Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Habari nilizopata toka polisi Magomeni ni kwamba ofisi ya mbunge mmojawapo wa Manispaa ya Kinondoni imevunjwa na kuibwa kompyuta na nyaraka mbalimbali. Kwa mujibu wa chanzo hicho wizi huo umetokea juzi usiku. Hatahivyo, chanzo hicho ambacho hakikuta kutaja jina kimeeleza kuwa kituo chao kimeelekezwa kuwa taarifa za kina zitatolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari hapo kesho.