Nzega kwanoga, Kigwangalla alalamikia 'rafu za mapema'

Mkuu ni Nzega sio Igunga

Tuweni makini na watu wasiyo raia wa nchi yetu, sasa mtu anaenda kuzuia watu wasilime zao la biashara, anataka nini mtu huyu? Yeye anagawa pesa, wali na nyama basi! Mwenzake anahamasisha maendeleo ya kilimo cha pamba!

Ila Kigwangalah kweli ni jembe la mapinduzi, mpaka Bashe hakukaliki Dar, ameona aanze kampeni mapema ili kushindana na spidi ya Kigwangalah! Saidi Bagaile achana na siasa za FB, endelea kupeleka maendeleo kwa wananchi tu hawatokusahau wakati ukifika kama utaendelea hivi!

Suala la Bashe na uraia wake tunalifahamu vizuri na wala lisikukoseshe usingizi...huyo atauona Ubunge kama uchi wa mtoto, maana ili awe Mbunge ni lazima JK atoke madarakani kwanza na yeye aweke sawa ishu ya Uraia wake (kitu kitakachochukua miaka 10!)Mara ya kwanza alilazimika kugushi nyaraka zake za Uraia (jinai hii) na sisi tunao ushahidi, ili agombee Uenyekiti wa UVCCM na pia alilazimika kufoji cheti chake cha kuzaliwa (jinai nyingine hii) ili apate fursa ya kugombea UVCCM. Pia alilazimika kugushi cheti cha kuzaliwa cha Mama yake mzazi ili kuhalalisha uraia wa Mzazi wake mmoja na kurahisisha utaratibu wa kupata Uraia kwa njia ya kuukana Uraia wa Baba yake na hapo kukwepa kuingia kwenye utaratibu wa kusubiri miaka 10 ipite kabla hajafikiriwa kuwa raia! Yote haya tunayajua, Kigwangalah acha kuhangaika na huyu Al-shabaab, fanya kazi bhana!

Zul
 
Bashe anadhani kwa kupambana na mtoto wa Rais ugomvi usio na maana yoyote wala chanzo chochote ndiyo atapata sympathy ya watu. Upuuzi mtupu tu
 
Hamis Kigwangalla Facebook status:

"Kuna mtu mmoja anahangaika jimboni Nzega sasa hivi eti anazuia watu wasilime pamba kwa kuwa Mbunge amehamasisha kilimo hicho na watu sasa wameitikia vizuri, na yeye anaogopa wanavyozidi kuongezeka kwa kasi atashindwa kuniangusha kirahisi 2015! Siasa za kipumbavu namna hii hazitomsaidia, atamaliza hela zake bure. Badala ya kuwasaidia wazazi wake na ndugu zake anapita akigawa pesa hovyo. Badala hata ya kujenga nyumba anapita akigawa pesa na ahadi! Badala aanze kurekebisha utata uliogubika uraia wake anahangaika kuanza kampeni mapema hii akipika pilau na nyama!"

Lakini kama ni kweli anawapa watu pesa wasilime zao la biashara, huu sio uhujumu uchumi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom