Nyumba ya Sanaa inabomolewa!

Jamani mbona jumba hilo liliisha achana na biashara ya wasanii na usanii?
Mara ya mwisho nilipitia pale palikuwa ni mahali pa mvinyo wa bei mbaya, makutano ya sister-do waendeshao mb na wanabees wa mtaani. Kumuenzi JKN kulifutika tangu awamu ya pili, sema tu wengi wetu inakuwa ni vigumu kulikubali hilo na mpango wa kulipinga hatuna.
Ni kweli jumba hilo limekuwa kijiwe cha masister doo na washabiki wa Arsenal kila jumamosi lakini huwezi kuliadhibu jengo kwa makosa ya utawala.
Ndio yale niliyokuwa nikisema kwamba tulibinafsisha mashirika yetu kuyaadhibu mashirika wakati waliofisadi ni viongozi ambao tunawapa madaraka zaidi. Toka CEO wa shirika lililokufa leo tunampa Uwaziri wa wizara nyeti ya serikali, kweli hii akili?

Sawa kama Nyumba ya sanaa haitumiki ipaswavyo basi zifikiriwe mbinu mpya za kuiwezesha kufanya kazi kifasaha na hao viongozi wake waondolewe kwanza, kisha mipango mipya inayolenga kuinua vipaji na kukuza biashara za sanaa ndio iwe msingi wa kuingia Ubia. Wanaweza weka recording studio hapo nasikia JK kanunua vifaa vya kurekodia, Wafungue maduka ya vinyago na sanaa, Ofisi za wafunzo ya Ujasiliamali ktk biashara, Ajira kama vile shule ya kufundisha maswala ya Art, ku produce TV, music, movie na kadhalika..
 
kuna vitu vinanikeraga sana, eti preserve nyumba ya sanaa for heritage, usiweke mradi wa umeme kihansi, utaua vyura, usipitishe barabara kandokando ya serengeti, utabughudhi wanyama......usipofikiria sana utagundua wazungu wanatuona sisi waafrika kama makumbusho flani hata mahitaji yetu ya kibinadamu yanapimwa katika mtazamo huo.. vunja weka vitu vya maana hao vyura wa kihansi waite wazungu wakaweke huko kwao sisi tunao wakutosha, na hiyo nyumba ya sanaa inafaida gani kwa mtanzania wa kawaida?vitu vyote vinapatikana slipway,makumbusho,bagamoyo hakuna sababu ya kuwa nazo kama uyoga kila sehemu.

Muangalieni na HUYU!!, sidhani kama ni mzima......!!!!!

Mimi nahisi tatizo kubwa tulilonalo ni watu wa kuplani MIJI.

Hiyo wizara ya maendeleo ya makazi ipo hapo kama BOSHENi, maana hakuna sababu ya wahusika kushindwa kufanya mipango ya kuweza kuhamisha mji...

Thamani ya ardi imebaki eneo moja, kwa mfumo wa planning nzuri, mimi nahisi Serikali ingetenga maeneo sehemu hapa hapa Dar es eslaam ( amini usiamini eneo kubwa la DSM bado liko wazi, ingawa ni mkoa mdogo kuliko yote Bara TZ) Kuwa ili ni la SANAA,Hili ni la nyumba za aina flani, hapa hotels, hapa godowns,apartmets za mfumo flani nk nk.

Ardhi bado tunayo kubwa sana, tatizo bado tunataka KUJENGA KILA KITU PALE POSTA.

Serikali ikipima eneo hapa mjini na kuweka criteria flani za ujenzi, basi ardi hiyo kesho yake inapanda thamani hata mara 20, hata kama ni nje ya mji.

Wizara inatakiwa kupima viwanja nje ya City centre na kutoa maelekeze kwa anayetaka kujenga " KUWA KAMA UNATAKA KUJENGA ENEO HILI, UTAJENGA GHOROFA TISA au zaidi na unatakiwa kujenga kwa muda flani, so ingeweza kuweka mfumo wa yule anaeytaka kuwa na kuwanja eneo husika kuwa tayari amejiandaa, hasa maeneo yatakayotengwa kibiashara.

Salamanda ilivunjwa, kesho tutavunja hata ikulu, kwa kuwa tu.... serikali itajenga ingine sehemu... hamna wa kufikiria kuwa keshokutwa tunatakiwa kuwaeleza wajukuu wetu kuwa hapa alikaa rais wa kwanza nk nk.

Marekani wanazo trains za miaka 1800 (late or mid) ambazo zinakarabatiwa na kuwekwa sehemu kwa ajili ya kuingizia pato taifa kwa wanaokuja kuangalia.

LINGINE:
Wachumi wetu ni Vilaza, ingawa ni wazuri sana wa kutoa TAKWIMU, (naomba kama wapo hapa wakubaliane nami) wameshindwa kabisa ku"impose" tax kwenye vyanzo vingine ikiwemo sanaa.Ndo maana leo serikali ya MKWERE, HAIWEZI KUONA UMUHIMU WA SANAA, ILA BANK.

Ukweli sanaa , kama ikiangaliwaqa vizuri, inafukuzana na UTALII katika kuiingizia taifa pato kubwa, maana ina wigo mpana SANAA.

Wao (wachumi wetu) wamekalia kuongeza ushuru ktk, sigara, pombe, magari nk.

tunatakiwa tuwe na maeneo haya kwa kumbukumbu za baadae, ila serikali INATAKIWA SASA KUPANGA JINSI YA KUAMISHA MJI kama ABUJA, Nigeria.

Wa kulaumiwa ni serikali, hasa wateuliwa walioko ardhi kwa kushindwa kuupangilia mji kwa miaka 200 ijao.

Tanzania TUMELAANIKA

Nawasilisha
 
Ujue hata hoteli ya Sheraton wakati inataka kujengwa pale palikua na viwanja vya wazi vya michezo, na kulikua na viwanja viwili vya basketball ambako timu ya Pazi ndio ilikua inafanya mazoezi na vijana wengi walikua wanajifunza mchezo wa kikapu pale bure, michuano ya basket mingi ilikua inafanyika pale kati ya timu za mashirika, jeshi wizara na hata timu ya taifa ya Misri iliwahi kucheza mechi pale na Pazi tena usiku na taa zilikuwepo miaka ile. wakaja wakubwa na sera kama hizi na kukawa na ugomvi mkubwa watu (wanamichezo) wakitetea viwanja vyao ila ikawa bure hoteli ikajengwa, Nyerere aliwahi sema mtu akikupa wazo la kipuuzi na akijua wewe unajua ni la kipuuzi na ukalikubali atakudharau maisha. What is happening ti TZ?

Teke:

Kwanini prime locations ni zilezile alizoacha mkoloni?
 
Teke:

Kwanini prime locations ni zilezile alizoacha mkoloni?
Zakumi,
Mkoloni alijua kuwa DSM ina ardhi bwerere. Kwa hiyo master plans zake zilikuwa zina maeneo mengi tupu na kwa hakika tungezifuata hizo plans tusingekuwa na msongamano tulio nao hivi sasa. Tukubali kuwa sisi hatujui kupanga. Wewe ukijenga kibanda chako cha biashara mahali na umefanikiwa na mimi nitajitahidi kujenga hapo hapo next to you tushindanie wateja badala ya kufikiria kuwa nikianzisha kibanda changu elsewhere nitavutia wateja wapya na labda kuwa na mafanikio makubwa zaidi. Some years back I visited Casablanca, Morocco. The place reminded me of Dar, but what the king did to avoid congestion, he built the new Casablanca away from the old city and all the social activities, like hotels, movies, restaurants are in the new Casablanca where the old Casa has remained a port town. We could have done the same with our Dar lakini sisi tumeng'ang'ania kubanana hapo hapo.
 
Zakumi,
Mkoloni alijua kuwa DSM ina ardhi bwerere. Kwa hiyo master plans zake zilikuwa zina maeneo mengi tupu na kwa hakika tungezifuata hizo plans tusingekuwa na msongamano tulio nao hivi sasa. Tukubali kuwa sisi hatujui kupanga. Wewe ukijenga kibanda chako cha biashara mahali na umefanikiwa na mimi nitajitahidi kujenga hapo hapo next to you tushindanie wateja badala ya kufikiria kuwa nikianzisha kibanda changu elsewhere nitavutia wateja wapya na labda kuwa na mafanikio makubwa zaidi. Some years back I visited Casablanca, Morocco. The place reminded me of Dar, but what the king did to avoid congestion, he built the new Casablanca away from the old city and all the social activities, like hotels, movies, restaurants are in the new Casablanca where the old Casa has remained a port town. We could have done the same with our Dar lakini sisi tumeng'ang'ania kubanana hapo hapo.

Jasusi:

Sasa hivi naanza kuwa-convinced kuwa labda nchi inahitaji benevolent dictator. Nimepata bahati ya kufika au kukaa Mwanza, Musoma, Arusha, DSM, Morogoro na miji mingine. Sehemu zenye mitaa ni zile alizoacha mkoloni baada ya hapo ni slums. Na wakita kufanya chochote kizuri wanarudi kubomia kulekule alikoacha mzungu.

Wakati huo huo nchi ina chuo cha ardhil. Sijuhi kwanini nchi inapoteza pesa kusomesha watu ambao hawawezi kutumia ujuzi wao.
 
Wasanii kwanini msipange siku kuandamana kuleta attention ya hili suala.. barua hazina nguvu siiku hizi!
 
  • Thanks
Reactions: Paw
Wasanii kwanini msipange siku kuandamana kuleta attention ya hili suala.. barua hazina nguvu siiku hizi!

Haya ndio matatizo yetu. Suala hili si la wasanii peke yao. Kama vile suala la wastaafu wa EAC si lao peke yao. Mpaka hapo tutakapoona kuwa SOTE tunaathirika na dhuluma anayotendewa mwenzetu hatutafika mbali.

Amandla.....
 
Nyumba ya sanaa wana floor 1 sasa hivi. Baada ya hii joint venture watakuwa na floor 4 kati ya 25 zinazotegemea kujengwa.
Tatizo nini hapa?
 
Nyumba ya sanaa wana floor 1 sasa hivi. Baada ya hii joint venture watakuwa na floor 4 kati ya 25 zinazotegemea kujengwa.
Tatizo nini hapa?

Ghorofa nne wapi katika jengo? Hawatapewa ground floor kwa sababu hiyo ni prime na hawatapewa penthouse kwa sababu hizo hizo. Hawa watabanwa kati ya ghorofa ya kwanza hadi ya 24. Hivi unaamini kweli wakipewa ghorofa ya 11 hadi ya 13 itawasaidia lolote? Sasa hivi eneo lao lina courtyard na parking ya kutosha. Hayo watapata kwenye hilo jengo jipya? Sasa hivi wasanii wanaweza kutumia eneo la nje ya jengo kwa maonyesho yao, hilo nalo litawezekana? Hawa watakatiwa kasehemu kaduchu katika eneo lisilouzika au kupangishika. Kwa namna yeyote ile watakuwa wamedhulumiwa. Ni kama vile aje mtu akuambie anahitaji eneo lako ambako una nyumba ya mbavu za mbwa na atakupata sehemu katika nyumba ya kisasa atakayojenga. Akimaliza unajikuta unapewa chumba cha uani, na ukilalamika unaambiwa kuwa si heri hapo una bati na kuta za saruji! Wajinga kweli ndio waliwao.

Amandla.....
 
Ghorofa nne wapi katika jengo? Hawatapewa ground floor kwa sababu hiyo ni prime na hawatapewa penthouse kwa sababu hizo hizo. Hawa watabanwa kati ya ghorofa ya kwanza hadi ya 24. Hivi unaamini kweli wakipewa ghorofa ya 11 hadi ya 13 itawasaidia lolote? Sasa hivi eneo lao lina courtyard na parking ya kutosha. Hayo watapata kwenye hilo jengo jipya? Sasa hivi wasanii wanaweza kutumia eneo la nje ya jengo kwa maonyesho yao, hilo nalo litawezekana? Hawa watakatiwa kasehemu kaduchu katika eneo lisilouzika au kupangishika. Kwa namna yeyote ile watakuwa wamedhulumiwa. Ni kama vile aje mtu akuambie anahitaji eneo lako ambako una nyumba ya mbavu za mbwa na atakupata sehemu katika nyumba ya kisasa atakayojenga. Akimaliza unajikuta unapewa chumba cha uani, na ukilalamika unaambiwa kuwa si heri hapo una bati na kuta za saruji! Wajinga kweli ndio waliwao.

Amandla.....

Yote uliyoandika ni mambo ya kudhania...

1 kwa 4 in modern building ni win situation.
 
Tanzania hatuna heritage kwenye miji yetu sie?

Kama ni lazima watumie eneo hilo walishindwa nini kubakisha jengo kama lilivyo kwa nje, kisha wakaporomosha hayo maghorofa kwa juu?

Ufundi huo ndio unaotumika nchi za nje kwenye maeneo yaliyo mazuri kwa kibiashara.
 
1 kwa 4 in modern building ni win situation.

Insurgent, why win situation, when the title belongs to you. I tend to think that it is a loose situation. And by the way mijamaa haina hela itachukua loan kujenga hizo ghorofa kwa nini menejment ya nyumba ya sanaa wasijenge wao?

Isijekuwe management ya nyumba ya sanaa walifanya kama siganature yako inavyosema!!!!!
 
Wasanii kwanini msipange siku kuandamana kuleta attention ya hili suala.. barua hazina nguvu siiku hizi!
taarifa sahihi...Nyumba ya Sanaa wameingia ubia na NMB na Mirambo Developers kujenga jengo kubwa la bank pale. patatengwa sehem ndogo kwa jaili ya wasanii. Sr. Jean Pruitt (mwanzilishi) amepambana kuzuia huu mradi lakini ameshimdwa....bila shaka kama unavyoona wabia hapo juu kuna mkono wa RA
 
kuna vitu vinanikeraga sana, eti preserve nyumba ya sanaa for heritage, usiweke mradi wa umeme kihansi, utaua vyura, usipitishe barabara kandokando ya serengeti, utabughudhi wanyama......usipofikiria sana utagundua wazungu wanatuona sisi waafrika kama makumbusho flani hata mahitaji yetu ya kibinadamu yanapimwa katika mtazamo huo.. vunja weka vitu vya maana hao vyura wa kihansi waite wazungu wakaweke huko kwao sisi tunao wakutosha, na hiyo nyumba ya sanaa inafaida gani kwa mtanzania wa kawaida?vitu vyote vinapatikana slipway,makumbusho,bagamoyo hakuna sababu ya kuwa nazo kama uyoga kila sehemu.

Mjepu unasamehewa na jamii kwa vile hujui hata unazungumzia issue gani. Pole sana
 




What is happening to the Nyumba ya Sanaa, also known as Mwalimu Nyerere Cultural Centre, is tragic as the photo above indicates. The quote below on Mwalimu Nyerere's rationale for its establishment makes this demolition much more unbearable! Save Nyumba ya Sanaa - this is it?​

"To ensure sustainability of the arts, Nyerere created opportunities for artists to produce and survive on their own. Despite the fact that there was no clear policy, his speeches were mostly translated as policy directives. From his speeches one could sense his ideas, creativity and passion for art. He established Nyumba ya Sanaa (a house for artists) in 1974, positioning it in the middle of Dar es Salaam. He believed that if it could be efficiently utilised, it would reduce the syndrome of artists needing to beg to donors and the state, which enslaves them" - Vicensia Shule on 'Mwalimu Nyerere: The Artist' in 'Africa's Liberation: The Legacy of Nyerere'

 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom