Nyumba za Kigamboni Kuanza Kuvunjwa

Haki

JF-Expert Member
Jan 14, 2009
356
17
Kuna habari zilizogaa mjini Dar, kwamba nyumba zote zilizojengwa Kigamboni zitaanza kuvunjwa Dec 2009. Uvunjwaji wa nyumba hizo utaikumba nyumba zote zilizojengwa kuanzia ferry, Magogoni mpaka kupita downtown Kigamboni. Kuna nyumba nyingi mpya na nzuri zilizojengwa hivi karibuni. Wananchi wa Kigamboni wameanza kukumbwa na hofu ya kuvunjiwa nyumba zao wakati wowote; wengi wao wakiwa hawajui kama Serikali itawalipa.
Vilevile thamani ya viwanja vya Kigamboni vimepungua ghafla tu baada ya Wananchi wa Kigamboni kugundua mpango wa Serikali wa kuwahamisha. Mwaka 2006 viwanja vya Kigamboni Magogoni vilikuwa vinauzwa kwa wastani wa shilling millioni 25-35; lakini sasa hivi ni kati ya millioni 1-5.

Habari zilizopo mjini ni kwamba, eneo la Kigamboni linatakiwa na Serikali kwa ajili ya kujenga TZ Business Centre.
 
Duh! kama hizi ni habari za kweli nitafilisika! nina kiwanja Kigamboni.
 
Back
Top Bottom