Obama kama Karl Peters; Kikwete kama Mangungo wa Msovero

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Sisi sote ni mashuhuda wa historia ya nchi hii kwa kumbukumbu mbalimbali ambazo leo hii zimekuwa kama hekaya kwa vizazi vijavyo.Hali ya uchumi na mfumuko wa bei ukiendelea kushika kasi huku wananchi wakiendelea kuishi chini ya dola moja ya kimarekani.

Tanzania ya leo haina tofauti sana na enzi Za akina Sultani Mangungo wa Msovero,kwa kujiona mwema na kukabidhi ardhi yake kwa wakoloni kwa kupewa shanga na nguo akimini watamsaidia katika kukabiliana na changamoto mbalimbali katika ushindani wa kichifu miaka dahali iliyopita.

Ni bora sana na sultani huyo hakuwa na elimu ya kutosha japokuwa aliongozwa na fikra,kuliko viongozi wetu waliosoma lakini wakashindwa kusoma alama za nyakati na kukabidhi ardhi yetu kwa wageni wanyonyaji huku nchi ikisheheni migogoro mikubwa ya ardhi katika ya wafugaji na wakulima.

Nilishawahi kusema migogoro ya ardhi ndani ya nchi yetu italiangamiza taifa na kuwaacha waliopewa dhamana ya uongozi wakitumbua raha ughaibuni.Hali ya nchi ni tete kwasasa lakini rais wa nchi hana wasiwasi,kazi yake kukwea pipa kwenda kufanya umatonya kwa sifa ya kurudi na kibaba huku nchi ikizidi kuteketea.

Yaliyo jiri leo hii huko Ikwiriri kati ya vita ya wafugaji na wakulima ina dhihirisha hali ya nchi si shwari.Ilipoanzia Babati watu walipuuzia lakini sasa si Ubakuru huko Mbarari pekee bali moto huu unazidi shika kasi pembe zote za nchi.Hali hii inashika kasi kama moto wa petrol huku rais wa nchi akizidi kuwalika wawekezaji kuja kuwamiliksha ardhi yetu kitu ambacho kitaleta mgogoro mkubwa mwingine kama ule uliosababisha vita vya maji maji kushika kasi.

Kinacho sikitisha kwa nchi hii ni ardhi kugawiwa wageni huku nchi ikiwa na uhaba mkubwa wa chakula karibu kila mwaka.Nchi imekosa mwenyewe,kiasi kimuonekano ni kama nasi tumeuzwa tunasubiri kukabidhiwa kwa mnunuzi.

Kitendo cha rais wetu kualikwa kwenye mkutano wa G8,ni lazima tulitafakari kwa kina nini hasa makakati wa weupe hawa na ahadi zao lukuki.Tunashindwaje kukumbukla yaliyopita yaliyo wakuta machifu wetu nasi leo kuingia kwenye mtego ulel ule.Tofauti na wakati ule wakoloni walikuja wenyewe lakini leo tuna wafuata huko huko kwao na kuwakaribisha kuja kuchukuwa hata kile kilichokombolewa na mababu zetu mara baada ya kujitambua walifanya makosa.

Urafiki huu wa mashaka na weupe hawa utatufikisha wapi kama si kujichimbia kaburi letu sisi wenyewe.Tumeona yaliyotokea huko Zimbabwe,si miaka mingi lakini hatuna kumbukumbu zozote,tumekuwa vichwa panzi makamasi yametawala mpaka akili zetu.

Tuna hitaji mapinduzi ya kifikra na kuacha kuwa tegemezi hata kwa shughuli zetu za maendeleo.Jirani zetu wanapiga hatua kubwa kujikomboa kwa kujiendesha wenyewe kiuchumi wakati sisi tumeshika kasi na kuwa taifa omba omba,hali hii mpaka lini?

Ehud Barak alipotubeza kuwa sisi ni irrelevant,tulipiga sana kelele lakini leo yanayojiri ni yale yale aliyoyasemea.Tunaposutwa na kero zetu kwa weupe hawa tunalaani kwa nguvu zote,lakini tuna shindwa kupambana na wakati.Ifike mahali tupige hatua kimaendeleo bila kutegemea misaada ambayo itakuwa kero kwa vizazi vijavyo.
 
Rais wa Marekani ni Balozi wa Marekani Tanzania wote ni Black American. Na tumeshuhudia u-Karl Peters wao Africa (Tanzania). Je, Black American wana moral authority to question history kuhusu wazungu kunyonya waafrica? Kuna tofauti yoyote kati ya mzungu na Black American when it comes to exploiting Africa?
 
Tatizo lako ni kuona unaonewa na unaibiwa kila siku. Kaa na ardhi yako uendelee kuwa masikini milele.

Unachoshindwa kufahaamu ni kuwa na rasilmali sio maisha bora, maisha bora ni unapoweza kuzitumia hizo rasilmali kwa faida. Leo uwe na Ng'ombe elfu, hutaki kuuza mia moja ujenge nyumba nzuri, faida yake nini?
 
Tatizo lako ni kuona unaonewa na unaibiwa kila siku. Kaa na ardhi yako uendelee kuwa masikini milele.

Unachoshindwa kufahaamu ni kuwa na rasilmali sio maisha bora, maisha bora ni unapoweza kuzitumia hizo rasilmali kwa faida. Leo uwe na Ng'ombe elfu, hutaki kuuza mia moja ujenge nyumba nzuri, faida yake nini?

Tuna nufaika nini tangu ardhi yetu ilipouzwa kwa wageni?Hakuna utmwa mbaya kama utumwa wa akili,ukikubali kutawaliwa kifikra basi ujue kila kilicho chako nacho kitatawaliwa.Wasomi tunao wengi tena they doing good in Botswana,Namibia even USA ambao tungekuwa na mfumo mzuri tungekuwa mbali.

Pili marafiki zetu China mbona wao walifanya mapinduzi ya kijani yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi yao ikiwa pamoja na kufanya kazi kama mchwa huku wakithamini ardhi yao kama mainly resources.Umangungo huu utatufikisha wapi kama si kubaki na kauli mbiu za kwenye makabrasha zisizo na tija wala mashiko.
 
Tuna nufaika nini tangu
ardhi yetu ilipouzwa kwa wageni?Hakuna utmwa mbaya kama utumwa wa
akili,ukikubali kutawaliwa kifikra basi ujue kila kilicho chako nacho
kitatawaliwa.Wasomi tunao wengi tena they doing good in Botswana,Namibia
even USA ambao tungekuwa na mfumo mzuri tungekuwa mbali.

Pili marafiki zetu China mbona wao walifanya mapinduzi ya kijani
yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi yao ikiwa pamoja
na kufanya kazi kama mchwa huku wakithamini ardhi yao kama mainly
resources.Umangungo huu utatufikisha wapi kama si kubaki na kauli mbiu
za kwenye makabrasha zisizo na tija wala mashiko.

hakuna cha faida ni migogoro na wenyeji. mfano kapunga!
 
Sisi sote ni mashuhuda wa historia ya nchi hii kwa kumbukumbu mbalimbali ambazo leo hii zimekuwa kama hekaya kwa vizazi vijavyo.Hali ya uchumi na mfumuko wa bei ukiendelea kushika kasi huku wananchi wakiendelea kuishi chini ya dola moja ya kimarekani.

Tanzania ya leo haina tofauti sana na enzi Za akina Sultani Mangungo wa Msovero,kwa kujiona mwema na kukabidhi ardhi yake kwa wakoloni kwa kupewa shanga na nguo akimini watamsaidia katika kukabiliana na changamoto mbalimbali katika ushindani wa kichifu miaka dahali iliyopita.

Ni bora sana na sultani huyo hakuwa na elimu ya kutosha japokuwa aliongozwa na fikra,kuliko viongozi wetu waliosoma lakini wakashindwa kusoma alama za nyakati na kukabidhi ardhi yetu kwa wageni wanyonyaji huku nchi ikisheheni migogoro mikubwa ya ardhi katika ya wafugaji na wakulima.

Nilishawahi kusema migogoro ya ardhi ndani ya nchi yetu italiangamiza taifa na kuwaacha waliopewa dhamana ya uongozi wakitumbua raha ughaibuni.Hali ya nchi ni tete kwasasa lakini rais wa nchi hana wasiwasi,kazi yake kukwea pipa kwenda kufanya umatonya kwa sifa ya kurudi na kibaba huku nchi ikizidi kuteketea.

Yaliyo jiri leo hii huko Ikwiriri kati ya vita ya wafugaji na wakulima ina dhihirisha hali ya nchi si shwari.Ilipoanzia Babati watu walipuuzia lakini sasa si Ubakuru huko Mbarari pekee bali moto huu unazidi shika kasi pembe zote za nchi.Hali hii inashika kasi kama moto wa petrol huku rais wa nchi akizidi kuwalika wawekezaji kuja kuwamiliksha ardhi yetu kitu ambacho kitaleta mgogoro mkubwa mwingine kama ule uliosababisha vita vya maji maji kushika kasi.

Kinacho sikitisha kwa nchi hii ni ardhi kugawiwa wageni huku nchi ikiwa na uhaba mkubwa wa chakula karibu kila mwaka.Nchi imekosa mwenyewe,kiasi kimuonekano ni kama nasi tumeuzwa tunasubiri kukabidhiwa kwa mnunuzi.

Kitendo cha rais wetu kualikwa kwenye mkutano wa G8,ni lazima tulitafakari kwa kina nini hasa makakati wa weupe hawa na ahadi zao lukuki.Tunashindwaje kukumbukla yaliyopita yaliyo wakuta machifu wetu nasi leo kuingia kwenye mtego ulel ule.Tofauti na wakati ule wakoloni walikuja wenyewe lakini leo tuna wafuata huko huko kwao na kuwakaribisha kuja kuchukuwa hata kile kilichokombolewa na mababu zetu mara baada ya kujitambua walifanya makosa.

Urafiki huu wa mashaka na weupe hawa utatufikisha wapi kama si kujichimbia kaburi letu sisi wenyewe.Tumeona yaliyotokea huko Zimbabwe,si miaka mingi lakini hatuna kumbukumbu zozote,tumekuwa vichwa panzi makamasi yametawala mpaka akili zetu.

Tuna hitaji mapinduzi ya kifikra na kuacha kuwa tegemezi hata kwa shughuli zetu za maendeleo.Jirani zetu wanapiga hatua kubwa kujikomboa kwa kujiendesha wenyewe kiuchumi wakati sisi tumeshika kasi na kuwa taifa omba omba,hali hii mpaka lini?

Ehud Barak alipotubeza kuwa sisi ni irrelevant,tulipiga sana kelele lakini leo yanayojiri ni yale yale aliyoyasemea.Tunaposutwa na kero zetu kwa weupe hawa tunalaani kwa nguvu zote,lakini tuna shindwa kupambana na wakati.Ifike mahali tupige hatua kimaendeleo bila kutegemea misaada ambayo itakuwa kero kwa vizazi vijavyo.

Nadhani huu ni upeo mdogo wa kuelewa, tutambue zama hizi ni tofauti kabisa na zama za ukoloni. mahusiano ya sasa kati ya nchi na nchi ni ya kodiplomasia na siyo kama ambavyo tunafikiria. Dunia ya sasa bila mahusiano haya nchi inaweza kujikuta kama iko kisiwani. Ni dhana potofu kuwa Rais kuwalikwa kwenye mkutano wa G8 kuwa ni ukoloni. Hivi angealikwa Mwai Kibaki ama Yoweri Museveni kweli tusingesema unaona sasa hata wazungu hawana imani naye? Hiyo ni ishara kuwa nabii hakubaliki nyumbani. Siasa za majungu, unafiki , fitina ndizo zinazokwamisha maendeleo ya taifa hili. Tumsadie Rais wetu ili katika kukabiliana na maadui wa nchii ambao hawataki kuona serikali ikitekeleza majukumu yake kwa wananchi ilimradi tu eti wengine wapate kuonekana wao ndiyo bora.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais JK
 
Tuna nufaika nini tangu ardhi yetu ilipouzwa kwa wageni?Hakuna utmwa mbaya kama utumwa wa akili,ukikubali kutawaliwa kifikra basi ujue kila kilicho chako nacho kitatawaliwa.Wasomi tunao wengi tena they doing good in Botswana,Namibia even USA ambao tungekuwa na mfumo mzuri tungekuwa mbali.

Pili marafiki zetu China mbona wao walifanya mapinduzi ya kijani yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi yao ikiwa pamoja na kufanya kazi kama mchwa huku wakithamini ardhi yao kama mainly resources.Umangungo huu utatufikisha wapi kama si kubaki na kauli mbiu za kwenye makabrasha zisizo na tija wala mashiko.

Well said mkuu!yaani majitu mengine kama huyo RIBOSOME hata hiyo elimu kidogo aliyo nayo haimsaidii,yeye hata mambo ya msingi kwa taifa ili yeye anaingiza UCCM,ni aibu sana kwa taifa kua na watu kama hawa,hv hao wachukuaji wa ardhi wanaokuja kwa udanganyifu wa uwekezaji tumefaidika nao nini so far?sana sana dalili zimeanza kua mbaya kwa either wanavijiji kupambana na wawekezaji,au watanganyika kwa watanganyika kuuana kwa kugombea ardhi,na ili suala linashika kasi sana,na hata mwaka juzi kama sijakosea wabunge wa Canada walikuja juu kuhusu wawekezaji wa Tanzania kama Barrick wanavyofaidika kupita kiasi kupitia mikataba mibovu tuliyoingia na kuwaacha Watanzania wakibaki kwenye dimbwi la umaskini,kuna madudu mengi sana yanafanywa na serikali kwy suala la ardhi kwa unafiki wa uwekezaji,mfano hai ni mikataba ya kipuuzi ya juzi juzi tu kama ule wa Agrisol Energy ambapo wamepewa 800,000 acres ambazo ni already under cultivation by small farmers ambazo zilikua zina feed local communites,na watu 162,000 watakua displaced kwa upuuzi huo!na upuuzi zaidi ni kua hao Agrisol watakua wanalipa land rent ya (USD 0.11) yaani Tshs 200/ kwa acre na watakua wanalipa council fee ya $ 0.28 yaani Tshs 500/= kwa acres, tena ni per year na legal advisor wa Agrisol oi Masha!huyo RIBOSOME ambae si kua tu ni maskini wa hali bali mpaka akili,ajaribu kusumbua ubongo wake kwa kusoma report kama za Oakland institute organization aone madudu yanayofanyika,sio kuja na mawazo ya kila kitu ni C.c.m vs other political part,huo ni udumavu wa fikra!
 
Nadhani huu ni upeo mdogo wa kuelewa, tutambue zama hizi ni tofauti kabisa na zama za ukoloni. mahusiano ya sasa kati ya nchi na nchi ni ya kodiplomasia na siyo kama ambavyo tunafikiria. Dunia ya sasa bila mahusiano haya nchi inaweza kujikuta kama iko kisiwani. Ni dhana potofu kuwa Rais kuwalikwa kwenye mkutano wa G8 kuwa ni ukoloni. Hivi angealikwa Mwai Kibaki ama Yoweri Museveni kweli tusingesema unaona sasa hata wazungu hawana imani naye? Hiyo ni ishara kuwa nabii hakubaliki nyumbani. Siasa za majungu, unafiki , fitina ndizo zinazokwamisha maendeleo ya taifa hili. Tumsadie Rais wetu ili katika kukabiliana na maadui wa nchii ambao hawataki kuona serikali ikitekeleza majukumu yake kwa wananchi ilimradi tu eti wengine wapate kuonekana wao ndiyo bora.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais JK

Umejikita kwenye propaganda za aina ya Lukuvi zaidi kuliko kujibu hoja za mleta hoja kua Watanzania wanafaidika vipi na rasilimali/ardhi yao kutoka kwa hao wanaojiita wawekezaji wakati ni wachukuaji,na je dalili za mapigano ya kugombania ardhi baina ya wawekezeji na wanavijiji au wanavijiji kwa wanavijiji si kua ni ishara mbaya kwa taifa letu kunakoletwa na ufujwaji na ubakwaji wa rasilimali ardhi unaosababishwa na wachukuaji wanaoletwa na viongozi wetu!jaribu kuconsider issues in positive way rather than dwelling kwenye uchama!
 
Bwana Ribosome Nadhani Si Mtanzania wewe!!!.... Kama hayo unayopost ndo Imani Yako Basi wewe si mt ni nyoka pole kwa Kukuambia Hivyo Lakini wewe huendi Kabisa na Mtazamo wa WanaMageuzi!... Hivi Kweli kabisa UnaUnga Mkono Hatua ya Wageni Kukabidhiwa Ardhi na rasiliimali zetu Ukadhani kuwa Inatufaa!!?????? Nakushangaa Sana.. Kama ni Mtanzania Basi Ni Msaliti No.1
 
Rais wa Marekani ni Balozi wa Marekani Tanzania wote ni Black American. Na tumeshuhudia u-Karl Peters wao Africa (Tanzania). Je, Black American wana moral authority to question history kuhusu wazungu kunyonya waafrica? Kuna tofauti yoyote kati ya mzungu na Black American when it comes to exploiting Africa?

Balozi wa USA Tanzania ni ex army general. What do you expect? This is a strategic mission to them. They really need to get on top of critical energy issues here.
 
Tatizo lako ni kuona unaonewa na unaibiwa kila siku. Kaa na ardhi yako uendelee kuwa masikini milele.

Unachoshindwa kufahaamu ni kuwa na rasilmali sio maisha bora, maisha bora ni unapoweza kuzitumia hizo rasilmali kwa faida. Leo uwe na Ng'ombe elfu, hutaki kuuza mia moja ujenge nyumba nzuri, faida yake nini?

Watu wa aina yako wamesoma lakini hawajaelimika!! Sawa ni bora nikauza baadhi ya ng'ombe wangu halafu nikajenga nyumba lakini hao ng'ombe nitawauza kwa bei ninayotaka mimi na sio anayotaka mnunuzi!! Afadhali nikae na n'gombe wangu na kuishi kwenye tembe mpaka hapo nitakaporidhika kuwa bei nitakayopata kwa kuuza hao ng'ombe italingana na thamani ya hao ng'ombe!! Hawa wakina Mangungo wa leo wanauza nchi yetu bila kujua thamani yake na athari za muda mrefu kwa wananchi zitakazotokana na wao kuwauzia Saudi Arabia maelefu ya ekari za ardhi!! Hatima yake ni kuwafanya wananchi vibarua wa hawa waarabu. Utaratibu mzuri ingekuwa hawa wawekezaji wanakuja na mtaji na wananchi wanatoa ardhi yao na kuingia ubia wa kuzalisha mazao na hiyo ndio ingekuwa win win situation.
 
Nadhani huu ni upeo mdogo wa kuelewa, tutambue zama hizi ni tofauti kabisa na zama za ukoloni. mahusiano ya sasa kati ya nchi na nchi ni ya kodiplomasia na siyo kama ambavyo tunafikiria. Dunia ya sasa bila mahusiano haya nchi inaweza kujikuta kama iko kisiwani. Ni dhana potofu kuwa Rais kuwalikwa kwenye mkutano wa G8 kuwa ni ukoloni. Hivi angealikwa Mwai Kibaki ama Yoweri Museveni kweli tusingesema unaona sasa hata wazungu hawana imani naye? Hiyo ni ishara kuwa nabii hakubaliki nyumbani. Siasa za majungu, unafiki , fitina ndizo zinazokwamisha maendeleo ya taifa hili. Tumsadie Rais wetu ili katika kukabiliana na maadui wa nchii ambao hawataki kuona serikali ikitekeleza majukumu yake kwa wananchi ilimradi tu eti wengine wapate kuonekana wao ndiyo bora.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu mbariki Rais JK

Mkuu Kengemumaji
Kinachogomba hapa siyo hiyo globalisation unayoipigia debe. Ni upeo wa viongozi kuingia kwenye mahusiano yenye faida. Ardhi ni raslimali isiyooza. Uwekezaji unatakiwa umakini na umahiri wa kuangalia maslahi ya wenye mali. Kuingia mikataba isiyo na tija kwa wavuja jasho wenye mali/nchi yao huo ni uhaini. Usultani Mangungo unaozungumziwa hapa ni ukosefu wa umakini katika uwekezaji. Tumeshuhudia madini yetu yanaisha bila mabadiliko ya maisha kwa ajili ya 'mrahaba wa 3%!! unaolindwa hata na sheria za kibepari za kimataifa. Sasa ndugu yangu unachohitaji ni kuona Kenya inahamia Tanzania? Kwa sababu Kenya ndivyo walivyoingia mkenge na kuwaacha raia wengi wakijaa kwenye squarters za KIBERA wakati akina Uhuru na wazungu wachache wakimiliki karibu nusu ya ardhi ya nchi kwa kisingizio kama hiki hapa cha OBAMA- KIKWETE contract. Ndugu yangu hapa Nairobi wasionacho wako jehanam!! walionacho wako peponi. Hasira za wakenya kutaka kugawanyika na mitafaruku ya kikabila chanzo chake ni umiliki wa raslimali hasa Ardhi!!
Afadhali maendeleo ya polepole kuliko haya mabadiliko ya ghafla yatakayopeleka watanzania wengi jehanam na wachache wakishirikiana na wageni kwenda PEPONI. Umesikia mafuta ya TURKANA yanavyoanza kujadiliwa hapa kenya!? hapo wanajaribu kurekebisha makosa yaliyokwisha tokea bila mafanikio! Mambo yameanza hapo TZ wananchi wanapambana na wawekezaji wanaoletwa na wakubwa bila makubaliano na raia!! subiri hilo bomu muone. SULTANI MANGUNGO ATAKAVYOWAUZA NA RASLIMALI ZENU KWA MIJISIFA TU!
 
I am supporting my president 100% tuna ardhi kubwa ipo mapori tu , bora waje walime wanaojua kulima na sisi tujifunze kutoka kwao.

Mkuu uwe unapitia report za tafiti mbalimbali za wataalamu wa ndani na nje ya nchi,maana inaonekana hata ulicho post hauna huakika nacho,sikulaumu kwa ilo,ukisoma post yangu ya juu na ukasoma report ya Oakland ndio utajua kua ardhi wanazopewa ni mapori au lah!unajua ukiwa kimya kwa jambo usilolijua na upumbavu wako unafichika na kuonekana mwenye hekima
 
Tatizo lako ni kuona unaonewa na unaibiwa kila siku. Kaa na ardhi yako uendelee kuwa masikini milele.

Unachoshindwa kufahaamu ni kuwa na rasilmali sio maisha bora, maisha bora ni unapoweza kuzitumia hizo rasilmali kwa faida. Leo uwe na Ng'ombe elfu, hutaki kuuza mia moja ujenge nyumba nzuri, faida yake nini?

Uwezo wako ni mdogo wa kufikiri ukiwa na RASILIMALI unapaswa uzitumie vizuri kama ni mwekezaji asizifaidi yeye mwenyewe tu.USA wana mafuta ila hawayachibi kwa sasa mpaka pale mafuta yatakapokuwa adimu duniani.so hata sisi tunaweza kutunza rasilimali zetu na kuzitumia taratibu kwa faida yetu na si kunufaisha WAHINDI,WAARABU,WACHINA NA WAZUNGU
 
Tatizo lako ni kuona unaonewa na unaibiwa kila siku. Kaa na ardhi yako uendelee kuwa masikini milele.

Unachoshindwa kufahaamu ni kuwa na rasilmali sio maisha bora, maisha bora ni unapoweza kuzitumia hizo rasilmali kwa faida. Leo uwe na Ng'ombe elfu, hutaki kuuza mia moja ujenge nyumba nzuri, faida yake nini?

Hivi wewe Ribosome uko serious unapotetea maamuzi ya kijuha ya kugawa ardhi bure kwa wageni? Yaani wewe unaona ili kuondokana na umaskini, ni bora ardhi ya nchi itapanywe kwa wakoloni? Au una ajenda fulani labda kuona anayesimamia ubaradhuli huo ni 'mwenzenu' hivi anahitaji utetezi? Unapopost uzi, jaribu kupima kwanza uzito wake na fikra za walio weng.
 
Tuna nufaika nini tangu ardhi yetu ilipouzwa kwa wageni?Hakuna utmwa mbaya kama utumwa wa akili,ukikubali kutawaliwa kifikra basi ujue kila kilicho chako nacho kitatawaliwa.Wasomi tunao wengi tena they doing good in Botswana,Namibia even USA ambao tungekuwa na mfumo mzuri tungekuwa mbali.

Pili marafiki zetu China mbona wao walifanya mapinduzi ya kijani yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi yao ikiwa pamoja na kufanya kazi kama mchwa huku wakithamini ardhi yao kama mainly resources.Umangungo huu utatufikisha wapi kama si kubaki na kauli mbiu za kwenye makabrasha zisizo na tija wala mashiko.

Huna ulichonufaika na wala hautonufaika daima ikiwa huzioni fursa zilizokuwepo. Hiyo ardhi yako iliyouzwa iko wapi na nani aliyekudanganya kuwa ardhi imeuzwa? kama kweli imeuzwa, wewe ulikuwa wapi? na ulikuwa unaifanyia nini hiyo ardhi?

Kuwaaalika wawekezaji ni sera ya nchi yeyote isiyo na taaluma na iliyo na taaluma, Tumia fursa kibao zilizokuwepo, ni ipi kati ya fursa zilizopo ulizozitumia wewe? Leo wanakuja watu wa nje kufunguwa makampuni yanayo wa supply hao wanaochimba migodi, kwa kuwa wewe bado umelala, hivi unafikiri uamshwe namna gani zaidi ya kuwekewa wazi kila kitu?

Mnafikiri shirika au kampuni ya kigeni ikija hapa kuwekeza wanakuja wenyewe? kuna taasisi kabisa ya nchi inayoitwa TIC ambayo inashughulikia uwekezaji wote, wa nje na wandani. Unawajuwa walipo?

Kama kukodishwa ardhi katika nchi hii unaona ni muhali ungeanza na kanisa katoliki linalo hodhi ardhi kubwa baada ya Serikali, tena 90% ya ardhi wanayo hodhi kanisa hawaitumii, imekaa tu. Umeshajiuliza hilo? wewe ardhi inayohodhiwa na kanisa inakusaidia nini?
 
Back
Top Bottom