Nyerere, Mwinyi, Mkapa and Kikwete: Leadership Styles and A Lesson to Learn!

Kwa mujibu wa taarifa za utendaji wa serikali ya CCM. imaonyesha raisi kikwete amefanikiwa sana kuliko maraisi wote waliopita. natoa mifano michache tu hapa kuthibitisha hoja yangu. 1. Wanafunzi wa shule za sekondari kutoka 524.325 mwaka 2005 hadi kufikia wanafunzi 1.884.272 mwaka huu haya ni mafanikio makubwa sana. Wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka 40.719 mwaka 2005 mpaka 166.484 mwaka huu haya nimafanikio makubu sana katka elimu. yapo mambo mengi sana ya mafanikio yaliyo fanywa na kikwete haya hayaonwi na dk slaa nampongeza mbowe kuuona ukweli huu.chazo gazeti la uhuru toleo la leo.

Nikiwa nakubaliana kuwa Kikwete kaongeza nafasi za wanafunzi wengi vyuo vikuu kuliko wakati wowote ule katika Tanzania ukweli ni kwamba kwa idadi ya wanafunzi waliokuwa wanaingia vyuo vikuu 2005 bado ilikidhi mahitaji ya graduate katika uchumi wa Tanzania kwa sasa wahitimu ni wengi na hawana pa kwenda pamoja na degree zao na isitoshe hao graduate hawana quality ya elimu wengi wao wakienda kutafuta kazi waajiri wanajiuliza hawa kweli walimaliza degree kwa lugha nyingine tunazalisha quantity badala ya quality.

Jambo la maana katika nchi na kubwa kuliko vyote iwapo tayari kuna idadi ya wasomi hata wengi wa kawaida ni ajira na mfumuko wa bei kwa Jk alivyoingia mwaka 2005 na kwa idadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu tuliokuwa nao Tanzania jambo muhimu ilikuwa ni utengenezaji wa nafasi za kazi na sio kuanzisha vyuo vikuuu vingi ambayo wanafunzi wakihitimu hawana ajira kwa sababu mtu anaweza kuishi bila degree lakini hawezi kuishi bila kazi. Na siku hizi nafasi za watu wa diploma zimejazwa na watu wenye degree matokeo yake tumeharibu mfumo wa elimu nafasi ya technician inafanywa na mhandisi maana vyuo vya tech vimelazimishwa kuwa vyuo vikuu na cha kushangaza huyo mhandisi sio mzuri kama yule technician wa zamani pamoja na kuwa mhandisi ana degree

Marekani na nchi za ulaya sio kila anayemaliza high school lazima aende chuo kikuu bali wana mifumo ya elimu kuwa mwingine anaweza kwenda kupata degree mathalani ya biashara na mwingine akaenda kupata diploma mathalani ya unesi lakini mwenye diploma ya unesi analipwa mshahara zaidi ya yule mwenye degree ya biashara kwa lugha nyingine kuwa na maisha mazuri sio kuwa na degree inatokana na taaluma na mahitaji yake kwa wenzetu kitu cha muhimu ni ajira, kudhibiti mfumuko wa bei na huduma bora za afya. Kwa kuangalia indicators za uchumi yaani ajira, mfumuko wa bei, pato la mmoja mmoja na social services kama wenzetu wa ulaya Mkapa was much better kuliko Kikwete maana Kikwete ni msanii kabakiza kutaja idadi ya vyuo vikuu na urefu wa barabara mambo ambayo watu wanaweza kusihi bila kuwa nayo na kuacha vitu muhimu kama ajira, mifumuko ya bei na huduma za afya ambazo zimedhoofika.
 
hivi hawa statician wa siku izi no vilaza gani, 1961 kulikuwa na populatuion gani iliyohiotaji tuwe na vyuo vikuu viwili au kama sasa?
 
Shule za kata zinazozalisha form foum failures ni mafanikio ya kimilenia ya Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.

Na hii Pesa isiyo na Thamani nayo ni kwa sababu ya Tunu ya Uongozi uliotukuka wa Mh. JK.

Awamu hii ni shida tupu....
 
Mtu akiongeza matatizo zaidi tunaweza kusema amefanikiwa? Well wapo wanaojaribu kujenga hoja kuwa ndio "amefanikiwa" kwani kama matatizo yalikuwa kidogo halafu akayaongeza basi amefanikiwa kuongeza.
 
Hivi unajua kuwa mhariri wa hilo gazeti ni zomba utategemea nini kutoka hapo?
 
Last edited by a moderator:
Gosbertgoodluck

Nyerere "alipong'atuka" Tanzania haina pesa, foleni za hata mafuta ya taa wacha petroli na dizeli, bank kuu oimechomwa moto, wizara ya mambo ya ndani imechomwa moto, yote kuficha madudu yake aliokuwa akiyafanya.

Maviwanda na mashamba "alio taifisha" yote dead. Hakuna chema alicho kiacha, ukisafiri nje ukija na colgate airport unang'ang'aniwa kama kama umeleta johari za ughaibuni.

Ukipita na kikapu tu, hao mgambo wamesha kusimamisha wanataka kujuwa kuna nini? Foleni za hata vitu basic kama sukari na unga wa ugali vilikuwa vitu vya kawaida wakati wa Nyerere.

Na mengi sana mabaya hayasemeki yote.

Leo unasema Nyerere kajenga? Ni nini alicho kijenga? To the contrary, kaharibu na kabomowa kila kitu.

Mwinyi, hakuna malumbano, tunajuwa aliposhika madaraka nyoyo za wa Tanzani zikaanza kupowa, umaarufu wa RUKSA ulitokana na kila kitu basic kuwa luxury kwa wa Tanzania wakati wa Nyerere. Hata sabuni ya Lux ilikuwa ni kioja kuogea wakati wa Nyerere.

Mkapa, duhhh, ndio hayo madudu tunayaona Kikwete akiyafukuwa na kuyashughulikia taratibu na scientifically kabisa. Madudu yote ya ubadhirifu, ya wizi ya epa, yalikuwa wakati wa nani? MKAPA.

Kikwete, tunaona mema anayoyafanya, wala hatuna shaka nae. Mashule, leo kama kuna mtoto wa kiTanzania hafiki japo sekondari, ni kosa la jinai hilo. Maji, visima na upatikanaji wa maji safi Tanzania kwa kipindi kifupi cha Kikwete ni kushinda awamu zote za kabla yake. Ma-barabara, juzi tu wakati wa Mkapa ukitaka kwenda Mwanza inabidi uzungukie Kenya! Au nalo hulijui? Licha ya hiyo, nenda katazame Singida-Katesh-Babati-Minjingu. Nenda katazame Tanga-Horohoro. Nenda katazame Mbeya-Chunya- Tabora. Nenda Mkata-Handeni-Korogwe. Nenda Dodoma-Babati. Nenda, nenda, nenda.

Sijaongelea bado ya zahanati, sijaongelea vitengo vipya vya moyo na meno Muhimbili, sijaongele kutokomeza Malaria, sijaongelea madawa ya kupunguza makali ya Ukimwi, sijaongelea vyuo vikuu. Sijaongelea mengi tu.

Huoni? Au Husikii?

Ponda, radio imaan, moh'd said n co ltd.. Ideologies @ work
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom