NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

Ni bora iweke kama attachment, na ziwe numbered ili tujue follow ikoje
 
Hizi barua hazimsafishi Nundu bali inaonyesha kuwa alikuwa ana kaurafiki haramu na hii kampuni ya China Merchants Holdings nje ya njia zinazokubalika yaani kiofisi maana hawa wanaonekana hawafuati njia sahihi zinazotakiwa kufuatwa na kampuni bali wanatumia kiongozi mla rushwa/mlafi kama Omar Nundu kuipiga bao kampuni ya China Communications construction Ltd ambayo tayari proposal yake imekubalika na imeshapata fedha toka Exim Bank China! Sasa sijui ni punda gani anaweza kuacha mradi ulioiva namna hiyo wa China Cummunications Construction Ltd akaenda kwa huu wa China Merchants Holdings ambao haujasema ni kiasi gani ita-finance huo mradi na kwa riba kiasi gani! hapa simply hii barua inaonyesha jinsi mawaziri wetu vilaza walivyo tayari ku-take risky decisions na ku-subotage miradi mikubwa ya maendeleo ili mradi tu wamehakikishiwa kushibishwa matumbo yao na miradi fake inayokosa transparency bali kupitia kwa vimemo viinavyoweza kui-cost nchi kama mikataba ya umeme ta Tanesco! Omar Nundu lazma ajiuzulu manina.....!

Hivi huwa mnaelewa mnachokisoma au mnakurupuka tu. Onesha ni barua ipi katika hizo inazoonesha uharamu wa Nundu.

Wacheni majungu yasiyo na mpango wala ukweli.
 
The bottom line hapa baada ya kusoma documents zote....na kwa uzoefu wangu......Waziri plus Naibu wake, Katibu Mkuu Omar Chambo, Shallanda, Dr, Nshama, Eng Fungafunga, Ngosha Magonya na DG wa TPA Mr. Mgawe........THEY MUST GO.....

Ramadhani Kijjah yeye apewe ONYO KALI..........

Nini kosa la Nundu hapo? Nundu amezuia kampuni moja isipewe huu mradi kwani wao ndio wapange bei, wafanye utafiti, wapewe kazi nayo ni CCCC na hayo ni kabla Nundu hajawa Waziri. Kwa hiyo afukuzwe kwa kuzuia ubadhirifu?

Mnaelewa mnachokisoma na kukisema?
 
OK, let's cut to the chase. Hilo deal la Bandari Kikwete kala ngapi? Wachina rekodi yao wanatuliza wakulu kwanza ili huku chini kuwe na urahisi. Tumeona hawa CCCC wakifanya hivyo Angola kwa nini Tanzania iwe any difference?
Mkuu Kiranga, there you are!, jana nilipomsikiliza Nundu, nilimhurumia kujaribu kuzuia deal la ulaji kwa nia njema kabisa ili kuliokoa taifa, bila ya kujua who is behind!. Hao CCCC wameshaanzia juu!. Sasa huyu Nundu kutia kauzibe atageuzwa mbuzi wa kafara!.

Comonsense logic inalazimisha kuamini ile deal ya rada, gulf stream, richmond etc sio tuu zilikuwa na baraka kutoka juu, bali pia mgao ulitangulia na ndio final benefisharies wa ile tozo!.
 
Nimeshawahi kusema kwasasa Serikali ya JK nguo,zinaanza kudondoka mojamoja. Hatimaye itabaki uch *** hapo ndipo kwenye swali nani ataitupia TAULO Serikali ya JK ili isibaki uch***?
 
Heee mbona mambo!

Juzi nilisikia Bungeni wakisema CCCC ilifanya feasibility study kumbe siyo hivyo tu bali ilifanya Detailed Design na kupata estimate za mradi! Kisha tunaambiwa wao ndio wapewe huo mradi bila ushindani!

Hii haiingii akilini labda ingekuwa mradi unatekelezwa kwa mpango wa design and build.
 
Conclusion utaipata ukisha-download nyaraka hizi, hatutamwaga mtama kwenye kuku wengi:)
attachment.php


Invisible:
Hapo ndiyo kwenye UTATA.

Naomba mwenye kujua zaidi aelezee kwa nini imegongwa MUHURI wa SIRI aka SECRET???

Ninadhani neno SIRI kumbe kwa Serikali linamaanisha DILI
 
Mbona vipi? Kwani wewe unafikiri CCM inalipiaje chaguzi zake? Kwa michango ya wanachama?
Sasa ndio nimeshakuelewa ni kwa nini unashauri tuwe na short term Contract, maana kuna wahuni walipogunduwa mkataba wa Dowans ni wa miaka 2 tu basi walifanya hila kuuvunja miezi michache kabla ya ukomo wa mkataba ule ili wapate kutuibia pesa kupitia Mahakamani.

Nadhani huu uhuni uliofanyika kwenye sakata hili kama ungekuwa umefanyikia China na Beneficially ingekuwa ni kampuni au Serikali ya Tanzania basi wahusika wote ambao ndio kina Nundu wa kule China basi wasingekuwa na adhabu nyingine mbadala zaidi ya kukabiliwa na adhabu ya kunyongwa.

Bado kuna kitu kinanitatiza kama Serikali ya China kwa jinsi ilivyokuwa haina mzaha na vitendo vya rushwa kama inaweza kufumbia macho uhuni kama huu. bado sijawaelewa Wachina kwenye hili sakata na nataka kujuwa their true colour.
 
Jamani sasa hivi Wachina si watu tena mtajawasikia kwani hata kipande cha barabara kati ya Dodoma Iringa wapo hao CCCC ni corrupt mpaka wanatishia vifo km utaingilia biashara zao
 
mi nathani hiyo miaka 45 haitakuwa na shida kama kodi watakayokuwa wanalipa hao wawekezaji itawekwa in such a way ina appreciate! Maana hata tukipewa tuendeshe hizo berths nakuhakikishia hata hiyo miaka 40 haitafika! na isitoshe kuna nyingine 12 ambazo TPA na TICTs wanazimiliki kwahiyo sioni tatizo!

Heeeyyyy....!!!! Shut up..... Shame..... Think twice or thrice.... i got shocked with ur IQ, whaaat....??? BOOT is purely theft, i warn people of Tz hawa Chinise wa leo are PURELY CAPITALISTS, yaani mabepari wabaya sana, sio wale wa ujamaa, watch out..... 530 mil USD, then uwape for 45 yrs...?? Wachina wanajua within 2 years hela yao imerudi ndio maana wanafukuzia sana, wachina ni wanyonyaji kuliko mjuavyo..... May be RA is behind the CONTRACT.....
 
Mkuu Kiranga, there you are!, jana nilipomsikiliza Nundu, nilimhurumia kujaribu kuzuia deal la ulaji kwa nia njema kabisa ili kuliokoa taifa, bila ya kujua who is behind!. Hao CCCC wameshaanzia juu!. Sasa huyu Nundu kutia kauzibe atageuzwa mbuzi wa kafara!.

Comonsense logic inalazimisha kuamini ile deal ya rada, gulf stream, richmond etc sio tuu zilikuwa na baraka kutoka juu, bali pia mgao ulitangulia na ndio final benefisharies wa ile tozo!.
Mkuu Pasco una maana beneficiaries walishachukua chao mapema hivyo PIGA GEUZA CCCC lazima wapewe na ili waweze kurejesha pesa walizotoa. Hata hizo za Mfutakamba ni sehemu ya hizo pesa. Watu wanachukua upfront Mkuu. Unaambiwa chetu mapema kabisaaa sasa Nundu anapoingia kuzuia ndipo yanapomkuta hayo yanayomkuta! Anapigwa dana dana, anabezwa na kushambuliwa toka kila upande!

Jana nilivyomuangalia kwenye TV nikaona ana siri kubwa moyoni hakutaka tu kutaja ila Naibu wake ametaja. Ustaarabu tu wa kikazi na kutawalana mahala pa kazi; hata kama Naibu Waziri anapata ruhusa toka kwa Waziri Mkuu lakini si inabidi umuage Waziri wako? Utaondokaje bila Waziri wako kufahamu? Mfutakamba alitumwa?
 
Sasa ndio nimeshakuelewa ni kwa nini unashauri tuwe na short term Contract, maana kuna wahuni walipogunduwa mkataba wa Dowans ni wa miaka 2 tu basi walifanya hila kuuvunja miezi michache kabla ya ukomo wa mkataba ule ili wapate kutuibia pesa kupitia Mahakamani.

Nadhani huu uhuni uliofanyika kwenye sakata hili kama ungekuwa umefanyikia China na Beneficially ingekuwa ni kampuni au Serikali ya Tanzania basi wahusika wote ambao ndio kina Nundu wa kule China basi wasingekuwa na adhabu nyingine mbadala zaidi ya kukabiliwa na adhabu ya kunyongwa.

Bado kuna kitu kinanitatiza kama Serikali ya China kwa jinsi ilivyokuwa haina mzaha na vitendo vya rushwa kama inaweza kufumbia macho uhuni kama huu. bado sijawaelewa Wachina kwenye hili sakata na nataka kujuwa their true colour.

Wewe una assume Wachina wanajali fairness ndiyo maana unashindwa kuwaelewa. Hawajali. Wanajali economic interests zao tu. Ndiyo maana wanawekeza popote pale, kwa Gaddafi, Mugabe, Al-Bashir, Ahmadinejad etc.Human Rights na fairness kwao si jambo kubwa.

Wachina hawana tatizo na kampuni ya kichina kutoa rushwa kwa mtendaji wa kampuni/ serikali ya Tanzania ili kupata tender kirahisi Tanzania.Sina hakika hata kama Wachina wana sheria za kubana makampuni yao yasitoe rushwa nje kama sheria za Kimarekani zilivyo kwa mfano "Foreign Corrupt Practices Act" http://en.wikipedia.org/wiki/Foreign_Corrupt_Practices_Act (Wal-Mart wana scandal kwa kutoa rushwa ili wapate competitive advantage Mexico, rushwa imetolewa Mexico na Wal-Mart Mexico lakini kwa kuwa kampuni tanzu ni la Kimarekani wanataka kushtakiwa Marekani)

Ila kama unatoa rushwa kwa mtendaji wa Kichina ili kampuni ya Tanzania ipate tenda kirahisi rahisi China, ikijulikana huyo mtendaji wa kichina anaweza hata kupewa adhabu ya kifo.

Mambo ya mkuki mtamu kwa nguruwe kidizaini fulani hivi. Wanacheza rafu sana lakini hawataki kuchezewa.
 
wewe acha ujinga. Wewe unaleta lugha za kipuuzi za mitaani za kumwaga mboga ati wote mkose! otherwise nakuona mbumbumbu na kusema kweli huwa sioni mantiki ya ubishi wako wa kipuuzi wa kila siku humu ndani Otherwise nakuona kama una-interest na kampuni ya Omari Nundu...!
Geza Ulole, thanks!.
 
Hivi hawa watu walikuwa wapi siku zote mpaka haya yote yafike kwenye hii stage. Hapa naona ni kifo cha mfa maji tu.
 
Hivi hawa watu walikuwa wapi siku zote mpaka haya yote yafike kwenye hii stage. Hapa naona ni kifo cha mfa maji tu.
Na bado kuna siku utajiuliza hili swali ilikuwaje mpaka leo ukakubali kuwa kibaraka wa CCM ili hali nchi inaangamia na kuna wanaoishi bila hata ya nusu dollar achilia mbali wale wa chini ya dollar 1.
 
Hamna usafi wowote hapa, hawa wote wezi! Ukiona wezi wa mali yetu wanagombana, chukua jembe ukalime!
 
Back
Top Bottom