Nyumba Imara ni ile yenye msingi imara; Je, Nyerere hakuweza kujenga msingi Imara wa viongozi?

Sasa huo walakini alaumiwe mzazi wako? Leo wewe ukiamua kuwa jambazi licha ya kwamba baba yako kakusomesha na kukuwezesha utasema baba yako ndio wa kulaumu? When do we take our own responsibilities?

Ikiwa hivyo mkuu, basi elewa kwamba mzazi wangu hakunipa malezi na mwongozo ulio bora. Mtoto akizaliwa anakua na almost zero memory (kichwa chake kinakua hakina aina yoyote ya jambo jema au baya). Sasa huo ujumbazi kajifunzia wapi? Inaweza ikawa hajajifunza kutoka kwa mzazi; akawa amejifunza kutoka pengine kwa ndugu, jamaa au marafiki. Hapo napo kuna swali,kwanini huyu mtoto apate nafasi ya kujifunza mambo mabaya kutoka kwa watu wengine? Mzazi wake alikua anafanya nini mpaka iwe hivyo? Kwanini mzazi hakufahamu mapema kwamba mwanae anajifunza mambo mabaya?! Kwa nini mzazi kama aligundua mwanae anaelekea kuwa jambazi, kwanini hakumwelekeza na kumfundisha ubaya wa ujambazi?!?

Hapo ndio linakuja pungufu jingine la Mwalimu; aliwaadhibu na kuwaogopesha sana viongozi wa wakati wake, lakini hakuwaelekeza na kuwafundisha kwanini aliwaadhibu; yaani makosa waliyofanya hao viongozi wake, Mwalimu hakuwafundisha namna ya kuyaepuka na kwanini yalikua ni makosa.
 
Hatujasema kuwa kumkosoa Mwalimu ni kosa. Lakini tusimbebeshe Mwalimu lawama kwa hulka ya wizi aliyo nayo Mkapa, au hulka ya ufisadi aliyo nayo Kikwete. That is all what we are saying. Mwalimu alituwekea misingi ya usawa, Azimio la Arusha, misingi ya maadili, leadership code. Sasa ni nani aliyevifuta hivyo? Mbona sijakusikia unamlaumu lakini eti tu Mwalimu hakutuwekea misingi? Aliweka. Ndiyo, alikuwa na mapungufu yake, lakini hayo unayoyasema si katika mapungufu aliyokuwa nayo Mwalimu. Hapo tutabishana mpaka liyamba.

Mwalimu is one of my role models...lakini katika hili naona alikosea.
Mkuu hao wote ni watoto wa Mwalimu (kwa context ya uongozi)..sasa kama ni watoto wake halafu wanakuwa wezi na mabazazi, tatizo lazima lirudi kwa mzazi wao! Ndio waswahili wakasema "Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo!!


Mkuu kumbe wewe unabishana...mimi siwezi kubishana...nilidhani tunaelemishana na kushindana kwa hoja.
Kama kubishana, umeshinda mkuu!

 
Mwalimu is one of my role models...lakini katika hili naona alikosea.
Mkuu hao wote ni watoto wa Mwalimu (kwa context ya uongozi)..sasa kama ni watoto wake halafu wanakuwa wezi na mabazazi, tatizo lazima lirudi kwa mzazi wao! Ndio waswahili wakasema "Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo!!


Mkuu kumbe wewe unabishana...mimi siwezi kubishana...nilidhani tunaelemishana na kushindana kwa hoja.
Kama kubishana, umeshinda mkuu!

OK, Take the word kubishana away. Tuelimishane. Lakini tusimbebeshe Mwalimu makosa ya hulka za akina Kikwete na Mkapa. That is all that I am saying. Nimeuliza swali: hivi baba yako akikusomesha, akikulea vizuri, lakini hatima yake wewe unageuka kuwa jambazi, tumlaumu baba yako?
 
OK, Take the word kubishana away. Tuelimishane. Lakini tusimbebeshe Mwalimu makosa ya hulka za akina Kikwete na Mkapa. That is all that I am saying. Nimeuliza swali: hivi baba yako akikusomesha, akikulea vizuri, lakini hatima yake wewe unageuka kuwa jambazi, tumlaumu baba yako?

Ndio wa kulaumiwa ni baba yangu!! Hakunilea vizuri. Angenilea vizuri mkuu nisingiweza kuwa jambazi; mimi nimejifunzia wapi ujambazi wakati nimezaliwa sijui ujambazi?!?
 
Ndio wa kulaumiwa ni baba yangu!! Hakunilea vizuri. Angenilea vizuri mkuu nisingiweza kuwa jambazi; mimi nimejifunzia wapi ujambazi wakati nimezaliwa sijui ujambazi?!?
Baba yako kakueleza kwa vitendo. Alikuwa mwadilifu. Alikutunza vizuri. Kakusomesha na kuhakikisha unapata elimu na kazi nzuri. Leo unageuka kuwa jambazi umlaumu tena baba yako? Haya kwa mantiki hiyo, na kwa kigezo cha kuelimishana, katika muktadha huu ni kipi ambacho Mwalimu hakukifanya ambacho kingewafanya Mkapa, Lowassa na Kikwete kuwa viongozi waadilifu?
 
Baba yako kakueleza kwa vitendo. Alikuwa mwadilifu. Alikutunza vizuri. Kakusomesha na kuhakikisha unapata elimu na kazi nzuri. Leo unageuka kuwa jambazi umlaumu tena baba yako? Haya kwa mantiki hiyo, na kwa kigezo cha kuelimishana, katika muktadha huu ni kipi ambacho Mwalimu hakukifanya ambacho kingewafanya Mkapa, Lowassa na Kikwete kuwa viongozi waadilifu?

Mkuu msisitizo wangu ni malezi; Mwalimu hakutoa malezi mazuri kwa hiyo cohort. Sasa siwezi kuanza kukuelimisha juu ya parenting!! In short hakufanya good leadership parenting kwa hiyo cohort!
 
Tuliyo nayo leo ni mapungufu yetu wenyewe, siyo msingi wa Nyerere. Nyerere alifanya kazi yake vizuri sana, tena wakati wa vita baridi. Kikwete amekuwa na kawaida ya kulalamika kwa kila anachoshindwa kuwa hata Nyerere alishindwa bila kuangalia tofauti za mazingira ya kazi. Iwapo Nyerere angekuwa madarakani katika mazingira ya leo, tungekuwa tunakwenda kwa kasi ya mwanga! Hamna kaburu, hamna Mreno, hamna Eastern Block against Western Block, na mengineyo mengi.
 
@Jasusi. Nakubaliana na wewe kwamba taasisi huru na za kidemokrasia zinatengenezwa na sisi wananchi. Lakini sikubaliana na mtazamo wako kwamba Mwalimu hakua na mchango mkubwa ktk kutupatia taasisi imara. Kwangu mimi,licha ya huyu mzee kubakia ni kiongozi mzalendo,mchapa kazi na mwenye kuwapenda watanzania wenzake hilo lilikua moja ya makosa aliyofanya. Na kabla ya kifo chake,akawa anawalalamikia watawala kama sisi wananchi wa kawaida. Hatuwezi endelea kulalamika sasa hivi tupo ktk mchako wa kupata Katiba mpya,turekebishe makosa yetu ya nyuma.
 
@Jasusi. Nakubaliana na wewe kwamba taasisi huru na za kidemokrasia zinatengenezwa na sisi wananchi. Lakini sikubaliana na mtazamo wako kwamba Mwalimu hakua na mchango mkubwa ktk kutupatia taasisi imara. Kwangu mimi,licha ya huyu mzee kubakia ni kiongozi mzalendo,mchapa kazi na mwenye kuwapenda watanzania wenzake hilo lilikua moja ya makosa aliyofanya. Na kabla ya kifo chake,akawa anawalalamikia watawala kama sisi wananchi wa kawaida. Hatuwezi endelea kulalamika sasa hivi tupo ktk mchako wa kupata Katiba mpya,turekebishe makosa yetu ya nyuma.
Lakini alituachia misingi. Azimio la Arusha lilikuwa ni msingi kama vile declaration of independence na bill of rights ulivyokuwa msingi wa Wamarekani.
Akaenda mbali zaidi akatuwekea leadership code. Mfanyibiashara asiwe kiongozi wa wakulima na wafanyikazi. Huo ulikuwa ni msingi. Sasa wewe ulitaka afanye nini? Baada ya kuondoka mamlakani hakuwa na mamlaka tena. Angeamua kukaa kimya, lakini kwa kadri alivyokuwa anaona mambo yanakwenda mrama hakusita kupaaza sauti yake kuwatahadharisha viongozi na watawaliwqa. How much more could he have done?
 
Mkuu msisitizo wangu ni malezi; Mwalimu hakutoa malezi mazuri kwa hiyo cohort. Sasa siwezi kuanza kukuelimisha juu ya parenting!! In short hakufanya good leadership parenting kwa hiyo cohort!
Labda sijakuelewa. Unaposema Mwalimu hakutoa malezi mazuri una maana gani? Yaani mfano wa ufisadi Mkapa aliuiga kutoka ofisi ya Mwalimu? Naomba unielimishe kwa hili. Kwa mtazamo wako, kama wewe ungekuwa ni Mwalimu, ungefanya nini ili kuhakikisha hatutakuwa na Mkapa aliye fisadi au Kikwete na Lowassa? Naomba unisaidie katika hili.
 
Tuliyo nayo leo ni mapungufu yetu wenyewe, siyo msingi wa Nyerere. Nyerere alifanya kazi yake vizuri sana, tena wakati wa vita baridi. Kikwete amekuwa na kawaida ya kulalamika kwa kila anachoshindwa kuwa hata Nyerere alishindwa bila kuangalia tofauti za mazingira ya kazi. Iwapo Nyerere angekuwa madarakani katika mazingira ya leo, tungekuwa tunakwenda kwa kasi ya mwanga! Hamna kaburu, hamna Mreno, hamna Eastern Block against Western Block, na mengineyo mengi.

Huoni kama ni dhaifu kwa huyo aliemlea na kumfunda Kikwete!? (hapa naomba nieleweke simtetei Kikwete wala cohort yake)
 
Lakini alituachia misingi. Azimio la Arusha lilikuwa ni msingi kama vile declaration of independence na bill of rights ulivyokuwa msingi wa Wamarekani.
Akaenda mbali zaidi akatuwekea leadership code. Mfanyibiashara asiwe kiongozi wa wakulima na wafanyikazi. Huo ulikuwa ni msingi. Sasa wewe ulitaka afanye nini? Baada ya kuondoka mamlakani hakuwa na mamlaka tena. Angeamua kukaa kimya, lakini kwa kadri alivyokuwa anaona mambo yanakwenda mrama hakusita kupaaza sauti yake kuwatahadharisha viongozi na watawaliwqa. How much more could he have done?

Mkuu hivyo vitu vingekuwa vimewekwa kupitia misingi imara hakika yasingetokea yaliyotokea Zanzibar (Azimio la Zanzibar); hizo leadership codes hadi leo zingekua zinafanya kazi na kuheshimiwa!!

Kumkataza tu mfanyabiashara hasiwe kiongozi wa wakulima na wafanyakazi bila kueleza sababu ya mfanyabiashara huyo kutokuwa kiongozi wa hilo kundi, hakutoshi!! Mwalimu mzuri ataenda zaidi ya kukataza; kukataza kunaweza kumfanya unaemkataza akubali akiwa mbele yako,lakini ukiondoka tu anafanya yale uliyomkataza kwavile haelewi kwanini anakatazwa!!
 
Labda sijakuelewa. Unaposema Mwalimu hakutoa malezi mazuri una maana gani? Yaani mfano wa ufisadi Mkapa aliuiga kutoka ofisi ya Mwalimu? Naomba unielimishe kwa hili. Kwa mtazamo wako, kama wewe ungekuwa ni Mwalimu, ungefanya nini ili kuhakikisha hatutakuwa na Mkapa aliye fisadi au Kikwete na Lowassa? Naomba unisaidie katika hili.

Naomba kwanza nikuulize jambo moja kabla sijakujibu. Ukiwa kama mzazi, ukamwona mtoto wako wa kiume akivuta bangi kwenye backyard kwa siri, utamfanya nini huyo mtoto?
 
Naomba kwanza nikuulize jambo moja kabla sijakujibu. Ukiwa kama mzazi, ukamwona mtoto wako wa kiume akivuta bangi kwenye backyard kwa siri, utamfanya nini huyo mtoto?
Hili ni swali zuri. Nikimwona mwanangu anavuta banngi kwenye backyard, nitamwita, nitamkanya na pia nitampa lecture juu ya madhara ya uvutaji bangi na kinachoweza kumtokea huko mbele. Lakini hatimaye ni yeye mwenyewe anayepaswa kufanya uamuzi. Na tukiichukulia dhana hiyo kuhusu Mwalimu na Mkapa, Mkapa ameanza kuiba baada ya kifo cha Mwalimu. Mwalimu alijua Lowassa ni fisadi akamwita pale Msasani akamwambia hafai kuwa rais wetu. Kikwete yeye alipigwa kijembe kwamba hajakomaa. Kwa mantiki hiyo, Mwalimu kama mzazi alitimiza wajibu wake. Ilitupasa na sisi tumsaidie, hasa baada ya Mkapa kubainika kuwa tapeli, tusiwarudishe hao watoto wahalifu mamlakani. Lakini ndipo tukapendezwa na tabasamu la Kikwete tukampa nchi. Na leo tunajuta na tunajaribu kumlaumu Mwalimu.
 
Mkuu hivyo vitu vingekuwa vimewekwa kupitia misingi imara hakika yasingetokea yaliyotokea Zanzibar (Azimio la Zanzibar); hizo leadership codes hadi leo zingekua zinafanya kazi na kuheshimiwa!!

Kumkataza tu mfanyabiashara hasiwe kiongozi wa wakulima na wafanyakazi bila kueleza sababu ya mfanyabiashara huyo kutokuwa kiongozi wa hilo kundi, hakutoshi!! Mwalimu mzuri ataenda zaidi ya kukataza; kukataza kunaweza kumfanya unaemkataza akubali akiwa mbele yako,lakini ukiondoka tu anafanya yale uliyomkataza kwavile haelewi kwanini anakatazwa!!
Hapa bado hujaeleza una maana gani kwa kusema "misingi imara." Leadership code ilikuwepo. Aliyeiondoa ni Mwinyi na genge lake la CCM. Tukawekewa Azimio la Zanzibar. Viongozi wakaanza kutuna matumbo na kufisidi nchi. Sasa ulitaka Mwalimu afanye nini zaidi ya hapo? Badala ya kuwalaumu walioondoa hiyo misingi, hata kama haikuwa imara, unamgeuzia kibao Mwalimu. OK, tuseme wewe ni Mwalimu. Umeongoza nchi kwa miaka 23 unaona ni wakati mwingine aingie mamlakani, umeshaweka leadership code, anayekufuata wanakubaliana kiujanja ujanja, katika chama hicho hicho kilichounga mkono azimio la Arusha na leadership code, kuviondoa huku wakipiga makofi na kusema wanakwenda na wakati. Hebu niambie wewe katika hali hii ungefanyaje?
 
Huoni kama ni dhaifu kwa huyo aliemlea na kumfunda Kikwete!? (hapa naomba nieleweke simtetei Kikwete wala cohort yake)
Nadhani lawama yako ungeielekeza kwa mtu asiyehusika kwani jambo unaloongelea hapa linahusu kufutika kwa miiko ya uongozi iliyoachwa na Nyerere na kufutwa na Mwinyi.
 
Hili ni swali zuri. Nikimwona mwanangu anavuta banngi kwenye backyard, nitamwita, nitamkanya na pia nitampa lecture juu ya madhara ya uvutaji bangi na kinachoweza kumtokea huko mbele. Lakini hatimaye ni yeye mwenyewe anayepaswa kufanya uamuzi. Na tukiichukulia dhana hiyo kuhusu Mwalimu na Mkapa, Mkapa ameanza kuiba baada ya kifo cha Mwalimu. Mwalimu alijua Lowassa ni fisadi akamwita pale Msasani akamwambia hafai kuwa rais wetu. Kikwete yeye alipigwa kijembe kwamba hajakomaa. Kwa mantiki hiyo, Mwalimu kama mzazi alitimiza wajibu wake. Ilitupasa na sisi tumsaidie, hasa baada ya Mkapa kubainika kuwa tapeli, tusiwarudishe hao watoto wahalifu mamlakani. Lakini ndipo tukapendezwa na tabasamu la Kikwete tukampa nchi. Na leo tunajuta na tunajaribu kumlaumu Mwalimu.

Exactly, kama ulimfunda vyema mwanao na yeye kuelewa somo, hakika hatavuta bangi tena. Lakini akivuta bangi, basi ujue mwanao hakuelewa somo vizuri...alijifanya kuelewa ili ukuridhishe kwamba ameleewa. Na hapa ndipo mzazi alieweka misingi imara kwa mwanae anapopimwa.

Huyo Mkapa hakuelewa mafundisho ya Mwalimu; na huyo Lowasa hakuelewa pia mafundisho ya Mwalimu; Kikwete nae hakuelewa alivyoambiwa hajakomaa.

Hapa ndipo Mwalimu alipokosea, pengine alitumia falsafa sana katika mafundisho yake kiasi kwamba wengi wa wanafunzi wake hawakuelewa somo. Angetumia namna rahisi ya kueleza somo ili wanafunzi wake waliokua hawajakomaa katika falsafa kama alivyokua Mwalimu wamwelewe.
 
Hapa bado hujaeleza una maana gani kwa kusema "misingi imara." Leadership code ilikuwepo. Aliyeiondoa ni Mwinyi na genge lake la CCM. Tukawekewa Azimio la Zanzibar. Viongozi wakaanza kutuna matumbo na kufisidi nchi. Sasa ulitaka Mwalimu afanye nini zaidi ya hapo? Badala ya kuwalaumu walioondoa hiyo misingi, hata kama haikuwa imara, unamgeuzia kibao Mwalimu. OK, tuseme wewe ni Mwalimu. Umeongoza nchi kwa miaka 23 unaona ni wakati mwingine aingie mamlakani, umeshaweka leadership code, anayekufuata wanakubaliana kiujanja ujanja, katika chama hicho hicho kilichounga mkono azimio la Arusha na leadership code, kuviondoa huku wakipiga makofi na kusema wanakwenda na wakati. Hebu niambie wewe katika hali hii ungefanyaje?


Pengine hujaelewa kusudio langu hapa...mimi siko kumlaumu Mwalimu...ninachoongelea hapa ni namna ya kutafuta chanzo cha ubovu wa viongozi tulionao leo; kwanini viongozi wetu leo si waadilifu? kwanini wakati wa Mwalimu walionekana waadilifu? Leo waonekane waovu?

Bado nasisitiza Mwinyi na genge lake hawakumwelewa Mwalimu na hizo leadership codes zake na Azimio la Arusha; wangeelewa kamwe wasingefuta Azimio au kuzikiuka hizo codes. Pia nasisitiza falsafa (aina ya mafundisho aliyokua anatoa Mwalimu pengine yalikua ni magumu mno kwa hao wanafunzi kuelewa; mfano alipomwambia Lowasa hafai kua rais, alieleweka? Au alipomwambia Kikwete hajakomaa, alieleweka?)
 
Nadhani lawama yako ungeielekeza kwa mtu asiyehusika kwani jambo unaloongelea hapa linahusu kufutika kwa miiko ya uongozi iliyoachwa na Nyerere na kufutwa na Mwinyi.

Kwanini Mwinyi aliifuta hiyo miiko kama alielewa maana ya hiyo miiko?
 
Kwanini Mwinyi aliifuta hiyo miiko kama alielewa maana ya hiyo miiko?

Taifa halijengwi na mtu mmoja hujengwa na watu wengi kwa pamoja; Nyerere alikuwa muasisi tu na ilitakiwa waliomfuata nao waendeleze jitihada ili kuimarisha ujenzi wa taifa imara. Unfortunately hatukuwa na akina Nyerere wengi.

Nyerere alitekeleza jukumu la kwake, waliomfuata hawakutekeleza ya kwao; wakajiswagia kiholela bila hata vision.
 
Back
Top Bottom