kimya kimya....kama unamvizia kiziwi kwenye carpet la manyoya huku umevaa sox.....
Ukipata mpenzi mpya, usianze kupigia watu kelele ukihisi unadate malaika......malaika wote wapo mbinguni hakuna anayeishi Yaeda Chini.....usidhani huyo ni bora kuliko uliyemuacha....ni kuvumiliana tu....
Ukiuza paka wako wa nyumbani...ukanunua mbwa.....there is no progress....they are all domestic animals....
sawa jamani....?
Ukipata mpenzi mpya, usianze kupigia watu kelele ukihisi unadate malaika......malaika wote wapo mbinguni hakuna anayeishi Yaeda Chini.....usidhani huyo ni bora kuliko uliyemuacha....ni kuvumiliana tu....
Ukiuza paka wako wa nyumbani...ukanunua mbwa.....there is no progress....they are all domestic animals....
sawa jamani....?
Loh hapa pako na kitu.............Mamaa Preta hebu funguka mpenzi.
But kipenda roho dada, acha atambie wakati kwa sababu anao uhakika nao kwa sasa, we subiria tu ukisikia kimya jua kafikwa!! Au ndo mambo ya debe tupu?
dunia ya Mungu ,utajiri ni wa wazungu
te h teh teh kwa hiyo mdada unataka aache kumuita mwenzake honey? wewe bana! sasa atajuaje anapendwa?kinachoniuma ni kelele ndugu yangu.....hatupumui ujue......
ha ha...nimefurahi nukuu imekutoa chimbo.......
hakuna la zaidi mpenzi....ni kufunzana tu baadhi ya sehemu za maisha......
nukuu hii inaenda na msemo wa wahenga kuwa....'ivumayo haidumu....'
Ukipata mpenzi mpya, usianze kupigia watu kelele ukihisi unadate malaika......malaika wote wapo mbinguni hakuna anayeishi Yaeda Chini.....usidhani huyo ni bora kuliko uliyemuacha....ni kuvumiliana tu....
Ukiuza paka wako wa nyumbani...ukanunua mbwa.....there is no progress....they are all domestic animals....
sawa jamani....?
Ukipata mpenzi mpya, usianze kupigia watu kelele ukihisi unadate malaika......malaika wote wapo mbinguni hakuna anayeishi Yaeda Chini.....usidhani huyo ni bora kuliko uliyemuacha....ni kuvumiliana tu....
Ukiuza paka wako wa nyumbani...ukanunua mbwa.....there is no progress....they are all domestic animals....
sawa jamani....?
KAMA PRETA NA WENZAKE WALIPATA CHANJO YA NDUI/ small pox vaccine( which seems far from possible as they were born after the era of ndui) wataweza kuwa kwenye nafasi ya kuwahi kusikia maudhui matamu ya wimbo huu uliopigwa 80s. wimbo ulikuwa unaitwa busu pande tatu za uso....just take one min to pass through these lyrics and u will realise how talented this guys were in those days. their theme matches perfectly your nukuu
kwa wanaoukumbuka wimbo wakiwa wanafuatilia mashairi ni kama wanasikia sauti ya mzee bushoke na Jerry nashon a.k.a Dudumizi...unafahamu sauti ya ndege dudumizi
BUSU PANDE TATU - BIMA]
(Bima Lee, kibao kilitungwa na Max Bushoke, kuimbwa
nae pamoja na Jerry Nashon, Athumani Momba, naBwana Mugunda)
(Bushoke)
vipi penzi lajisuta lenyeweeeeeee
vipi sasa mbona lajisuta lenyewe
ulipokubali kunipenda ah ah
hukulazimishwaa
uliahidi kwa ahadi na viapo pia
uliahidi kwa ahadi na viapo pia
mwanzoni ilikuwa penzi motomoto
busu pande zote tatu za uso ohooooo
(wote)
ukweli nimeuona kwenye hili penzi letu
mwenye pendo la udanganyifu sasa ameonekana
kwenye mapenzi ya kweli
watu hushirikiana sheri
kwenye dhiki na faraja
kote hushirikiana
viko wapi sasa jamae
maneno ulionieleza
NAKUPENDA HAKUNA MWENGINE TENA
KUMBE YOTE NI UONGO
(Nashon)
uko wapi sasa moto wa mapenzi yetu mimi na wewe.. mimi nawe mamaa
uko wapi sasa moto wa mapenzi yetu mimina wewe
mbona umezimika hata majivu hayaonekani
mamiii mamiiiii
(wote) Kibwagizo
ama ni kweli mapenzi hayana mdhamini
nimeamini
yaweza vunjika wakati wowote
(Nashon)
ama ni kweli mapenzi hayana mdhamini
duniani duniani siku hizi
I love you busu nyingi ........ uongohuo
mamii mamiii
(wote) kibwagizo
(Nashon)
uko wapi sasa moto wa mapenzi yetu mimi na wewe
mbona umezimika hata majivu hayaonekani
mamii mamii