Nyerere ndio alisababisha Rushwa, Umaskini, Ufisadi Tanzania

Enough with romantization of Mwalimu.

99% ya watawala wetu leo wote walilelewa na mwalimu hivyo ni uzao wake

kwa hiyo its fair to say matatizo yetu yalianza toka enzi zake na sasa wanaendelea kuruthishana kama ambavyo CCM wanawapitisha watoto wao kuchukua na nafasi na CHADEMA akina mtei kuwaandaa akina Mbowe kututawala

Mimi naona Mwalimu ndio cause ya matatizo yetu yote haya

hakutaka accountability wala transparency kwa hiyo wanasiasa wetu wa leo wanaendeleza yale yale ya mwalimu.

Kama hamuamini Tazama Cabinet imejaa akina nani na wametokea wapi? Mtu kama Mathias Chikawe tazama profile yake utaelewa naongelea nini

Yaani wewe kununua simu,gari na nyumba ya vyumba kadhaa tayari unajiona tajiri na kusahau kabisa kazi kubwa

aliyoifanya Hayati.Mwl.J.K Nyerere ambayo ndio hio hio inayokufanya leo kupata aka ka uhuru ka kuzungumza haya.

Hayati.Mwl J.K Nyerere alifanya kazi kwa unyenyekevu,busara na hekima kubwa

1.kuhakikisha nchi inakuwa salama kwa gharama yoyote.

2.Kuunganisha makabila zaidi ya 124 kuzungumza kwa lugha moja.

3.Kuwandoa watanzania katika fikra za kufanyishwa kazi kama manamba na kuwajengea uwezo wa pamoja katika kazi zao

hasa zile za kilimo,mifugo,uvuvi na viwandani.

4.Kuyabaini mapungufu ya kiutawala mapema na kuyasemea bila woga,hofu au upendeleo wa kundi fulani kwa maana ya

rangi,dini,kabila au sehemu litokako.

Utawala wake Mwl.Nyerere uligubikwa na misukosuko mingi hasa ile iliyotoka nje ya nchi na hata majirani zetu hivyo

mpaka anastaafu Urais tayari mfumo wa dunia ulikwisha zorotesha mambo mengi muhimu na bora ambayo aliyaanzisha

kwa nia njema kwa taifa lake.Hivyo kumlaumu kwa maana ya materils si sawa,sote yatupasa kumkumbuka na kumuenzi

mwalimu kwa kuwa ndiye alikuwa muasisi wa amani ya roho(spiritual) hata kama hakuna kitu mifukoni.

Kaa tena ufikiri kwa kina hii post yako kama ni sawa au si sawa kwa mkuu wetu kama yule aliyetutoka na kutuachia

pengo kubwa kwa ushauri na maelekezo muhimu yanayojitokeza hasa wakati huu wa Dunia ya utandawazi.
 
kwahiyo waliofuata walishindwa, wana shindwa na watashindwa kukabiliana na ufisadi, udin, ukanda, ukabila, mikataba feki, hela za uswisi, elimu za kata na nk kwasababu nyerere alikosea?

Mzee mawazo yako ni kama yangu. Jamaa anataka kutuaminisha kama nyerere ndio chanzo cha huu u.j.i.n.g.a wa akina nchemba? Je nasi tumekubali kuwa masikini sababu nyerere alianzisha? Huo ni umaskini wa mawazo.
 
kutokea alipotuachia ilikuwa rahisi waliofuata kutupeleka kwenye maendeleo ya haraka na imara. ilikuwa waje watu makini na wenye nia ya kuendeleza nchi. resources za nchi ndo za kuiendeleza nchi. yeye aliacha zote. aliacha nchi bikira. leo hii hatuzitumii kutuendeleza wazung, wachna na waarabu wanajichukulia tu. halaf tunamlaumu marehemu
 
Hakuna mtu ambae ameua nchi kama huyo Nyerere.Na haya yanayoendelea ni matunda yake.Kwanza alikuwa mdini mkubwa mpaka wanampa mwanaheri
 
JULIUS NYERERE asilaumiwe, alikwisha sema yeye si malaika hata asifanye makosa, ila alikwisha tuambia "TUACHE YELE MABAYA ALIYOFANYA NA TUCHUKUE NA KUENDELEZA MEMA ALIYO YAANZISHA, lakini alishangaa sana kuona "TUNA ACHA MEMA ALIYO YAANZISHA halafu TUNACHUKUA MABAYA!

Mfano; Kama baba yako alikuwa mlevi lakini akaweza kukusomesha mpaka form 6 kisha akashindwa kukulipia ada ya kujiunga na chuo kwa sababu ya ulevi, lakini baada ya yeye kustaafu kazi akakwambia, "Mwanangu usije kuwa mlevi kama mimi ila somesha wajukuu zangu mpaka chuo kikuu". Wewe pamoja na kipato kikubwa kuliko alichokuwa nacho baba yako, umeamua kukesha kwenye starehe za ufisadi, umalaya, ulevi wa safari zisizo na tija ukashindwa hata kumnunulia mtoto wako wa primary madaftari halafu unaanza kumlaumu baba yako eti hakukusomesha mpaka chuo, huo ni upumbavu na dhambi kubwa ambayo lazima itakutafuna baadaye!

JKN asilaumiwe kwani alijitahidi hata kutuachia nyumba za serikali na viwanda vya kila aina lakini Nkapa na JMK wamevinywa kwa kuendekeza ufisadi!

Wenye mtazamo kama wako wa kumtupia lawama JKN wanajulikana maana walifikiri watafika peponi bila kufa, sasa wanaona kufa hawafi na jehanum inawaita wana anza kumtupia lawama Hayati Mzalendo wa ukweli wa Taifa na watu wake!
 
Nahisi mawazo haya yanasukumwa zaidi na chuki binafsi dhidi ya Hayati baba wa Taifa, Mwl. JK Nyerere; na, kwa kweli chuki hizo hazina msingi wowote.
 
tuachane na longolongo za marehemu. katuacha hai, hatuko vitani, na muundo wa nchi unaoeleweka. tukae chin tupige kazi

Labda ahali yangu utubainishie HAI KWA KITU GANI.

Kumbuka Tanganyika haijawahi kabisa kuwa na ulanguzi toka enzi za ukoloni. Ulanguzi na bidhaa kuadimika madukani na kuwafanya wananchi waache kazi zao kwenda kuhemea chakula katika maduka ya kaya aliviasisi JKN.

Si hilo lakin pia alipopewa nchi toka kwa wakolon mwaka 1961, Thamani ya paund ya UK ilikuwa sawa na 1.20 Shiling ya Tanzania. Je unajua alipoondoka aliiacha vipi.

Lakin kubwa zaidi ni kuiganisha vita kwa kutaka kurejesha rafiki yake Uganda na kuwa hadaa watanzania kuwa wafunge mikanda ya kiuchumi kwa miezi 18. Jiulizeni mpaka anatoweka Duniani aliwahi kutamka kuwa fungueni hiyo mikanda? Na jambo hilo ndio mporomoko mkubwa wa uchumi wa Tanzania mpaka leo.

Kwani waarabu tunasema in order to build something strong, it helps to start with best and possible material. SASA TANZANIA MLIJENGA MSINGI MBOVU WA UCHUMI WENU.
 
Nahisi mawazo haya yanasukumwa zaidi na chuki binafsi dhidi ya Hayati baba wa Taifa, Mwl. JK Nyerere; na, kwa kweli chuki hizo hazina msingi wowote.

SIKU ZOTE UKWELI UNABAKI KUWA UKWELI NA HAUWEZI KUFA HATA SIKU MOJA. nafikiri ni nafasi yako kukanusha kile unachoona si cha kweli kwani JKN ni mwan'Adam na kila mwan'Adam ni mkosefu lakin mbora ni yule mwenye kikiri na kutubia makosa yake.

Sema ukweli usifungwe na umaarufu au udini kichwani mwako.
 
Labda ahali yangu utubainishie HAI KWA KITU GANI. Kumbuka Tanganyika haijawahi kabisa kuwa na ulanguzi toka enzi za ukoloni. Ulanguzi na bidhaa kuadimika madukani na kuwafanya wananchi waache kazi zao kwenda kuhemea chakula katika maduka ya kaya aliviasisi JKN. Si hilo lakin pia alipopewa nchi toka kwa wakolon mwaka 1961, Thamani ya paund ya UK ilikuwa sawa na 1.20 Shiling ya Tanzania. Je unajua alipoondoka aliiacha vipi. Lakin kubwa zaidi ni kuiganisha vita kwa kutaka kurejesha rafiki yake Uganda na kuwa hadaa watanzania kuwa wafunge mikanda ya kiuchumi kwa miezi 18. Jiulizeni mpaka anatoweka Duniani aliwahi kutamka kuwa fungueni hiyo mikanda? Na jambo hilo ndio mporomoko mkubwa wa uchumi wa Tanzania mpaka leo. Kwani waarabu tunasema in order to build something strong, it helps to start with best and possible material. SASA TANZANIA MLIJENGA MSINGI MBOVU WA UCHUMI WENU.
Nyerere alishangaa kuona "MISINGI YA TAIFA" inavunjwa na mafisadi. Mkaondoa Miiko ya Uongozi-kumbuka Hotuba yake ya Mbeya siku ya Mei mosi. Alisema hakuna serikali duniani isiyo kuwa na miiko! Je, serikali yako miiko yake ni ipi? Raisi na Waziri mkuu wote wanasema, "mafisadi hawakamatiki, wala unga hawakamatiki na wala rushwa ni vigumu kuwakamata! Enzi za Mwalimu kitu wasingethubutu!
 
Nyerere alishangaa kuona "MISINGI YA TAIFA" inavunjwa na mafisadi. Mkaondoa Miiko ya Uongozi-kumbuka Hotuba yake ya Mbeya siku ya Mei mosi. Alisema hakuna serikali duniani isiyo kuwa na miiko! Je, serikali yako miiko yake ni ipi? Raisi na Waziri mkuu wote wanasema, "mafisadi hawakamatiki, wala unga hawakamatiki na wala rushwa ni vigumu kuwakamata! Enzi za Mwalimu kitu wasingethubutu!

Siku zote ukitaka kutibu jambo ni vizuri ujue chaanzo chake.

Hebu fikiria ni nani aliyeasisi huko Tanzania. Enzi za Nyerere aliweza kuasisi uhujumu wa uchumi ambao sasa umekoma na kuwa Ufisadi.

Kumbuka kuwa Nyerere alikuwa anaongea mambo ambayo yeye mwenyewe aliya asisi na baadae kumshinda na kuliacha zigo kwa wenzake.

Pasi na shaka hotba hiyo aliitoa baada ya yeye kukimbia urais wa Tanzania. Ama kweli nyani haoni Kund...
 
Inasikitisha sana na pia naamini katika uwazi na ukweli. kila mmoja anahaki ya kuchangia anavyoona inafaa. ushauri wangu ni kwamba kwa kuwa Mwl Nyerere ni marehemu aliyewahi kuwa kiongozi wa taifa letu wa kwanza baada ya uhuru basi yeyote anayetaka kumchambua katika mchango wa ujenzi wa taifa hili ni vema akazungumza kwa ulinganifu na watangulizi wake katika maeneo yafuatayo: -

1. Uwezo wa mapato kama taifa kwa mwaka yalikuwa ni kiasi gani wakati wake na wakati wa watangulizi wake.
2. Mapato hayo yalitokana na aina gani ya uzalishaji katika taifa letu (je ni kilimo, viwanda, madini, uvuvi, utalii n.k).
3. Ukuzaji wa uwekezaji katika viwanda nchini kama serikali (kiasi gani cha viwanda vipya vilianzishwa na serikali).
4. Ujenzi na ukuzaji wa elimu kwa kujenga mashule na vyuo vya elimu za juu kwa umiliki wa serikali.
5. Upanuaji wa huduma ya usafirishaji na mawasiliano kwa kutumia vyombo vya serikali katika bahari, maziwa, mito, Anga, barabarani, reli na mtandao wa mawasiliano kwa kutumia vyombo vya umma.
6. Ushirikwaji wa umma katika tasnia nzima ya ulinzi na usalama wa nchi yetu.
7. Ujenzi wa taifa la tanzania kwa kutuweka kama wamoja bila kuweka tofauti za kidini na kikabila wal kimajimbo.
8. Uhifadhi na usimamizi wa rasilimali za taifa kwa manufaa ya watanzania wote.
9. Usimamizi wa watumishi wa umma na viongozi kwa ujumla katika masuala ya rushwa.
10. Kumlinganisha na watangulizi wake katika suala zima la utaifa na usimamizi wa mali za umma kwa manufaa ya umma au maslahi binafsi.
11. Utegemezi wa wafadhili wa nje, mikopo na wawekezaji wa nje katika miradi ya maendeleo nchini.
12. Suala zima la uchimbaji wa madini, usimamizi wake na mapato yake katika taifa.

Tukijadili katika maeneo haya na mengine mengi yaliyopo, tutakuwa tumepata majibu ya kuhusu Mwl Nyerere katika taifa letu anastahili heshima ipi na siyo kuwa na watu wanakuja hapa JF wakiwa hawana kumbukumbu yoyote ila kumshutumu na kutaka historia imsahau ama imweke kando kwa kukosa uwelewa wa mambo kwa sababu ya cheap politics.

Nawakilisha kwenu wana JF.
 
Labda ahali yangu utubainishie HAI KWA KITU GANI.Kumbuka Tanganyika haijawahi kabisa kuwa na ulanguzi toka enzi za ukoloni. Ulanguzi na bidhaa kuadimika madukani na kuwafanya wananchi waache kazi zao kwenda kuhemea chakula katika maduka ya kaya aliviasisi JKN.Si hilo lakin pia alipopewa nchi toka kwa wakolon mwaka 1961, Thamani ya paund ya UK ilikuwa sawa na 1.20 Shiling ya Tanzania. Je unajua alipoondoka aliiacha vipi.Lakin kubwa zaidi ni kuiganisha vita kwa kutaka kurejesha rafiki yake Uganda na kuwa hadaa watanzania kuwa wafunge mikanda ya kiuchumi kwa miezi 18. Jiulizeni mpaka anatoweka Duniani aliwahi kutamka kuwa fungueni hiyo mikanda? Na jambo hilo ndio mporomoko mkubwa wa uchumi wa Tanzania mpaka leo.Kwani waarabu tunasema in order to build something strong, it helps to start with best and possible material. SASA TANZANIA MLIJENGA MSINGI MBOVU WA UCHUMI WENU.
tunategemea wenye weredi kama wako awe na macho yanayoona wengine wasichokiona, lkn wewe hauko hivyo, unachoongea hakifanani wala kulingana na elimu yako. Unakuwa kama wale jamaa zangu fulani ambao niliwakuta sehemu wanashangilia watu wanaotoana ngeu bila kujua kuwa wale jamaa wanaenda kuitia hasara serikaliBadilika Baru2, elimu ikukomboe kifikra elimu sio kukariri bali kufunguka kichwani. Funguka Mkuu
 
Enough with romantization of Mwalimu.

99% ya watawala wetu leo wote walilelewa na mwalimu hivyo ni uzao wake

kwa hiyo its fair to say matatizo yetu yalianza toka enzi zake na sasa wanaendelea kuruthishana kama ambavyo CCM wanawapitisha watoto wao kuchukua na nafasi na CHADEMA akina mtei kuwaandaa akina Mbowe kututawala

Mimi naona Mwalimu ndio cause ya matatizo yetu yote haya

hakutaka accountability wala transparency kwa hiyo wanasiasa wetu wa leo wanaendeleza yale yale ya mwalimu.

Kama hamuamini Tazama Cabinet imejaa akina nani na wametokea wapi? Mtu kama Mathias Chikawe tazama profile yake utaelewa naongelea nini
Kwa hapo mkuu hatukubaliani. Lazima nyerere alindwe kwa kua alikua mtu mwadilifu sana na mwenye nia njema kwa taifa. Hizi ndude zinazotawala sasa ni kizazi cha nyoka. Naona mwalimu baada ya kuwa mtu mzima ili asije kufa kwa ugonjwa wa moyo, aliona awaachie wananchi wapambane na hizo ndude baada ya kuasisi utawala wa vyama vingi.
 
Enough with romantization of Mwalimu.

99% ya watawala wetu leo wote walilelewa na mwalimu hivyo ni uzao wake

kwa hiyo its fair to say matatizo yetu yalianza toka enzi zake na sasa wanaendelea kuruthishana kama ambavyo CCM wanawapitisha watoto wao kuchukua na nafasi na CHADEMA akina mtei kuwaandaa akina Mbowe kututawala

Mimi naona Mwalimu ndio cause ya matatizo yetu yote haya

hakutaka accountability wala transparency kwa hiyo wanasiasa wetu wa leo wanaendeleza yale yale ya mwalimu.

Kama hamuamini Tazama Cabinet imejaa akina nani na wametokea wapi? Mtu kama Mathias Chikawe tazama profile yake utaelewa naongelea nini

Umetoroka hosipitali ya vichaa wewe. RUDI huko unatafutwa
 
Back
Top Bottom