Nyerere alishiriki Mauaji ya Kassim Hanga?

Status
Not open for further replies.
Junius,
Uadilifu wa Nyerere unabaki palepale. Kumbuka kabla ya Hanga kwenda Guinea (kumfuata mkewe) alisetiriwa mainland na Nyerere. Alipofika Guinea akaungana na Kambona katika mipango ya kupindua serikali. Katika mazingira kama hayo Nyerere hakuwa na sababu tena ya kumhifadhi Hanga. Ndio maana nimesema Hanga alijichimbia kaburi lake mwenyewe/

Tuseme kweli kulikuwa na mpango huo kama unavyotaka, kwa nini Nyerere akaamuru aidha kwa kauli au matendo, Hanga auwawe?
Hanga alikutana na Bibi Titi Mohammed wakati harakati hizo za kina Kambona na Maganga, Nyerere alipomkamata Bibi Titi na kumpeleka Zanzibar gereza la kiinua miguu kwa Mandera au "kwa bamkwe", alihakikisha kuwa Bibi Titi anateswa na kukashifiiwa tu lakini asiuwawe, naye kama kama Hanga alikuwa akituhumiwa na madai hayo hayo unayoseama, na Bibi Titi alipotaka kukutana na Nyerere Zanzibar kwa kile alichokieleza "...anieleze kile hasa nilichomfanya mpaka kustahili kuvuliwa nguo na kukashifiwa na watoto wadogo ni nini...", Nyerere alikwenda akaonana naye na kumhakikishia vyombo vyake vya usalama vitafanya kazi yake, kwa nini hii isiwe kwa Hanga na wenzake ambao Nyerere aliwatoa kutoka mikononi mwake?
Nikauliza hata kama kulikuwa na mpango gani, kwa nini asishitakiwe kama Bibi Titi na badala yake akauwawa?
 
Hivi yule aliyepelekewa Yesu akanawa mikono ndo nani vile?

wanatheolojia mpo?

Yule aliyenawa mikono alishiriki kifo cha Yesu ama la?

Maana si ailjuwa kabisa kuwa ataenda kusulubiwa na mayahudi lakini hakuzuia licha ya kuwa na uwezo huo?

Labda nitapata mwanga zaidi hapa baada ya kuona alichukuliwaje mnawa mikono yule,sijui alikuwa mfalme Herode?

Kwenye picha sura ya mwalimu ilionyesha kuna something serious,kuna mwenye kuweza kutuwekea nakala ya hotuba hiyo?

Tunaweza kuona muungano ulikuwa na matatizo mengi, pengine mambo binafsi yakiingilia,sasa kama under utanzania,Kambona na kina Babu hawaku uwawa ama walilindwa, what happen to huyo Hanga?

Kama makosa aliyoyafanya yeye ni sawa tu na wezake hao kina Kambona,why him?

Kwani si mmesema hata Kambona alitaka kumpindua mwalimu? same issues with Othman and others..

Sasa kama mwalimu aliwa protect hao kina Babu et al, ina maana alijua kabisa fate ya huyo Hanga huko Zenji itakuwa tofauti na hao aliowaprotect, certainly kwamba atauwawa...

Lakini wengine hapa mnadai eti alijichimbia kaburi kwasababu alitaka kumpindua mwalimu yeye na Kambona, kama mwalimu alikuwa muumini mzuri wa muungano, pamoja na utawala wa kisheria, basi ange mprotect Hanga kama alivyomprotect Kambona, Abdulrahman Babu na wengineo, kwasababu makosa yao wote yanalingana...

There's something missing here.
 
Junius, kwako kupindua serikali halali ni kitu kizuri? Mapinduzi yanaendana na umwagaji wa damu. Na ndiyo aliyotaka kuyafanya Hanga. Kumbe badala ya kumpa nafasi Hanga amwage damu ya wengi tena wasio na hatia ikabidi yeye apotezwe na mzee Karume. Hatuwezi kumlaumu Nyerere kwa yale aliyoyafanya Karume kwani kama Rais wa Zanzibar alikuwa na uwezo wa kufanya lolote kwa wale waliokuwa chini yake. Siamini kama Nyerere alijua yale yatakayompata Hanga. Pengine alifikiri atashtakiwa na akipatikana na makosa atafungwa jela. Kumbe ikawa si hivyo! Katika jambo kama hili si rahisi na si vema kumlaumu Nyerere kwa makosa/matendo ya Karume. Kufanya hivyo si kumtendea haki. Nyerere asingeweza kujua yaliyo moyoni mwa Karume.[/QUOTE]
Mkuu nikueleze kitu, Hanga na Othman Shariff walipelekwa Zanzibar kutoka mikononi mwa Nyerere, na mda mrefu Nyerere alijuwa siasa za kimapinduzi zilivyokuwa zikiendelea Zanzibar za watu kuwawa, kupotea kusikojuulikana, kuporwa wake zao, kulazimishwa ndoa, kunyang'anywa mali zao n.k (rejea maelezo ya A.K Twala na ugomvi wake na Karume anaeleza mkasa huu akiwa gerezani)
Wakati Karume alipopeleka ujumbe wake kwa Nyerere amlete Othman Sharriff na Hanga, wazee kutoka mkoa wa Iringa ambako Sharriff alifanya kazi kama dakatari wa wanyama na kuishi nao vizuri waliandamana mpaka ikulu kumsihi na kumpigia magoti Nyerere kuwa asiwapeleke Hanga na Sharriff kwa Karume maana atawauwa tu.
Kama kweli Nyerere hakuwa na dhamira mbaya kwao kwanini asiwasikilize wazee wale na badala ya kuwapeleka Zanzibar akaamuru wafunguliwe mashitaka Dar au kuhakikisha wanakuwa salama kwa kuwa yeye alikuwa boss siyo!
Au bado unakata kusema kuwa Nyerere hakujuwa dhamira ya Karume kwa watu aliowaona kama maadui wa utawala wake?
 
Un authibitisho juu ya mawasiliano kati ya Sekou Toure na Mwalimu? Mawasiliano kati ya Marais siku zote huwa ni siri (Top Secret) sasa wewe mwenzetu uliyapataje maana wakati huo na kwa utaalamu upi uliokuwepo wa kudaka mawasiliano kama hayo?

Mkuu jifunze mwanyewe usingoje kila kitu uambiwe au usikie watu barazani wanasema, nakwambia nafahamu ugomvi wa Nyerere na Nkurumah itakuwa ya Sekou Toure?
Hanga hakuwa peke yake Guinea.
 
Mkuu jifunze mwanyewe usingoje kila kitu uambiwe au usikie watu barazani wanasema, nakwambia nafahamu ugomvi wa Nyerere na Nkurumah itakuwa ya Sekou Toure?
Hanga hakuwa peke yake Guinea.

Alikuwa na nani zaidi ya huyo Kambona ambaye watu washamtaja humu?
 
Alikuwa na nani zaidi ya huyo Kambona ambaye watu washamtaja humu?

Hanga na Kambona walikuwa marafiki wakubwa tu kabla hata Kambona hajazushiwa na Nyerere kutaka kupindua serikali. Hanga alipokuwa Guinea alikuwa mgeni wa raisi Toure ingawa machache kati ya wawili hao yapo vitabuni, ukitaka unaweza kutafuta maandishi ya binti yake Hanga aliyezaa na mkewe wa Kirusi binti huyu akiitwa Elena Hanga aliandika kuhusu historia ya wazazi wake sana tu. Zaidi unaweza kusoma katika link hapo chini. tujifunzeni tu wakuu haya majambo yamefichwa fichwa na siasa za ujamaa na kujitegemea hazikutaka tujitegemee kielimu na kifikra bali kuwa watiifu na mawazo ya mtu mmoja tu.

http://wshao.blogspot.com/2007/02/mungu-ataihukumu-dhuluma-hii.htm
l
 
Hanga na Kambona walikuwa marafiki wakubwa tu kabla hata Kambona hajazushiwa na Nyerere kutaka kupindua serikali. Hanga alipokuwa Guinea alikuwa mgeni wa raisi Toure ingawa machache kati ya wawili hao yapo vitabuni, ukitaka unaweza kutafuta maandishi ya binti yake Hanga aliyezaa na mkewe wa Kirusi binti huyu akiitwa Elena Hanga aliandika kuhusu historia ya wazazi wake sana tu. Zaidi unaweza kusoma katika link hapo chini. tujifunzeni tu wakuu haya majambo yamefichwa fichwa na siasa za ujamaa na kujitegemea hazikutaka tujitegemee kielimu na kifikra bali kuwa watiifu na mawazo ya mtu mmoja tu.

http://wshao.blogspot.com/2007/02/mungu-ataihukumu-dhuluma-hii.htm
l

Give us a break aloo! Huyo Hanga SIYO innocent kama unavyojaribu kwa bidii kupotosha watu hapa. Hanga alishiriki bega kwa bega kwenye mapinduzi ya Unguja & Pemba na aliwahi kuwa Makamu wa kwanza wa Rais Karume mara tu baada ya Mapinduzi. Kwa mantiki hiyo naye ni GUILTY sawa kabisa na Karume kwa mauaji ya halaiki yaliyofanyika wakati wa Mapinduzi. Its fair to suppose Hanga was a ruthless, dangerous and capable killer like Karume himself. So what's the big deal kama Chinjachinja mmoja kamwahi mwenzake? Wewe sema you got issues with Nyerere na nia yako ni kumchafulia tu jina mzee wa watu. Pambaaf!
 
aah! huu ni upumbavu, mikono ya muhammad ilijaa damu,
na ufirauni wake kuliko nyerere,
na watu wamwona mtume wa mungu, na bado wana mswalia wakidhani atasamehewa,
kama hakutubu yeye mwenyewe, wamtubie wengine?
ili hii maada ieleweke vua kwanza kofia yako ya udini,

Mheshimiwa hapa ume offend sana,na ulichokifanya ni kutangaza vita na Muumba wa mbingu,ardhi na vilivyomo baina yake bila kusahau mimi na wewe.Mtume Muhammad(SAW) ataendelea kuwa mtume wa MwenyeziMungu despite the attacks from every angle,kwa mtu mwenye akili na kutafakari,angepata majibu ya haraka sana juu ya uislam.Ina kila sifa ambazo ,kwa mujibu wa adui zake,isingestahili kuendelea kuwepo.Madai yako mengi:waumini wake ni un educated,uncivilised,backwarded etc,but still it's the fastest growing religion in the developed countries ambako wana kila aina ya maendeleo.
We have no comparative military mighty but yet tunatumiwa kila aina advanced weaponry,psychological warfare etc....,sijitetei na wala silalamiki..kwa sababu muislam yyte ana expect kupata hizi consequences as the test of faith.What am trying to do is to assure u that....HAKUNA kitakacho angusha uislam katika hii dunia....utaendelea kuhimili vishindo vyote na itaendelea kuwa ndio dini ya haki mbele ya Muumba.Kwa hiyo ukifanyacho wewe na watu kama wewe ni kupoteza muda na kujiongezea stress za life
Muislam wa kweli kausiwa subra dhidi ya vitimbi muvifanyavo huku akiwa na uhakika kuwa no matter how....the truth always floats
above lies.

Nakutakia kila kheir mkubwa
Qadhi
 
Ukitaka kuelewa kifo cha Hanga chambua uhusiano tete wa Nyerere na Karume katika muktadha tata wa Mapinduzi na Muungano!
 
Junius kaleta changamoto, inayohusu historia yetu na si kutukuza kila kitu alichofanya Nyerere (RIP)..Nyerere hakua mtakatifu kama wengi mnavyotaka iwe. Tujibu kwa hoja na facts kama alizoleta Junius.
 
Junius,
Uadilifu wa Nyerere unabaki palepale.... Alipofika Guinea akaungana na Kambona katika mipango ya kupindua serikali. Katika mazingira kama hayo Nyerere hakuwa na sababu tena ya kumhifadhi Hanga. Ndio maana nimesema Hanga alijichimbia kaburi lake mwenyewe/

"Alipofika Guinea akaungana na Kambona katika mipango ya kupindua serikali..."

Umejuaje hilo jambo Jasusi wewe?

Ili kumnyonga mtu, tuhuma kama hiyo inatakiwa ithibitishwe mahakamani Jasusi. Julius Nyerere kama Rais, tena msomi, ungetegemea aelewe maswala la utawala wa sheria. Unapomtembeza mtu gwaride mbele ya wananchi kwenye viwanja vya mnazi mmoja huku ukimnyanyapaa kwamba haini haini huoni hapo alishamhukumu kifo?

Mara nyingi tunaambiwa Nyerere, katika wakati wake, ni moja ya wa kwanza kabisa kuelimika, kuwa mjanja, kuelewa mambo ya kimataifa, ukombozi, siasa, haki na sheria, sanaa, mpaka kutafsiri vitabu vya Shakespear, usomi kwa ujumla. Lakini mmh, kuelimika kwenyewe kumbe ndo huko. Huyu nae alikuwa mtu wa kawaida tu Nyerere huyu.
 
Junius kaleta changamoto, inayohusu historia yetu na si kutukuza kila kitu alichofanya Nyerere (RIP)..Nyerere hakua mtakatifu kama wengi mnavyotaka iwe. Tujibu kwa hoja na facts kama alizoleta Junius.
Hivi June ameleta fact gani besides hiyo picha?lol
 
ipoiku utajua ukweli ila itaku too late watz blind ili hali tuna macho huyu babu alikuwa balaa ila watu hamjui tu
Lets hide as salary yangu mwisho wa mwezi heshima baa
Conquest.
 
Hivi June ameleta fact gani besides hiyo picha?lol

The late Colonel Seif Bakari ndio alimuua Abdallah Kassim Hanga na Othman Shariff pamoja na Mwalimu kujaribu kuwalinda...funny enough Bakari was never taken to task despite all the evidence and his own admission to the killings...sometimes Mwalimu hakuwa na uwezo na mambo ya Wazanzibari ndio maana dhan ya muungano shinikizi inapata nguvu.....sadly hata ndugu zao hawajui walipozikwa
 
Ili hoja hii iwe wazi isiangaliwe itikadi ya yule aliyeileta uwanjani halafu akili ya wachangiaji iwe huru! Kashfa na matusi juu ya watu nadhani hapa hayana nafasi!!Ukiona uwezo wako ni mdogo katika kuchambua mada, ninasihi usome tu halafu uondoke tu. Hapa kuna watu wanasemwa kuwa wamepata tu ki elimu baada ya kumegewa toka kwa watu wengine! Hoja isiyo na mashiko!!maana wenye kujiona wamegaji hawajui chanzo cha elimu. Ifahamike kuwa JF ina kauli mbiu yake kuwa "it's the.............of Great thinkers"
 
Hivi June ameleta fact gani besides hiyo picha?lol

Ameleta fact iliyoko kwenye picha, kwa nini uiweke picha "besides"?

Mtu kaleta ushahidi fulani unamwambia hapana, lete ushahidi mwingine pembeni ya huo, atakwambia niambie kwanza huu una nini, kwa nini niweke huu pembeni?

"...ameleta fact gani besides hiyo picha?" kwa nini "besides"?
 
Kuna tofauti kubwa baina ya madai na facts, sasa kaa hujui tofauti ni wazi hujui unachokiongea.

Wewe unayejua unachokiongelea, sasa sema unachokijua. FACTS :- Nyerere yuko kwenye hiyo picha na haya ndio maelezo
President Julius Nyerere is pictured on January 16th when he addressed an open air rally where the detained former Tanzania Minister and Vice-President of Zanzibar was brought to face the people. Mr. Kassim Hanga (seated between two police officers) is under detention with a number of other top Tanzanians after allegedly boasting that he had been called from voluntary exile in Guinea to lead an army coup on Zanzibar."
 
Ameleta fact iliyoko kwenye picha, kwa nini uiweke picha "besides"?

Mtu kaleta ushahidi fulani unamwambia hapana, lete ushahidi mwingine pembeni ya huo, atakwambia niambie kwanza huu una nini, kwa nini niweke huu pembeni?

"...ameleta fact gani besides hiyo picha?" kwa nini "besides"?

Sijui unataka nikujibu nini? Kwa hiyo unataka kusema kwene hiyo picha Nyerere anamchinja Hanga? LMFAO
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom