Mkuu kwa taarifa hizi hamna Waziri Mzalendo kama Mh. Nundu, ila kwa Mafarisayo au wala rushwa mapapa Nundu ni adui namba moja? Kwa ukweli huu hivi Serukamba ni mbunge mwenye nia ya dhati kwa maendeleo ya nchi hii au ni mla rushwa bingwa, tena siyo yeye tu hata kamati yake yote ni wala rushwa, wahenga walisema samaki mmoja akioza ni wote wameoza.
Huyu jamaa anaitwa Mtulivu...hakurupuki...:smile-big:Mkuu tokea 2006 hadi leo hii umepost 2 tu ila umeshusha vitu duh.. tunakutegemea tena utakuja 2020 kwa post yako ya tatu
Omar Nundu hata kwa kumtazama tu unagundua kuwa hana ishara za ufisadi kama walizonazo akina Ngeleja, Maige. Hii nchi inachezewa kwa kuwa maovu yote yanaishia kwenye vyombo vya habari.
Kama hili swala lingeenda mahakamani ingethibitika bila shaka nani ni fisadi na nani ni mzalendo. Kwa serikali hii ya CCM ambayo imegoma kuwafikisha mafisadi mahakamani na imegoma kuwawajibisha TAKOKURU kwa kusinda wanaangalia FACEBOOK badala ya kukamata rushwa.
Mie ninaomba RAIS WETU Dr. Slaa akiwa na kundi lake la watu makini na hasa Ndugu (sitaki kumuita Muheshimiwa) Tundu Lissu waje walivalie hili swala njuga na kuweka wazi Pumba na mchele.
Kama swala lina utata namna hii, basi Zitto Kabwe pia atupe ukweli wake maana inaonekana na yeye kadanganywa na Homeboy wake Serukamba.
Nilishangaa sana kumuona Serukamba ghafla kawa MZALENDO mkubwa namna hiyo akitetea maslahi ya Taifa ila alipoona mambo yanakwenda vibaya kiasi kwamba hata Naibu Waziri wa Nundu anakwenda na maji, ghafla mdomo ukapata maji kinywaji na akashindwa kabisa kuweka sahihi kwenye listi ya Zitto. Na niseme wazi kabisa na wengine kama mimi mkumbuke milele kuwa ukimuona Peter Serukamba anamshambulia MTU WA CCM basi ujuwe hapo kazibiwa ulaji. Nafikiri hili inabidi liwe wazi milele. Ukimuona anamshambulia mpinzani, hapo ndiyo unaweza kushindwa kuelewa katangulia Tumbo mbele au CCM mbele. Huyu jamaa Serukamba kama ni kweli, ni mtu mbaya sana na wa kuogopa kama ukoma.
Kama hayo madudu ni kweli basi Nundu ahamie kabisa Chadema maana huko ndiko wapo Wazalendo wa kweli. Tunashukuru sana kuona bado wapo Watanzania wanataka kuokoa hata kidogo kilichobaki maana hii mifisadi ipo tayari kuwauza hata mama zao ili muradi itajirike. Mijitu hatari sana hii, khaaa!!!!!
Tafadhali sana CHADEMA, hili swala mliingilie kati na mlivalie njuga na mchukue msimamo mapema. Nundu lazima abaki kama waziri hapo alipo akama itaonekana kweli ni MZALENDO kama makaratasi yanavyoonyesha.
Serukamba, najua hukumu ya Ubunge wako imehamia Mahakama kuu, naombea Mungu na wewe ushindi wako wautengue. Wengine watasema dua la kuku..... Ila kuna siku Dua la watu laweza kukupata.
Mkuu kwa taarifa hizi hamna Waziri Mzalendo kama Mh. Nundu, ila kwa Mafarisayo au wala rushwa mapapa Nundu ni adui namba moja? Kwa ukweli huu hivi Serukamba ni mbunge mwenye nia ya dhati kwa maendeleo ya nchi hii au ni mla rushwa bingwa, tena siyo yeye tu hata kamati yake yote ni wala rushwa, wahenga walisema samaki mmoja akioza ni wote wameoza.