Nyerere Hakuwa na mapungufu, alikuwa Kiongozi Mbovu!

Wanajamii wote mmeshindwa kutofautisha mambo ya msingi yaliyohitaji kufanywa zama za Nyerere na baada ya hapo. Mazingira ya wakati wake, nikimaanisha kuwa ndio wakati alikuwa anaanza kutengeneza nchi baada ya kupata uhuru bila wataalam, na kama walikuwepo basi ni wale ambao walitaka kutuandaa kuwa koloni mamboleo (wazungu na vibaraka), yalilazimisha kuangalia tu kwanza mambo ya msingi kama elimu, afya and the like. Sikatai kuwa alikuwa na mapungufu yake lakini si sahihi kusema alikuwa 'mbovu'. Wabovu walikuwa wale mababu zako waliokuwa wanacharazwa bakora na waarabu, wajerumani na waingereza. Kama unataka kulaumu kwa historia, anza na hao. Wewe unaona Nyerere ni mbovu umefanya nini kuonyesha utofauti. Kila siku tukiamka hapa tunakuta bei mpya ya petroli wala sikuoni barabarani ukirusha mawe. Matatizo yenu wasomi wa siku hizi mmekaa kama majibwa koko. Mabingwa wa kuandika humu kwa kujificha, lakini kwenda kukabiliana na maji ya kuwasha mnaogopa. Watu wamerisk maisha yao kwa ajili ya mtu kama wewe kwa kufichua maovu chungu nzima yanayofanywa na viongozi mbalimbali. Umefanya nini kusupport juhudi hizi? au unafikiri kujificha humu kwenye JF na kumzungumzia Nyerere ndio dawa ya kutibu matatizo tuliyo nayo sasa. Unataka kutuambia kwamba Prof. Shivji wa Kigoda cha Mwalimu yuko kimaslahi binafsi zaidi. Kama ni hivyo si vingekuwepo vigoda vingi tu. Anzisha chako basi cha nani sijui uone kama utakikalia.

Kama kuna watu walimsaliti Nyerere si muwaseme wao. Kwani hamuwajui? Mtu unakaa unatunga lihabari lilreeeefu kumsakama Hayati Mzee wetu. Hamna heshima hata kidogo. Kama mnakula kula majani yenu huko halafu mnatuleta habari zenu mbovu humu JF mkome kabisa.
 
Mkapa tu ndiye rais bora kabisa aliyeiongoza TANZANIA kwa mafanikio mengi. Waliobaki wote ni vilaza tu.
 
Ndugu yangu NasDaz, ni kweli Nyerere aliacha vyuo vikuu viwili UDSM na SUA. Lakini unakumbuka enzi za DarTech, Arusha Tech, Mbeya Tech, Chuo cha Usafirishaji, Mbegani, DSA, Chang'ombe Ufundi etc? Havikutoa degree but was the best in EAST AFRICA!! Hivi ni vyuo vilikuwa vinatoa hasa elimu ya ufanyaki kazi viwandani n.k. Enzi zile mtu akiwa na FTC anakuwa amewiva kweli kweli!! Hata kwenu NMB enzi zile kulikuwa na Chuo chenu pale Iringa sema nyie hamkukuta mambo hayo...
 
Tatizo kubwa la threads nyingi humu jamvini kuhusu Nyerere ni pale mapungufu ya wakati wa utawala ule wa awamu ya kwanza yanatumika kujustfy uzembe, wizi, ufisadi na kukosekana uwajibikaji wa serikali zilizofuata. Lakini dimensions na vigezo vinakuwa jumla jumla tu. Mfano mtu anasema JK ameleta zahanati nyingi kuliko raisi mwingine yeyote, lakini ukichallenge kwamba mbona hamna wauguzi wala madawa inaletwa hoja wakati wa Nyerere zilikuwa ngapi???????

....


1. Lakini kama watu wangekuwa wanafahamu mfano enzi zile kila shule ya sekondari ilikuwa na zahanati yenye qualified medical assistants, madawa yalikuwepo na hiyo ilisaidia sana kuelimisha watu kuondokana na imanai za kichawi ambazo walitoka nazo makwao kabla ya kuja shule. Leo hii hata shule hizo zinazotoza mamilioni zina zahanati au hata first aider?

Usisahau kuwa wakati huo hizo shule ndiyo kwanza zilikuwa zimetaifishwa. Walipowanyan'ganya madhehebu ya dini hizo shule walikuta hiyo mifumo ya afya yalikuwepo.

Angalia hata uwanja wa taifa tuliokabidhiwa na Wachina mwaka juzi, bado una upya wake kwa kiasi. Hebu rudi baada ya miaka kumi ya uendeshaji wa serikali uone kama bado litakuwa linafanana na sasa.

Unachotakiwa kuelewa hapa ni kwamba tunasema kuwa tatizo ni Nyerere alitaka kila kitu kifanywe na serikali, jambo ambalo limeshindikana ulimwenguni kote.


2. Enzi zile kila shirika la umma lilkuwa na chuo chake ukitoka shule ukaajiriwa na shirika hilo unaenda kwanza kusomea mambo ya hilo shirika, mfano chuo cha bandari, chuo cha reli, chuo cha posta na simu nk. huu ulikuwa utaratibu mzuri sana na haishangazi kuona makampuni ya migodi yamekuja tena na huu utaratibu. Sasa je vijana wanaoajiriwa siku hizi huku kukiwa na wababishaji lukuki kwenye makampuni na mashirika ya umma wanajifunza wapi?

SU kuwa na chuo siyo kitu cha ajabu sana. Ni uamuzi tu wa uwekezaji wa mapato. Na hata hivyo vyuo vilikua ni mianya mikuwa tu ya ubadhirifu.

3. Sijui kama kuna watu wanakumbuka enzi zile kwamba ATC ilishawahi kuwa mpaka na Boeing 767, leo watu wanajisifia kuleta nembo halafu wanajilinganisha na wakati ule.

ATC lilikuwa ni monopoly. Na wakati ule biashara ya ndege ilikuwa rahisi. Zilikuwepo pia Pan AM, TWA etc - ziko wapi leo. Hii haina uhusiano na umahiri wa Nyerere

4. Shule bure afya bure pamoja na uchache lakini mfano shule ilikuwa ni uwezo wako tu wa darasa utasoma mpaka ukimbie mwenyewe.

Haikuwa sustainable. Hamna kitu cha bure kitachoweza kudumu milele

5. Vijana wengi sana hawafahamu kwamba miaka ile ya mchonga karibu makao makuu ya mikoa yote ile ya zamani kulikuwa na lami na taa za barabarani ambazo siku hizi mnasubiri A1 outdoor wawawekee na kuchafua mandhari ya miji kwa matangazo kibaoo!

Wacha uongo wako bana. Barabara zimeanza kujengwa wakati wa Mwinyi. Kabla ya hapo ni barabara za mkoloni ndizo zilikuwepo, na zilikuwa hazifanyiwi maintenance. Kutoka Morocca kwenda Mwenge ulikuwa unatumia masaa mawili kwa sababu ya ubovu wa barabara. Samora Avenue ilikuwa ni mahandaki tupu. Dar - Arusha ilikuwa ni janga la taifa, basi likifika salama linabidi libadilishe springs zote.

Tuangalie mbele. Nyerere alifanya vyake lakini sasa hayupo tena. Hatafufuka kuja kutuongoza tena, ni sisi wenyewe tutajiongoza.
 
unajua ukiandika ubaya wa Nyerere unaweza jaza maktaba zote za CCM

Tanganyika ikitaka ukombozi sharti Jina la Nyerere lkifutwe na liitwe the most disgraced leader on planet!

sijui nianzie wapi!
 
Humu ndani, kuna watu wakiona Hayati Julius Nyerere, the First Preisdent wa URT anasemwa vibaya basi wanakuja juu!! Kinachonikera mimi, ni wengi wao kuhusisha na imani za dini! Kwamba, mtu akisema ubaya wa Nyerere, na hasa mtu huyo akihisiwa ni Mwislamu, basi hoja ya wapofu wa hoja watachukulia ukosoaji huo ni chuki ya waislamu dhidi ya Nyerere!! Hivi ni lini Waislamu wamepata kuwa na chuki na mwalimu?! Sasa haya mambo kwamba mtu akitaja mabovu ya Mwalimu basi ni chuki za waislamu dhidi ya mwalimu yanatoka wapi?! Binafsi, am muslim, na kama utaniambia nikutajie my favorite president sitasita kumtaja Julius Nyerere. lakini pamoja na yote hayo, kama nitaambiwa nitaje top two poorest presidents ever happaned in our history, basi Nyerere ni mmoja wapo, akiwa sambamba na mwinyi! Binafsi, nikimwangalia Nyerere, ni eneo moja peke yake ambalo linaweza kumweka kama best leader! hakuwa corrupt leader ingawaje serikali yake ilikuwa very corrupt government!! Na wala si kweli kwamba Nyerere alikuwa mkali kwa corrupt leaders, vinginevyo nchi hii Mwinyi asingeikuta alipoikuta! Sana sana ki2 ambacho labda Nyerere aliweza kuzuia ni kutokuwa na State House corrupt leaders...lakini ukitoka hapo, wengi walikuwa corrupts!

Serikali ya Nyerere ilijaa watendaji ambao walikosa kabisa uwajibikaji na ndio maana Mwinyi alikuja na kitu kilichojulikana kama Fagio La Chuma! Kwanini awe na fagi la chuma wakati uwajibikaji ulikuwapo?! Serikali isiyo corrupt, haiwezi kuwa na irresponsible leaders. Ni kweli, Nyerere hakuwa corrupt leader, lakini aliendesha corrupt government na anayebisha aniambie kwanini viwanda vyote vilifia mikononi mwake!!

Ni kweli JK ni goi goi! hata Nyerere alikuwa ni goi goi kupita kiasi!! hakuwa mkali kama tunavyoaminishwa watu ambao hatukuwa na ufahamu wakati wa utawala wake. Nyerer alikuwa mkali kwa wapinzani wake wa kisiasa, and not otherwise!! Kama alikuwa mkali kweli, umasikini tulionao ulitokea wapi?! Aliwafanya nini waliokuwa wanaharibu mali za umma zaidi ya kuwahamisha?! kama sio ugoi goi tuite nini hii?!

Kulikuwa na miradi kadhaa ambayo ilianzishwa wakati wa utawala wake, na vilevile ilikufa hata kabla haijafika kokote....sasa kama sio ubadhirifu huo tuite nini?! Siwezi kumsifia kiongozi aliye msafi yeye pekee na familia yake wakati serikali yake imejaa watu irresponsible!!

Amekaa Ikulu more than 20 years lakini ametoka akiwa ameachwa barabara zimejaa mahandaki kila mahali!! Bahati mbaya sana, sehemu ambazo zilikuwa na corrupt leaders toka kwenye serikali yake ndio sehemu pekee ambazo angalau zilikuwa na barabara nzuri kidogo! Sehemu ambazo walitoka honest leaders kama yeye, ndizo zikabaki balaa tupu!!! Hiyo ndio sababu kuu iliyofanya mikoa ya kusini kuwa hoe hae zaidi kwani viongozi wake wengi walikuwa honest kama yeye...hawa ni pamoja na akina Kawawa na Nnauye! Hivyo, umaskini wa kusini haukusababishwa na Nyerere kama Nyerere, bali ulisababishwa na irresponsible central government ambayo ugawaji wa keki ya taifa haukuwa the same! ilitegemea sana sehemu husika ana power gani serikalini and how corrupt s/he is!!!

Nyerere ameondoka akiwa ameacha vyuo vikuu viwili tu, UDSM na SUA na kuishia tu ktk kujenga vyuo vya kati ambavyo hata hivyo navyo productivity yake ilikuwa chini. Chuo pekee cha kati ambacho kilikuwa kinatoa elimu ya maana labda ni Mzumbe peke yake....na sababu kuu ni kwavile kilikuwa more political! Tena hata nina mashaka kama kweli kilikuwa kinatoa elimu ya maana!! tangu lini katibu wa nini sijui mwenye miaka 45++ akaweza kuhimili mikiki mikiki ya elimu ya juu?! Tunaambiwa enzi zake elimu ilikuwa na ubora kuliko sasa!! na hii ndio tabia ya wazee....kwamba kila ki2 chao kilikuwa bora!!! Huo ubora ulisaidia nini basi katika kutatua matatizo ya uchumi wa nchi hii?! Sana sana hao tunaoambiwa walikuwa wasomi wakati wa elimu bora ndio hao hao waliogeuka kuwa corrupts wasio na haya wakati wa Mwinyi.....bisheni!!! Kama ni kweli wakati huo elimu ilikuwa bora basi vilevile ilisaidia kuzalisha BEST CORRUPT LEADERS!!! Serkali corrupt haiwezi kuwa na jeuri ya kujenga vyuo vikuu vya kutiosha kwavile haina fedha.....kutokuwa na fedha ni dalili ya serikali corrupt!!!
MATATIZO ya umeme tuliyonayo hivi sasa source yake ilikuwa enzi za mwalimu!!! Serikali ya Mwalimu haiku-forecast mahitaji ya umeme over the next 50 years!! Ni kweli, wakati wa Nyerere, haukuwa wa mgao! Sasa mgao ungetoka wapi wakati nyumba zenyewe za umeme zilikuwa chache?! Mgao ungetoka wapi wakati hakukuwa na uzalishaji mkubwa wa kuhitaji matumizi ya umeme?! Mgao ungetoka wapi wakati hata kumiliki radio ilikuwa ni anasa?! Kwahiyo, si kwamba ni uongozi bora wa Nyerere ambao ulifanya nchi isiwe na mgao/upungufu wa umeme, bali hiyo ilikuwa ni matokeo ya serikali mbovu!

Tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Huduma gani za jamii?! hizo za kufuata zahanati kilometa 50 na shule ya msingi kilometa 10?! Dar es salaam yote hii aliacha shule saba tu za sekondari (za serikali, ambazo hata hivyo hakujenga yeye)-Jangwani, Azania, Tambaza, Forodhani, Kisutu na Kibasila!!! Nani atakayethubutu kusema kwamba shule hizo zilikuwa zinakidhi mahitaji ya elimu ya sekondari jijini? Huko mikoani ndo ilikuwa balaa tupu, unaweza kukuta mkoa mzima una shule moja au mbili za serkali.....bado tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Ni serikali gani ingeshindwa kuhudumia shule chache kama hizo?!

Ubovu wa serikali ya Nyerere ni mwingi kuliko uzuri wake, otherwise, wale wanaoona kwamba mgtu akisema basi ana chuki za kidini (styupid thinking) basi anitajie hapa mazuri yaliyofanywa na serikali yake ambayo natarajia yawe mengi kuliko mabovu!

wapo watakaosema kwamba Nyerere amewezesha nchi hii kuwa na amani! Kwani aliichukuwa wakati nchi haina amani?! Sifa kama hizo anatastahili kupewa Kagame aliyechukua nchi baada ya mauaji ya kutisha nchini mwake! Anyway, waliosoma historia wanisaidie kunitajia ni vita gani vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimepata kupiganwa Tanganyika katika karne ya 19! Kama hakuna au zilikuwa si za kutisha sana, basi inawezekana Watanganyika hatuna silika ya kupigana tangu zama hizo!!

Hivyo basi, mtu anavyotaja ubovu wa Nyerere inakuwa ni ujinga uliepitiliza kusema kwamba ni chuki binafsi...Na inakuwa sio ujinga, bali ni upumbavu mtu akisema ni chuki za kidini! Nyerere kama Nyerere alikuwa was a very good person BUT NOT A GOOD LEADER! He was a good person who was a poor leader! Kutokana na hayo, sipati kigumumizi hata chembe kusema wazi kwamba SI KWAMBA NYERERE ALIKUWA NA MAPUNGUFU, BALI ALIKUWA KIONGOZI MBOVU! Ukweli wenyewe ndio huo, ukiona mgumu kuumeza, chukua maji ushushie!

Anayekataa, atoe data za mazuri yake kama kiongozi yenyewe manufaa kwa Tanzania!

Mkuu mimi nakuunga mikono na miguu yote kwa huo mtazamo wako, unayoyasema yanaukweli sana, ni kwa mvivu tu wa kutafakari ndiye atakayepingana nawe. Mimi hilo jambo nimekuwa nikilitafakari kwa muda mrefu sana.
 
Mimi kwa mtazamo wangu what I can say in brief ni kwamba Nyerere was a greater leader who did
a great mistake.

Mojawapo ya makosa ambayo sitamsamehe kabisa Nyerere ni kuwa pioneer wa uchakachuajia wa kura
Tanzania. Pale alipochakachua ushindi wa Maalim Seif dhid ya Dr. Salmin Amour, Zazinzibar 1995. Hii dhambi ya
"kula nyama ya mtu" aliyo warithisha CCM ndiyo inaendelea kututesa hadi hii leo.

Nyerere set a bad precedence of vote rigging in Tanzania and History will be always there to judge him.
 
mm nimkatoliki lakini kwa hili lakutaka kumuita Nyerere mtakatifu ni ujuha mkubwa/ Yesu mwenyewe aliitwa baba akakataaga sembuse huyo nyerinyeri
 
Nimesoma kwa makini hii post. Nadhani vichwa vya waafrika vina shida fulani na ninadhani ni matokeo ya kitu kinachoitwa mental slavery, utumwa wa mawazo na umaskini wa mawazo pia ambao Nyerere alisisitiza pia. Pia ukiangalia kwa makini ndicho kilichotokea Libya (kwa kufananisha kwa uchache as a broader concept...).

Umaskini wa mawazo huja kwa hali ya kuwa proud na mawazo finyu ambayo mara nyingi ni zao la kutawaliwa na kukosa elimu sahihi ju ya maswala muhimu. Kwa mfano kutokana na kutwaliwa muda mrefu na wazungu, ilifikia wakati wazungu kutulazimisha kuingia katika vyama vingi na kusema ni demokrasia, kumbe maskini kwa nchi changa na maskini kama zetu ni sumu mbaya ya kuleta malumbano na utengano hivyo kuvunja kabisa nguvu moja ambayo matokeo yake yangekuwa pigo baya kwa wazungu, wazungu wenyewe waliwaza mbali na wao siku zote ni huleta mawazo ambayo kwa nje huonekana mazuri sana lkn kwa muda mrefu huwa ni mafanikio yao, kitaalam na kayika intelligensia ya maendeleo huwa ni matumizi ya doctrine mbili tofauti, moja ikiwa ni initiator na ingine ni sacred. Siku zote huwezi jua lengo la mwisho ni kama unavyoletewa zawadi ya vito na almasi huku wakichukua almasi au barabara na uranium, hii imeendelea kwa muda mrefu.

Sasa basi wanaomlaum Nyerere ni upungufu wa mawazo tu maskini, kumbe watu wengi hawakujua lengo lake kwenye nchi hii, na bahati mbaya watu wamekua wanashabikia kuongea hovyo tu bila hata takwimu. Hawajui wakati Mwinyi amechukua nchi ilikuwa na hali gani na baada ya kuachia kwa Mkapa aliiacha na hali gani, hata hivyo vipimo hawavijui jinsi vinavyotumika, again ni jambo la elimu finyu. Kwa uchache tu hata inflation na GDP ni vipimo ambavyo watanzania wengi hawavijui maskini na uhusiano na maendeleo ya nchi pia hawajui. Ni shida kubwa!!


Kifupi tu- Nyerere aliongoza na kuacha nchi na inflation ya chini ya asilimia 5. Wazungu waliona Tsh ni very strong currency na hivyo walishinikiza kudevalue Tsh kwa vipingamizi kadhaa mara baada ya vita ya Kagera na kwa mshtuko wa uchumi wa dunia baada ya cold war, baada ya Mwinyi kuchukua nchi inflation ilipanda kufikia 30%!Government revenue ikashuka mpk 30 billion per month! Hali ya uchumi iliharibika wakati wa Mwinyi kwa kuwa wazungu kupitia IFM na World bank kushinikiza mambo mengi yaliyolenga total control kwa nchi za afrika. Rushwa ikashamili zaidi maana walilenga pia kanuni za kijinga za utawala bora, free trading etc, zilizoleta upenyo wa mashirika ya umma kufa na kuruhusu sector binafsi.

Wengi hawajui hata New World Order ambayo Nyerere alijua from start, na hata katika kikao cha NEC cha dom alipokuwa anahutubia south south commission report aliongea, lengo la Nyerere lilikuwa ni kupambana na nguvu hizi kwa kutumia umoja wa afrika, hakuwa akingalia karibu kama viongozi wengi wafinyu wa mawazo, tafuteni elimu hii mpate kujua wazungu wanatumia mbinu gani kudidimiza mawazo endelefu, acheni kulaum.

Read more books, history and facts..--
 
Haya wa dunia leteni mazuri ya Nyerere maana mimi nikisema hakuna, mtabisha lakini kuonesha zuri lake hamuwezi.
Yule babu na apumzike kwa amani tu, ila kiukweli hakuwa kiongozi mzuri japokuwa binafsi alikuwa mtu mzuri. Kama aliweza kutumia nguvu nyingi kuwadhibiti wapinzani wake kisiasa, kwa nini asingetumia nguvu hiyohiyo kuwawajibisha wala rushwa na watumia madaraka vibaya? Kuna wakati alikuwa mbishi sana kufuata ushuri wa maana toka kwa watu wa chini yake, huo ni udikteta. Nchi hii mtu akifa basi hata mabaya yake yote hugeuka kuwa mazuri.
 
Nyerere sio bure....kuna kitu anacho some other guys are missing. Kwahiyo sasa we attempt to silence his name for good. Is it that simple?
 
Mh hata wewe watu waki analyse watapata ubovu wako mpaka ukashangaa. Anyway kama ni mfatiliaji mzuri wa hotuba za orig JK ipo anayokiri kabisa walifanya makosa na anahoji kwa nini wasifanye makosa kwani wao Malaika, anazidi kushangaa ''Ubaya wenu ni pale munapoacha mazuri na kuyahoji na kukumbatia maovu yao'', Nadhani ni kiongozi aliyekubali kujikosoa. Ni kweli alikuwa na mapungufu kama tulivypo mimi na wewe, but He did his best na alikuwa na mapenzi ya dhati na nchi yake. Swala la kuwa shambulia adui zake ni kawaida kwa kila binadamu hata mimi na wewe si ajabu tungefanya vibaya zaidi.
 
Mimi kwa mtazamo wangu what I can say in brief ni kwamba Nyerere was a greater leader who did
a great mistake.

Mojawapo ya makosa ambayo sitamsamehe kabisa Nyerere ni kuwa pioneer wa uchakachuajia wa kura
Tanzania. Pale alipochakachua ushindi wa Maalim Seif dhid ya Dr. Salmin Amour, Zazinzibar 1995. Hii dhambi ya
"kula nyama ya mtu" aliyo warithisha CCM ndiyo inaendelea kututesa hadi hii leo.

Nyerere set a bad precedence of vote rigging in Tanzania and History will be always there to judge him.

Leta ushahidi wa huo uchakachuaji wa kura Zanzibar! Otherwise, ukiambiwa mkeo/mumeo anachakachiliwa, kwa mawazo hayo uliyonayo utakimbilia kuvunja ndoa bila kwanza kufanya utafiti na kupata ushahidi!
 
Hakuna kama Nyerere. Kampeni yoyote chafu kuchafua jina lake haitashinda.

Kauli kama hizi ndizo wanazozitumia Wazanzibari na kubaini kama kumbe Watanganyika hawana akili vichwani mwao bali wana Matope ambayo yanawafanya wasiwe na mawazo ya maana!
 
Nyerere alitengeneza mabomu mengi ambayo sasa tunaona yakilipuka, na bado yataendelea kulipuka siku za mbele. mpaka chembe chembe za matengenezo yake zitakapokuwa zimetoweka kabisa.
 
Tatizo lililokuwepo chini ya mwalimu la kuwahamisha viongozi wabovu na wala rushwa kama punishment badala ya kuwavua madaraka na kuwafikisha kwenye mkono wa sheria, kusema kweli limetu cost na bado linaendelea kufanya hivyo...Ni culture mbovu ambayo mizizi yake ni CCM.

watu wazima ni vizuri kusema kitu unaweka na evidence badala ya kushupalia kitu ambacho umekuwa ukisikia kwa wengine na mwingine alisikia kwa mwingine and so on..., je unaweza kuweka mifano michache ya viongozi waliokuwa wabovu halafu baada ya kuvurunda wakahamishiwa sehemu nyingine!? Ni wakati wa Nyerere ambapo suala la uwajibikaji ilikuwa si suala la kubembelezana, mtu akiboronga anaachia ngazi mwenyewe, kumbuka Ali Hassan Mwinyi alipokuwa waziri wa mambo ya ndani(ishu ya kilombero),aliwajibika mwenyewe bila kushurutishwa wala kusubiri labda mambo yanaweza kupoa,alikuwa anajua msimamo wa Nyerere na vile vile hiyo ndio ilikuwa ni discipline ya viongozi wakati ule, sio leo hii kiongozi anaharibu,tume inaundwa na anapatikana na makosa lakini hawajibiki na mamlaka inayotakiwa kumwajibisha nayo inakaa kimya, katika hali hiyo ufisadi utaisha? lazima tuwe maskini omba omba na mwishowe ndio tunaambiwa tukitaka misaada lazima tubong'oe!
 
Humu ndani, kuna watu wakiona Hayati Julius Nyerere, the First Preisdent wa URT anasemwa vibaya basi wanakuja juu!! Kinachonikera mimi, ni wengi wao kuhusisha na imani za dini! Kwamba, mtu akisema ubaya wa Nyerere, na hasa mtu huyo akihisiwa ni Mwislamu, basi hoja ya wapofu wa hoja watachukulia ukosoaji huo ni chuki ya waislamu dhidi ya Nyerere!! Hivi ni lini Waislamu wamepata kuwa na chuki na mwalimu?! Sasa haya mambo kwamba mtu akitaja mabovu ya Mwalimu basi ni chuki za waislamu dhidi ya mwalimu yanatoka wapi?! Binafsi, am muslim, na kama utaniambia nikutajie my favorite president sitasita kumtaja Julius Nyerere. lakini pamoja na yote hayo, kama nitaambiwa nitaje top two poorest presidents ever happaned in our history, basi Nyerere ni mmoja wapo, akiwa sambamba na mwinyi! Binafsi, nikimwangalia Nyerere, ni eneo moja peke yake ambalo linaweza kumweka kama best leader! hakuwa corrupt leader ingawaje serikali yake ilikuwa very corrupt government!! Na wala si kweli kwamba Nyerere alikuwa mkali kwa corrupt leaders, vinginevyo nchi hii Mwinyi asingeikuta alipoikuta! Sana sana ki2 ambacho labda Nyerere aliweza kuzuia ni kutokuwa na State House corrupt leaders...lakini ukitoka hapo, wengi walikuwa corrupts!

Serikali ya Nyerere ilijaa watendaji ambao walikosa kabisa uwajibikaji na ndio maana Mwinyi alikuja na kitu kilichojulikana kama Fagio La Chuma! Kwanini awe na fagi la chuma wakati uwajibikaji ulikuwapo?! Serikali isiyo corrupt, haiwezi kuwa na irresponsible leaders. Ni kweli, Nyerere hakuwa corrupt leader, lakini aliendesha corrupt government na anayebisha aniambie kwanini viwanda vyote vilifia mikononi mwake!!

Ni kweli JK ni goi goi! hata Nyerere alikuwa ni goi goi kupita kiasi!! hakuwa mkali kama tunavyoaminishwa watu ambao hatukuwa na ufahamu wakati wa utawala wake. Nyerer alikuwa mkali kwa wapinzani wake wa kisiasa, and not otherwise!! Kama alikuwa mkali kweli, umasikini tulionao ulitokea wapi?! Aliwafanya nini waliokuwa wanaharibu mali za umma zaidi ya kuwahamisha?! kama sio ugoi goi tuite nini hii?!

Kulikuwa na miradi kadhaa ambayo ilianzishwa wakati wa utawala wake, na vilevile ilikufa hata kabla haijafika kokote....sasa kama sio ubadhirifu huo tuite nini?! Siwezi kumsifia kiongozi aliye msafi yeye pekee na familia yake wakati serikali yake imejaa watu irresponsible!!

Amekaa Ikulu more than 20 years lakini ametoka akiwa ameachwa barabara zimejaa mahandaki kila mahali!! Bahati mbaya sana, sehemu ambazo zilikuwa na corrupt leaders toka kwenye serikali yake ndio sehemu pekee ambazo angalau zilikuwa na barabara nzuri kidogo! Sehemu ambazo walitoka honest leaders kama yeye, ndizo zikabaki balaa tupu!!! Hiyo ndio sababu kuu iliyofanya mikoa ya kusini kuwa hoe hae zaidi kwani viongozi wake wengi walikuwa honest kama yeye...hawa ni pamoja na akina Kawawa na Nnauye! Hivyo, umaskini wa kusini haukusababishwa na Nyerere kama Nyerere, bali ulisababishwa na irresponsible central government ambayo ugawaji wa keki ya taifa haukuwa the same! ilitegemea sana sehemu husika ana power gani serikalini and how corrupt s/he is!!!

Nyerere ameondoka akiwa ameacha vyuo vikuu viwili tu, UDSM na SUA na kuishia tu ktk kujenga vyuo vya kati ambavyo hata hivyo navyo productivity yake ilikuwa chini. Chuo pekee cha kati ambacho kilikuwa kinatoa elimu ya maana labda ni Mzumbe peke yake....na sababu kuu ni kwavile kilikuwa more political! Tena hata nina mashaka kama kweli kilikuwa kinatoa elimu ya maana!! tangu lini katibu wa nini sijui mwenye miaka 45++ akaweza kuhimili mikiki mikiki ya elimu ya juu?! Tunaambiwa enzi zake elimu ilikuwa na ubora kuliko sasa!! na hii ndio tabia ya wazee....kwamba kila ki2 chao kilikuwa bora!!! Huo ubora ulisaidia nini basi katika kutatua matatizo ya uchumi wa nchi hii?! Sana sana hao tunaoambiwa walikuwa wasomi wakati wa elimu bora ndio hao hao waliogeuka kuwa corrupts wasio na haya wakati wa Mwinyi.....bisheni!!! Kama ni kweli wakati huo elimu ilikuwa bora basi vilevile ilisaidia kuzalisha BEST CORRUPT LEADERS!!! Serkali corrupt haiwezi kuwa na jeuri ya kujenga vyuo vikuu vya kutiosha kwavile haina fedha.....kutokuwa na fedha ni dalili ya serikali corrupt!!!
MATATIZO ya umeme tuliyonayo hivi sasa source yake ilikuwa enzi za mwalimu!!! Serikali ya Mwalimu haiku-forecast mahitaji ya umeme over the next 50 years!! Ni kweli, wakati wa Nyerere, haukuwa wa mgao! Sasa mgao ungetoka wapi wakati nyumba zenyewe za umeme zilikuwa chache?! Mgao ungetoka wapi wakati hakukuwa na uzalishaji mkubwa wa kuhitaji matumizi ya umeme?! Mgao ungetoka wapi wakati hata kumiliki radio ilikuwa ni anasa?! Kwahiyo, si kwamba ni uongozi bora wa Nyerere ambao ulifanya nchi isiwe na mgao/upungufu wa umeme, bali hiyo ilikuwa ni matokeo ya serikali mbovu!

Tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Huduma gani za jamii?! hizo za kufuata zahanati kilometa 50 na shule ya msingi kilometa 10?! Dar es salaam yote hii aliacha shule saba tu za sekondari (za serikali, ambazo hata hivyo hakujenga yeye)-Jangwani, Azania, Tambaza, Forodhani, Kisutu na Kibasila!!! Nani atakayethubutu kusema kwamba shule hizo zilikuwa zinakidhi mahitaji ya elimu ya sekondari jijini? Huko mikoani ndo ilikuwa balaa tupu, unaweza kukuta mkoa mzima una shule moja au mbili za serkali.....bado tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Ni serikali gani ingeshindwa kuhudumia shule chache kama hizo?!

Ubovu wa serikali ya Nyerere ni mwingi kuliko uzuri wake, otherwise, wale wanaoona kwamba mgtu akisema basi ana chuki za kidini (styupid thinking) basi anitajie hapa mazuri yaliyofanywa na serikali yake ambayo natarajia yawe mengi kuliko mabovu!

wapo watakaosema kwamba Nyerere amewezesha nchi hii kuwa na amani! Kwani aliichukuwa wakati nchi haina amani?! Sifa kama hizo anatastahili kupewa Kagame aliyechukua nchi baada ya mauaji ya kutisha nchini mwake! Anyway, waliosoma historia wanisaidie kunitajia ni vita gani vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimepata kupiganwa Tanganyika katika karne ya 19! Kama hakuna au zilikuwa si za kutisha sana, basi inawezekana Watanganyika hatuna silika ya kupigana tangu zama hizo!!

Hivyo basi, mtu anavyotaja ubovu wa Nyerere inakuwa ni ujinga uliepitiliza kusema kwamba ni chuki binafsi...Na inakuwa sio ujinga, bali ni upumbavu mtu akisema ni chuki za kidini! Nyerere kama Nyerere alikuwa was a very good person BUT NOT A GOOD LEADER! He was a good person who was a poor leader! Kutokana na hayo, sipati kigumumizi hata chembe kusema wazi kwamba SI KWAMBA NYERERE ALIKUWA NA MAPUNGUFU, BALI ALIKUWA KIONGOZI MBOVU! Ukweli wenyewe ndio huo, ukiona mgumu kuumeza, chukua maji ushushie!

Anayekataa, atoe data za mazuri yake kama kiongozi yenyewe manufaa kwa Tanzania!


Mkuu, vipi? Hii rap iliyoitema hapa japokuwa umejihami huna chuki binafsi lakini mnh! ninapata shida sana kukuamini.
Si kweli kwamba Mwalimu alikuwa 100% perfect. Mwalimu mwenyewe alishakiri kuwa hakuwa malaika na alishauri mabaya waliyofanya wamuachie lakini yapo mazuri wayachukue na kuyaendeleza.
Napenda sana kukujibu kwa kirefu hoja zako zote, kwa sababu kwa kweli nadhani ni hoja nyepesi sana kujibika. Lakini napenda kuweka msingi wa majibu yangu kwa kuomba ulist vyanzo vya mapato ya serikali ya Mwalimu ili tulinganishe na aliyoyafanya. na kisha utupe na vyanzo vya mapato ya serikali zilizofuata nazo tulinganishe na zilichofanya., halafu kisha tumhukumu Mwalimu kwa pamoja.
 
Nimesoma kwa makini hii post. Nadhani vichwa vya waafrika vina shida fulani na ninadhani ni matokeo ya kitu kinachoitwa mental slavery, utumwa wa mawazo na umaskini wa mawazo pia ambao Nyerere alisisitiza pia. Pia ukiangalia kwa makini ndicho kilichotokea Libya (kwa kufananisha kwa uchache as a broader concept...).

Umaskini wa mawazo huja kwa hali ya kuwa proud na mawazo finyu ambayo mara nyingi ni zao la kutawaliwa na kukosa elimu sahihi ju ya maswala muhimu. Kwa mfano kutokana na kutwaliwa muda mrefu na wazungu, ilifikia wakati wazungu kutulazimisha kuingia katika vyama vingi na kusema ni demokrasia, kumbe maskini kwa nchi changa na maskini kama zetu ni sumu mbaya ya kuleta malumbano na utengano hivyo kuvunja kabisa nguvu moja ambayo matokeo yake yangekuwa pigo baya kwa wazungu, wazungu wenyewe waliwaza mbali na wao siku zote ni huleta mawazo ambayo kwa nje huonekana mazuri sana lkn kwa muda mrefu huwa ni mafanikio yao, kitaalam na kayika intelligensia ya maendeleo huwa ni matumizi ya doctrine mbili tofauti, moja ikiwa ni initiator na ingine ni sacred. Siku zote huwezi jua lengo la mwisho ni kama unavyoletewa zawadi ya vito na almasi huku wakichukua almasi au barabara na uranium, hii imeendelea kwa muda mrefu.

Sasa basi wanaomlaum Nyerere ni upungufu wa mawazo tu maskini, kumbe watu wengi hawakujua lengo lake kwenye nchi hii, na bahati mbaya watu wamekua wanashabikia kuongea hovyo tu bila hata takwimu. Hawajui wakati Mwinyi amechukua nchi ilikuwa na hali gani na baada ya kuachia kwa Mkapa aliiacha na hali gani, hata hivyo vipimo hawavijui jinsi vinavyotumika, again ni jambo la elimu finyu. Kwa uchache tu hata inflation na GDP ni vipimo ambavyo watanzania wengi hawavijui maskini na uhusiano na maendeleo ya nchi pia hawajui. Ni shida kubwa!!


Kifupi tu- Nyerere aliongoza na kuacha nchi na inflation ya chini ya asilimia 5. Wazungu waliona Tsh ni very strong currency na hivyo walishinikiza kudevalue Tsh kwa vipingamizi kadhaa mara baada ya vita ya Kagera na kwa mshtuko wa uchumi wa dunia baada ya cold war, baada ya Mwinyi kuchukua nchi inflation ilipanda kufikia 30%!Government revenue ikashuka mpk 30 billion per month! Hali ya uchumi iliharibika wakati wa Mwinyi kwa kuwa wazungu kupitia IFM na World bank kushinikiza mambo mengi yaliyolenga total control kwa nchi za afrika. Rushwa ikashamili zaidi maana walilenga pia kanuni za kijinga za utawala bora, free trading etc, zilizoleta upenyo wa mashirika ya umma kufa na kuruhusu sector binafsi.

Wengi hawajui hata New World Order ambayo Nyerere alijua from start, na hata katika kikao cha NEC cha dom alipokuwa anahutubia south south commission report aliongea, lengo la Nyerere lilikuwa ni kupambana na nguvu hizi kwa kutumia umoja wa afrika, hakuwa akingalia karibu kama viongozi wengi wafinyu wa mawazo, tafuteni elimu hii mpate kujua wazungu wanatumia mbinu gani kudidimiza mawazo endelefu, acheni kulaum.

Read more books, history and facts..--

Sielewi kwa nini mchangiaji unadhani watu wanaotoa mawazo tofauti na ya kwako hawana akili. Usidhani wewe ndiyo mwenye akili kupita wote waliopo kwenye jamvi hili. Na wala Nyerere hakuwa na akili kupita Watanzania wote.

Nakushangaa sana unaposema Kifupi tu- Nyerere aliongoza na kuacha nchi na inflation ya chini ya asilimia 5. Wazungu waliona Tsh ni very strong currency ....

Siamini kama uyasemayo yanatoka moyoni mwako. Nyerere hakuacha pesa yoyote ya maana pale BOT. Inflation rate na Foreign Exchange rate vilikuwa vinatamkwa na serikali na hakuna wa kubishia. Wewe hushangai itakuwaje Inflation rate iwe 5% wakati hakuna mkate, sukari, mafuta ya kupikia, sembe, toilet paper, mchele, n.k? Unahitaji akili gani kung'amua udanganyifu huo? wewe hushangai itakuwaje exchange rate iwe Shs 7 kwa dola lakini unaambiwa tatizo la kutokuwepo vitu madukani ni ukosefu wa pesa za kigeni? Unahitaji akili gani kung'amua udanganyifu huo?

Where is the New World Order ambayo Nyerere alijua from start or was he fighting a losing war?
 
Back
Top Bottom