Nyongeza ya Mishahara Kwa wafanyakazi wa Taasisi za Umma

analysti

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
729
612
Ndugu wana JF, naomba kama kunamtu yoyote mwenye updates za mchakato wa nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa taasisi za umma anipatie!!
 
WAZIRI WA KAZI KAPUYA ALITANGAZA MISHAHARA HIYO KABLA YA BAJET KAMA IFUATAVYO:

macinkus

"VIWANGO VIPYA VYA MISHAHARA"

Viwango vya zamani vya kima cha chini kisekta pamoja na viwango vipya sasa vimetangazwa vitumike ni:
kutoka Sh65,000 hadi Sh130,000) kwa sekta ya kilimo;
meli za mizigo na za abiria (Sh225,000 hadi Sh450,000);
meli za uvuvi za ndani (Sh196,000 hadi Sh392,000);
makuli na wajenzi wa meli (Sh300,000 hadi Sh600,000).

Wafanyakazi wa majumbani wapo katika makundi matatu;
wanaofanya kazi kwa mabalozi (Sh90,000 hadi Sh180,000),
wanaowafanyia maofisa wanaolipiwa huduma hiyo na waajiri wao (Sh 80,000 hadi Sh160,000) na wengine (Sh65,000 hadi 130,000).

Wanaofanya kazi mahotelini (Sh150,000 hadi Sh300,000),
hoteli za kitalii na hoteli za kati (Sh100,000 (200,000)
na hoteli ndogondogo, baa, nyumba za wageni na migahawa (Sh80,000 hadi Sh160,000).

Katika sekta ya madini, upande wa migodi mikubwa, wafanyakazi wanalipwa Sh350,000 na hivyo watatakiwa kulipwa Sh700,000, lakini waajiri wanaoshughulika na machimbo ya chumvi au chokaa waliwekwa kwenye kundi la viwanda vidogo kwa kuwa uwezo wao ni mdogo.

Viwanda vidogo itakuwa kutoka Sh80,000 hadi 160,000,
ulinzi binafsi, kampuni za kigeni (Sh105,000 hadi Sh210,000)
na kampuni nyingine (S 80,000 hadi Sh160,000),

Sekta ya biashara na viwanda inayojumuisha mabenki, kima cha chini kilikuwa Sh150,000 na sasa kitatakiwa kiwe Sh300,000.

Sekta ya afya imegawanywa katika makundi mawili yanayohusisha hospitali kubwa na maduka ambayo mshahara wake wa kima cha chini ni Sh120,000 na sasa itakuwa Sh240,000)

Na hospitali ndogo na zahanati (Sh80,000 hadi Sh160,000).

Wafanyakazi wa huduma za anga mshahara wa kima cha chini ulikuwa Sh350,000 na sasa utakuwa Sh700,000,

Wasafirishaji wa mizigo (clearing and forwarding) ilikuwa Sh230,000 na sasa itakuwa Sh460,000),

Mawasiliano ya simu Sh 300,000 (600,000), usafiri wa nchi kavu (makondakta na madereva) sh 200,000 (400,000).

Wafanyakazi katika vyombo vya habari wamegawanywa katika makundi mawili. Katika kundi linalohusisha vyombo vinavyojiendesha kibiashara, mshahara wa kima cha chini utabadilika kutoka Sh 250,000 hadi Sh500,000.

Vyombo vingine ni vile visivyojiendesha kibishara kama vile vinavyorusha matangazo ya kidini, ambavyo kima cha chini kilikuwa ni Sh150,000 na sasa kitakuw
"
 
unazungumzia mishahara serikalini siyo!
mishahara bado imefichwa, waziri alisema hapendi kuitangaza ili wafanyabiashara wasitumie huo mwanya vibaya (makubaliano na TUCTA). ila alisema ni nyongeza kubwa kupita za huko nyuma.

Mwenye data alete
 
unazungumzia mishahara serikalini siyo!
mishahara bado imefichwa, waziri alisema hapendi kuitangaza ili wafanyabiashara wasitumie huo mwanya vibaya (makubaliano na TUCTA). ila alisema ni nyongeza kubwa kupita za huko nyuma.

Mwenye data alete

do you believe these guys? look on this; the 2010/11 budget salary has an increased of 38%, in which its biggest part will be used for recruiting new workers (According to Hawa Ghasia). The Govt expect to employ 49,000 new workers (hii ni zaidi ya 10% ya wafanyakazi waliopo). That means hakuna nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa sekta za umma kama ipo ni kidogo sana.
 
Back
Top Bottom