Inatia mashaka mtu akachome nyumba kwa siri halafu aache ujumbe wa kujitambulisha! Kama alitaka ajulikane si angekuja mchana?
Kisa hiki kinanikumbusha tukio la wizi kwenye duka moja ambapo mwenye duka alidai kuokota picha iliyodondoshwa na wezi kwenye duka. Nilipofuatilia kwa makini nikagundua kuwa polisi walipofika kwa mtuhumiwa, kwa kuwa walikuwa hawamjui waliamua kuomba albam kwa mkewe na wakachomoa picha moja ambayo iklikuwa ikimuonyesha vizuri. Baada ya kukosa ushahidi, wakaamua kumpa picha hiyo mwenye duka aseme kuwa waliidondosha dukani wakati wa kuiba. Hakika hakimu mwenye busara alikataa kukubaliana na ushahidi huo kwani hakuona sababu ya mwizi kwenda kuiba akiwa na picha kama hiyo tena picha yenyewe ilionekana kupigwa wakati wa arusi yake.
Mimi nilimfuata mwenye duka na kumweleza kuwa kama kweli yeye ni muumini mzuri basi ukweli utakuja kukusuta hapa hapa duniani. Baada ya hakim kutilia mashaka ushahidi huo, jamaa hakuedelea na kesi!
kwani huyu aliyechomewa kubanda cha kuku, si yule Hamisi, aliyekuwa katibu wa CUF na baada ya kuchakachuliwa kabla ya kampeni akajoin CCM?? na hiyo si nyumba yake wala chochote, ni banda tu lililokuwa kwenye nyumba ya jirani yake.. ni kijana mbaba mfyoko sana huyo, anapenda fedha kuliko chochote, ndiye yule aliyemparamia Nape baada ya kutoka kutoa pole that time, yeye na kundi lake wakajipendekezea kikao ili wapate chichote ,thats why wakasema cuf and ccm lao moja Igunga, ni kwa sababu ya huyo mpuuzi wa Nyandekwa. Nape aliwaahihi kuwafanyia makubwa ataporudi kuanza kampeni, sasa hamisi Nape hamuoni wala nini, kaona mwenzie waliomwagiana tindikali kwa uroho wa fedha ya kubandika mabango kapanda ndege kuja DSM, na yeye katupia kuku kiberiti, apate chochote. wewe Toka lini nyumba ikaungua kiasi kile Kuku wakapona na karatasi haikuungua..aende kule bongo amuone jamaa aliyemwagiwa Tindikali.. keshatelekezwa.. ash we unacheza na ccm?
kijana huyu ni mpuuzi, ni msaliti wa CUF, ni kiherehere flan.. akamatwe na kuhojiwa.
Nyumba inaungua lakini karatasi inapona!!
Tafakari Chukua ...
Hii habari imenichekesha sana, sasa leo mzee wa watu wa CUF kapigwa kasema ni CCM , ikabidi vijana wa CUF waje juu maana wameona hii ndoa feki, CCM haina soni piga mpaka wazee...
Shigela anaongea na povu...kavaa jezi ya ukamanda haswa! Heheh!!
Ukitaka fitna nchi hii...