Nyerere azidi kumkaba Mkapa ataka kiongozi huyo aondolewe pensheni yake

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
Na Sitta Tumma, Mwanza

MBUNGE wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA), amezidi kumkaba koo Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, safari hii akitaka kiongozi huyo aondolewe pensheni yake, akidai kuwa anaitumia kwa maslahi ya chama chake cha CCM.

Nyerere aliingia kwenye mabishano na Mkapa wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki baada ya Rais huyo kudai kuwa mwanasiasa huyo si mmoja kati ya wanafamilia wa Julius Nyerere.


Hata hivyo, siku moja baada ya Mkapa kutoa kauli hiyo, familia ya Nyerere kupitia kwa mwanaye Madaraka Nyerere, ilijitokeza na kusema Vicent ni mwanafamilia wao kwa vile ni mtoto wa baba mdogo wao, Kiboko Nyerere.



Toka wakati huo, Vicent amekuwa akimwandama Mkapa, akidai kuwa anatumia nafasi yake vibaya kama Rais mstaafu kwani anagharamiwa mafao yake ya uzeeni (pensheni) kutokana na kodi ya Watanzania wote.



Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Mara baada ya kurejea kutoka Arumeru ambako chama chake kilitwaa kiti cha ubunge na yeye akiwa meneja kampeni msaidizi, Nyerere aliwaambia wananchi kuwa mpaka anapaswa kuiga mfano wa marais wenzake wastaafu.



"Mkapa anapaswa kuachana kabisa na ushabiki wa kisiasa Wakati wa chaguzi ndogo ikiwa ni pamoja na kukumbatia chama kimoja, wakati maisha yake anahudumiwa kwa fedha zetu wote, vinginevyo aondolewe pensheni ili abakie ‘mpiga debe' wa CCM," alisema.



Katika mkutano huo uliyohudhuriwa na mamia ya wananchi ukilenga kuzungumzia maendeleo ya jimbo na kujipongeza kwa ushindi wa Arumeru Mashariki, Nyerere alisema kuwa Mkapa kwa nafasi yake hiyo anapaswa awe mshauri wa vyama vyote na si kuipigia debe CCM.



"Akumbuke kwamba maisha yake yanaendeshwa na fedha za walipakodi wa Kitanzania hadi sasa, aache kabisa ubaguzi huo; atajenga chuki kubwa kwa wananchi," aliongeza.



Nyerere alilazimika kuzungumzia sakata lake na Mkapa baada ya wananchi kumwomba aelezee kidogo kauli ya kiongozi huyo ya kudai kuwa yeye si mwana familia wa hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere.



Kuhsu miradi ya maendeleo jimboni kwake humo, Nyerere aliuagiza uongozi wa manispaa ya Musoma mjini kuhakikisha unamfungulia mashtaka mahakamani mmiliki wa kampuni moja ya Ngeja iliyopewa tenda ya kusambaza umeme katika soko la Kamunyonge, iwapo itafika kesho pasipo kuanza kusambaza nishati hiyo sokoni humo.



Alisema tayari manispaa ilimpa hundi ya fedha za malipo ya kazi hiyo na kwamba ameonekana kutaka kutapeli fedha hizo.


 
Suluhisho ni katiba mpya,kama pension walipwe na nssf/ppf na sio sirikali kama mbwai mbwai bwana!
 
Walipwe na vyama vyao kwa maana ya mshahara na marupurupu mengine. Pension huwezi kumuondelea au useme alipwe na chama hiyo itakuwa ni kumuonea.
 
Baba yake alikuwa campaigner mkubwa wa CCM toka alipostaafu mwaka 1985 na 1990
 
Walipwe na vyama vyao kwa maana ya mshahara na marupurupu mengine. Pension huwezi kumuondelea au useme alipwe na chama hiyo itakuwa ni kumuonea.

Wenzetu wa Malawi waliweza kumuondolea pensheni rais mstaafu kwa kushiriki siasa akiwa mstaafu.
Watanzania bana!
 
"HIVI MKAPA KWANINI ULIMUUA BABA WA TAIFA!!?"
Huyu dogo hatokuacha kamwe hadi useme ukweli toka rohoni mwako na UTUBU!! Ole wako ujifanye kumjibu........!!!
Ulidhani yameisha!!? Dogo ana sapoti kubwa ya ukweli, na familia inamtumia kama chambo, sasa ropoka uone!!
 
vicent kampiga knock nut mkapa!hatokuja shiriki kampeni yoyote tena,i believe
 
Hili liwe fundisho kwa viongozi wetu wastaafu kuacha kubagua watz kwa misingi ya itikadi na kushiriki kampeni za vyama. Nilipigwa na butwaa pale mauaji ya wakereketwa wa Chadema yalipokuwa yanatokea kule Igunga yeye(Mkapa) aliendelea na kampeni. Sasa tufike mwisho tujali utanzania wetu na sio tofauti zetu.
 
Siku zote mi huwa nasema kwamba hili lijibwa mkapa ni lichawi sana na jambazi kubwa la rasilamali zetu so tuliache tu lipate vidonge vyake hadi life kwa pressure na ikidi baada ya hapo twende over-politics tufanye uchaguzi mdogo wa Rais mstaafu ili tumchague hata wasira kuliko hili jambazi undertaker.
BIGUP NYERERE.
 
Namchukia Mkapa, ni msaliti mkubwa sana wa nchi yetu.Ni jitu kuburi lisilo dhamini utanzania hata kidogo. Nani alishaona rais anawasemea mbovu wananchi kama alivyofanya Mkapa? Mwalimu alikosea kweli kuliona ndio linafaa kura rais.
Huyu mtu katukosesha fursa kubwa, madini hasa dhahabu. aliwapa wazungu bureee! sisi tukaishia kukandiwa kuwa tuna wivu wa kike, wavivu wa kufikiri nk...tena kweny hotuba ya kufungua mgodi mpya (Tulawaka). siamini mpaka leo kama Mkapa ni kweli mtanzania au Mmsumbiji kama walivyosema watu...hata hivyo niliona mtu kwenye Tim tv ya msumbiji anafanana na Mkapa kweli!
Conclusively, Mkapa si mzalendo hata kidogo...huwezi fananisha na Mwinyi aum Kikwete, hawa jamaa unaona kabisa ni watz halisi na wanadhamini wananchi...achana na madhaifu yao kama binadamu.

I HATE YOU MKAPA.
 
Suluhisho ni katiba mpya,kama pension walipwe na nssf/ppf na sio sirikali kama mbwai mbwai bwana!

Duh hapa mnataka kummaliza mama Maria Nyerere; maana naye hayo mafungu ya Serikali ndiyo yanamsaidia kuendesha hiyo Familia yake na yeye mwenyewe kwa ujumla"
 
Hawezi kupata ujasiri huo Nkapa. Anajua mahesabu yamekosewa ametumia formula isiyokuwa yenyewe. Kagusa mahali pabaya.
 
Back
Top Bottom