DALLAI LAMA
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 8,651
- 2,627
Mbunge wa Tarime, Nyambari Chacha Nyangwine amesema kuwa ahadi kubwa alizoahidi jimboni Tarime amezitekeleza ikiwemo kusambaza umeme maeneo mbalimbali jimboni humo.
Akizungumza na Jambo press hapa arusha hii leo Nyangwine ameeleza kuwa mbali na umeme amefanikiwa kusimamia malipo ya fidia kwa watu 13 walioathiriwa na maji ya kemikali ktk mgodi wa North Mara hatua itakayowezesha kampuni hiyo kutoa malipo haraka iwezekanavyo siku chache zijazo.
Katika kuhakikisha kuwa mgodi huo unawasaidia wakazi wa Tarime, bw. Nyangwine ameeleza kuwa amefanya mazungumzo yaliyozaa matunda kwa kampuni ya North Mara kukubali kutenga mfuko maalum wa maendeleo na pia kutengwa kwa fedha za fidia za wakazi waliohamishwa kupisha upanuzi.
Aidha kutokana na mafanikio hayo mbunge huyo wa Tarime amedokeza kuwa CHADEMA ina kazi ngumu kumwangusha ktk kiti cha ubunge jimboni humo mwaka 2015.
TARIME NI JIMBO LILILOTAWALIWA NA WABUNGWE WATATU NDANI YA MIAKA MINNE ILIYOPITA.
Akizungumza na Jambo press hapa arusha hii leo Nyangwine ameeleza kuwa mbali na umeme amefanikiwa kusimamia malipo ya fidia kwa watu 13 walioathiriwa na maji ya kemikali ktk mgodi wa North Mara hatua itakayowezesha kampuni hiyo kutoa malipo haraka iwezekanavyo siku chache zijazo.
Katika kuhakikisha kuwa mgodi huo unawasaidia wakazi wa Tarime, bw. Nyangwine ameeleza kuwa amefanya mazungumzo yaliyozaa matunda kwa kampuni ya North Mara kukubali kutenga mfuko maalum wa maendeleo na pia kutengwa kwa fedha za fidia za wakazi waliohamishwa kupisha upanuzi.
Aidha kutokana na mafanikio hayo mbunge huyo wa Tarime amedokeza kuwa CHADEMA ina kazi ngumu kumwangusha ktk kiti cha ubunge jimboni humo mwaka 2015.
TARIME NI JIMBO LILILOTAWALIWA NA WABUNGWE WATATU NDANI YA MIAKA MINNE ILIYOPITA.