Ni kweli jumba hilo limekuwa kijiwe cha masister doo na washabiki wa Arsenal kila jumamosi lakini huwezi kuliadhibu jengo kwa makosa ya utawala.Jamani mbona jumba hilo liliisha achana na biashara ya wasanii na usanii?
Mara ya mwisho nilipitia pale palikuwa ni mahali pa mvinyo wa bei mbaya, makutano ya sister-do waendeshao mb na wanabees wa mtaani. Kumuenzi JKN kulifutika tangu awamu ya pili, sema tu wengi wetu inakuwa ni vigumu kulikubali hilo na mpango wa kulipinga hatuna.
Ndio yale niliyokuwa nikisema kwamba tulibinafsisha mashirika yetu kuyaadhibu mashirika wakati waliofisadi ni viongozi ambao tunawapa madaraka zaidi. Toka CEO wa shirika lililokufa leo tunampa Uwaziri wa wizara nyeti ya serikali, kweli hii akili?
Sawa kama Nyumba ya sanaa haitumiki ipaswavyo basi zifikiriwe mbinu mpya za kuiwezesha kufanya kazi kifasaha na hao viongozi wake waondolewe kwanza, kisha mipango mipya inayolenga kuinua vipaji na kukuza biashara za sanaa ndio iwe msingi wa kuingia Ubia. Wanaweza weka recording studio hapo nasikia JK kanunua vifaa vya kurekodia, Wafungue maduka ya vinyago na sanaa, Ofisi za wafunzo ya Ujasiliamali ktk biashara, Ajira kama vile shule ya kufundisha maswala ya Art, ku produce TV, music, movie na kadhalika..