Baadhi ya maneno ya wafiwa
"Chadema ndio ambao wameonyesha huruma ya kutusaidia"
"Chadema watasimamia mazishi ya mwanangu".
"Aprili mwaka jana nilimzika mdogo wangu, Mwita Ngoka, baada ya kupigwa risasi na mwaka huu mdogo wake, Chacha Ngoka, amekufa kwa kupigwa risasi na polisi hao hao"
Soma habari kamili (Mwananchi)
"Chadema ndio ambao wameonyesha huruma ya kutusaidia"
"Chadema watasimamia mazishi ya mwanangu".
"Aprili mwaka jana nilimzika mdogo wangu, Mwita Ngoka, baada ya kupigwa risasi na mwaka huu mdogo wake, Chacha Ngoka, amekufa kwa kupigwa risasi na polisi hao hao"
Soma habari kamili (Mwananchi)
MIILI ya watu wanne kati ya watano waliouawa na polisi katika mgodi wa African Barrick North Mara katika eneo la Nyabirama Nyamongo, wilayani Tarime itazikwa Jumatano wiki Ijayo baada ya kufanyiwa uchunguzi utakaowasaidia wafiwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya serikali.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na ndugu wa marehemu pamoja na uongozi wa Chadema, zinaeleza kuwa baada ya kutokutendewa haki na viongozi wa Serikali ndugu hao wamekubaliana mazishi hayo yagharimiwe na Chadema ambao wameonyesha kuwajali.
Ndugu hao wa marehemu waliiambia Mwananchi Jumapili kuwa wamepanga mazishi hayo kufanyika Jumatano baada ya shughuli za kuaga kufanyika katika Uwanja wa Sabasaba mjini Tarime.Vile vile wamesema wamekataa kuchukua rambirambi za Serikali kwa wakidai kuwa ni sawa na kuuawa kwa makusudi kwa ndugu zao halafu wao wachukue rushwa ya rambirambi.
Mmoja wa ndugu hao wa marehemu, Magige Gati, alisema wafiwa wamekubalia kuipa kazi ya kuratibu mazishi Chadema kwa sababu ndio ambao wameonyesha huruma ya kuwasaidia.Alisema Serikali imeshindwa kuwasaidia zaidi ya kuanza kuwatisha kuwa wazike haraka kabla ya kufanyika kwa uchunguzi wa kisheria.
Naye Samson Chacha Ngoka, mkazi wa Kewanja alisema Aprili mwaka jana alimzika mdogo wake, Mwita Ngoka, baada ya kupigwa risasi na mwaka huu mdogo wake mwingine, Chacha Ngoka, amekufa kwa kupigwa risasi na polisi hao hao, hivyo wananchi wameweka msimamo wa kutokubali kudanganywa na Serikali kukubali kuzika mapema kabla ya uchunguzi kufanyika.
"Mimi sikupenda mwanangu afe, nimehangaika naye halafu leo naambiwa siasa kweli, waue mwanangu kisha waje kunibembeleza kwa fedha haki ikowapi hapa," alisema huku akitokwa na machozi na kuongeza: "Chadema watasimamia mazishi ya mwanangu".
Katika hatua nyingine, viongozi wa juu wa Chadema, akiwamo Mbunge wa Singida Kaskazini, Tundu Lissu na Kada wa chama hicho, Mabere Marando, walitarajiwa kufika jana mjini Tarime kushughulikia taratibu za kisheria. Mkurugenzi wa Sera na utafiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mwita Waitara, alisema jana kuwa chama chake kimechukua jukumu la kuratibu mazishi ya watu hao wanne.
Akieleza jinsi Chadema ilivyojipanga katika kuhakikisha inawasaidia wafiwa katika shughuli hiyo, Waitara alisema: "Mazishi ni Mei 24. Tutabeba miili ya marehemu na kuileta Uwanja wa Sabasaba kabla ya kutawanyika kulingana na mipango ya ndugu wa marehemu kwa ajili ya maziko."Alisema Chadema haihofii vitisho vya polisi vya kuongeza vikosi vya askari polisi pamoja na magari ya maji ya kuwasha siku ya tukio hilo.
Alisema kabla ya siku hiyo watahakikisha wanamwona Mkuu wa Wilaya na Kamanda wa Polisi wa Wilaya kuweka wazi msimamo wao dhidi ya mauaji hayo.Kauli hiyo ya Chadema imekuja muda mfupi baada ya wanasheria wawili kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHCR), Onesimo Ole Ngurumwa na Pasience Mlowe, kukutana na wafiwa na kuwaahidi kuwa wamekusudia kuwapatia msaada wa kisheria kudai haki baada ya tukio hilo.
Wakati huo huo, polisi wamegonga mwamba katika jutihada za kutaka kuwalazimisha wafiwa kuzika miili ya ndugu zao mapema kabla ya kukamilisha taratibu za kisheria.Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji, Mwikwabe Makena aliliambia Mwananchi Jumapili kuwa polisi waligonga mwamba kutokana na msimamo wa familia kuwa hawatazika mpaka haki ipatikane.
Diwani amwaga machozi
Kutokana simanzi iliyojaa eneo hilo diwani Viti Maalumu (Chadema), PhelomenaTontora, huku akitokwa machozi alisema, "Ukimwi, ajali na risasi zinamaliza vijana wetu…"
Mkuu wa wilaya alipoulizwa kuhusiana na tuhuma za wasiwasi wao alijibu; "Suala lao liko mikononi mwa polisi uwaulize wao watakupa taarifa zote.