MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Kwa miaka mingi wakulima wa Kisarawe tumekuwa tukisumbuliwa sana na wanyama waharibifu hasa nyani na nguruwe, mwaka huu neema ya ajabu imetuzikia, kwani sasa hivi wapo wawindaji wengi sana kutoka jijini Dar es Salaam wakiwinda na kutega mitego kuwakamata wanyama hawa. Ni wiki ya pili sasa niko shamba sijaona nyani wala kishindo cha nguruwe mwitu usiku kama tulivyozoea miaka ya nyuma, tulikuwa tukiweka mtego jioni, asubuhi mtakuta bonge la nguruwe limeshikwa kwenye mtego, jamani leo ni wiki ya pili tukiamka asubuhi mitego zaidi ya mitano haina kitu.
Nyama ya nyani inauzwa Dar kama nyama ya mbuzi, baada ya watu wengi kushidwa kuhimili bei za nyama ya ng'ombe na mbuzi kwenye mabucha. Naomba hali hii ya iendelee hadi msimu wa mwaka huu uishe, utupunguzie gharama za ulinzi wa mashamba.
Nyama ya nyani inauzwa Dar kama nyama ya mbuzi, baada ya watu wengi kushidwa kuhimili bei za nyama ya ng'ombe na mbuzi kwenye mabucha. Naomba hali hii ya iendelee hadi msimu wa mwaka huu uishe, utupunguzie gharama za ulinzi wa mashamba.