VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Blandina Nyoni aliyetangazwa kusimamishwa kazi na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda bado yuko kazini.Ziara yangu ya 'kiintelijensia' Wizarani hapo asubuhi ya leo imebainisha hayo.Nikijifanya ni mtu mwenye 'appointment' na msimamishwa huyo ili nimletee nyaraka zake toka kwenye Kampuni yetu ya Uwakili,nilielezwa kuwa ingawa Nyoni hapatikani ofisini tangu tarehe ya tamko la Waziri Mkuu,bado anaendelea kufanya kazi zake zinazoambatana na posho na marupurupu stahiki,akiwa nyumbani kwake au mahali popote pengine.
'Hatakiwi kuonekana hapa Ofisini ili vuguvugu la mgomowa Madaktari liishe' alieleza mmoja wa wasaidizi wa Nyoni. Imebainika kuwa hadi leo,si Nyoni wala Mtasiwa(Mganga Mkuu wa Serikali-Deo Mtasiwa) aliyepokea barua rasmi ya kusimamishwa kazi.Madaktari na watanzania kwa ujumla wamefanywa mazuzu? Mwenye masikio na asikie...
'Hatakiwi kuonekana hapa Ofisini ili vuguvugu la mgomowa Madaktari liishe' alieleza mmoja wa wasaidizi wa Nyoni. Imebainika kuwa hadi leo,si Nyoni wala Mtasiwa(Mganga Mkuu wa Serikali-Deo Mtasiwa) aliyepokea barua rasmi ya kusimamishwa kazi.Madaktari na watanzania kwa ujumla wamefanywa mazuzu? Mwenye masikio na asikie...