Nyumba aliyoishi RC wa Iringa Dr. Kleruu kabla ya kuuawa na Said Mwamwindi

Mkuu J.Kuu, watu wanacho sahau ni kwamba kinacho fanyika ni kwamba unangalia nyumba ulijengwa kwa gharama gani, je tangu wakazi/tenants waanze kulipa kodi, je, sum total ya kodi over the years ilishavuka return of investment na kuhanza kuvuna faida au la?

Tukiweka maanani kwamba nyumba hizo zilijengwa zamani sana ni dhahili ziliisha jilipa na faida juu, hivyo Serikali ikiwahuzia wapangaji kwa bei ya kawaida haitapata hasara after all lengo la Serikali lilikuwa ni kuwawezesha wapangaji kumudu kununua nyumba hizo kwa bei ndogo siyo Serikali kupata faida ya ziada.

Zamani hata National Housing Corp iliwahi kuwauzia tenants nyumba, hata Ulaya specifically Uingereza huwauzia wapangaji Council flats bila ya kujali kama mpangaji ni raia au la - what counts ni hela yako tu.

Kwa hiyo suala hili ya nyumba za Serikali tusilivalie njuga sana, hakuna haja ya kulichukulia kama ni suala la uhaini vile, mimi mpaka sasa nina imani kwamba Serikali ilikuwa na nia safi kuwauzia wapangaji nyumba.
Huku mabondeni tu viwanja bei mbaya achilia mbali nyumba sasa iweje kati ya zilizouzwa ziko prime areas zikauzwa bei sio ya soko?
 
Na Mwamwindi kilipata nini baada ya hapo?
CC . RC Mwanza..!
Ni miongoni mwa watu wawili ambao rais Nyerere katika utawala aliidhinishwa wanyongwe. ni Mwamwindi na Muhindi ambaye alimuua mkewe kwa makusudi, eti kisa gari yake ilikuwa imechoka hivyo akataka BIMA wamlipe gari jipya,hiyo alivyokuwa kwenye milima ya huko Nyanda za Juu kusini, alifika kwenye mlima, walikuwa na mkewe kwenye gari, alichofanya akashuka yeye halafu akasukumiza ile gari (mkewe akiwa ndani) kwenye maporomoko. in short Nyerere katika utawala aliidhisha kunyongwa hao wawili tu.
 
Huku mabondeni tu viwanja bei mbaya achilia mbali nyumba sasa iweje kati ya zilizouzwa ziko prime areas zikauzwa bei sio ya soko?

Duu! Kama wangeuza bei ya soko na kujali suala la prine area mbona wote wangetimuka zabaki kununuliwa na wazungu na wahindi, je hilo.ndilo tulikuwa tunataka?
 
Duu! Kama wangeuza bei ya soko na kujali suala la prine area mbona wote wangetimuka zabaki kununuliwa na wazungu na wahindi, je hilo.ndilo tulikuwa tunataka?
Yes govt ingepata pesa nyng na ingeweza jenga zingne thru NHC kwa kuwapa hzo funds sasa niambie ka unaona sawa viongozi wa govt kuishi mahotelini
 
Yes govt ingepata pesa nyng na ingeweza jenga zingne thru NHC kwa kuwapa hzo funds sasa niambie ka unaona sawa viongozi wa govt kuishi mahotelini

Mbona wamekwisha jengewa nyumba nyingine labda kana kuna watu hawataki kuhamia, kana nakumbuka vizuri mwaka jana au juzi kuna Kiongozi alilazimishwa kuhama Hotelini yeye na famila yake kwenda Nyumba za Serikali.

Actually the whole idea ya kuuza nyumba ilikuwa ni kukusanya pesa na kutoka kwa wapangaji alafu Serikali kuongezea pesa nyingine kwa ajili ya kujenga nyumbani nyingine - that was stated from the begining watu wamesahau tu.
 
Nilitaka nishangae tangu lini Mwafrika akawa tayari kuuwa kwa ajili ya kutetea kile anachokiamini yaani itikadi? Sana sana ukisikia Mwafrika kaua ujue ni mapenzi tu hapo hamna kingine, ngono ndiyo namba moja!
Huyu Mzee alikuwa na maekari ya kumwaga ambayo yalikuwa yanalimwa na kuhudumiwa! Then anakuja mtu anakwambia unatakiwa ubaki na ekari moja!! Huwezi kumtwanga risasi hasa ukikumbuka machungu ya kupasua msitu?!
 
HII NIMEIPATA SEHEMU MTOTO WA SAID MWAMWINDI AKIITWA Aman Mwamwindi AKISIMULIA (21/06/2012)
(NOTE: Nimechukua kipande tu sio mahojiano. My Take...mtoto hakudiclose sababu hasa ya mauaji japo alienda kuongea na baba yake siku ile ile ya mauaji)


Je, ni kwanini Dk Kleruu alikwenda nyumbani kwa Mwamwindi siku ya Jumapili na hususan siku ya Krismasi?
Je, yawezekana Mwamwindi na Dk Kleruu walikuwa na ugomvi mwingine kabla ya tukio?
Kuna waliokuwepo na wanasimulia kana kwamba ilikuwa ni jana tu. Mmoja wa watu hao ni mwana wa Mwamwindi aitwaye Amani Mwamwindi ambaye ndiye Meya wa Manispaa ya Iringa kwa sasa. Amani Mwamwindi anakumbuka nini juu ya siku hiyo?
MKE wake Mwamwindi alimwona mume wake akichukua bunduki na kusimama dirishani. Mama huyo alidhani mumewe amepanga kwenda kuwinda. Kumbe, Mwamwindi alitokea dirishani na kumwelekea Kleruu, aliyedhani Mwamwindi angetoka nje kwa kupitia mlangoni.
Basi, Mwamwindi akamlenga Mkuu wa Mkoa kichwani. Dk. Kleruu alinyosha mikono juu na kuomba asemehewe. Mwamwindi alikaa kimya. Kisha akafyatua risasi. Kishindo kilisikika kijijini. Baada ya hapo, kwa mikono yake, Mwamwindi akaubeba mwili wa Mkuu wa Mkoa na kuuweka nyuma ya boneti ya gari alilotumia mkuu huyo wa mkoa.
Mwamwindi alichukua kofia ya pama aliyovaa Kleruu. Akaivaa kichwani na kuanza kuendesha gari hilo hadi kituo cha polisi Iringa. Waliokutana na Mwamwindi njiani walimshangaa akiendesha gari hilo la Mkuu wa Mkoa akiwa amevalia kofia ya mkuu huyo. Hatimaye Mwamwindi akafika kituo cha Polisi.
Akatoka na kwenda mapokezi. Hapo akaripoti tukio kwa kutamka; "Nendeni mkamchukue mbwa wenu nyuma ya gari!".
Tukio lile bado linatuachia maswali? Je, ni kwa nini Dk. Kleruu alikwenda nyumbani kwa Mwamwindi siku ya Jumapili, tena siku ya Krismasi?
Je, yawezekana Mwamwindi na Dk. Kleruu walikuwa na ugomvi mwingine kabla ya tukio? Tuendelee na simulizi hii kama ifuatavyo.
“Niliporudi nyumbani kutoka Ifunda nikazikuta habari hizo mbaya. Nikaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Mzee pale Mshindo. Nikawakuta akina mama wanalia.
“Ilikuwa ni kilio. Hiyo bado ilikuwa, siku ya Krismasi. Nikauliza; kuna aliyekwenda kumwona baba pale polisi? Jibu likawa hapana. Nikaenda moja kwa moja polisi ili nikamwone baba na nimsikie kauli yake.
Nilipofika polisi nikaanza kujieleza kwa askari polisi kuomba ruhusa ya kuongea na Mzee. Wakati nikifanya hivyo mzee nae alisikia sauti yangu. Akatamka; ” Mwanangu huyo, mruhusu niongee nae”. Nikaongea na Mzee.
“Niliweza kuongea na Mzee na kupata picha ya kilichotokea. Niliondoka kurudi nyumbani. Habari zilishasambaa. Hali haikuwa nzuri. Mji wa Iringa ulitulia sana. Halafu ukaja mtikisiko mkubwa. Wazee wengi walioishi mjini na waliokuwa wakilima na Mzee kule Isimani walisombwa na vyombo vya usalama.”
Je, ni kina nani hao? Namwuliza Amani Mwamwindi. Anajibu; “Mzee kama Ibrahim Khalili, Mursali na wengine. Watu kama 30 hivi walisombwa na kupelekwa sehemu mbalimbali za nchi. Kuna waliopelekwa Mwanza, Shinyanga hata Zanzibar. Kwa namna fulani walitenganishwa katika sehemu hizo.”
Je, na wewe ulikumbwa na msukosuko huo? “Ndio, hata mimi nilihojiwa ingawa niliachwa niendelee na kazi zangu. Kumbuka nilikuwa kijana wa miaka 21 tu, na siku ya tukio nilikuwa shambani kwangu Ifunda. Hapa nyumbani kwangu kulikuwa na askari wa FFU muda wote. Katika kuhojiwa kwangu maswali mengine yalikuwa hayana msingi.
Kwa mfano, niliulizwa; Mzee alipokuja hapa kwako kutoka Isimani siku ya tukio alitaka kukwambia nini? Sasa, mimi hakunikuta nyumbani na hatukuongea, nitajuaje alichotaka kuniambia siku hiyo? Anaeleza Amani Mwamwindi, akionyesha kushangaa, hata hii leo.
Je, kwa wakati huo, wewe na familia yenu mlihisi kutengwa na jamii kutokana na kitendo alichofanya Mzee Mwamwindi? Namwuliza. Namwona Amani Mwamwindi akionyesha kuguswa sana na swali hili.
“Tulikuwa na wakati mgumu sana kama familia. Kibaya zaidi kwetu ilikuwa ni kuingia kwenye uhasama na ndugu wa jamaa ambao wazee wao walisombwa na vyombo vya usalama na kwenda kusikojulikana.
“Kwao waliamini kama isingekuwa Mzee wetu Mwamwindi kufanya tendo lile, basi, wazee wao wangebaki salama na kuendelea na shughuli zao za kilimo. Hivyo basi tulisakamwa na wengine ambao ni ndugu zetu.”
Mlifanyaje kuikabiili hali hiyo? “Tulifikia uamuzi mimi niende Dodoma kwenye gereza alikokuwa Mzee Mwamwindi. Niende nikamjulishe baba juu ya hali iliyotokea huku nyumbani. Kwamba tuna uhasama na jamaa wa waliosombwa na vyombo vya dola.
Nilipata kibali cha DC hapa Iringa. Kibali cha kwenda kumwona Mzee kule Dodoma. Nilipofika Dodoma nikaonana naye. Tukazungumza. Nikamwambia shida ya nyumbani. Alisikitika sana.
Akaniuliza; “Sasa tufanyeje?”. Nikamshauri aandike barua kwenda kwa Nyerere kumwomba atusaidie. Baba aliandika barua siku hiyo hiyo. Alimwandikia Nyerere kumwambia na kumhakikishia kuwa ni yeye Said Mwamwindi na si mtu mwingine yeyote aliyehusika na tendo alilofanya; kumpiga risasi na kumuua Kleruu.
Barua ile ilifika kwa Nyerere, na haukupita muda mrefu, wazee wale wakulima wa Isimani waliachiwa huru na kurudishwa Iringa. ”
Je, hali ya uhusiano na waliowachukia ilibadilika na kuwa njema baada ya wazee hao kurudi Iringa? Namuuliza Mzee Amani Mwamwindi.
“Ndio, kabisa. Hali ikawa shwari. ” Je, wazee wale wakulima wa Isimani walirudi na kuendelea na kazi zao za kilimo?
“Niseme kuwa walirudi Iringa wakiwa wameathirika kisaikolojia. Kuna ambao hawakutaka kabisa kurudi tena Isimani. Baadhi yao hawakuishi muda mrefu, walifariki. Sijui nini kiliwatokea.”
Je, unafikiri Iringa ingekuwaje kama tukio lile la siku ya Krismasi mwaka 1971 lisingetokea?
“Naamini kabisa, Iringa isingekuwa kama ilivyo sasa. Ingeendelea sana. Unajua kulikuwa hakuna mahala pengine katika nchi hii ambapo kulikuwa kunazalishwa mahindi kushinda Isimani.
“Mzee na wenzake walilima ekari nyingi sana. Naamini wangelima zaidi. Walianza kujijenga na hata waliunda ushirika wao. Tukio lile lilisimamisha kasi ya kilimo Isimani. Ni kama laana fulani vile, maana, tangu wakati ule mvua zimekuwa za taabu Isimani,” anasema Mzee Amani Mwamwindi. Kisha namwuliza tena.
“Nilifika pale nyumbani kwenu Isimani, nikaona mnara wa kumbukumbu ya Dk. Kleruu, kwanza nilifikiri ni kumbukumbu ya Mwamwindi. Je, unajisikiaje kuona nyumbani kwenu kuna mnara wa kumbukumbu ya Dk. Kleruu na si ya baba yenu?”
“Mimi naona ni sawa kabisa kwa mnara ule kuwa pale”. Ananijibu Mzee Amani Mwamwindi huku akionyesha kuchangamka. Anaendelea.
“Unajua hata Nyerere alipofika Isimani wakati fulani aliuliza; ” Hivi huu mnara ni wa kumbukumbu ya Dk. Kleruu au Said Mwamwindi?” Nyerere alikuwa na maana yake.” Ananiambia Mzee Amani Mwamwindi. Kuna kitu anataka kufafanua, anasita. Namwacha aendelee kutafakari.
 
Mbona wamekwisha jengewa nyumba nyingine labda kana kuna watu hawataki kuhamia, kana nakumbuka vizuri mwaka jana au juzi kuna Kiongozi alilazimishwa kuhama Hotelini yeye na famila yake kwenda Nyumba za Serikali.

Actually the whole idea ya kuuza nyumba ilikuwa ni kukusanya pesa na kutoka kwa wapangaji alafu Serikali kuongezea pesa nyingine kwa ajili ya kujenga nyumbani nyingine - that was stated from the begining watu wamesahau tu.
Kabla Magesa hajamwagwa fuatilia alikuwa anakaa wapi
 
Duu! Kama wangeuza bei ya soko na kujali suala la prine area mbona wote wangetimuka zabaki kununuliwa na wazungu na wahindi, je hilo.ndilo tulikuwa tunataka?

..mbona sasa hivi wao wanapangisha au kuuza kwa wahindi na wazungu?
 
halafu hizi story za mwamwindi na dr .kleru kipindi hiki ndio zimeshika kasi kweli sijui kwann?
 
halafu hizi story za mwamwindi na dr .kleru kipindi hiki ndio zimeshika kasi kweli sijui kwann?

..kuna mambo ya udini-udini.

..lakini ukifuatilia hii habari utaona kwamba Mwamwindi alikuwa na matatizo ya akili.

..mtu wa aina gani anaweza kumuua binadamu mwenzake halafu akampakia kwenye gari, akazunguka na mwili wa marehemu maeneo mbalimbali, na baadaye kuupeleka mwili wa marehemu polisi na huko akautukana na kuukejeli mwili wa marehemu!!!
 
Wewe ndo unayepotosha. Toka lini mkuu wa mkoa akaenda oparesheni peke yake, na gari la ofisi, bila walinzi hata dereva!!!!

Fikiria mara mbili kabla ya kuubishia ukweli

Mkuu wakati ule wa mwalimu maRC na maDC walikuwa hawatembei Na jeshi kama ilivyo Sasa.Na Kwa sababu ya Mwandindi ndio unaona maRC Na maDC wanalindwa sana.
 
..kuna mambo ya udini-udini.

..lakini ukifuatilia hii habari utaona kwamba Mwamwindi alikuwa na matatizo ya akili.

..mtu wa aina gani anaweza kumuua binadamu mwenzake halafu akampakia kwenye gari, akazunguka na mwili wa marehemu maeneo mbalimbali, na baadaye kuupeleka mwili wa marehemu polisi na huko akautukana na kuukejeli mwili wa marehemu!!!

JokaKuu msipindishe ukweli.Udini umetoka wapi hapo? Hivi mtu yeyeto Yule aje nyumba kwako Au Sehemu yako ya kazi akuletee dharau Au akudhalilishe mbele ya familia yako utakubali kweli? Afadhali nife nimesimama kuliko kuisha nimepiga magoti.
Hata kama hukubaliani Na maamuzi yake lakini mpe haki yake.
 
JokaKuu msipindishe ukweli.Udini umetoka wapi hapo? Hivi mtu yeyeto Yule aje nyumba kwako Au Sehemu yako ya kazi akuletee dharau Au akudhalilishe mbele ya familia yako utakubali kweli? Afadhali nife nimesimama kuliko kuisha nimepiga magoti.
Hata kama hukubaliani Na maamuzi yake lakini mpe haki yake.

..hapa JF tunajuana. Sasa mimi kuna wakati niliona wadini-dini fulani wakitetea na kusifia mauaji haya.

..mimi napinga unyanyasaji na udhalilishaji. Lakini hata siku moja siwezi kusifia mauaji yale.

..matendo ya Mwamwindi baada ya mauaji yale yanatia mashaka kama alikuwa ni mzima kiakili.

..mwisho, tuwe waangalifu na kauli zetu. Kuna familia(Kleruu n Mwamwindi) zilizopoteza wapendwa
wao.

NB.

..Kama una familia jiepushe na mambo ambayo yanaweza kusababisha ukakosa fursa ya kuilea na kuitunza familia yake.
 
..kuna mambo ya udini-udini.

..lakini ukifuatilia hii habari utaona kwamba Mwamwindi alikuwa na matatizo ya akili.

..mtu wa aina gani anaweza kumuua binadamu mwenzake halafu akampakia kwenye gari, akazunguka na mwili wa marehemu maeneo mbalimbali, na baadaye kuupeleka mwili wa marehemu polisi na huko akautukana na kuukejeli mwili wa marehemu!!!
Yaani Mimi bado naona kama vile hii movie wala si tukio la kweli!! Daaah Mwamwindi huyu jamaa ni mtu wa aina yake sijawahi sikia!
 
Alikua akimmegea demu wake akamwonya jamaa akamweka ndani kwa kutumia cheo, sasa jamaa alivyotoka akaamua liwalo na liwe, maamuzi ya mkuu wa kaya kua jamaa auawe alijayajutia baada ya kupata store kamili
 
Back
Top Bottom