Nyumba inapangishwa ipo kijitonyama

Kitomai

JF-Expert Member
May 21, 2009
1,060
281
Ina vyumba vitatu. Ipo kijitonyama Kisiwani. Ipo vizuri sana. Inapangishwa kwa sh 400,000 kwa mwezi. Maelewano yapo. Wahi usichelewe. Mawasiliano 0784 225 000
 

Attachments

  • DSC06370.JPG
    DSC06370.JPG
    57.2 KB · Views: 143
  • DSC06369.JPG
    DSC06369.JPG
    56.2 KB · Views: 132
  • DSC06368.JPG
    DSC06368.JPG
    33.6 KB · Views: 120
  • DSC06366.JPG
    DSC06366.JPG
    51 KB · Views: 119
  • DSC06361.jpg
    DSC06361.jpg
    31.5 KB · Views: 120
  • DSC06360.jpg
    DSC06360.jpg
    24.9 KB · Views: 110
  • DSC06358.JPG
    DSC06358.JPG
    36.1 KB · Views: 125
  • DSC06357.jpg
    DSC06357.jpg
    34.2 KB · Views: 114
  • DSC06362.JPG
    DSC06362.JPG
    26.6 KB · Views: 104
Ina vyumba vitatu. Ipo kijitonyama Kisiwani. Ipo vizuri sana. Inapangishwa kwa sh 400,000 kwa mwezi. Maelewano yapo. Wahi usichelewe. Mawasiliano 0784 225 000

Vyumba vingapi vya kulala?
 
Kitu kimesimama hiki kwa wale wenye nyumba ndogo changamkeni
 
Subiri niangalie mshahara : 350,000*12= 4,250,000. Less PAYE,NSSF,mh! Anyway,Kodi 400,000*12= 4800,000 /=duh! Nkikopa lak 6 sawa ila mwaka huu sitakula wala kulipa nauli. Sijui nkope? Nimeshtuka sitaki tena,ntakufa kwa presha bure!!
 
Hahahahaha hapo si bora uishi mwenyewe na mama nanihii

mkuu yaani maisha ya bongo ni utapeli mtupu. Hivi hii nchi ina mcha Mungu kweli ukitoa watoto wadogo. Maana vipato na matumizi ya watu haviendani kabisa.
Utashangaa mpangaji wa hiyo nyumba mshahara wake ni 500,000 kwa mwezi na ana mke na watoto wawili na hana biashara nyingine, wife yuko home na jamaa ana gari la kutembelea na anatumia simu tatu zinazouzwa laki sita kila moja.

Hapo ndipo ninachoka kabisa!
 
mkuu yaani maisha ya bongo ni utapeli mtupu. Hivi hii nchi ina mcha Mungu kweli ukitoa watoto wadogo. Maana vipato na matumizi ya watu haviendani kabisa.

Unakuta kalani wa mahakama ya mwanzo amempangia nyumba ndogo hapo bado bili za umeme na maji, chakula, usafiri, vinywaji, kujiremba n.k
 
Unakuta kalani wa mahakama ya mwanzo amempangia nyumba ndogo hapo bado bili za umeme na maji, chakula, usafiri, vinywaji, kujiremba n.k

nchi hii hakuna wala rushwa wakubwa kama watumishi wa mahakama. Nilikuwa najiuliza kila siku kwa nini vijana wengi wanakimbilia kusoma sheria au kwenda kusoma Lushoto chuo cha usimamizi wa mahakama, kumbe wanajua ukitoka huko unanyookewa milele mradi uajiriwe tu. Makarani, mahakimu na majaji nchi hii hakuna msafi hata mmoja.

Kuna mmoja alikuwa pale kimara mahakama ya mwanzo kama hakimu inasemekana kwa siku alikuwa anatoka na pesa nyingi sana. imagine hakimu mahakama ya mwanzo ana nyumba kadhaa hapa mjini za kupangisha, ana simu za nguvu, anaishi kijitonyama kwenye nyumba yake mwenyewe, watoto wake wa kike wanasoma Marian girls bagamoyo-ada kwa mwaka 1.2ml plus na pengine anao wawili au watatu au wako aga khan mzizima. na ana daladala kama nne hivi coaster-Japan, na amenunua zote kwa mkupuo..................... na pay slip yake inasomeka tsh 260000
 
nchi hii hakuna wala rushwa wakubwa kama watumishi wa mahakama. Nilikuwa najiuliza kila siku kwa nini vijana wengi wanakimbilia kusoma sheria au kwenda kusoma Lushoto chuo cha usimamizi wa mahakama, kumbe wanajua ukitoka huko unanyookewa milele mradi uajiriwe tu. Makarani, mahakimu na majaji nchi hii hakuna msafi hata mmoja.

Kuna mmoja alikuwa pale kimara mahakama ya mwanzo kama hakimu inasemekana kwa siku alikuwa anatoka na pesa nyingi sana. imagine hakimu mahakama ya mwanzo ana nyumba kadhaa hapa mjini za kupangisha, ana simu za nguvu, anaishi kijitonyama kwenye nyumba yake mwenyewe, watoto wake wa kike wanasoma Marian girls bagamoyo-ada kwa mwaka 1.2ml plus na pengine anao wawili au watatu au wako aga khan mzizima. na ana daladala kama nne hivi coaster-Japan, na amenunua zote kwa mkupuo..................... na pay slip yake inasomeka tsh 260000

Mnahamrabia jamaa biashara yake ya kupangisha....fungua mjadala mpya wa hiyo topic....issue hapa ni nyumba inapangishwa are u interested or not ....basi!!!
 
Hakuna sheria inayomkataza mtu kuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya kimoja. Nadhani ili halina marumbano. Mtu mmoja anaweza kuwa na vyanzo zaidi ya mia moja vya mapato.
Matharani, kuna mtumishi mmoja wa serikali ambaye naye analipwa mshahara wa sh 500,000. Mtumishi huyu ana duka hapo nyumbani kwake, ana genge la nyanya, vitunguu, matunda na mboga mboga. Amefuga ng'ombe, mbuzi, nguruwe, kuku wa nyama na mayai, ana guest house, ana nyumba moja ya kupangisha ambayo mbele yake ina frem za maduka ambayo nayo anayapangisha. Ana vijibaiskeli vya kusambaza maji kawapatia vijana ajira , ana baba shop ya kunyoa manywele n.k.. Mkewe nyumbani anapika maandazi, vitumbua na chapati anasambaza katika migahawa.Huyu jamaa ana vyanzo visovyopungua kumi ninavyovijua mimi. Huyu ni mtu hodari na mchapakazi kweli kweli. Anatoka mikoa ya kaskazini, anaishi Mbezi ya shamba. Ukienda kumtembelea nyumbani kwake unakutana ana kwa ana na shombo la mifugo kama una-aleji nalo unaweza kuondoka bila kusema bai bai! Lakini yeye na familia yake wamelizoe kama wale jamaa wanaoishi kandokando ya dampo la kigogo. Majira zake hawlipendi hilo shombo wanapenda maziwa,mayai na nyama, maana huyu jamaa kila ifikapo siku kubwa lazima achinje! Wewe una vyanzo vingapi vya mapato? Kama unachokimoja tu cha huko Sirikalini, ushauri wa bure fungua banda la chips mayai hapo mtaani kwenu maana wakazi wa Dar hawapendi wugari! wanataka sana rede medi chips mayai zilizoandaliwa na mafuta ya koreeeeea!
 
Pengine ana vyanzo vingine vya mapato ambavyo ambavyo havipo bayana kwetu.
 
Hakuna sheria inayomkataza mtu kuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya kimoja. Nadhani ili halina marumbano. Mtu mmoja anaweza kuwa na vyanzo zaidi ya mia moja vya mapato.



Matharani, kuna mtumishi mmoja wa serikali ambaye naye analipwa mshahara wa sh 500,000. Mtumishi huyu ana duka hapo nyumbani kwake, ana genge la nyanya, vitunguu, matunda na mboga mboga. Amefuga ng'ombe, mbuzi, nguruwe, kuku wa nyama na mayai, ana guest house, ana nyumba moja ya kupangisha ambayo mbele yake ina frem za maduka ambayo nayo anayapangisha. Ana vijibaiskeli vya kusambaza maji kawapatia vijana ajira , ana baba shop ya kunyoa manywele n.k.. Mkewe nyumbani anapika maandazi, vitumbua na chapati anasambaza katika migahawa.Huyu jamaa ana vyanzo visovyopungua kumi ninavyovijua mimi. Huyu ni mtu hodari na mchapakazi kweli kweli. Anatoka mikoa ya kaskazini, anaishi Mbezi ya shamba. Ukienda kumtembelea nyumbani kwake unakutana ana kwa ana na shombo la mifugo kama una-aleji nalo unaweza kuondoka bila kusema bai bai! Lakini yeye na familia yake wamelizoe kama wale jamaa wanaoishi kandokando ya dampo la kigogo. Majira zake hawlipendi hilo shombo wanapenda maziwa,mayai na nyama, maana huyu jamaa kila ifikapo siku kubwa lazima achinje! Wewe una vyanzo vingapi vya mapato? Kama unachokimoja tu cha huko Sirikalini, ushauri wa bure fungua banda la chips mayai hapo mtaani kwenu maana wakazi wa Dar hawapendi wugari! wanataka sana rede medi chips mayai zilizoandaliwa na mafuta ya koreeeeea!

naona mpaka umebold, yaani biashara ya magenge nayo inaielezea kwa kudefend mpaka unaibold? unadhani hata tume ya maadili ya watumishi wa umma ina inawaangalia watumishi wenye biashara za magenge za mtaji wa sh 50,000 na mabanda ya swine? pathetic.
ni vyema kusoma posts za wengine ukazielewa wanachomaanisha. if you can not analyse, it is better not to comment anything.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom