Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Yes, Ofisi ya Bunge wanafuata utaratabu. Hatuwezi kuwalaumu.
Hili suala limeonyesha udhaifu wa huu utaratibu...ipo haja ya kuweka idadi ya siku (mfano 7 au 14) ambazo Chama chochote kinatakiwa kitoe taarifa Tume ya Uchaguzi kuhusu kujiondoa/kuondolewa uachama kwa kiongozi/ mgombea yoyote.
Udhaifu huo ndio unaoiwezesha CCM kukaa kimya kwa manufaa ya chama chao.
Lakini hata bila kupewa siku, mbona majimbo ambayo yalipoteza wabunge kwa sababu zozote zile yalitangazwa mara moja? Nadhani CCM hawana haraka kwa sababu hakuna uchaguzi mdogo huko Kishapu. Na kwa kudhania hivyo, wanajikuta katika mazingira ya ajabu kwa kushindwa kutoa taarifa kuwa mbunge wao amejivua uanachama na kupoteza sifa za kuwakilisha jimbo lake.
Labda wataalamu watusaidie, mwenye jukumu la kutaarifu tume ya uchaguzi/bunge kuwa Mbunge X amepoteza sifa za kuwa mbunge kwa sababu kadhaa (Y, X) ni nani? Na kama ni mbunge mwenyewe, hali inakuwaje katika mazingira ya kifo?