Mtu anaweza kukishangaa sana kichwa cha habari hapo juu. Lakini niliguswa sana na hotuba ya Nyerere jana kipindi cha Wosia wa baba utadhani alikuwa anamponda JK. Nilitokwa na machozi baada ya hotuba kwani niliona fikra nzuri sana za wazee wetu zinapuuzwa kwa sasa na zinaonekana hazina maana. Alisema mambo yafuatayo:
(i) Ni aibu rais na mawaziri wake kusafiri sana kwenda US, China, Russia nk kwa ajili ya kuomba
(ii) Si ushujaa kufanikiwa kupata misaada kutoka nje
(iii) Hatima ya kuombaomba nje ni kupuuzwa na mataifa yanayotoa misaada
(iv) Ni aibu nchi kutokusanya kodi na kuwategemea nchi nyingine wakusanye kodi kwao waje watusaidie
(v) Misaada hata siku moja haitapunguza umaskini. Alitoa mfano wa makanisa na misikiti kila siku tunatoa sadaka lakini hawajawahi kutosheka
(vi) Alisisitiza swala la uwajibikaji, matumizi mazuri ya rasilimali na kutoza matajiri kodi bila ya mzaha ili tuweze kujiendesha wenyewe kama nchi
Baada ya kusikiliza hotuba hii nimezikumbuka safari za JK nje kila mara kwa kisingizio cha kwenda kuomba na hata wakati wa kampeni alisema asiposafiri watanzania tutakufa njaa.
My take. Viongozi wa leo wamekosa fikra sahihi za kukomboa wananchi wanaona ni rahisi kuomba nje kuliko kujenga na kutekeleza mipango ya kujitegemea. Nashauri Mod aanzishe mijadala kati ya wana JF na viongozi wa siasa kuhusu sera za vyama katika mambo ya msingi kama kujitegemea, maendeleo, ajira, mambo ya nje nk. Tukifika hapo JF tutaacha kushabikia vyama "blindly" na badala yake tutajiunga na vyama kutokana na sera zake zinazozingatia uhuru na maendeleo ya Tz ya leo. Ijumaa Karim!
(i) Ni aibu rais na mawaziri wake kusafiri sana kwenda US, China, Russia nk kwa ajili ya kuomba
(ii) Si ushujaa kufanikiwa kupata misaada kutoka nje
(iii) Hatima ya kuombaomba nje ni kupuuzwa na mataifa yanayotoa misaada
(iv) Ni aibu nchi kutokusanya kodi na kuwategemea nchi nyingine wakusanye kodi kwao waje watusaidie
(v) Misaada hata siku moja haitapunguza umaskini. Alitoa mfano wa makanisa na misikiti kila siku tunatoa sadaka lakini hawajawahi kutosheka
(vi) Alisisitiza swala la uwajibikaji, matumizi mazuri ya rasilimali na kutoza matajiri kodi bila ya mzaha ili tuweze kujiendesha wenyewe kama nchi
Baada ya kusikiliza hotuba hii nimezikumbuka safari za JK nje kila mara kwa kisingizio cha kwenda kuomba na hata wakati wa kampeni alisema asiposafiri watanzania tutakufa njaa.
My take. Viongozi wa leo wamekosa fikra sahihi za kukomboa wananchi wanaona ni rahisi kuomba nje kuliko kujenga na kutekeleza mipango ya kujitegemea. Nashauri Mod aanzishe mijadala kati ya wana JF na viongozi wa siasa kuhusu sera za vyama katika mambo ya msingi kama kujitegemea, maendeleo, ajira, mambo ya nje nk. Tukifika hapo JF tutaacha kushabikia vyama "blindly" na badala yake tutajiunga na vyama kutokana na sera zake zinazozingatia uhuru na maendeleo ya Tz ya leo. Ijumaa Karim!