Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka

Kuwaza kwako rafiki yangu ni kufupi sana. You run into conclusions. Kufikia conclusion kwamba Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa kuwa alimwachia Kawawa uwaziri Mkuu badala ya kina Kambona kama ungekuwa mwanafunzi wangu wa political science ningekupa 8% ya upendeleo.

Je unasahau Nyerere, japo ya kuwa raisi kwa mika 23, alikuwa raisi mojawapo wa kwanza Africa kuachia madaraka kwa hiari? Na kumbuka alitaka kuachia mapema, lakini akasema basi ngoja angalau nisaidie kurekebisha makali ya vita ya Kagera. Angalia kwamba kina Museveni waliokuja baada ya Nyerere wamekuwa maraisi muda mrufu zaidi ya Nyerere!

Angalia kina Puttin wamerudi tena kwenye uraisi!

Nyerere alikjua nini kifanyike baada ya uhuru ili kuwafaidisha watanzania wote, vijijini na mijini, ki-elimu, afya na umasikini. akawa na mtazamo wa kisiasa wenye kupambana na haya mambo matatu; ujinga (elimu kwa wote), maradhi (huduma ya afya kwa wote) na umasikini (umiliki wa umma wa uchumi).

Kina Kambona walikuwa na mtazamo tofauti, walitaka tufuate sera za kibepali (capitalism). Nyerere akawa ana argue kwamba capitalism itazua tabaka la watanzania masikini sana na wachache matajiri sana - watwana na mabwana. Akasema mkiwinda mnyama kijijini, ni vema mwanakijiji apewe mgawo sawa, hata kama hakuhusika moja kwa moja kuwinda kwa kuwa alikuwa na kazi nyingine kijijini. (Kenyatta alisema hapana, waindaji wanapaswa kupata maini, na kama hukuwapo uambulie kitakachobaki baada ya wawindaji kuchukua sehemu nzuri nzuri!)

Sasa niambie, ungekuwa wewe ndio Nyerere, katika mazingira hayo, ungewaachia nchi kina Kambona ambao ukijua wazi mna mitazamo tofauti katika uongozi wa nchi? Nyerere alichofanya ni tamaa ya madaraka au rational thinking?

Unafikiri nini kingetokea iwapo angewaachia kina Kambona? Angefanya hivyo nadhani leo hii tungekuwa na historia inayosema Nyerere ailikufa kifungoni mwaka 1961, na wengi wetu lecture halls za UDSM tungekuwa tunazisikia redioni tu. Huenda baba yako hata darasa la saba asingefika!

Asante sana kwa kumueleza vizuri.
 
Mwenyeheri, DIKTETA Mwalimu Julius Kambarage Nyerere baba wa Taifa la Tanzania

[/QU umechemka sana toa hoja

Kwan hiyo sio hoja kwan sio mwenyeheri anaetaka kufanywa mtakatifu? Kwan hakuwa dikteta? Sio mwalimu sio ''baba'' wa Taifa? cha kushangaza kardinal Rugambwa hajatangazwa mwenyeheri Nyerere dikteta eti mwenye heri, no wonder RC wanamiliki ardhi kubwa ikitoka serikal... zidumu fikra za mwenyekiti
 
we nawe bwabwaee.nenda mombasa kama tz hufaidiki

Jibu hoja acha viroja! Ka wewe bwabwa unafkiri kila mtu bwabwa? Kwa utawala wa huyo dikteta Watz wanaofaidika ni wachache sana wengine tunastruggle kimpango wetu au wewe kasisi nini? Afu wewe na huyo Nyerere hamna uwezo wa kunihamisha Tanzania mlivyowahamisha babu zangu eti kuwapeleka kwenye vijiji vya kijamaa inatosha Mungu amuweke Dikteta Nyerere panapostahili
 
Kuwaza kwako rafiki yangu ni kufupi sana. You run into conclusions. Kufikia conclusion kwamba Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa kuwa alimwachia Kawawa uwaziri Mkuu badala ya kina Kambona kama ungekuwa mwanafunzi wangu wa political science ningekupa 8% ya upendeleo.

Je unasahau Nyerere, japo ya kuwa raisi kwa mika 23, alikuwa raisi mojawapo wa kwanza Africa kuachia madaraka kwa hiari? Na kumbuka alitaka kuachia mapema, lakini akasema basi ngoja angalau nisaidie kurekebisha makali ya vita ya Kagera. Angalia kwamba kina Museveni waliokuja baada ya Nyerere wamekuwa maraisi muda mrufu zaidi ya Nyerere!

Angalia kina Puttin wamerudi tena kwenye uraisi!

Nyerere alikjua nini kifanyike baada ya uhuru ili kuwafaidisha watanzania wote, vijijini na mijini, ki-elimu, afya na umasikini. akawa na mtazamo wa kisiasa wenye kupambana na haya mambo matatu; ujinga (elimu kwa wote), maradhi (huduma ya afya kwa wote) na umasikini (umiliki wa umma wa uchumi).

Kina Kambona walikuwa na mtazamo tofauti, walitaka tufuate sera za kibepali (capitalism). Nyerere akawa ana argue kwamba capitalism itazua tabaka la watanzania masikini sana na wachache matajiri sana - watwana na mabwana. Akasema mkiwinda mnyama kijijini, ni vema mwanakijiji apewe mgawo sawa, hata kama hakuhusika moja kwa moja kuwinda kwa kuwa alikuwa na kazi nyingine kijijini. (Kenyatta alisema hapana, waindaji wanapaswa kupata maini, na kama hukuwapo uambulie kitakachobaki baada ya wawindaji kuchukua sehemu nzuri nzuri!)

Sasa niambie, ungekuwa wewe ndio Nyerere, katika mazingira hayo, ungewaachia nchi kina Kambona ambao ukijua wazi mna mitazamo tofauti katika uongozi wa nchi? Nyerere alichofanya ni tamaa ya madaraka au rational thinking?

Unafikiri nini kingetokea iwapo angewaachia kina Kambona? Angefanya hivyo nadhani leo hii tungekuwa na historia inayosema Nyerere ailikufa kifungoni mwaka 1961, na wengi wetu lecture halls za UDSM tungekuwa tunazisikia redioni tu. Huenda baba yako hata darasa la saba asingefika!

Asante kwa kueleza Mazuri na kutokuwa mbinafsi kwa Hayati Julius.Mapungufu kila mtu anayake; huwa tunatakiwa kupima mema na, yakizidi mabaya tuna kila sababu ya kumsifu mtu huyo kwa mema yake!

Mabaya yake hawa waiomfuatia katika Urais naona kila siku twalalama kuwa wanayafanya kupita hata Julius alivyo-imagine kuwa yanaweza kufanywa!
 
Kama binadamu wote tulivyo ndivyo na Nyerere alivyokuwa,Biblia inasema wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa sababu hakuwa mkamilifu,hakuna binadam aliye mkamilifu,udhaifu wa Nyerere unaonekana dhahiri alipoachia madaraka ya kuongoza chama cha Tanu na kumkabidhi mtu aliyekuwa dhaifu wa kutupwa Kawawa
kulikuwa na watendaji wengi wenye uwezo mzuri kama wakina Kambona,Msekwa,Mwanjisi wengi tu ambao walikuwa very intelligent,Nyerere aliogopa kuwaachia mmojawapo wa hao kwa sababu alihofia watakuja kumzidi na kuchukua nafasi yake,kama binadamu naye alikosea mambo mengi hasa hili la kumpa uenyekiti wa chama mtu ambaye ni dhaifu
Nyerere alifanya kazi na watu wote hao na alijua uwezo wao,Rashidi Kawawa alikuwa hana sifa hata kidogo ila kutokana na woga wa Nyerere kumpa mwenye uwezo aliamua kumwachia
kumbe nyerere naye ni binadam na alijaa madhaifu kama binadamu sisi

Episionage;
Kuna aliyewahi kumu-UNGUsha (yaani kumpa sifa ya u-UNGU) Nyerere ndani ya jukwaa hili, labda tuseme? So you hate him, isn't it?
 
Kama binadamu wote tulivyo ndivyo na Nyerere alivyokuwa,Biblia inasema wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa sababu hakuwa mkamilifu,hakuna binadam aliye mkamilifu,udhaifu wa Nyerere unaonekana dhahiri alipoachia madaraka ya kuongoza chama cha Tanu na kumkabidhi mtu aliyekuwa dhaifu wa kutupwa Kawawa
kulikuwa na watendaji wengi wenye uwezo mzuri kama wakina Kambona,Msekwa,Mwanjisi wengi tu ambao walikuwa very intelligent,Nyerere aliogopa kuwaachia mmojawapo wa hao kwa sababu alihofia watakuja kumzidi na kuchukua nafasi yake,kama binadamu naye alikosea mambo mengi hasa hili la kumpa uenyekiti wa chama mtu ambaye ni dhaifu
Nyerere alifanya kazi na watu wote hao na alijua uwezo wao,Rashidi Kawawa alikuwa hana sifa hata kidogo ila kutokana na woga wa Nyerere kumpa mwenye uwezo aliamua kumwachia
kumbe nyerere naye ni binadam na alijaa madhaifu kama binadamu sisi

Kwenye blue, unasema alikuwa na Tamaa ya madaraka kwasababu hakuwa mkamilifu na hakuna binadamu mkamilifu. Kwa sababu hizo ulizotoa, viongozi wote pamoja na sisi na wewe (kama wewe ni binadamu) wana tamaa ya madaraka, kwa vile hakuna mkamilifu.


Kwenye red, ningependa tu kujua kutoka kwako, je Nyerere J.K mwenyewe aliwahi kukwambia kuwa alikuwa na hofu hiyo? Au ndio psychology yako uliyopata kijiweni ndio imekupa hiyo conclusion?
 
Kwan hiyo sio hoja kwan sio mwenyeheri anaetaka kufanywa mtakatifu? Kwan hakuwa dikteta? Sio mwalimu sio ''baba'' wa Taifa? cha kushangaza kardinal Rugambwa hajatangazwa mwenyeheri Nyerere dikteta eti mwenye heri, no wonder RC wanamiliki ardhi kubwa ikitoka serikal... zidumu fikra za mwenyekiti

kwani ni nyerere mwenyewe ndio alitaka kuitwa mtakatifu au mwenye heri au watu wengine ndio walioamua kumuita hivyo? yeye hana kosa lolote. na kumuita dikteta mwal sio mbaya kwani si kila dikteta ni mbaya, hata wewe wanao wanaweza kukuita dikteta ikiwa unawalazimisha kufanya yale unayoyaamini kuwa ni sahihi. na udikteta wake kwangu mimi sioni kuwa ulikuwa ni mbaya tena bado tunauhitaji kuliko sasa tuishivyo kila mtu ana madevu.
 
Jibu hoja acha viroja! Ka wewe bwabwa unafkiri kila mtu bwabwa? Kwa utawala wa huyo dikteta Watz wanaofaidika ni wachache sana wengine tunastruggle kimpango wetu au wewe kasisi nini? Afu wewe na huyo Nyerere hamna uwezo wa kunihamisha Tanzania mlivyowahamisha babu zangu eti kuwapeleka kwenye vijiji vya kijamaa inatosha Mungu amuweke Dikteta Nyerere panapostahili

kwa hiyo unataka kusema kuliko nyerere dikteta bora kikwete au mwinyi aliyeruhusu mambo yafanyike namna yoyote apendavyo. na kumopa madaraka kila mtu anayeyahitaji hata kama hana sifa?
 
Heri tamaa ya Madaraka kuliko Ufisadi na uasherati kama hao unaowajua wewe

mkuu elli,
hakuna heri yoyote kati ya hizo mbili,
hata hivyo kwa wale wanaofikiri nyerere alikuwa na uchu wa madaraka wanakosea,nyerere hakuwa na tamaa ya madaraka kama watu wanavyofikiri.angekuwa nayo asingeling'atuka kwani alikuwa na uwezo wote wa kuendelea kukaa katika madaraka na dola ikamlinda. kwa busara hakutaka kufanya hivyo.
 
Kama binadamu wote tulivyo ndivyo na Nyerere alivyokuwa,Biblia inasema wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa sababu hakuwa mkamilifu,1.hakuna binadam aliye mkamilifu,udhaifu wa Nyerere unaonekana dhahiri alipoachia madaraka ya kuongoza chama cha Tanu na kumkabidhi mtu aliyekuwa dhaifu wa kutupwa Kawawa. 2
kulikuwa na watendaji wengi wenye uwezo mzuri kama wakina Kambona,Msekwa,Mwanjisi wengi tu ambao walikuwa very intelligent,Nyerere aliogopa kuwaachia mmojawapo wa hao kwa sababu alihofia watakuja kumzidi na kuchukua nafasi yake,kama binadamu naye alikosea mambo mengi hasa hili la kumpa uenyekiti wa chama mtu ambaye ni dhaifu, 3
Nyerere alifanya kazi na watu wote hao na alijua uwezo wao,Rashidi Kawawa alikuwa hana sifa hata kidogo ila kutokana na woga wa Nyerere kumpa mwenye uwezo aliamua kumwachia 4
kumbe nyerere naye ni binadam na alijaa madhaifu kama binadamu sisi 5


1.
hakuna uhusiano, mtu anaweza akawa sio makamilifu lakini hana tamaa ya madaraka
2. kumuachia kawawa madaraka bado haithibitishi kuwa alikuwa na uchu wa madaraka isipokuwa aliamini kuwa kawawa pamoja na kutokuwa na kisomo kikubwa na mapungufu mengine aliaminika, lakini bado kwa kumuachia kawawa madaraka hakuoneshi kuwa alikuwa na uchu wa madaraka kwani ansingemuachia angekaa mwenyewe uwezo huo alikuwa nao.
3. pamoja na elimu walizonazo mwal hakuwa ameridhika kuwa wana uzalendo wa kuendeleza nchi hii kwa wakati huo na mtazamo wao pasishaka haukuwa alivyoona ungelipekeleka taifa pazuri. aliamua kwa busara kwa maslai ya taifa si kwa maslai yake yeye . maana yeye mwal aliwajua haio vizuri kuliko mimi na wewe leo hii
4.maelezo ya 3 yanajibu na hapa pia
5. ni kweli hakuwa mungu alikuwa na mapungu kama wengine.lakini alijitahidi kufanya yale mazuri aliyoamini yangetufaa sote. sio leo watu wanafanya yale yanayowafaa wao tu. ona tulipo.
haya ni maoni yangu
 
hoja hapa ni kuogopa wenye uwezo wa kuongoza kuWAWEKA KARIBU

mkuu una uhakika kuwa hao uliowataja wana uwezo wa kuongoza wano huo uwezo? wamelifanyia nini taifa hadi hivi tunavyosema. je ni wazalendo? je una hakika alikataa kuwapa nafasi jkwa sababu hiyo unayoifikiri?
 
Jibu hoja acha viroja! Ka wewe bwabwa unafkiri kila mtu bwabwa? Kwa utawala wa huyo dikteta Watz wanaofaidika ni wachache sana wengine tunastruggle kimpango wetu au wewe kasisi nini? Afu wewe na huyo Nyerere hamna uwezo wa kunihamisha Tanzania mlivyowahamisha babu zangu eti kuwapeleka kwenye vijiji vya kijamaa inatosha Mungu amuweke Dikteta Nyerere panapostahili

tena si bwabwa tu ni shehtwani
 
Asante sana kwa kumueleza vizuri.

kwanza mtoa mada anaongea lakini hajui HISTORY vipi uhuru ulipatikana na akina nani walikua na ushawishi mpaka uhuru ukapatikana na kama ange waacha hao madhalagani yangetokea...nyerere bila SIR G. KAHAMA..PAULO MWANI..NA AKINA BOMANI..NA CHEEF.MAREALE..UHURU TUSINGEPATA..hawa ndio walikua washawishi wakuu kwa WAKULIMA na ndio walikua wakuu wavyama vya Ushilika wakati huo...Rashidi M.Kawawa nae alikua muhim sana kwa Nyerere sababu ndio
 
Asante sana kwa kumueleza vizuri.

kwahiyo NYERERE bila Kawawa asinge fanikiwa malengo kwani Kawawa alikua ndio mwenyekiti na mwanzilishi wa Chama cha wafanyakazi TANGANYIKA na alikua haogopi Wazungu na alikua ana ushawishi mkubwa kwa wafanyakazi kama alivyokua CHILUBA..ZAMBIA...sasa mtu waaina hiyo usipo mshaka kalibu akiasi ana wafuasi wengi hilo ndio nyerere aliliona na akawa makini sana juu ya hilo ...kwahiyo Nyerere aliishi kwa kukumbuka wapi alikotokea..NYERERE
 
mkuu huku jf watu wengi wanamtukuza nyerere kupindukia, hawawezi kukuelewa.
Nyerere ndio alomaliza uchumi wa nchi yetu kwa sera zake mbovu,
ndie alielea matatizo mengi kama ya udini na muungano kwa kuwanyima wananchi uhuru wa kusema.

Wanaomtetea watuambie kilicho mkimbiza mzee mtei serekalini kama sio madudu ya nyerere.

Chakushangaza leo anataka kupewa utakatifu.

Ponda ametuharibia watu jamani. Anza na matatizo ya pale kwenu Nshara, nani chanzo?? Mnajazwa ujinga na nyie mnadanganyika kirahisi. Go to hell.
 
Kama binadamu wote tulivyo ndivyo na Nyerere alivyokuwa,Biblia inasema wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,Nyerere alikuwa na tamaa ya madaraka kwa sababu hakuwa mkamilifu,hakuna binadam aliye mkamilifu,udhaifu wa Nyerere unaonekana dhahiri alipoachia madaraka ya kuongoza chama cha Tanu na kumkabidhi mtu aliyekuwa dhaifu wa kutupwa Kawawa
kulikuwa na watendaji wengi wenye uwezo mzuri kama wakina Kambona,Msekwa,Mwanjisi wengi tu ambao walikuwa very intelligent,Nyerere aliogopa kuwaachia mmojawapo wa hao kwa sababu alihofia watakuja kumzidi na kuchukua nafasi yake,kama binadamu naye alikosea mambo mengi hasa hili la kumpa uenyekiti wa chama mtu ambaye ni dhaifu
Nyerere alifanya kazi na watu wote hao na alijua uwezo wao,Rashidi Kawawa alikuwa hana sifa hata kidogo ila kutokana na woga wa Nyerere kumpa mwenye uwezo aliamua kumwachia
kumbe nyerere naye ni binadam na alijaa madhaifu kama binadamu sisi

haisaidii kwa sasa, mwache apumzike kesho ni mimi na wewe.
 
toka prezidaa aitwe dhaifu na JJ Mnyika bac wapambe wake wanahangaika kutaka kudissolve kaul,huwezi kumwita nyerere dhaifu au alikuwa na uroho wa madaraka, labda utupe ushahid wa uroho wa madaraka wa nyerere
 
kwahiyo NYERERE bila Kawawa asinge fanikiwa malengo kwani Kawawa alikua ndio mwenyekiti na mwanzilishi wa Chama cha wafanyakazi TANGANYIKA na alikua haogopi Wazungu na alikua ana ushawishi mkubwa kwa wafanyakazi kama alivyokua CHILUBA..ZAMBIA...sasa mtu waaina hiyo usipo mshaka kalibu akiasi ana wafuasi wengi hilo ndio nyerere aliliona na akawa makini sana juu ya hilo ...kwahiyo Nyerere aliishi kwa kukumbuka wapi alikotokea..NYERERE

MKUU naomba kuuliza,Kawawa alikuwa anajua kiingilishi?
 
Na kwa nini tunakaa hapa kumjadili Nyerere na uongozi wake wa miongo mingi iliyopita, ambao hatuwezi hata kuurekebisha hivi sasa, na tunaacha kutumia hizo nguvu kujadili matatizo ya uongozi uliopo sasa ambayo tuna uwezo wa kurekebisha?

Jadili jinsi kundi letu litakavyopanda treni ambayo ipo kituoni sasa hivi, sio jinsi ambavyo tulipaswa kupanda treni ambayo tayari ilishaondoka na kutuacha.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom