Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
- Thread starter
- #21
Rev. Kishoka:
Ideologically mpaka sasa sioni mnachopigania ni nini? CHADEMA ambao wanajifanya kuwa ni wa mkondo wa kuria, wafuasi wao mashuhuri hapa JF ni wajamaa wa kutupwa.
Hivi kuna principle gani katika harakati zenu? Hivi CCM wakiweza kuizima au kuifanyika kazi UFISADI, mtakuwa na kitu gani cha kuzungumza?
Let's face it. Critics wengi wa CCM mko brankrupty ki-ideas kama CCM yenyewe. Enlight me if I were wrong.
Zakumi,
Kwa sasa hivi sipigi baragumu la Ideology bali ni kuhusu Principle ambazo tunazo ambazo zimepuuziwa. Si suala la CHADEMA versus CCM au CUF versus CCM, bali it is about Doing Right things versus doing wrong things.
Tanzania tunahitaji tubadilishe attitude, na hili ni Taifa zima na si CCM pekee. Zitto kato wito kwa Watanzania kubadilisha mazoea na kuanza khoji vitu.
Hata kama CHADEMA au CUF wakiingia madarakani na Watanzania wakaendeleza libeneke kama tuliloliendeleza na CCM< hatutapata maendeleo kupitia falsafa ya Ubepari au Soko Huria.
Kukwama kwa Tanzania kwenye tope si kuhusu Itikadi au Sera, bali ni kukosekana kwa mwamko wa kufanya lile lililo sahihi.
Angalia Mizengo Pinda analia kuwa Uongozi ni mbaya na dhaifu, yeye ndiye mkuu, na badala ya kubadilisha mwelekeo ili kuwajibisha watu wawe wachapa kazi, anaishia kulalamika kama sisi Wananchi.
Angalia Kikwete, analia hajui chimbuko la umasikini wetu, kama Rais wa nchi, lakini hajafanya lolote la mwamko kuamsha mbegu mpya ya kutaka uwajibikaji.
Swala sasa hivi si Ujamaa au Ubepari, bali ni kufuata sheria, kanuni, maadili, kuwajibika na ufanisi.