Nyumba ya Mengi Yaungua...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Habari ambazo zinaingia sasa hivi ni kuwa nyumba ya mmojawapo wa wafanyabiashara wakubwa nchini imepata madhara ya moto usiku wa kuamkia leo... moto huo umeteketeza vyumba viwili.. kikiwemo alichokuwa amelala mfanyabiashara huyo.. Taarifa zaidi baada ya muda kidogo.. Polisi wanaendelea na uchunguzi kujua chanzo cha moto huo!!
 
hii sasa ni habari mchanganyiko ! nilidhani upo hapa muda mwingi kuelewa not to put this in politics yakhe !

Hata hivyo asante kwa hiyo breaking nyuz !
 
Hapo ndo watu tunakuamini kaka,
na ile article yako ya jana TanzaniaDaima naona hao jamaa kweli umewashika pabaya...ila ukweli ndo umeshausema ingawa wengi wetu wanawaona hao jamaa kama vile wadogo zake Mungu hivyo hawawezi kuchambuliwa ilhali wao ni washirika wakubwa wa mafisadi...kaka Mungu akuzidishie zaidi na zaidi...
 
hii sasa ni habari mchanganyiko ! nilidhani upo hapa muda mwingi kuelewa not to put this in politics yakhe !

Hata hivyo asante kwa hiyo breaking nyuz !

kada hii habari has so many political implications than tunavyoweza kufikiri. Ingawa hadi hivi sasa hakuna anayehisi hujuma lakini kama unavyojua waswahili wenzetu... nothing happens by accident.. Ile yeye na familia wote ni wazima.
 
hii sasa ni habari mchanganyiko ! nilidhani upo hapa muda mwingi kuelewa not to put this in politics yakhe !

Hata hivyo asante kwa hiyo breaking nyuz !

sema wewe nikisema mie nitaambiwa naharibu threads lakini hii nayo inahusiana vipi na siasa?
 
hapo brazameni hata sijui mkuu lakini hapa ni sawa sawa na kipindi kileee tukiwa tunacheza ule mpira wa BORA LIENDE, longi kichizi shuleni Tanga, yaani ukibutua tu wee usijali wapi unaelekea wee ufuate tu ndio hapa !
 
Nyumba ya tajiri yateketea kwa moto


Na Christina Gauluhanga, Polisi

MOTO mkubwa umezuka ghafla katika nyumba inayomilikiwa na Reginald Mengi (62), ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni za IPP na kuteketeza mali yote iliyokuwemo ndani.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Kanda Maalum Dar es Salaam, Pius Sheka amesema kuwa tukio hilo limetokea jana saa 5 usiku, Kinondoni Hananasif.

Amesema nyumba hiyo ya ghorofa ina vyumba sita ambapo viwili vilivyokuwa ghorofani viliteketea vyote na mali iliyokuwemo ndani.

Chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyoanzia chumba kikuu (Master bedroom) kwenye kiyoyozi.

Moto huo ulizimwa na Kikosi cha Zimamoto cha Jiji kwa kushirikiana na wananchi na thamani ya mali iliyoteketea bado haijafahamika.

Nao, watoto wawili wamekufa na wengine wawili wamejeruhiwa baada ya moto kuzuka ghafla chumbani kwao wakiwa wamelala Manzese Midizini.

Kamanda Sheka amesema tukio hilo limetokea leo alfajiri saa 7 usiku, Manzese Midizini.

Amesema nyumba hiyo ina vyumba tisa ambavyo vinakaliwa na wapangaji ambapo chumba cha mpangaji Getrude Mwiru (40), kiliteketea chote na kusababisha vifo cha watoto hao wa ndugu yake waliokuja jijini wakitokea Dodoma kusalimia.

Amewataja watoto hao kuwa ni Allex Mtenda (7) na mwingine Baraka. Waliojeruhiwa ni Getrude na Farida Brigthon (22).

Majeruhi wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na maiti wamehifadhiwa chumba cha maiti ya Hospitali ya Mwananyamala.

Katika tukio lingine, mtoto Samiha Mohamed (2), mkazi wa Mwananyamala kwa Manjunju amekufa baada ya kushika mlango wa chuma katika kibanda cha biashara kilichopo nje ya nyumba yao.

Kamanda Sheka amesema kuwa tukio hilo limetokea jana saa 1 asubuhi, Mwananyamala.

Amesema mtoto huyo alifikwa na mauti hayo baada ya kushika mlango wa chuma uliokuwa na hitilafu ya umeme katika kibanda cha biashara cha Shaban Hozza.

Maiti wamehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Mwananhyamala na polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi wa tukio hilo.

Naye, mwanaume mmoja ambaye hakuweza kufahamika mara moja jina wala makazi yake anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30 amekufa baada ya kugongwa na gari wakati akivuka barabara ya Bagamoyo.

Kamanda Sheka amesema kuwa tukio hilo limetokea jana saa 1 asubuhi, Basihaya.

Marehemu alikuwa amevaa shati la maua maua na suruali nyeusi.

Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti hospitali ya Mwananyamala.

finito...



Naona ni bahati mbaya tu imetokea ajali hii.
 
kada hii habari has so many political implications than tunavyoweza kufikiri. Ingawa hadi hivi sasa hakuna anayehisi hujuma lakini kama unavyojua waswahili wenzetu... nothing happens by accident.. Ile yeye na familia wote ni wazima.

Mwanakijiji,

unadhani kuungua kwa nyumba ya Mengi kuna mkono wa mtu?

hii nchi nimeanza kuiogopa sasa. siasa imekuwa kila sehemu!
 
nimezungumza na mtu wa karibu na hawahisi ni hujuma ni ajali tu.. ila mitaani itakuwa ni maneno. Hiyo habari ya majira haiko sahihi sana.. siyo nyumba yote imeungua.. at least from what I hear ila vyumba viwili ndiyo vimeungua kikiwemo alichokuwa amelala Mengi...
 
Huu ni mkono wa mtu! Tusubiri tusikie, maana THIS DAY linamilikiwa na Mengi na limekuwa mstari wa mbele katika kuandika maovu ya awamu ya tatu na ya nne. Kabla hatujafikia conclusion tuwe na subira.
 
Tusubiri tu... itakuwa hatari kama kuna mtu anaweza kwenda hadi chumbani kwa Mengi na kuleta tatizo..!!
 
kada hii habari has so many political implications than tunavyoweza kufikiri. Ingawa hadi hivi sasa hakuna anayehisi hujuma lakini kama unavyojua waswahili wenzetu... nothing happens by accident.. Ile yeye na familia wote ni wazima.

Mwanakajiji, dont make me believe what you just said ! Nadhani kuna threads ambazo zina political contents nyingi tu na huwekwa kwenye recycle bin, lakini hii ahhh !

Kama kweli watu tukijizoesha kupindisha sheria basi tusilalamike wao wanaopindisha sheria serikalini maana mambo huanza hivi hivi kuanzia katabia kadogo hadi kanakuwa habit ya mtu !

Lakini ndio viongozi wetu wa kesho nyie hivyo endelezeni ..............
 
Mwanakijiji,

unadhani kuungua kwa nyumba ya Mengi kuna mkono wa mtu?

hii nchi nimeanza kuiogopa sasa. siasa imekuwa kila sehemu!

wee acha tu, si unasikia watu wanasema manji amehusika na kuungua kwa nyumba, jamani inasikitisha watu wanamsahau Mungu wao, akisemwa Manji basi ujue nasikia udi na uvumba ccm kuwa involved, tusubiri tuone !

siasa siku hizi ipo kila sehemu babu, na tena kila mtu mwanasiasa ! na saa nyingine tunajifanya tunajua zaidi ya watu waliokuwepo madarakani, how bad is that !
 
Lakini Manji si ana beef na Mengi...?

Kaka Nyani Taratibu Mkuu!,Maneno yako yananifanya nisisimke.Tungoje kwanza!!!, speculation sio nzuri!.Kauli yako hapa inaweza kuchukuliwa kuwa ni ukweli kwamba Manji kachoma nyumba ya Mengi!.Si unajua tena, Jambo imekuwa kama "Gazeti la Asubuhi" huko nyumbani.We unaandika mambo hayo upo PeachTree lakini yule wa Masaki anaona kauli yako ndio ukweli wa mambo!!
 
Tusubiri tu... itakuwa hatari kama kuna mtu anaweza kwenda hadi chumbani kwa Mengi na kuleta tatizo..!!

Heee,

hata mimi nimeanza kuogopa sasa. Kumbe chumba cha kulala cha Mengi kimewaka moto?

Kazi kweli, Hii inaweza kabisa isiwe accident. Juzi iliandika makala hapa kuwa Mengi ndiye anafadhili upinzani ili agombee urais mwaka 2010. leo hii habari kuwa chumba chake cha kulala kimewaka moto wakati yeye akiwa ndani?

mungu wangu weeeeeeee
 
huu ni UDAKU GRADE "A" ready for shipment to Europe ! Kumbukeni hii habari inapikwa na wapishi hapa JF hivyo mtasikia mengi tu kuhusiana na wanayopika !
 
sasa na hao watoto waliokufa mdizini manzese wametegewa nao au ? kumbe moto wa kwa mengi umeanzia master bedrom kwake, kwenye kyoyozi nae akiwa ndani (sijui?) lakini hapa kuna wataalamu ukidhani walikuwepo mle ndani watatuambia zaidi hapo ndipo habari hii itakuwa UMBEA HIGH QUALITY 5 Star !
 
Back
Top Bottom