta kipengele cha Katiba kinacholazimisha wagombea kuwa wa vyama vya siasa. Wanasema hili ni jambo kubwa na kuwa chombo pekee cha kutunga sheria ni Bunge na hivyo mahakama ingeweza kutoa hukumu bila kuashiria uwepo wa sheria mpya (yaani kuruhusu wagombea binafsi kabla ya uchaguzi huu mkuu).

Sasa kama hili ni kweli (kwamba chombo pekee cha kutunga sheria ni bunge), serikali hiyo hiyo inakuja na sheria yenye vipengele ambavyo havikujadiliwa wala kupitishwa na bunge na kwa maneneno ya AG vimeongezwa na jopo la wataalamu (ambao si wabunge ni wa serikali). Kwa maneno mengine, nguvu ambayo serikali inaikatalia mahakama kwenye suala la mgombea binafsi inajipa yenyewe kwenye suala la sheria ya gharama za uchaguzi. Hiki kinaitwa "double standard"..
 
Back
Top Bottom