Nyie Bakwata vipi? Eid el fitr mna mwezi wenu, Eid el Hajj mnafuata huohuo wa Kimataifa

Mipangomingi

JF-Expert Member
Mar 16, 2011
2,713
2,058
Kwa kalenda ya Saudia na nchi nyingi kama sio zote duniani ambazo hazina msuguano na ujanjaujanja katika masuala ya Ibada, zitafunga funga ya arafa kesho Jumamosi tarehe 5 Novemba na kuswali idi keshokutwa Jumapili tarehe 6 Novemba 2011. Je Bakwata hata sikukuu hii ya dhulhija mnataka kuwaswalisha watu Jumatatu au hiyo Jumapili kama duniya nzima itakavyoswali? Nakumbuka zamani mlikuwa mnawafungisha watu funga ya arafa wakati mahujaji wanakuwa washamaliza kisimamo cha arafa na kuingiya katika ibada ya swala na kuchinja "فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ" . Then ikaja zama baada ya vituo vya televisheni kufunguliwa na watu kuona live kupitia madishi na siku ya kusimama arafa kuonekana live na kila mmoja, mkawa mnawaambia waislamu wafunge siku arafa, siku inayofuata wasiswali eid ili waswali siku ya tatu yake ambayo kwa bakwata ni tarehe kumi ya mwezi wao wa kitanzania. Jumuiya za Kiislamu zinatoa elimu mbalimbali, naona sasaivi wengi wa waislamu wanafunga siku ya arafa na kuswali eid siku ya pili yake, aidha Kidongochekundu, Jangwani, Masjidi Haqi-Morogoro, Masjid Bukhari, viwanja vya Lumumba, masjid Kibweni na kwengineko Tanzania. Je Bakwata tunawauliza, mwezi wenu ni ule wa Ramadhani tu au Hata huu?
 
Back
Top Bottom