nyumba inahitaji mwekezaji kariakoo

mendezz2009

Member
Sep 3, 2009
8
0
nyumba ipo kwenye kona karibu na soko la kariakoo! ni sehemu iliyochangamka sana kwa biashara. nyumba za karibu yake kodi kwa kila fremu ni kati ya 300,000 mpaka 700,000 kutegemea na ukubwa wa fremu. nyumba ikishajengwa ina uwezo wa kutoa fremu 10 hadi 18 kutegemea na ramani yake.

masharti yao
1.wanataka pesa ya kujikumu tsh millioni 60 ila maongezi kidogo yapo
2.wanataka wajengewe ghorofa 2 ila wawekewe msingi wa ghorofa 6 mpaka 8 huko juu watamalizia wenyewe muda wowote.
3. wanataka wajengewe kwa mkataba wa miaka 10 mpaka 12 na sio ubia.
4.nyumba ikishakamilika kujengwa ndani ya mwaka 1 wao wanachukua fremu 3 na ghorofa ya pili kwa ajili ya kuishi na sehemu yote iliyobaki atachukua mwekezaji kwa muda wa miaka hiyo 10 ili arudishe pesa yake na kupata faida.

aliye serious aniPM sikuweka namba za simu maana kuna watu wasumbufu sana. dalali naye atafikiriwa
 
kwa hesabu ya haraka haraka tu hailipi. uwape mil.60, ujenge, uwape nusu ya jengo! upangishe vyumba 10 miaka 10! ingekuwa miaka 20 hiv.
 
Back
Top Bottom