Nyerere: Tusitegemee 'Fedha za nje' kuleta maendeleo

Gagurito

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
5,600
803
Mwaka 1968 katika kitabu chake cha Ujamaa Mwl. J. K. Nyerere alipata kuzungumzia juu ya madhara ya utegemezi wa fedha toka nje! Ktk kitabu hicho alipaswa kunena haya, namnukuu...

Ni jambo la kijinga kuchagua fedha kuwa ndiyo chombo chetu kikubwa cha maendeleo na hali tunajua kuwa nchi yetu ni masikini. Ni ujinga vile vile, kwa kweli ni ujinga zaidi, tukidhani kuwa tunaweza kuondoa hali hii ya unyonge wetu kwa kutegemea fedha za kutoka nje badala ya fedha zetu wenyewe.

Ni ujinga kwa sababu mbili.

1. HATUWEZI KUZIPATA: Nikweli kwamba ziko nchi ambazo zaweza na zapenda kutusaidia. Lakini hakuna nchi moja duniani ambayo iko tayari kutupa misaada au mikopo au kuja kujenga viwanda ktk nchi yetu kwa kiasi cha kuiwezesha nchi yetu kutimiza shabaha zake zote za maendeleo.
2. Misaada na Mikopo vitahatarisha Uhuru wetu. Kujitawala kwa kweli hakuwezekani ikiwa Taifa moja linategemea misaada na mikopo ya taifa jingine kwa maendeleo yake.
MY TAKE:
Tumekua tukishuhudia safari za mara kwa mara za viongozi wakuu wakitaifa nje ya nchi kutafuta wawekezaji pia kuomba msaada, pia tumekuwa tukishudia nchi yetu ikipokea misaada kadhaa kutoka nje kwa malengo ya kuleta maendeleo.

SWALI: Je kwa mwendo huu twaenda vyema? Je tutafikia maendeleo kwa mendo huu?
 
Hazina tija. Tujipange upya!
<br />
<br />
Leo TBC HABARI nimemwona Mustafa Mkulo akisign mkataba wa makubaliano ya fedha za misaada za maendeleo toka kwa Nchi za Korea na Belgium/sweden (*sina uhakika), kwa mwendo huu kazi ipo!
 
<br />
<br />
Leo TBC HABARI nimemwona Mustafa Mkulo akisign mkataba wa makubaliano ya fedha za misaada za maendeleo toka kwa Nchi za Korea na Belgium/sweden (*sina uhakika), kwa mwendo huu kazi ipo!
Kwa hawa vilaza wetu wasio na vision hiyo ndiyo imebaki kazi ya kujisifia.
 
Hakuna kitu Tanzania tulijaliwa kama Nyerere!
<br />
<br />
Kwa Tanzania ya sasa, watu design ya Nyerere ni ngumu kupenyeza katika vyombo vya maamuzi hapa nchini. Ufisadi umetawala uzalendo wetu, tumekua watumwa wa wanasiasa na matajiri..
 
Kwa hawa vilaza wetu wasio na vision hiyo ndiyo imebaki kazi ya kujisifia.
<br />
<br />
Katika kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010, kuna mgombea wa urais toka upinzani alisikika akisema kuwa Rais wa sasa hawezi kuleta Maendeleo na hata maisha bora kama alivyo ahidi coz yeye yupo kimiradi zaidi, kwama anafiti kuwa afisa miradi na sio rais kwan urais waitaji thinking wkt ubwana miradi wataka mtu awe na ujuzi wa field survey na kuomba misaada. Huu mtazamo una'logic ndani yake!
 
Kwa hawa vilaza wetu wasio na vision hiyo ndiyo imebaki kazi ya kujisifia.
<br />
<br />
Kujisifia pasipo performance ni kazi bure! Chamsingi wapunguze safari zisizo na tija na kuomba omba!
 
Back
Top Bottom